Elections 2015 Updates Kutoka Arusha: Mkutano wa kumtambulisha mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA

Elections 2015 Updates Kutoka Arusha: Mkutano wa kumtambulisha mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA

M/kiti wa ccm mkoa wa shinyanga Mgeja:
Nataka niseme maneno machache,
Kwanza juzi mpaka saa nne na dk 59 nilikuwa mwenyekiti wa ccm, saa tano na dk nikajitoa ccm, baada ya kugundua ndani ya ccm hakuna hakuna haki, nami nikaona nijiunge na chadema chama chenye haki.
Jana mmemsikia vuvuzela ikipiga kelele kuwa tunamfuata Lowassa, ningekuwa namfuata Lowassa ningeenda Monduli nyumbani kwake.
Nashangaa vuvuzela Nape eti nimehama chama kisa mtoto wangu ameangushwa ubunge, nataka nimwambie Nape kuwa nina uzefu wa kushindwa, nampa Salamu kuwa tutakutana Mtama.
Nimepigiwa simu zaidi ya 800 zote zinanipongeza, simu sita tu zilikuwa zinanisikitia.
Niseme tu nyumba ya ccm inaungua unasubiri nini kuaga?
Nataka niwaambie Nape na wenye akili kama ya Nape kuwa waeleze wale vigogo wanaojihusisha na ujangili(Kinana) Waeleze fedha za escrow ziko wapi, ccm ni kichaka cha waizi, ccm waeleze kwanini shilingi inashuka, ccm mwulizeni Kikwete unatuachaje? Ataacha umaskini, chuki, husda na rushwa.
Pombe mwisho kaunta, mtaani ni Lowassa

Hahahahaha...

Mgeja bana...
 
CCM ndani ya ukawa,,, mapinduzi na ukombozi vimeporwa na mijoka iliyokuwa inaitafuna Ccm,, na bado mtapokea wengi maana tunawajua waliobaki bado hawauelewi upepo bado,, CCM sasa inaenda kuwa safi na kurudi kwa wenyewe wananchi,, asante Jk kwa kuwasha moto kichaka na kukimbiza mijoka tafuna, kifuatacho ni kazi na mchamchaka...
 
Hivi Sioi bado alikuwa CCM? Masha alishinda kura za maoni kule Sengerema kweli?

Hayo hayatusaidii sana kwa sasa,tunaangalia kuanzia tulipo na hatma yetu dhidi ya CCM .Unaweza kuwauliza wahusika utapata jibu la uhakika
 
Baiskeli yenye magurudumu ya barafu, jua likiwaka magurudumu yanayeyuka na safari inakuwa na mwisho.

Mzee wa utabiri...

Vipi roho inakuuma sana...

Magufuli naye si alipita kila mahali "Kujitambulisha"

Au na wewe umehemewa...
 
Ilani ya chadema(ukawa)inasimamia nini hao wote watabadilika sawa anaeingizwa kwenye pipa la lami ukimtumbukiza humo na kumtoa atafanana vip nao pia watafanana malengo ya ukawa(ilani)wacha waende.
 
Yona Nnko:
Nimetoka ccm, ninafuraha kuwa mwanachama wa ccm, nimekuwa mwanachama wa ccm kuanzia TANU mwaka 1964.
Lowassa anajua siasa, ni mwalimu wangu wa siasa, ni mtulivu hana papara, ni fundi wa maendeleo.
 
Kumuona na kumpigia kura lowassa ni vitendo viwili tofauti""" umati wa watu sio tiketi ya lowassa kuwa rais,,, kaa ukijua tanzania ni kubwa sana na tuko zaidi ya 15 mil tuliojiandikisha,, je huo umati ni asilimia ngapi ya waarusha waliojiandikisha?? Vipi huo umati ni wangapi wana sifa za kupiga kura,, je huo umati unawageni wangapi ambao waliokuwa dar mbeya na leo ARusha?? Mabadiliko yanahitaji watu wenye dhamira ya dhati,,

Lowasa atachaguliwa na watu 20m ni kura za ndio kwa lowasa
 
Ila tu waendelee kuwa waanchama wa CHADEMA hata baada ya Tarehe 25-Octoba. Wasije wakaanza kuhama tena wakishindwa na huko.
 
Mzee Mtei:
Ninaambiwa kuwa muasisi wa hiki chama, roho yangu inadunda, nikiona umati huu na jinsi vyama hivi vimeungana nasikia furaha sana. Nashukuru kutuunga mkono, nawatakia kila la kheri katika safari hii ya ukombozi.
Ninashukuru sasa kwakuwa chama nilichokiasisi kimempata mtu wa kutupeleka ikulu
 
Ilani ya chadema(ukawa)inasimamia nini hao wote watabadilika sawa anaeingizwa kwenye pipa la lami ukimtumbukiza humo na kumtoa atafanana vip nao pia watafanana malengo ya ukawa(ilani)wacha waende.
Acha lugha nyepesi wewe kwani CCM hakukuwa na ilani??!! Watoto hawakai chini, dawa zipo??!!

Hawa wamechezea side A leo wanaenda side B na bado wanachekewa tu??!!!
 
Back
Top Bottom