Uongo kuhusu ATCL ni tone tu kwenye bahari, Tumedanganywa mengi tu!

Uongo kuhusu ATCL ni tone tu kwenye bahari, Tumedanganywa mengi tu!

Hapo kwenye ATCL, Mama Samia kaangushiwa jumba bovu. Hana budi kuchukua hatua za haraka kutafuta mbia/wabia toka sekta binafsi nchini na hata nje kuliendesha shirika hilo. Na huo ni mtihani mkubwa sana hasa nyakati hizi za janga la covid-19. Kupata mbia makini ni kazi ngumu sana sasa hivi. Aidha, usimamizi wa hali ya juu unahitajika katika mchakato mzima hadi utendaji wake.

Akichelewa ni mwendo wa kuendelea kumimina mabilioni kuhakikisha ndege zinaendelea "kuremba" viwanja na anga la Tanzania kuwafurahisha wanaofikiri ndege ni toys za kujivunia kwa majirani! Na serikali ndio ina zigo hilo la ndege kama mmiliki. ATCL wao wanasubiri tu kukabidhiwa hela ya kula (operating funds) waendelee "kuzitembeza" popote. Sijui Watanzania wangapi wanajua kwamba ukiirusha Dreamliner toka Dar es Salaam hadi Mwanza (459 nautical miles) kwa nauli za ushindani ni hasara hata ikiwa imejaa kabisa. Hata zisiporuka, pesa ya uhakika lazima itoke.

Rwandair iliwatoa jasho hadi ikabidi wawakabidhi Qatar Airways 49% ya hisa na jukumu la uendeshaji. Hiyo ilikuwa kabla ya corona. Kabla ya hapo walijaribu kulibinafsisha shirika lakini hakuna aliyekuwa akitoa bei inayoeleweka. Hii sio biashara inayochangamkiwa duniani na sasa corona ndio imeharibu kabisa. Kuna mashirika kadhaa yaliyokuwa yakienda vizuri kama Air Mauritius, sasa hivi linaelekea kufilisika.

I wish Her all the best. She'll certainly solve the problem, I believe.

privatisation waulize rwanda nn kinaendelea, na kama hujamaliza rwwanda fuatilia kenya airways! mind you kenya ways ilikua privatised way before covid ni miaka mingi nyuma results zake umeziona lakini?
 
alafu mashirika yote binfasi yakishaingia hasara hela za kuendesha wanatoa wap? wao sio serikali kwamba wanatoa huduma hawaangalii faida serikali inaweza kubypass profit na bado shirika likaendelea, kwa saaahv ukitoa precision ambayo inapumuliwa mashine, hakuna shirika lingine, precision sidhan kama itakuepo kwa mda mrefu kwa biashara kwa sababu parent company yake kenya airways nayo ni imekufa!

- kwenye situation kma hii mkono wa serikali unahitajika sana, msile story zenu za raia maskini maana sio kla anaishi tanzania ni maskini na sio watanzania peke yao wanapanda
Muwe mnaona na aibu kidogo basi...
 
An ndege tu watu wanataka na kulia je yakija ya bwawa na reli c Atakufa mtu
 
hakuna biashara inaanzishwa apo apo inamke profit, for an airline bussiness its even worse you have to do trial and error nyingi tafauti but you still need to pay your workers.
Sasa kwanini tuambiwe imeleta faida wakati siyo kweli? Sasa kwanini ununue ndege nyingi hivyo bila business plan ikiwa trial na error ni nyingi?
 
Mwendazake 😂😂😂😂😂😂😂😂


Screenshot_20210329-180038.png
 
Sasa kwanini tuambiwe imeleta faida wakati siyo kweli? Sasa kwanini ununue ndege nyingi hivyo bila business plan ikiwa trial na error ni nyingi?


Shauri ya Mwendazake hiyo.
 
privatisation waulize rwanda nn kinaendelea, na kama hujamaliza rwwanda fuatilia kenya airways! mind you kenya ways ilikua privatised way before covid ni miaka mingi nyuma results zake umeziona lakini?
Usipoteze muda na mahangaiko ya wengine. Ukishafanya kosa la kuanzisha shirika la ndege bila mpango maalum inabidi utafute njia ya kuliendesha bila hasara. Hao wote uliowataja wanahangaika kivyao kutatua matatizo waliyojiletea. KQ na SAA wako ndani ya tabu miaka mingi tu. Wamekalia ulaji badala ya kuwa makini na kufufua mashirika yao.

Na sisi tumefanya kosa kufikiri kufufua ATC ni kutumia pesa za umma kununua ndege kwa cash bila business plan inayoeleweka. Sasa sharti tutafute solution. Vinginevyo tuendelee kumwaga mabilioni kutengeneza hasara zaidi kwa kisingizio cha kufufua shirika. Sisi katika kutafuta ubia tunatakiwa kuwa makini zaidi badala ya kushabikia mafisadi walioshindwa kwao. Kosa limeshafanyika. Kama una jawabu bora leta.
 
Mambo sasa yanaanza kujianika kwenye mkeka wa uhakika. Ukweli unauzidi nguvu uongo kama mbegu inapochomoza kwenye udongo. Ukweli unaanza kutamalaki kama mashabiki kindakindaki au mwalimu na chaki. Tumedanganywa sana na kwa muda mrefu.

CAG amemwambia Mhe. Rais kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa hasara ya mabilioni ya shilingi za kitanzania kwa miaka mitano sasa. Lakini Mwendazake na wenzake wamekuwa wakituamisha kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa faida. Katika kuchagiza hilo, ATCL imekuwa ikitoa hadi gawio kwa Serikali. Tulikuwa tukidanganywa.

Serikali ya Mwendazake ilijaa propaganda na uongo mkubwa. Tumeanza kuona upande wa pili wa tulichokuwa tukiambiwa. Ukweli unaupiga kumbo uongo uliotaka kudumu kwa muongo mzima. Amini nawaambia, hilo ni tone tu kwenye bahari ya propaganda zilizokuwa zikiendelea wakati wa uongozi wa Mwendazake. Mengi yanafuata baada ya tuta.

Ndugu yangu Kichere, angekuwepo Mwendazake ungeiwasilisha Ripoti ile inayoanika ATCL na hasara zake?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Angepigwa ganzi kama jicho lililopigwa na kibanzi.
 
Usipoteze muda na mahangaiko ya wengine. Ukishafanya kosa la kuanzisha shirika la ndege bila mpango maalum inabidi utafute njia ya kuliendesha bila hasara. Hao wote uliowataja wanahangaika kivyao kutatua matatizo waliyojiletea. KQ na SAA wako ndani ya tabu miaka mingi tu. Wamekalia ulaji badala ya kuwa makini na kufufua mashirika yao.

Na sisi tumefanya kosa kufikiri kufufua ATC ni kutumia pesa za umma kununua ndege kwa cash bila business plan inayoeleweka. Sasa sharti tutafute solution. Vinginevyo tuendelee kumwaga mabilioni kutengeneza hasara zaidi kwa kisingizio cha kufufua shirika. Sisi katika kutafuta ubia tunatakiwa kuwa makini zaidi badala ya kushabikia mafisadi walioshindwa kwao. Kosa limeshafanyika. Kama una jawabu bora leta.

ni kweli kabisa unachosema! nadhan sasa ni mda mwafaka wa kutafuta suluhisho
 
Sasa kwanini tuambiwe imeleta faida wakati siyo kweli? Sasa kwanini ununue ndege nyingi hivyo bila business plan ikiwa trial na error ni nyingi?

tayar kosa limeshafanyika na hatuwezi jua alikua na plan gan kusema uongo, yameshapita apo mm nnachopingana nacho ni hawa wadada ambao wanataka mradi mzima uuzwe, yaaani kuna watu ni ulezi tu hii nchi
 
Mambo sasa yanaanza kujianika kwenye mkeka wa uhakika. Ukweli unauzidi nguvu uongo kama mbegu inapochomoza kwenye udongo. Ukweli unaanza kutamalaki kama mashabiki kindakindaki au mwalimu na chaki. Tumedanganywa sana na kwa muda mrefu.

CAG amemwambia Mhe. Rais kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa hasara ya mabilioni ya shilingi za kitanzania kwa miaka mitano sasa. Lakini Mwendazake na wenzake wamekuwa wakituamisha kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa faida. Katika kuchagiza hilo, ATCL imekuwa ikitoa hadi gawio kwa Serikali. Tulikuwa tukidanganywa.

Serikali ya Mwendazake ilijaa propaganda na uongo mkubwa. Tumeanza kuona upande wa pili wa tulichokuwa tukiambiwa. Ukweli unaupiga kumbo uongo uliotaka kudumu kwa muongo mzima. Amini nawaambia, hilo ni tone tu kwenye bahari ya propaganda zilizokuwa zikiendelea wakati wa uongozi wa Mwendazake. Mengi yanafuata baada ya tuta.

Ndugu yangu Kichere, angekuwepo Mwendazake ungeiwasilisha Ripoti ile inayoanika ATCL na hasara zake?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Kwani nilini hiyo Atcl ilisha leta faida toka enzi za Nyerere? Magufuri amelikuta shirika limekufa mpaka limeoza, ndio kwanza ananunua ndege,nyinyi nmagagania faida,hivi nyinyi mnajua serikali ikuwa inapata asara gani kulipa mshahara wafanyakazi wasio na vitendea kazi?
 
Pamoko..
Mambo sasa yanaanza kujianika kwenye mkeka wa uhakika. Ukweli unauzidi nguvu uongo kama mbegu inapochomoza kwenye udongo. Ukweli unaanza kutamalaki kama mashabiki kindakindaki au mwalimu na chaki. Tumedanganywa sana na kwa muda mrefu.

CAG amemwambia Mhe. Rais kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa hasara ya mabilioni ya shilingi za kitanzania kwa miaka mitano sasa. Lakini Mwendazake na wenzake wamekuwa wakituamisha kuwa ATCL imekuwa ikijiendesha kwa faida. Katika kuchagiza hilo, ATCL imekuwa ikitoa hadi gawio kwa Serikali. Tulikuwa tukidanganywa.

Serikali ya Mwendazake ilijaa propaganda na uongo mkubwa. Tumeanza kuona upande wa pili wa tulichokuwa tukiambiwa. Ukweli unaupiga kumbo uongo uliotaka kudumu kwa muongo mzima. Amini nawaambia, hilo ni tone tu kwenye bahari ya propaganda zilizokuwa zikiendelea wakati wa uongozi wa Mwendazake. Mengi yanafuata baada ya tuta.

Ndugu yangu Kichere, angekuwepo Mwendazake ungeiwasilisha Ripoti ile inayoanika ATCL na hasara zake?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
 
Kuna watu wanataka kupinga ripoti ya CAG,,
Tanzania yetu
Wewe acha ujinga,umeulizwa hizi ndege zimefanya kazi miaka mingapi?wakati hizi azina miaka mitatu.hiyo miaka mitano mnaesabu hipi?wakati Magufuri hajakuta hata ndege hata moja?
 
Kwenye ukweli uwongo ujitenga.

Soon tutayajua tusiyoyajua.

Mkuu ule uongo tulikuwa tunaujua na tulikuwa tunasema kuwa ule ni uongo, kwa sasa labda tusubiri kujua kwa uhakika uongo ule ulikuwa wa kiasi gani. Na huyu mama asipoweka ule uongo wazi, ataonekana ameshindwa kazi.
 
Kwa lipoti hipi!msilisema Atcl ilikuwa aikaguliwi tangia Magufuri ameingia madarakani?

Kama ilikuwa inakaguliwa tuambie mwaka jana ripoti ilisema ni hasara au faida kiasi gani. Hapo ndio utajua kuwa hujui.
 
Gawiwo linakikokotoo chake halihusiani na faida uliza ueleweshwe. Tatizo lenu you are overdoing hoja itakapojibiwa mtaaibika maana mnakubaliana na conclusive statements badala ya kutoa room of doubt. Haya endeleeni na sherehe.
Acha uongo unatoaje gawio wakati hujatengeneza faida mbona mnaona watu wote wajinga.
Na pia alienda zaidi kwa kutwambia imetengenezwa faida ya bil 28
 
Back
Top Bottom