Uongo kuhusu ATCL ni tone tu kwenye bahari, Tumedanganywa mengi tu!

Uongo kuhusu ATCL ni tone tu kwenye bahari, Tumedanganywa mengi tu!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Mambo sasa yanaanza kujianika kwenye mkeka wa uhakika. Ukweli unauzidi nguvu uongo kama mbegu inapochomoza kwenye udongo. Ukweli unaanza kutamalaki kama mashabiki kindakindaki au mwalimu na chaki. Tumedanganywa sana na kwa muda mrefu.

CAG amemwambia Mhe. Rais kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa hasara ya mabilioni ya shilingi za kitanzania kwa miaka mitano sasa. Lakini Mwendazake na wenzake wamekuwa wakituamisha kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa faida. Katika kuchagiza hilo, ATCL imekuwa ikitoa hadi gawio kwa Serikali. Tulikuwa tukidanganywa.

Serikali ya Mwendazake ilijaa propaganda na uongo mkubwa. Tumeanza kuona upande wa pili wa tulichokuwa tukiambiwa. Ukweli unaupiga kumbo uongo uliotaka kudumu kwa muongo mzima. Amini nawaambia, hilo ni tone tu kwenye bahari ya propaganda zilizokuwa zikiendelea wakati wa uongozi wa Mwendazake. Mengi yanafuata baada ya tuta.

Ndugu yangu Kichere, angekuwepo Mwendazake ungeiwasilisha Ripoti ile inayoanika ATCL na hasara zake?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
 
'… Nampongeza Mh.Rais kwa ununuzi wa Ndege ambao tumeambiwa zimeanza kuingiza Faida ndani ya muda mfupi…tehe tehe (cheko la kebehi) maana kwny hili lazima tukiri sie tulishindwa…'-Jk

Pia CAG atuambie nani anachomekea figure za deni la Taifa hadi linakuwa kwa kasi wakati Hayati alikuwa anatumia fedha za ndani kujenga miradi yote
 
Niachojua uchumi ni kama Nyuki. Hakumbatiwi wala hapigwi Busu. Dawa ni kuacha tu ajipambanue mwenyewe. Tulifikia mahali mpaka kunguru wanakata umeme Dar, tukafikia mahali mpaka vijana wa CCM wakatuambia wanataka kuwatia mimba wake zetu bila kujali wengine ni mama zao. Walifika mahali mpaka wakaanza kusema kama huoni ndege zinavyoleta hela wewe sio mzalendo.

Mungu tu anajua hawa watu na hii nchi.
 
whether it makes profit or not, ndege lazima ziwepo na wale wanaosomea urubani wapate pia ajira
Hakuna anaenzisha biashara ili ale hasara. hakuna huyo mtu.

ajira ni small part. isitoshe maruban wengi wanaajiriwa na private charters, na ndio zinalipa vizuri sana.

kama ATCL ingekuwa private company ingeshakufa kwa mentality kama yako.
 
hakuna anaenzisha biashara ili ale asara. hakuna huyo mtu.
ajira ni small part. isitoshe maruban wengi wanaajiriwa na private charters, na ndio zinalipa vizuri sana.
kama ATCL ingekuwa private company ingeshakufa kwa mentality kama yako

hakuna biashara inaanzishwa apo apo inamke profit, for an airline bussiness its even worse you have to do trial and error nyingi tafauti but you still need to pay your workers.
 
146b40726a1511e3828f1225728e27b1_8.jpg
 
hakuna biashara inaanzishwa apo apo inamke profit, for an airline bussiness its even worse you have to do trial and error nyingi tafauti but you still need to pay your workers.
proper plan ilihitajika before kuanzisha hili shirika.

kuwa na CEO ambao wana uzoefu wa kumanage mshirika mengine.
competitive individuals.

lisiwe drived kisiasa au wana siasa kuwa na access nalo
 
Back
Top Bottom