Uongozi wa Hospitali ya Muhimbili wapewa miezi miwili kujitafakari kuhusu huduma zao

Uongozi wa Hospitali ya Muhimbili wapewa miezi miwili kujitafakari kuhusu huduma zao

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
6df65cc6-500e-46d2-b58a-d7d22bfc399c.jpg

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Godwin Mollel ametoa muda wa miezi miwili kwa uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kujitafakari kuhusu uwezo wao wa kusimamia ubora wa huduma za afya.

Amesema hayo kufuatia malalamiko ya mara kwa mara yanayotolewa na wananchi wanaopewa huduma katika hospitali hiyo.

Dk. Mollel ametoa maagizo hayo leo Aprili 4, 2022 katika kikao cha ndani kilichomshirikisha Mganga Mkuu wa Serikali na viongozi wote wa Hospitali za Taifa za Kanda, Mikoa na waganga wakuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Pia, Waziri Mollel ameutaka uongozi wa hospitali hiyo kuhakikisha unakuja na suluhu za kudumu za upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi.

5f9d7e8b-8351-4c98-8dba-82e80409379f.jpg


Chanzo: Global Publishers
 
Ni matumaini yetu kuwa ujumbe wameusikia
Nalog off Z
 
Wanatakiwa waache nidhamu ya uoga
 
Aendelee kuwachekea simba wa yuda ameshaenda hakuna wakuwafanya kitu.
 
Kazi ndogo sana hiyo....
Ondoa Madaktari wote ngazi ya kati, Manesi, Wahudumu wa Afya na Vikaragosi wote pale Muhimbili tupilia mbali huko kwenye Vituo vya Afya vya Vijijini Rukwa, Kigoma, Mtwara, nk halafu wale walioko huko kwenye mazingira magumu waletwe Jijini, hii pekee itawapa motisha ya kupiga kazi na hawa waliotupwa huko akili itawakaa sawa tuu na wakiweza waache kazi kabisaaaaa waajiriwe wengine.
Kuna Mtumishi wa Afya unamkuta Kituo cha Afya Kazulamimba yuko Humbleee na anapiga kazi kwa tabasaaaam pamoja na mazingira magumu, halafu unakuja hapo Muhimbili unakutana na Danga fulani yuko hapa Jijini kazi kushinda Insta na Umbea wa Mange anafanyakazi kwa kunaaaaaaata na madongo, Rushwa na Majivuno kibao unabaki kusema hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii hiii Nchi imekosa watu wenye Ukichaa wa maamuzi magumu yenye tija kwa Jamiii bali wapo wadekezaji tuuuuuu.
 
View attachment 2175449
Naibu Waziri wa Afya, Dk. Godwin Mollel ametoa muda wa miezi miwili kwa uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kujitafakari kuhusu uwezo wao wa kusimamia ubora wa huduma za afya.

Amesema hayo kufuatia malalamiko ya mara kwa mara yanayotolewa na wananchi wanaopewa huduma katika hospitali hiyo.

Dk. Mollel ametoa maagizo hayo leo Aprili 4, 2022 katika kikao cha ndani kilichomshirikisha Mganga Mkuu wa Serikali na viongozi wote wa Hospitali za Taifa za Kanda, Mikoa na waganga wakuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Pia, Waziri Mollel ameutaka uongozi wa hospitali hiyo kuhakikisha unakuja na suluhu za kudumu za upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi.

View attachment 2175447

Chanzo: Global Publishers
Mama kasema yy uongozi wake sio wa kufokea kama Simba wa Yuda.

Ngoja tuone style yake ila akae akijua anadeal na mbongo.
 
Wakurugenzi na wakuu wa idara ndiyo changing cha kudorora huduma.Kuna viongozi muhimbili wameziongoza idara zaidi ya miaka 20. Wapo lazi hata kukutoa na utalaamu wako usikae kwenye idara yake. Ataleta wafanyakazi wasio na ujuzi huo matokeo yake huduma kudorora na hata na hospital kukosa viwango vya huduma.
 
Back
Top Bottom