Uongo uliowahi kutokea JF: Kila mtu kujifanya tajiri na ana maisha mazuri

Uongo uliowahi kutokea JF: Kila mtu kujifanya tajiri na ana maisha mazuri

Kwamba, kila mtu ni tajiri…

Kila mtu ana gari/ magari.

Kila mtu ana digrii. Kila mtu ana nyumba.

Kila mtu ana nguvu [nyingi] za kiume.

Kila mdada ana umri chini ya miaka 20.

Kila mtu hivi. Kila mtu vile.

Ili mradi tu ni ‘kila mtu’.

Huo ni uongo. Ni uzushi.

Hakuna sehemu yoyote ile ambayo ‘kila’ mtu anasema alivyo na/au alichonacho.

JF ina wanachama mamia ya maelfu.

Kusema kwamba kila mmoja wao hao watu huwa anasema hayo yanayosemwa, ni uzushi mkubwa.

Mliozoea kutunga uongo acheni mara moja.

Hamjawahesabu wanachama wote wa JF, wa kwanza hadi wa. mwisho, na kupata mitazamo yao juu ya mambo mbalimbali.

Kukaribisha uzushi kama huo kichwani mwako kunaonyesha jinsi mtu alivyo goigoi wa kufikiri.

And with that, I yield the balance of my time for others to chime in.

Happy hump day 😉.
Chai
 
Ki ukweli kuanzia mwaka 2015 kurudi nyuma watu ambao nilikuwa nawajua ambao walikuwa ni member wa jf walikuwa wamiliki magari, Na kati ya hao ni mmoja tu alikuwa ana diploma ya IT ila sasa hiv ana miliki jiwe.
 
Mimi sijui niko tofauti, mtu hata awe na nini aseme nini huwa hainisumbui kabisa. Ila nimeona kuna baadhi ya watu humu, inawasumbua na mbaya zaidi ni Fake ID.

Mtu akianza kusema gari, nyumba, biashara, kusafiri nje si ni vitu vya kawaida? Ila mtu akigusia kati ya hivyo na vingine, ataandamwa, tumeshajua una gari, una nyumba!!!

Tutafute pesa, tuache makasiriko, mtu hata kama anadanganya, ni anajidanganya mwenyewe, mwisho wa siku anabaki kwenye ulimwengu wa kuishi maisha mazuri kimtandaoni, kiuhalisia yuko vilevile.

Tuache watu wajifariji na kufurahia anachofanya, ili mradi hakugusi wewe moja kwa moja. Wivu ni ugonjwa tafuta dawa kama ukiona unaumia mafanikio ya mwingine.
Hujawahi kukosea luv, [emoji122][emoji122][emoji122]
 
Back
Top Bottom