Uongo wa vifurushi vya Intaneti vya Airtel Tanzania

Uongo wa vifurushi vya Intaneti vya Airtel Tanzania

Naweza kuwa nje ya mada, wasomaji mtaangalia wenyewe namna ya kuihusisha.

Moja wapo, niliingiza vocha ya Tzs 1,000/=, ila ikaingia Tzs 600/=. Bado pia wanatabia ya kupunguza vi shilingi hamsini hamsini na mia. Nilipopiga simu eti na wao hawaoni matumizi niliyoyafanya ila wanakiri ni kweli salio limepungua ghafla.

Nikamuuliza mhudumu kwa hiyo tunafanyaje, akajibu hata yeye hajui cha kufanya labda nifike kwenye Ofisi zao kudai Tzs 400/= yangu.
 
Voda wako vibaya kwenye Songesha. Wameanzisha wizi wa mchana kweupe. Unaambiwa una kiasi fulani umepata Toka Songesha kitumie kununulia bando au kamilishia muhamala. Ukisha Fanya hivyo,unaletewa madai yenye ribs juu.Wateja wenu wanadhani Songesha labda ni mapato yanayotolewa kama gawio la mapato yanayotokana jinsi mteja alivyotumia mtandao wenu.Ni Bora mhelimishe wateja wenu manufaa ya packages mbali mbali mnazotoa Kwa ku_ promote biashara ili waelewe kinacholengwa.Vinginevyo ujanjaujanja utawakimbizia wateja.
 
Kutokana na matumizi makubwa ya fedha kwenye manunuzi ya vifurushi vya Internet. Tarehe 01/08/2022, nilijiunga na kifurushi cha Tsh.1500 (Mb850) na niliamua kuanza kufuatilia na kujipimia matumizi ya vifushi vya Internet kwenye simu yangu kupitia Mobile data usage ambapo nilipata fursa ya kuweka ukomo wa matumizi ya kifushi nilichojiunga kwa siku nisizidishe Mb100.

Lakini cha ajabu niliweza kutumia Jumla ya Mb490 pekee na kuletewa ujumbe kuwa nimetumia kifurushi cha Internet kwa 100%.

Nilishangaa sana na kugundua kuwa kumbe hivi viwango wanavyotuandikia ni Uongo mtupu. Huu mtandao wanafanya utapeli mkubwa sana.

Pamoja na maelezo haya nimeambatanisha screenshot za manunuzi ya kifurushi na matumizi.

Kama kuna mtu anaweza fuatilia pia ajaribu atajionea mwenyewe.

View attachment 2316699View attachment 2316700View attachment 2316701
Hivi issues nafikiri ni Mimi tu kumbe ni majanga. Ninaomba kama Kuna mwanasheria humu tufungue kesi ya huu wizi ili kukomesha huu unyang'anyi na ujambazi... kwa sababu huu ni wizi kama wizi mwingne..

Sent from my TECNO KG6 using JamiiForums mobile app
 
Ndani ya dk kumi kifurushi kimetoka 75% hadi kuisha kabisa. Nimeamini airtel ni wezi. Ngoja tuendelee na zantel, naona ina unafuu 200%
Screenshot_20220812-101711_Messages.jpg
 
Hata mimi nimegundua natumia pesa nyingi sana katika wiki 2 hizi, aisee..., , ngoja na mimi niamze kupima aiseee!!!
 
Nawalia timing . Watakuja na matangazo tunawaangakia tu.
Wamuukize Dstv sasa anauza hadi 59k Azam anapeta, 210k. Kumtunza mteja iko shughuli.
Anayetaka Dstv maana nataka nikaangie samaki dish lao
 
Airtel wezi tu. Hawana jipya
Wewe umewahi kuona GB 1.3 inaisha kwa masaa mawili kwa kutuma text 9 za WhatsApp
Achana nao hao

Unanunua bando lenye text message 300 unatuma text 4 unaambiwa kifurushi chako kimeisha
 
Nisha achana na line yao kitambo wanaongoza kwa wizi wa mabando
 
Nimejiunga hiki kifurushi saa 7:20 asubuhi, mpaka saa 8:33 asubuhi hiyohiyo natumiwa ujumbe wa kumaliza kifurushi changu. Nimeingia whatsapp, JF na nimecheza game kidogo tu kama dk 10. Nahisi airtel leo wamenipiga mchana kweupee. Na sina mpango wa kujiunga tena, mpaka kesho hiyo ndio watapata buku yangu tena!
 
[emoji845]OFA OFA OFA [emoji3533]ZA LEO BEI CHEE SAWA NA BURE KWA HALOTEL Malipo baada ya kazi, Karibuni no kufungiwa laini.

GB ZA HALOTEL WIKI 2
GB5=5,000
GB6=6,000
GB7=7,000
GB8=8,000
Gb10=10000.

GB ZA HALOTEL MWEZI
Gb10= 10000
GB15=15000
GB20=20,000
GB25=24,000
Gb30=27,000
GB40=35,000
Gb45=38,000
Gb60=49,000
Gb90=70,000
Gb120=95,000
Ni chapu.. Uaminifu ndo siraha yetu, mambo iko huku we una subiri nini usajili sasa laini ya halotel leo usipitwe na uhondo, kabla bei hazijabadika
[emoji338] 0618279799
0712776823
 
Back
Top Bottom