DOKEZO Unyanyasaji kwa Walimu wanaofundisha shule ya St. Matthew

DOKEZO Unyanyasaji kwa Walimu wanaofundisha shule ya St. Matthew

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Ama kweli mambo yanabadilika,St. Mathew leo ndo imefikia hatua hii😂😂😂🙌🙌. Miaka ile darasa langu la form four tuliofanya mtihani wa taifa tulikuwa 406,hiyo ni kidato kimoja tu,walimu walikuwa wakijituma sana,walikuwa wakipewa motisha ya safari za nje,magari na pesa taslim kutoka kwa mmiliki wa shule,sikuwahi kusikia lawama za hivi. Hakikia imenivunjavunja moyo.
Kwenye mambo haya inajihidhirisha makosa ambayo wazazi wengi wanayafanya,unakuwa na mali na vitega uchumi lakini huwaandai warithi wako katika kuzisimamia mali na vitega uchumi vyao,mzee Mtembei nilisikia alikuwa akiumwa,akapelekwa India mara kadhaa sifahamu hali yake kwa sasa ila chini ya usimamizi wake ilikuwa vyema. Baada ya kuumwa NASIKIA aliweka watoto na mke wasimamie na kasheshe zikaanzia hapo na sasa ni wazi wameshindwa kabisa au wanaiharibu kabisa.
nakubaliana na wewe mimi nimesoma ile shule,Enzi za yule baba Mutembei ilikuwa St mattew's haswa jamani,Roho imeniuma sana kusikia haya dah,Sijui kwa sasa imekumbwa na nini eti usikie kuna disco shuleni wee! mwenyewe aliwahi kuwafukuza watu wa kampuni moja walikuja kufanya concert na wanafunzi walishiriki ummis balaa lake lilikuwa sio dogo alivyokuja akakuta hayo walimu walijuta,na zilikuwepo motisha nyingi kwa walimu
 
Ubuyu mwingine huyu mzee si ndio alitoa mawe ya balaa hata kusema naogopa, Kuna kanisa lipo Kijichi baada ya kuendelea vizuri Kama shukrani, kumbe walimu Wana Hali duni tu.
 
Shule za private kwa sasa hazina mapato. Serikali imejenga na inaendelea jenga Sekondari, na hakuna Ada.

Poleni sana.
Yaani shule yenye watoto 700,?haina mapato, na unafahamu karo ya pale, ni ndefu na huwa wana matokeo maxuri sana kwenye mitihani ya taifa.
 
nakubaliana na wewe mimi nimesoma ile shule,Enzi za yule baba Mutembei ilikuwa St mattew's haswa jamani,Roho imeniuma sana kusikia haya dah,Sijui kwa sasa imekumbwa na nini eti usikie kuna disco shuleni wee! mwenyewe aliwahi kuwafukuza watu wa kampuni moja walikuja kufanya concert na wanafunzi walishiriki ummis balaa lake lilikuwa sio dogo alivyokuja akakuta hayo walimu walijuta,na zilikuwepo motisha nyingi kwa walimu
Enzi zake bado ana nguvu mambo yalikuwa moto sana.
 
Natumaini mu-wenye afya njema. Poleni na mapambano ya kila siku. Ni mara yangu ya kwanza kuandika katika jukwaa hili hasa baada ya kuwa nasoma maandiko mengi tu ya wadau mbalimbali yanayohusu mambo mengi katika jamii zetu.

Ni jukwaa pendwa pia kuwazungumzia watanzania wenzetu ambao wanashindwa kupaza sauti pale wanapokuwa wanapitia masahibu katika maeneo yao ya kazi.

Kuna shule ipo Mkuranga, umbali tu kidogo kutoka Kongowe Mbagala, inaitwa St. Matthew's. Ni shule ya sekondari japo pia wana msingi. Shule hii ni shule dada na St. Mark's- Mbagala, Ujenzi sec.-Vikindu na Imagevosa-iringa.

Ni shule kubwa yenye wastani wa wanafunzi 680-700 kwa kidato cha kwanza hadi cha sita. Kwa muda sasa mrefu sasa, walimu wanahangaika kwa kutokulipwa mishahara. Ndugu yangu wa karibu anaefanya kazi pale ameniambia "kwa ushahidi" kwamba ni zaidi ya miezi saba na hajalipwa mahahara wake.

Kila anaesimama kuhoji mshahara wake anaondolewa kazi bila hata notice. Walimu wanaishi kwa shida sana. Wamewahi kuchukua hatua na kuripoti katika halmashauri ya mkuranga. Waliobanika kufikisha taarifa hizo walifukuzwa kazi na tena bila kulipwa stahiki zao na bado halmashauri ya mkuranga haikushughulika na suala hilo. Mwezi huu wa tisa baada ya likizo fupi kuisha, kuna walimu wengine wanne wameondoshwa.

Sababu ni kwamba watoto wapatao asilimia kumi katika masomo yao hawajafikisha wastani. Lakini hawa ni walimu wapya, wameajiliwa miezi mitatu tu iliyopita kabla ya kufanya mitihani ya midterm. Wanawazungusha kuwalipa stahiki zao.. Uongozi unawazungusha kuwalipa stahiki zao hasa baada ya kuachishwa kazi.

Naziomba mamlaka zinazohusika, kufuatilia suala hili hasa kwa kuzingatia kwamba vijana wengi wanaofanya kazi katika taasisi za binafsi wana malengo wanataka kuyafikia pia. Tukemee vitendo vya unyanyasaji katika sehemu za kazi.

Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye details za wapi pa kuanzia ili kuwasaidia kwa ngazi za kiserikali tafadhali toa maoni.

Asanteni sana.
Aisee
 
Mimi kama mzazi nina mtoto anasoma primary hapo St Matthews changamoto ni kuwa wale walimu wa zamani wazoefu kwa ngazi ya primary wameondolewa wengi na kwa sasa kuna walimu wapya ambao wana struggle ku copy na hali ya wanafunzi
 
Yaani shule yenye watoto 700,?haina mapato, na unafahamu karo ya pale, ni ndefu na huwa wana matokeo maxuri sana kwenye mitihani ya taifa.
Mambo mengine hayapaswi kuandikwa hapa. Ila elimu yetu inapaswa kuangaliwa Kwa jicho la tofauti sana. Ni muhimu serikali ifikie hatua mitihani iwe inafika wakati wa session ya mtihani tuu. Mitihani ya Mock ndio kabisa hovyo. Yanayoripotiwa kwenye hizi shule ni majanga Kwa kizazi Cha kesho.
 
Back
Top Bottom