Nilisema hapa ili Simba ijengwe upya na kupata mafanikio msimu ujao ianze usajili kwa kuwafukuza viongozi waliopo na chawa wao wote au wajiondoe wenyewe kabla ya kuanza usajili wa wachezaji wapya. Na hili la kuwafukuza ni rahisi tu Mo amufukuze kiongozi wake aliyemweka na wanachama waitishe mkutano wa dharura wamtimue kiongozi wao waliyemuweka "fullstop".Vinginevyo wapenzi, wanachama na mashabiki wa Simba wajiandae kisaikolojia kwa mwaka mwingine wa maumivu tena yatakuwa makali sana kuliko ya mwaka huu.
Bila Simba kupata viongozi wapya tena vijana wenye maono mapya na wanaoweza kukimbia huku na kule kama Hersi mafanikio yatakuwa historia. Najiuliza hivi mpaka sasa ni kwanini viongozi waliopo hawajiuzulu wakajiondokea walau na heshima kidogo au kuna madudu gani wamefanya nyuma ya pazia wanaogopa yatabubumburuka wakiondoka?
Makombe yote yameondoka mikononi mwao, wachexaji wazuri wameondoka na wanaendelea kuondoka chini yao na mbaya zaidi Simba imepigwa kipigo cha kihistoria cha goli 5 na mtani timu ikiwa mikononi mwao lakini hawaoni aibu bado wapo tu wanasubiri nini? Hivi hawana ndugu au marafiki wa kuwashauri waachie hizo nafasi?