Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Namfahamu jamaa mmoja alikuwa tajiri sana enzi sisi tunakuwa jamaa alikuwa anatumia baiskeli tu kama usafiri wake binafsi ila alikuwa na magari mengi tu.

Ajabu alikuwa na hilux ya mizigo ila bidhaa za duka lake alikuwa anafuata yeye mwenyewe kwa baiskeli yake ila kwa wengine anakodishia hizo gari za kubeba mizigo.

Sisi tulizoea kumuita TAJIRI MCHAFU wananzengo walikuwa wanasema kamtoa sadaka mdogo wake na huyo mdogo mtu alikuwa chizi fresh anakaa hapo dukani kwa kaka yake tu na hakuna wakumtoa hapo.

Haya mambo yanawezekana ila nafikiri ni mateso sana.
Labda alikuwa anapendelea baiskeli ili afanye mazoezi au kuficha mambo yake kwa watoza ushuru wasimsonge songe au anabeba mizigo ya bangi n.k
Sioni uhusiano wa moja kwa moja wa huyo tajiri aliyeamua kutumia baiskeli na uchawi.
 
Exactly japo hisia zinaweza kuwa sahihi au zisiwe sahihi
Tatizo linakuja kwamba kwanza unakuwa na hisia fulani kaenda kwa mganga(huna uhakika), unakuwa na hisia(huna uhakika)kwamba huyo mganga ni kweli amebadilisha mambo yake na unakuwa na hisia tu(huna uhakika) kwamba katika kuwekewa mambo yake sawa fulani ametolewa kafara kwa kuuwawa au kufanywa kichaa. Hapa unakuwa mlolongo wa hisia tu bila uthibitisho!
 
Uchawi , nguvu za giza, utajiri wa kafara upo!!!! Lakini uchawi wa aina yoyote ni Siri na gharama kuanzia pesa, muda,kujitoa na kila kosa utakalofanya Lina gharama zake..... Usijidanganye mchawi aje atoe Siri zake hapa au formular zake kwako wewe ambae ni key board fighter usiweza kumsaidia lolote na huna impact yoyote kwake....... Ukichagua kuamini uchawi upo amini na ukichagua kutokuamini amini hivyo pia.
 
Mimi namjua mmoja alikua rafiki wa mama yangu utajiri wake ni wa kutumia nyota za wafanyakazi wake
Ila ilipofika mwaka 2018 ikabidi amtoe mtoto wake na akafanya hivyo

Ashawahi kumshawishi mama yangu ajiunge huko mama akakimbia nduki na urafiki ukaisha.

Alikuja dar kama housegirl kutoka Upareni ila sasa hivi ni tajiri.
Kumbe hadi kuna wanawake wenye utajir wa namna hii
 
Uchawi , nguvu za giza, utajiri wa kafara upo!!!! Lakini uchawi wa aina yoyote ni Siri na gharama kuanzia pesa, muda,kujitoa na kila kosa utakalofanya Lina gharama zake..... Usijidanganye mchawi aje atoe Siri zake hapa au formular zake kwako wewe ambae ni key board fighter usiweza kumsaidia lolote na huna impact yoyote kwake....... Ukichagua kuamini uchawi upo amini na ukichagua kutokuamini amini hivyo pia.
Kama uchawi ni siri watu baki tu wa mtaani huwa wanafahumu vipi kwamba fulani ametajirika kwa sababu ya uchawi?
 
Kuna waziri mmoja wa afya familia yake ina story ya kutatanisha sana lako hata yule meneja wake diamond wa morogoro inasikitisha sana kuona utu umepotea.
Ukifuatilia story za kila familia duniani unaweza kusema ni za kutatanisha sana ila kiwango cha utajiri na umaarufu ndio unazifanya familia nyingine kuongelewa zaidi kuliko familia nyingine.
 
Kumbe hadi kuna wanawake wenye utajir wa namna hii
Huyo mama ni tajiri kabla ya kugundua pesa zake ni za madawa nilienda kukaa likizo kwake.
Hilo jumba la kifahari nilijihisi mtoto wa mfalme nikapewa chumba ghorofani kipo full kuanzia tv mpaka friji.

Kuna watu wanaishi kama wapo mbele vilee halafu kazi yake anayoifanya nikisema inachekesha

Niishie hapa labda yupo humu asije akaona akaunga dots usiku akanifata buree
 
Back
Top Bottom