Uongo Wa Vipimo Vya Corona Tanzania: Kwanini Waziri Mkuu Na Waziri Wa Afya wasijiuzulu?

Uongo Wa Vipimo Vya Corona Tanzania: Kwanini Waziri Mkuu Na Waziri Wa Afya wasijiuzulu?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Leo Rais wa Tanzania amehutubia taifa na kusema, utaratibu mzima wa upimaji na utoaji majibu ya vipimo kwa wahisiwa wa ugonjwa wa COVID-19 hapa Tanzania yamezungukwa na uongo, ujanja ujanja na ulaghai mkubwa. Hivyo takwimu zote za COVID-19 hapa Tanzania zilizotolewa na Waziri Mkuu au Waziri wa Afya zinapaswa kutiliwa mashaka na kutokuchukuliwa maanani tena. Ni upuuzi mtupu!

Sasa katika vita hii ya kupambana na Corona, jukumu la moja kwa moja lilikuwa chini ya Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa) na waziri wa Afya (Ummy Mwalimu) huku pesa nyingi zikielekezwa huko. Wao ndio waliwahakikishia watanzania toka mwezi January, 2020 kabla ya Corona kuingia nchini Tanzania kuwa, Serikali ilikuwa imejipanga vyema katika mapambano hayo kuanzia kupima, kuzuia na kujaribu kutibu maambukizi ya Corona. Na mpaka kufikia leo wao ndio waliokuwa wamesimama mstari wa mbele kutetea na kusimamia juhudi za upimaji na utoaji majibu ya Corona kwa Tanzania.

Pasipo kuegemea upande wowote (iwe shutuma hizi za Rais ni kweli au ni uongo uliozushwa), nadhani huu ni wakati muafaka kwa Mheshimiwa Kassim Majaliwa na Mama Ummy Mwalimu kutafakari namna ya kuachia ngazi.

Sababu za kufanya hivyo ni hizi hapa.
1. Kukubali kwao kuwajibika moja kwa moja kwa hizo shutuma dhidi yao (ikiwa ni kweli) na kulinda hadhi ya serikali na hadhi ya Rais aliyewateua.

2. Kukaa pembeni ili kulinda heshima zao au kuonyesha kutokukubaliana na hiyo kauli ya mheshimiwa Rais (ikiwa shutuma hizo ni uongo).

3. Kupisha uchunguzi kamili na wahusika wengine wachukue nafasi zao ili nao wawajibike kwa namna tofauti (maana juhudi zao za mwanzo zimeonekana ni uchafu na upuuzi mtupu mbele ya yule aliyewateua)
 
Umetumwa au ni ndoto mkuu.
Haitatokea kaa nyumbani nawa maji na sabuni.
Hayo wachie wanao husika utakufa na kihoro bule😂😂
 
Leo Rais wa Tanzania amehutubia taifa na kusema, utaratibu mzima wa upimaji na utoaji majibu ya vipimo kwa wahisiwa wa ugonjwa wa COVID-19 hapa Tanzania yamezungukwa na uongo, ujanja ujanja na ulaghai mkubwa. Hivyo takwimu zote za COVID-19 hapa Tanzania zilizotolewa na waziri mkuu au waziri wa Afya zinapaswa kutiliwa mashaka na kutokuchukuliwa maanani tena. Ni upuuzi mtupu!

Sasa katika vita hii ya kupambana na Corona, jukumu la moja kwa moja lilikuwa chini ya waziri mkuu (Kassim Majaliwa) na waziri wa Afya (Ummy Mwalimu) huku pesa nyingi zikielekezwa huko. Wao ndio waliwahakikishia watanzania toka mwezi January, 2020 kabla ya Corona kuingia nchini Tanzania kuwa, serikali ilikuwa imejipanga vyema katika mapambano hayo kuanzia kupima, kuzuia na kujaribu kutibu maambukizi ya Corona. Na mpaka kufikia leo wao ndio waliokuwa wamesimama mstari wa mbele kutetea na kusimamia juhudi za upimaji na utoaji majibu ya Corona kwa Tanzania.

Pasipo kuegemea upande wowote (iwe shutuma hizi za Rais ni kweli au ni uongo uliozushwa), nadhani huu ni wakati muafaka kwa Mheshimiwa Kassimu Majaliwa na Mama Ummy Mwalimu kutafakari namna ya kuachia ngazi.

Sababu za kufanya hivyo ni hizi hapa.
1. Kukubali kwao kuwajibika moja kwa moja kwa hizo shutuma dhidi yao (ikiwa ni kweli) na kulinda hadhi ya serikali na hadhi ya Rais aliyewateua.

2. Kukaa pembeni ili kulinda heshima zao au kuonyesha kutokukubaliana na hiyo kauli ya mheshimiwa Rais (ikiwa shutuma hizo ni uongo).

3. Kupisha uchunguzi kamili na wahusika wengine wachukue nafasi zao ili nao wawajibike kwa namna tofauti (maana juhudi zao za mwanzo zimeonekana ni uchafu na upuuzi mtupu mbele ya yule aliyewateua).
Shangaa kwanza wigulu chemba amerudi halafu jiandae kumwoma bangi logoro pia akirudi kwani watakufa wengi kwa yale matatizo ya pumzi.
 
Leo Rais wa Tanzania amehutubia taifa na kusema, utaratibu mzima wa upimaji na utoaji majibu ya vipimo kwa wahisiwa wa ugonjwa wa COVID-19 hapa Tanzania yamezungukwa na uongo, ujanja ujanja na ulaghai mkubwa. Hivyo takwimu zote za COVID-19 hapa Tanzania zilizotolewa na waziri mkuu au waziri wa Afya zinapaswa kutiliwa mashaka na kutokuchukuliwa maanani tena. Ni upuuzi mtupu!

Sasa katika vita hii ya kupambana na Corona, jukumu la moja kwa moja lilikuwa chini ya waziri mkuu (Kassim Majaliwa) na waziri wa Afya (Ummy Mwalimu) huku pesa nyingi zikielekezwa huko. Wao ndio waliwahakikishia watanzania toka mwezi January, 2020 kabla ya Corona kuingia nchini Tanzania kuwa, serikali ilikuwa imejipanga vyema katika mapambano hayo kuanzia kupima, kuzuia na kujaribu kutibu maambukizi ya Corona. Na mpaka kufikia leo wao ndio waliokuwa wamesimama mstari wa mbele kutetea na kusimamia juhudi za upimaji na utoaji majibu ya Corona kwa Tanzania.

Pasipo kuegemea upande wowote (iwe shutuma hizi za Rais ni kweli au ni uongo uliozushwa), nadhani huu ni wakati muafaka kwa Mheshimiwa Kassimu Majaliwa na Mama Ummy Mwalimu kutafakari namna ya kuachia ngazi.

Sababu za kufanya hivyo ni hizi hapa.
1. Kukubali kwao kuwajibika moja kwa moja kwa hizo shutuma dhidi yao (ikiwa ni kweli) na kulinda hadhi ya serikali na hadhi ya Rais aliyewateua.

2. Kukaa pembeni ili kulinda heshima zao au kuonyesha kutokukubaliana na hiyo kauli ya mheshimiwa Rais (ikiwa shutuma hizo ni uongo).

3. Kupisha uchunguzi kamili na wahusika wengine wachukue nafasi zao ili nao wawajibike kwa namna tofauti (maana juhudi zao za mwanzo zimeonekana ni uchafu na upuuzi mtupu mbele ya yule aliyewateua).
mkuu, mbona kama unataka kujisahaulisha spinning za CCM?
subiri jibu atakalokuja nalo PM.... draft yake inatengenezwa Chato!
 
Intelijensia ya kugundua yanayoitwa madudu maabara ya kuchakata vipimo kwanini isitumike kuchunguza hizi tuhuma tunazoambiwa kuna watu wanazikwa usiku?
Hizi sio tuhuma tena ni kweli na wizara imekemea jambo hilo! Wale waliokuwa wanabisha sijui watasema nini tena
Screenshot_20200503-120729.jpeg
Screenshot_20200503-120749.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Intelijensia ya kugundua yanayoitwa madudu maabara ya kuchakata vipimo kwanini isitumike kuchunguza hizi tuhuma tunazoambiwa kuna watu wanazikwa usiku?
Kwani ulitaka kwenda kuzika na wewe? Mbona ndugu za hao wanaozikwa usiku hawajitokezi kusema mpaka useme wewe nyuma ya keyboard?

You live on rumours, always a pessimist!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kupisha uchunguzi kamili na wahusika wengine wachukue nafasi zao ili nao wawajibike kwa namna tofauti (maana juhudi zao za mwanzo zimeonekana ni uchafu na upuuzi mtupu mbele ya yule aliyewateua).
Kwani wao ndio waliopima?
Hajiuzulu mtu hapa,kafanyeni kazi
 
Kwani ulitaka kwenda kuzika na wewe? Mbona ndugu za hao wanaozikwa usiku hawajitokezi kusema mpaka useme wewe nyuma ya keyboard?

You live on rumours, always a pessimist!

Sent using Jamii Forums mobile app

Umeona kuna mahali nimesema nataka nikazike? Acha kunichuria, lengo la kuandika hivyo ni watu wajue kwamba hizo nazo ni porojo au kuna ukweli kisha hatua stahiki zichukuliwe.
 
Back
Top Bottom