Uchaguzi 2020 Ununuzi wa ndege na ujenzi wa Chato Airport ni kashfa inayomtesa Magufuli?

Uchaguzi 2020 Ununuzi wa ndege na ujenzi wa Chato Airport ni kashfa inayomtesa Magufuli?

Lisu ndio anapoteza muda kuongelea hayo mambo.

Lisu kama anafikiri hizo ni kashfa za kumnyima kura Magufuli basi atakuwa hana akili kabisa.

Angekuwa na akili angefikiri kwamba kama hizo ninkashfa za kumnyima kura Magu basi Lowasa 2015 angepata kura zisizozidi 10
Mnajiamini kwa sababu ni majizi ya kuiba kura kama mnavyoaza kufanya sasa mnaandikisha watu majina
IMG_20200916_204547.jpeg
 
Sio siri tena, hoja ya matumizi ya pesa za serikali ili kununua ndege na ujenzi wa kiwanja kikubwa cha ndege tena cha kisasa katika kijiji cha Chato wilayani Geita ndio inarindima zaidi kwenye majukwaa ya kampeni za Urais za CCM kwenye huu uchaguzi mkuu wa 2020.

Karibu kila mahali Rais Magufuli alipofika kufanya kampeni ameweza kulizungumzia hilo huku akionyesha wazi wazi kuchukizwa na watu wanaozidi kuliibua hilo jambo kipindi hiki.

Hivi ni kweli hilo jambo linamtesa Magufuli kwa sasa?

Ni kwanini Magufuli anapoteza muda na nguvu zake kulitetea hilo jambo badala ya kujikita kwenye kuinadi ilani yake ya uchaguzi?
Katika kupiga hela Magufuli huwa ana pupa sana. Huwa hana maarifa ndiyo maana anaogopa Rais atakayekuja atafumua mambo yote na kumuanika. Anafanya kila awwzalo apate wabunge wa bendera fuata upepo ambao atawatumia kubadili katiba.

Angekuwa na akili asingempa kandarasi kampuni ambayo na yeye ana masilahi ya Mayanga Construction kujenga uwanja wa Chato. Ni wizi mtupu
 
La ununuzi wa ndege ni kashfa lakini afadhali ni rahisi kuitetea... Chato airport ni nyama ya kuku aliyekufa na kideri, hata uweke viungo gani, hainogi.
 
Sio siri tena, hoja ya matumizi ya pesa za serikali ili kununua ndege na ujenzi wa kiwanja kikubwa cha ndege tena cha kisasa katika kijiji cha Chato wilayani Geita ndio inarindima zaidi kwenye majukwaa ya kampeni za Urais za CCM kwenye huu uchaguzi mkuu wa 2020.

Karibu kila mahali Rais Magufuli alipofika kufanya kampeni ameweza kulizungumzia hilo huku akionyesha wazi wazi kuchukizwa na watu wanaozidi kuliibua hilo jambo kipindi hiki.

Hivi ni kweli hilo jambo linamtesa Magufuli kwa sasa?

Ni kwanini Magufuli anapoteza muda na nguvu zake kulitetea hilo jambo badala ya kujikita kwenye kuinadi ilani yake ya uchaguzi?
Hizo ndio sera za chadema?
 
Lisu ndio anapoteza muda kuongelea hayo mambo.

Lisu kama anafikiri hizo ni kashfa za kumnyima kura Magufuli basi atakuwa hana akili kabisa.

Angekuwa na akili angefikiri kwamba kama hizo ninkashfa za kumnyima kura Magu basi Lowasa 2015 angepata kura zisizozidi 10
Wanajitoa ufahamu hawa ndugu zetu.
 
Mbona unatoka nje ya mada.
Mada ni kwanini Magufuli anapambana kwa nguvu kubwa kulizima suala la ununuzi wa ndege na ujenzi wa kiwanja kikubwa cha ndege kijijini kwake?

Kabla sijajibu kwa Uelewa wangu nami naomba Kwanza nikuulize je, Ndege hazina Tija Kiuchumi? Je, Rais Kujenga Uwanja wa Ndege Kwao Kosa?
 
Haiwezekani mtu akwapue 2.7 trillions hazina, aminye uhuru na haki ya Watanzania, aminye uhuru na haki ya vyombo vya habari Nchini, ateke kutesa na kuwapoteza watu wanaomkosoa, adhulumu wafanyakazi, wakulima, wafanyabiashara na raia wa kawaida halafu isemwe kafanya vizuri! KAMWE HAIWEZEKANI!

Magufuli kafanya mambo mengi mazuri na pia ni binadamu ana mapungufu. Katika mambo anayopaswa kuyasahisha kama ataendelea awamu ya pili ya miaka mitano..

1. Kurudisha uhuru wa Bunge na Mahakama
2. Kupunguza na kupitia upya sheria kandamizi dhidi ya vyombo vya habari
3. Kurudisha imani ya wananchi kwenye vyombo vinavyosimamia chaguzi yaani NEC na ZEC
4. Kuzuia / kutokomeza matumizi ya watu wasiojulikana...
5. Kulegeza suala zima sheria za mifuko ya hifadhi ya kijamii (MAFAO)
6. Kupitia upya makato ya makopo ya Elimu ya juu.

Hayo mambo sita naimani kabisa yangekuwa hata ndani ya Ilani ya CCM, tungeongea mengine kwenye uchaguzi huu.

"maendeleo hayana chama"
 
Sio siri tena, hoja ya matumizi ya pesa za serikali ili kununua ndege na ujenzi wa kiwanja kikubwa cha ndege tena cha kisasa katika kijiji cha Chato wilayani Geita ndio inarindima zaidi kwenye majukwaa ya kampeni za Urais za CCM kwenye huu uchaguzi mkuu wa 2020.

Karibu kila mahali Rais Magufuli alipofika kufanya kampeni ameweza kulizungumzia hilo huku akionyesha wazi wazi kuchukizwa na watu wanaozidi kuliibua hilo jambo kipindi hiki.

Hivi ni kweli hilo jambo linamtesa Magufuli kwa sasa?

Ni kwanini Magufuli anapoteza muda na nguvu zake kulitetea hilo jambo badala ya kujikita kwenye kuinadi ilani yake ya uchaguzi?
iti izi bikozi ze gilti a afreidi!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mbona unatoka nje ya mada.
Mada ni kwanini Magufuli anapambana kwa nguvu kubwa kulizima suala la ununuzi wa ndege na ujenzi wa kiwanja kikubwa cha ndege kijijini kwake?
Mnatumia nguvu nyingi kuzipinga ndege lakini bado mnazipanda kwenda kwenye kampeni zenu za kumpinga Magufuli.

Muulize Zitto kama alipanda mtumbwi kwenda kigoma kufungua kampeni zake.
 
Lifisadi lenu Magufuli limeweka mtoto wa dada pale hazina hata taaluma hana akaingia ubia na mayanga ili aendelee na ufisadi ila sishangai maana aliwahi kuhonga nyumba za umma!
Chadema leo eti mnaujasiri wa kutamka neno fisadi? Mwaka 2015 mliliogopa hilo neno kama ukoma.
 
Sisi tunajipakulia wenyewe, hakuna wa kutukadiria.
Inapendeza kujilazimisha kuto ona uhalisia. Labda iwe ni makusudi kwa ajili ya propaganda ili kutovunja mioyo mashabiki wenye uwezo mdogo sana wa kuona na kutafsiri uhalisia.

Mfano mzuri huku Jimbo la Hai tulizungumza sana na jumbe kuzituma kwa bwana mkubwa jitahidi uwe unatembelea jimbo mara kwa mara muda utakavyo kuruhusu, tukaonekana hatufahamu majukumu ya Mkuu.

Sasa hatutaki kurusha picha tuu humu, wananchi wa kata mbili tofauti kwa siku mbili mfululizo mkubwa anazomewa na kufunga mkutano.
Asipopigiwa kura za ushindi kwa wenyeji hatuwezi kudanganyika kuwa kaibiwa kura. Japo kwenye mitandao tutaunga mkono kaibiwa, ila hali ni tete sana na labda yatokee maajabu mkubwa anavuka nguo.

Tujifunze kukubali uhalisi wa mwenendo wa kisiasa labda iwe propaganda.
 
Magu anapenda kujenga, mpaka pesa za wahanga wa tetemeko ameenda kujengea. TL awaambie wananchi kilichopo nyuma ya Magu kupenda majenzi.
Kwani anajenga Burundi au Malawi?? Wapinzani hamna hoja kabisa
 
Hata asipo shinda baada ya 28 oct wanzania watakua sio wale wa 2015.


Mradi wake wa kubadili katiba umesha buma.. atapata upinzani mkubwa sana.. hata akibadili hata tawala.

Kinacho takiwa kwa sasa Tanzania ifumuliwe tupate Tanzania mpya.


Muungano ufumuliwe na kila taasisi ifumuliwe.

Utawala ujengwe upya..
Ni mawazo yako au unachokisema kipo kwenye ilani yenu chadema?? Tumeomba mtupe ilani yenu mnapiga chenga
 
Inapendeza kujilazimisha kuto ona uhalisia. Labda iwe ni makusudi kwa ajili ya propaganda ili kutovunja mioyo mashabiki wenye uwezo mdogo sana wa kuona na kutafsiri uhalisia.

Mfano mzuri huku Jimbo la Hai tulizungumza sana na jumbe kuzituma kwa bwana mkubwa jitahidi uwe unatembelea jimbo mara kwa mara muda utakavyo kuruhusu, tukaonekana hatufahamu majukumu ya Mkuu.

Sasa hatutaki kurusha picha tuu humu, wananchi wa kata mbili tofauti kwa siku mbili mfululizo mkubwa anazomewa na kufunga mkutano.
Asipopigiwa kura za ushindi kwa wenyeji hatuwezi kudanganyika kuwa kaibiwa kura. Japo kwenye mitandao tutaunga mkono kaibiwa, ila hali ni tete sana na labda yatokee maajabu mkubwa anavuka nguo.
Tujifunze kukubali uhalisi wa mwenendo wa kisiasa labda iwe propaganda.
Una lipi la kumwambia huyo aliyezomewa na natural Allies?
 
Back
Top Bottom