Uongo mkubwa zaidi kutokea dunia - The biggest scam in the world

Uongo mkubwa zaidi kutokea dunia - The biggest scam in the world

Amini kuwa Mungu yupo ili siku ukifa uingie peponi. Pia haidhuru hata ukimwamini kuwa yupo na ikatokea akawa hayupo hutokuwa na cha kupoteza so Amini kuwa Mungu yupo brother.
Hapo ni kumbetia Mungu.

Utakuwa hujapoteza muda duniani?

Na sijui unamuongelea Mungu yupi aaminiwe, miungu wako zaidi ya 3000
 
Zaidi ya mara moja, katika kila mjadala tunao jadili kuhusu uwepo wa Mola, nimethibitisha juu ya uwepo.

Nipatie huo ushahidi
Au nitajie reply no ngapi niusome
 
Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyo taka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje
Sahihi kabisa, huu ni utaratibu ambao ameuweka ili tufikie ukamilifu.

Kingine yapo mengi tu amekupa na hujamuomba, amekupa uhai, je ulimuomba akupe uhai ? Amekupa rizki je ushawahi kumuomba akupe rizki ?

Kingine Allah anafanya yote, kwanza unaweza kuombwa unachotaka ukapewa, na ukaomba unachotaka usipewe, vyote kwake anafanya. Shida yenu mnampinga Mola msie mjua.

Kujua kwake Allah hayo hayakuzuii wewe kufanya unacho taka.
 
Katika hili sisi tunajua na nyinyi hamjui, ndio maana huwa nawaona hamna akili pale mnapo kana jambo msilo lijua.

Jibu maswali ninayo kuuliza yatakusaidia kufikiria kiundani kama unataka hilo.

Tukija kujadili Mungu wa kila dini utaona msingi wa Uungu ni nini ? Ukisoma maana ya Mungu katika kamusi utakuta lazima ni mwenye kuumba, mwenye nguvu, mwenye uwezo, mkamilifu.

Hao miungu wa dini nyingine ni miungu wa uongo, ndio maana tunasema hilo, huwezi kusema Ng'ombe ni Mungu wakati Hana sifa ya Uungu.

Mjifunze maana za maneno kabla ya kuyatumia, mnapotezea watu muda wakati hamna hoja yoyote.
🤣🤣🤣🤣Hamna dini unavyosema ng'ombe ni Mungu. Second of all, asa Kama mtu yoyote anaweza akasema Mungu wake kaumba kila kitu what's the point, mi naweza spiderman ndo muumba wengine wote wa uwongo...na huwezi bisha so it's pointless argument. Kila mtu anavuta upande wake...🤣we ukiambiwa una proof Gani kama huyu muumba yupo na alikuwepo bila kuumbwa utaanza kubwabwaja
 
Bado hujajibu swali langu, umejuaje ya kuwa Mungu hayupo ? Mpaka ukaanza kumkana ?

Usikimbie swali la msingi.

Suala la nanasi kuwa tamu na Tako kuwa zuri, hiyo ni kazi ya Mola muumba aliye viumba viwili hivyo. Hili tutalijadili wakati wake ukifika.
🤣we unajuaje spiderman isn't real buh ni fiction? Same answer you'll give ndo same answer I'll give.
 
Thibitisha hilo, usilete hitimisho la kimantiki, hitimisho la kitoto na uvivu wa kufikiria.

Ulimwengu ulitanguliwa na kutokuwepo kisha ukawepo ila kwa Mola hajatanguliwa na chochote.

Sasa msiletw ulinganyo kwa visivyo fanana ukahitimisha kitoto. Mungu aliyeumba na Ulimwengu ulio umbwa ni viwili visivyo fanana.
😙Na wewe thibitisha Mungu hajaumbwa
 
Halafu unataka kujadiliana kuhusu Mungu ?

Kitabu Qur'aan,suala la kuandamana na kupiga watu mawe hili Lina maelezo yake, na najiuliza hapa limeingiaje ?

Kucheka sio hoja, hoja kimeandikwa nini ? Maana hata huyo mtoto atakuwa na shida katika akili ndio maana akaitwa mtoto.

Mkiwa mnataka kujadili hizi mada, hakikisheni mnamjua Mungu ambaye mnamkana sio mnabanwa mnaruka ruka tu. Mnapotezea watu muda.
🤣Tuanze na swala la jua linazama kwenye tope na asubuhi linaomba ruhsa kwa Allah kuchomoza
 
Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani(magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani
Nani amekwambia ya kuwa Shetani ni msaidizi wa Mungu ? Huu ujinga mnaupata wapi ?

Mnatupa kazi kubwa sana, kazi ya kukosoa maneno yenu ya uongo, kadhalika kazi ya kusoma hoja zetu. Jaribuni kuwa mnafatilia kwanza ili msikosed hata katika haya ya uongo. Eti Shetani ni msaidizi wa Mungu ?

Shetani kazi yake ni kumshawishi mja afanye uovu, na Hana uwezo wa kuleta kitu na kuondoka kitu. Kuweno na akili kwanza ya udadisi ili ukijenga hoja usikosee.

Hii nukta ya kudai Shetani ni msaidizi wa Mola, umeipata wapi ?
 
Kivipi ? Hizi falsafa tu ambazo hazina ithibati ya kiakili, uhalisia na mazingira. Nataka ulete ithibati.

Huu utoto mwingine. Huu mfano katika hii nukta hauingii, tunaongelea uumbaji unaleta mfano dhaifu wa meza na chakula. Wewe tuambie imekuwaje hii Dunia ikawepo na utuonyeshe kutokuwepo kwa Mungu.

Kutokuwepo kwa chakula kwenye meza kinahitaji maelezo. Kwamba je kilikuwepo hapo kabla kisha kikawa hakipo, na hakikuwepo kabisa utuambie umejuaje kama hakipo ?

Hujaonyesha hilo, zaidi ya kurudia hichi ulichokiandika kwa kutoa mfano wa meza na chakula.
So Mungu alikuwepo afu kaondoka...🤣okay kama hivi sawa...anyways we r free
 
Kwahiyo hili ulichokiandika unasema hoja. Sasa njoo tujadili kwa masharti haya mawili tu :

1. Hakikisha kila swali ninalo kuuliza unajibu
2. Hakikisha unamjua huyu Mungu ambaye unamkana.

Naanzia hapa, Wapi kimeandikwa kama Dunia itaangamizwa kwa ajili yetu ? Mimi ni Muislamu, nataka ujadili jambo kwa mujibu wa Uislamu, maana Kuna sehemu ulijinadi kwamba unajua Uislamu ( Ila kiukweli kwa ulicho kiandika unaonyesha wazi huujui Uislamu).

Nukta ya kuiangamiza Dunia kwanza unatakiwa ulete ukweli wake.

Nakuja kwenye kuumba Moto, Mola wetu ametuumba kwa malengo, na akaweka utaratibu ya kuwa watakao faulu watalipwa pepo na watakao feli wataingizwa motoni, hili alilijua na anajua fulani wa motoni na fulani wa peponi.

Lakini alipo tuumba akatupa akili, matashi na hali wezekano ya kufanya mema na kufanya maovu. Katika hayo akaweka mlango wa kusamehe pale mtu utakapo kosea.

Hakuna sehemu ambapo kimeandikwa kwamba Mola wetu ametuumba ili tukosee, hili halipo. Haya maneno umeyapata wapi ? Bali ametuumba katika hali zote za kupatia na kukosea, na ukikosea ukiombwa msamaha kwake unasamehewa.

Sahihi kabisa na angetaka wote tumuamini angefanya hivyo, akatuumba na kutupa uhuru wa kufanya tunayotaka, ndio maana wewe Leo hii unamkana na humjui, lakini anakupa pumzi na kukulea.

Kwa akili ya mwanadamu, ungeumbwa katika hali hiyo unayo itaka pia ungelala, na Mola wetu ni Mjuzi wa kuumba.
If anajua majibu ya test kabla ya kutupa test na kashajua watakaofaulu na kufeli why test us...? 🤣🤣🤣🤣🤣Hii analogy yenu ya life is a test ishakuwa debunked sana it's illogical
 
Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake
Unaandika haya huenda hujawahi kusoma habari za Shetani mpaka kufikia hapo alipo, halafu unajadili kuhusu Mungu ?

Allah hajamshindwa Shetani, baada ya kuasi Shetani alimuomba Allah ambakize mpaka Kiama kinapo karibia, Allah akakubali ombi lake, na Shetani kwa uwezo alio pewa na Allah akasema atawashawishi waja wake, na Allah akasema atafanikiwa kuwashawishi wale ambao hawafati maamrisho ya Mola wetu muumba. Kwa ufupi jambo liko hivyo.

Mapenzi ya Allah ni makubwa sana kwetu, ndio maana akatuambia kwazi kabisa ya kuwa Shetani ni adui yetu pasi tuepukane nae, na akatupa uwezo wa kumuepuka, ukiona wewe unaongozwa na Shetani ujue wewe ni mzembe na umetaka mwenyewe.
 
Kwahiyo hili ulichokiandika unasema hoja. Sasa njoo tujadili kwa masharti haya mawili tu :

1. Hakikisha kila swali ninalo kuuliza unajibu
2. Hakikisha unamjua huyu Mungu ambaye unamkana.

Naanzia hapa, Wapi kimeandikwa kama Dunia itaangamizwa kwa ajili yetu ? Mimi ni Muislamu, nataka ujadili jambo kwa mujibu wa Uislamu, maana Kuna sehemu ulijinadi kwamba unajua Uislamu ( Ila kiukweli kwa ulicho kiandika unaonyesha wazi huujui Uislamu).

Nukta ya kuiangamiza Dunia kwanza unatakiwa ulete ukweli wake.

Nakuja kwenye kuumba Moto, Mola wetu ametuumba kwa malengo, na akaweka utaratibu ya kuwa watakao faulu watalipwa pepo na watakao feli wataingizwa motoni, hili alilijua na anajua fulani wa motoni na fulani wa peponi.

Lakini alipo tuumba akatupa akili, matashi na hali wezekano ya kufanya mema na kufanya maovu. Katika hayo akaweka mlango wa kusamehe pale mtu utakapo kosea.

Hakuna sehemu ambapo kimeandikwa kwamba Mola wetu ametuumba ili tukosee, hili halipo. Haya maneno umeyapata wapi ? Bali ametuumba katika hali zote za kupatia na kukosea, na ukikosea ukiombwa msamaha kwake unasamehewa.

Sahihi kabisa na angetaka wote tumuamini angefanya hivyo, akatuumba na kutupa uhuru wa kufanya tunayotaka, ndio maana wewe Leo hii unamkana na humjui, lakini anakupa pumzi na kukulea.

Kwa akili ya mwanadamu, ungeumbwa katika hali hiyo unayo itaka pia ungelala, na Mola wetu ni Mjuzi wa kuumba.
Hivi mfano ufike kule umkute Zeus ndo muumbaji na ana hasira kichizi coz umeamini miungu mingine kina Allah huko ..utamlaumu nani kwa kuzaliwa muislam bila kujua kwamba Zeus ndo Mungu wa ukweli?
 
Nani amekwambia ya kuwa Shetani ni msaidizi wa Mungu ? Huu ujinga mnaupata wapi ?

Mnatupa kazi kubwa sana, kazi ya kukosoa maneno yenu ya uongo, kadhalika kazi ya kusoma hoja zetu. Jaribuni kuwa mnafatilia kwanza ili msikosed hata katika haya ya uongo. Eti Shetani ni msaidizi wa Mungu ?

Shetani kazi yake ni kumshawishi mja afanye uovu, na Hana uwezo wa kuleta kitu na kuondoka kitu. Kuweno na akili kwanza ya udadisi ili ukijenga hoja usikosee.

Hii nukta ya kudai Shetani ni msaidizi wa Mola, umeipata wapi ?
Soma historia ya shetani alivyo evolve kutoka nyoka, mpaka msaidizi wa Mungu, mpaka malaika aliyetupwa mpaka a 7 headed dragon. Ndo ujue hizi story ni tungo tu za watu tofauti katika mda tofauti...kila dini Ina shetani wake... Greeks Wana hades nyie iblis Zoroastrianism wanae nae so unaemuongelea ni shetani yupi wa dini ipi maana wote Wana story tofauti ila wa kiyahudi alikuwa msaidizi wa Mungu na ndo maana tunamwona mbinguni akibet na Mungu juu ya maisha ya ayubu
 
Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair
Shida yenu haya mambo hamyasomi. Baba yetu Adamu na mama yetu Hawa walipo kuwa kwenye Ile Bustani wakiambiwa kila kitu, kwamba hiki wafanye na hiki wasifanye. Kwahiyo kumsikiliza kwao Shetani ni kuacha kusikiliza maagizo ya Mola wao, lakini mwisho wa siku walitubu kwa Mola na Mola wetu akawasamehe.

Kingine hawajaweka kwenye Bustani ili warubuniwe bali waliwekwa mule wastarehe, na ndio maana wakapewa angalizo. Sasa mapenzi gani mnayataka kutoka kwa Mola wetu zaidi ya hayo ?

Hiyo adhabu ya shuruba nani amekwambia imetokana na Adamu na Hawa ? Hakuna wa kubeba mzigo wa mwenzie kwenye dini. Hivi huu ujinga unao uandika hapa unao toa kwenye vitabu gani ?
 
Unaandika haya huenda hujawahi kusoma habari za Shetani mpaka kufikia hapo alipo, halafu unajadili kuhusu Mungu ?

Allah hajamshindwa Shetani, baada ya kuasi Shetani alimuomba Allah ambakize mpaka Kiama kinapo karibia, Allah akakubali ombi lake, na Shetani kwa uwezo alio pewa na Allah akasema atawashawishi waja wake, na Allah akasema atafanikiwa kuwashawishi wale ambao hawafati maamrisho ya Mola wetu muumba. Kwa ufupi jambo liko hivyo.

Mapenzi ya Allah ni makubwa sana kwetu, ndio maana akatuambia kwazi kabisa ya kuwa Shetani ni adui yetu pasi tuepukane nae, na akatupa uwezo wa kumuepuka, ukiona wewe unaongozwa na Shetani ujue wewe ni mzembe na umetaka mwenyewe.
🤣🤣🤣🤣hey my son, there is a cobra in ur room I'm giving u a stick and locking u with it ..all this because I love u....take care....
 
Shida yenu haya mambo hamyasomi. Baba yetu Adamu na mama yetu Hawa walipo kuwa kwenye Ile Bustani wakiambiwa kila kitu, kwamba hiki wafanye na hiki wasifanye. Kwahiyo kumsikiliza kwao Shetani ni kuacha kusikiliza maagizo ya Mola wao, lakini mwisho wa siku walitubu kwa Mola na Mola wetu akawasamehe.

Kingine hawajaweka kwenye Bustani ili warubuniwe bali waliwekwa mule wastarehe, na ndio maana wakapewa angalizo. Sasa mapenzi gani mnayataka kutoka kwa Mola wetu zaidi ya hayo ?

Hiyo adhabu ya shuruba nani amekwambia imetokana na Adamu na Hawa ? Hakuna wa kubeba mzigo wa mwenzie kwenye dini. Hivi huu ujinga unao uandika hapa unao toa kwenye vitabu gani ?
Hivi ukiambiwa hii story sio hata original kwenye bible utajiskiaje...hii creation myth ipo Hadi kwenye epic of Gilgamesh kwenye epic nyingine huko in sumerian myths zipo kibao it's just a story made up haina historical reference yoyote Kama una any archeological evidence tuletee...
 
Mungu yupo hata usemeje ni suala la muda tu ,utaelewa..kwa hata hao wanasayansi wako hawana hoja ni kama wewe tu hawajui kesho yao.
Naona huna hoja ila umeshika imani potofu.

Hii inaonesha kuwa umeshindwa kuthibitisha kama Mungu yupo.

Ila unaforce tu awepo.

Yaani unamawazo yako umeyang'ang'ania hayohayo ambayo huwezi kuyaelezea.

Imani za dini ni shambulio la akili.
 
Hivi mfano ufike kule umkute Zeus ndo muumbaji na ana hasira kichizi coz umeamini miungu mingine kina Allah huko ..utamlaumu nani kwa kuzaliwa muislam bila kujua kwamba Zeus ndo Mungu wa ukweli?
Kijana sisi hatuishi kwa kubahatisha, mngekuwa mnasoma kiundani hivi vitu usingeandika haya mambo.

Soma Historia na habari za huyo Zeus, kisha kaa tafakari ujue unaandika nini.

Wasomi wetu wameandika vitabu na vitabu kuelezea habari za hizo dini, ukitaka ujue tu usiende mbali soma Historia ya Uhindu na Budha sababu dini hizi zinafanan pakubwa, utajua kwanini si dini sahihi.
 
Back
Top Bottom