UPDATES: Madhara ya mvua iliyonyesha jijini Dar - Desemba 17, 2019

UPDATES: Madhara ya mvua iliyonyesha jijini Dar - Desemba 17, 2019

Tokyo massive flood protection facility
IMG_0004.JPG
IMG_0005.JPG
IMG_0008.JPG
Mnaweza kwenda YouTube weyewe mjionee sina cha kuongeza mtoa mada
 
Saint Ivuga, [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] Unajitambua wewe kwa haya uliyo yandika?

Naomba nikuulize swali; Civil Engineering iko mda gani nchini? Ma kuna Maengineer, Ma PHD na Ma-Professor wangapi wamehitimu shahada zao na kuingia katika System kwa malengo ya kuboresha maisha ya wananchi na kuleta maendeleo ya nchi?

Huyo Mheshimiwa unaye mpa lawama siku za nyuma alikuwa kama nani? Mbona hushangai kuwa vitendo hivi vya Maengineer kuhujumu uchumi si vilikuwepo pia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
areafiftyone, Nakushukuru mkuu kwa kunijuza.

Ni kweli nimetoa povu kweli kweli, hii imesababishwa na kukereka kwa kiasi kikubwa kuona kwamba wananchi masikini wanajitahidi kwa kidogo walicho nacho kuwa saidia nyie wakufunzi wa elimu ya civil Engineering mhitimu shahada zenu ili hatimaye mje kusaidia kujenga Taifa letu kwa kuwarahisishia wananchi masikini maisha yao kwa kuweka miundo mbinu iwe mahiri.

Lakini matokeo wanayo yapata watu hao masikini kwa jitihada zao zote hizo, is a kick on a buttock. Wahenga walisema; "Fadhila za punda ni mateke". Badala ya kujenga mna bomoa. Sasa hii maana yake ni nini?

Kama kweli ni awamu hii tu kumekuwa na nia ya kweli ya kuwasaidia Watanzania katika matatizo yao, ikiwa ni pamoja na eneo la miundo mbinu ya maji safi na taka, sasa haya matatizo ya mafuriko tunayo yaona mnashindwa nini kukabilina nayo?

Na kama tenda za miradi katika awamu zilizopita zilikuwa zinatolewa kwa upendeleo na hata kampuni isiyokuwa na weledi ilikuwa inapata tenda, na kulingana na kauli yako, kuathiri sana ubora wa miradi, sasa mbona nyie hamkuweza ku take appropriate measures in oder to make people aware of this kind of feudalism, kiasi kwamba wananchi wakaungana mkono na nyie katika kumshauri Rais wa wakati huo kuchukua hatua stahiki kukomesha ulaini huo?

A can only hope that siku za mbele mtakuwa mmejifunza kuchukua hatua zinastahili ili kurahisisha ufanis wa kazi zenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tokyo massive flood protection facility
View attachment 1295951View attachment 1295952View attachment 1295953Mnaweza kwenda YouTube weyewe mjionee sina cha kuongeza mtoa mada
Hii System haipo Japan tu bali nchi nyingi za Europe wana System hii. Ni Afrika zu na hasa Tanzania bado tuna solve Problems zetu kwa dhana za kikoloni ambazo zimepitwa na wakati. Na ndiyo maana ni kitu cha kushangaza kwanini Ma- Civil Engineer wetu wanashindwa kuiga solution za nchi zilizoendelea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilatha,
Watu wa mipango miji hawawezi kupita kila mahali na kila sehemu kukataza matumizi yasiyo sahihi ya ardhi maana wao ni watekelezaji ila sio wmiliki

Sheria za kuzuia ujenzi holela zipo ila wenye mamlaka ya kusimamia sheria ni watu wa utawala na polisi sasa kama wanasiasa wako kimya hao wengine huwa hawana nguvu maana hawana maamuzi ya moja kwa moja.Tuanze na wewe umejenga kwenye plot au squatter? kama ni squatter kwa nini hukufuata sheria? Ni lazima jambo hili litiliwe mkazo na uongozi wa nchi kwanza ndio law enforcers watawajibika bila bughudha
 
Sababu ndo hiyo,Aliyekubali kupitisha ramani ya kujenga barabara pale Jangwani alitakiwa anyongwe tu!!! Narudia kwa sauti ANYONGWE!!! hivi wakati jeshi wanakuja kuwaokoa raia mwaka 2014 kama sikosei hakuona madhara ya kuipitisha chinichini vile.China imeendelea kwa sababu haikopeshi wapuuzi wa dizaini hizo
Duuh! Hiyo kali! Haya tutajitahidi tufike huko!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ni mipango miji na watu kujenga bila ya ushauri wa kitaalamu.
Kwa mfano wewe uliyeleta Uzi huu nyumba yako umeijenga kwa kufuata utaratibu/kibali?
 
Watu wa mipango miji hawawezi kupita kila mahali na kila sehemu kukataza matumizi yasiyo sahihi ya ardhi maana wao ni watekelezaji ila sio wmiliki
Sheria za kuzuia ujenzi holela zipo ila wenye mamlaka ya kusimamia sheria ni watu wa utawala na polisi sasa kama wanasiasa wako kimya hao wengine huwa hawana nguvu maana hawana maamuzi ya moja kwa moja.Tuanze na wewe umejenga kwenye plot au squatter? kama ni squatter kwa nini hukufuata sheria? Ni lazima jambo hili litiliwe mkazo na uongozi wa nchi kwanza ndio law enforcers watawajibika bila bughudha
Mkuu huoni kama umetoka nje ya mstari? Hakuna mtu katika mada hii amezungumzia kuhusu watu wa mipango miji na matumizi holela ya ardhi.

Kwa upande mwingine naona kama unaji-contradict mwenyewe vile? Kama wewe mwenyewe unasema kuwa sheria za kuzuia ujenzi holela zipo, sasa itakuwaje watu wa utawala na wana siasa wanahusika katika mamlaka ya kusimamia na vizui sheria hizo?
Mimi nilifikiri Judiciary, polisi na magereza ndiyo wahusika wakuu?

Nafikiri sina ulazima wa kujibu personal question, hasa tukizingatia kuwa maswala yaliyongelea kwenye hii mada ni kuhusu legitimacy ya wananchi kuendelea kugharimia kitivo cha Civil Engineering kwenye vyuo vyetu kikuu, wakati out come yake ni very small.

Hakuna faida yeyote ile tunayo pata kutokana na hiki kitivo. Kwa kukosa umakini wao wa kufanya kazi kwa kujiamini hiki kitivo kina isababishia serikali hivyo umma kugharamia ujenzi wa miradi ya mabarabara, maculvert na madaraja mara dugu zaidi kuliko ilivyo tegenewa kwa kuroa tenda kwa makampuni ya nje ana kuwasomesha wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 


Awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Rais wetu Dr. John Joseph Magufuli kwa jitihada nyingi anazo zifanya katika kuipeleka nchi yetu kwenye nchi ya uchumi wa kati. Hata hivyo sina budi kutoa masikitika yangu kwa watendaji wake anao waamini kuto kuwa na uwezo wa kukabilina na janga la mafuriko ya kila mwaka.

By the way by definition:
Civil engineering is an engineering science that deals with the conception, planning, design, construction, calculation, manufacture and operation of buildings in civil engineering, transport and hydraulic engineering.

Sasa mbona inakuwa ni aibu kubwa sana kwa wasomi wetu wa hicho kitivo cha Civil Engineering kuendelea kujiona kama ni Ma-Professor na Ma-Engineer wakati ambapo hamna uwezo wa kulisaidia Taifa letu kutatua matatizo kama haya ya mafuriko yanayo tokea kila mwaka. Ni maengineer gani nyie ambao hmtambui wajibu kama wabobeaji wa maswala haya? Mnatia aibu kiasi kwamba hata sisi maengineer wa Faculties nyingine kama Mechanical, Elictrical na wengineo tunaoneka vilaza kama nyie.

Masikitiko yangu makubwa yawaende watu wanao jiita Ma Professor, wahandisi na wasomi wa vyuo vikuu vyetu vya Faculty ya Civil Engineering nchini kwa kushindwa kukabilina na changamoto kama hii ambayo kila mwaka ina wahathiri wakazi wa jiji letu la Dar es salaam na hivyo kuifanya nchi nzima iwe paralyzed.

Professor Mbalawa, Engineer Kamwelwe, Maprofessor na wahandisi wote mlio maliza na ambao bado mko masomoni kwenye Kitivo cha Civil Engineering wa vyuo vikuu nchini, mnadhani kuna umuhimu wa watanzania kuendelea kugharamia Faculty hii ya Civil Engineering kwenye vyuo vyetu?

Mimi inaniwia vigimu sana kuelewa kwa nini wasomi na wataalam walio bobea wa kitengo hiki cha ujenzi kushindwa kuthibiti hali hii ambayo kila mwaka hutokea na kuathiri maisha, mali na shughuli zetu wenyewe. Kama wasomi na wataalam mnaweza kulala vizuri na kwa amani kweli?

Professor Mbalawa na Engineer kamwelwe, Maprofessor na Ma-Engineer wengine wa hii Fuculty ya Civil Engineering na watu wa mipango miji wa mkoa au Taifa mnashindwa kweli kushauriana na Rais Magufuli na mawaziri wengine wanao husika kuacha mara moja miradi yote mingine ambayo iko katika pipe line ya mpango wa kutekelezwa, ili kuanza mara moja uwezekano wa kutafuta jawabu la hii changamoto ambayo ina wafanya wananchi wote kuwa paralyzed na maafa haya ya mafuriko kila mwaka? Kama mvua ya masaa machache inasababisha maafa ya aina hiyo je mvua za siku tatu mfululizo zita leta maafa ya namna gani?

Hivi, hamjitabui kuwa nyie ndiyo malaika wa nchi yetu, na kwamba ustawi wa miji yetu inawategemea nyinyi? Sasa kama nyie malaika wetu kwa vipaji mlivyo navyo, uwezo mlio nao na utashi wenu collectively mnashindwa kujituma kukabilina na matatizo haya, mnategemea nani atayatatua? Na je, mnategemea serikali inayo tawala na wananchi kwa ujumla wataweza kuwaamini nyie na kuwapa miradi ambayo kila mara mnashindwa kuitekeleza kwa ufanisi unao takiwa? Mnataka watu wawe wanawazomea kama wana CCM awamu ya nne walivyo kuwa wakinyanyasika kwa kuzomewa na kuwa mocked wakionekana wamevaa magwanda yao ya kijani na yellow?

Hivi, kitendo cha kukahidi au kushindwa kutekeleza wajibu wenu kama wataalam, mnadhani mnamkomoa nani? Hamjui kuwa nyie ndiyo watu mnaotakiwa kulisimamia Taifa letu lika imarika kwa manufaa yetu sote na vizazi vyetu vya baadae?
Kwenye daraja kama hili la Mbezi ya chini kuna ugumu gani kulitengeneza likawa imara na kudumu mda mrefu? Na hela ambazo serikali inge serve zingeweza kutumika katika maeneo mengine ambako hakuna miundo mbinu mizuri na watu kupata shida?

Lawama nyingine ningependa ziwaendee watendaji na watumishi wa serikali wanao husika na maswala ya uokoaji. Ina maana vitengo vyote vya serikali vinavyo husika na maswala ya uokoaji kama Zimamoto na vinginevyo vilishindwa kweli kupeleka wataalam na vifaa kwenye maeneo ambayo wana yaona critical?
Scene kama hii ina maana kikosi cha zimamoto kilishindwa kweli kupeleka wataalam na vifaa vinavyo husika kwa kazi hiyo ili kumwokoa huyu mwana dada kutoka kwenye hilo janga? Kama huyu mwana dada alikaa mda mrefu bila kuokolewa na Fire Briged, kunafaida gani kuendelea kuwa na kitengo kama hiki ambacho hakina faida kwa wananchi? Si afadhali hiyo kazi ikapewa private sector ikatoa Service nzuri kwa umma? Jangwani yote sijaona gari la zimamoto na wanajeshi wa zima moto wakiwa stand by. Ni polisi tu ambao walikuwa wakizuia watu wasipite na hiyo baadae sana.

Mimi nashindwa elewa inakuwaje mtu anapewa mafunzo ya kuperform task fulani na kuwa specialist, halafi kwenye incidents kama hizi, ambapo anatakiwa kuwajibika, anashindwa kutekeleza wajibu wake ambao umma umemwamini na badala yake kujichimbia kwenye ofisi zao au nyumba zao. Watu kama hawa watakuwa na akili gani hasa ya kukosa uelewa na wajibu wa kutekeleza kazi zao?

Kwa swala hili la kukosa utendaji wa majukumu waliyo pewa, ningependa kusikia majibu ya watumishi wa serikali wanao husika na maswala ya uokoaji, nini hasa mpangilio wao wa kazi, kiasi kwamba wakakosa ile uhodari na ujasiri wa kujituma kufanya kazi zao kwa Passion?

Rais Magufuli nakuomba hii hali ya kutopenda kjituma na kuwajibika kwa watu walio pewa dhana na umma inayoendelea nchini, kuiangalia kwa makini sana, maana inaonyesha kana kwamba kwenye jamii yetu kuna ugonjwa umetuingia ambao unatufanya sisi kuwa unconcerned. Hatu react ipasavyo katika Situation knapp bidi kufanya hivyo.

Watanzania tumekuwa watu wa porojo sana na wavivu katika kuwaza na kutenda pindi inapo bidi. Tukiendelea hivi sita shangaa wala kustaajabu kusikia kuwa vizazi vyetu huko mbele vinashindwa kukabilina na matatizo yanayo wahusu wao, na hivyo kukubali kirahisi kuwa watumwa tena wa vizazi vya wenzetu tunao dai wametuzidi maarifa.

Ombi langu kwa Rais Magufuli, tafadhali itisha mkutano wa wahandisi wote na maprofessor wote nchini ili tuli jadili hili tatizo la kukosa uwajibikaji wa wahandisi wetu. Huo mkutano usiwe wa siku moja unaweza ukachukua hata wiki moja ili wahandisi wengi wapate nafasi ya kujieleza na kutoa mawazo yao ili tujie nini kifanyike ili kurudisha ile hali iliyo kuwepo enzi ya Mwalim Nyerere.

Kingine wape maengineer wetu wajibu wa kusimamia na kuchimba bonde la Msimbazi kwa uwezo wao wenyewe na kulifanya liwe bahari mpaka Surrender na kuwa tuorist attraction. Wakishindwa hiyo project basi ningekushauri kitivo chote cha Civil Engineering kwenye vyuo vyetu kifutwe completelly na wanafunzi watakao chukua masomo hayo wapelekwe kusoma nje.

Inatisha! Maengineer wazima wanashindwa hata kuweka Dimensions za kutengeneza ma-Culvert?
Ni aibu kubwa sana!
Ni aibu kubwa sana!
Ni aibu kubwa sana!
Ni aibu kubwa sana!
Ni aibu kubwa sana!

Sent using Jamii Forums mobile app

Civil Engineers ndio ambao wanatoa vibali kujenga makazi ya watu kwenye njia na makazi ya maji?
Liko wapi 'ziwa Mwananyamara'?
Liko wapi 'ziwa Tandale'?
Liko wapi 'ziwa magomeni'?
Uko wapi 'mto Sinza'?
Kweli 'Ngwini' hamnazo!
 
ChoiceVariable,
Kuna vitu vingine vinawezekana Tanzania tu.

Kabla ata ujajenga ili kupata hati ya kiwanja ardhi inapimwa na surveyors wa serikari.

Ukiangalia hizo video haswa hiyo ya jamvi TV kuna sehemu huyo dada katembelea Sinza Kamanyola: unaona mtu analalamika kupoteza mali zilizochukuliwa na maji wakati jengo la biashara yake lipo on the edge of the ‘river bank’.

Cha kujiuliza huyo surveyor alieenda kuwapimia watu viwanja hayo maeneo hajui kwamba hiyo sehemu ipo juu ya saturated soil ambayo hata bila ya mvua chances ya hiyo ardhi kumomonyoka ni high, aoni hakuna buffer zone, aoni risk luluki zilizokuweko hapo.

Wanasiasa sio wataalamu per se in many cases ndio maana kuanzia kwenye ngazi za serikari za mitaa mpaka serikari kuu kila sehemu ina mwanasheria, kila aina wa engineer, surveyor; etc na wataalamu. Bado tena wanashirikiana na taasisi zingine kama NEMC ni jukumu lao kumshauri kiongozi actions gani muhimu za kuchukua katika kulinda usalama wa raia.

Sasa inakuwaje hadi inafikia hatua watu wanajenga maeneo kama hayo na hakuna anae liongelea, kuna lawama za kutosha hapo kugawanywa kwa wahusika mbali mbali zaidi ya wanasiasa.

Kuhusu mimi ninapoishi kwa kweli mafuriko hayajawahi kutokea wala umeme kukatika hata miaka ambayo mgao ulipokuwa tatizo sugu nchi nzima; kwa hilo nashukuru mungu.
 
Watu wa dar sijui wakoje yaani mvua kidogo tu wanalalamika, alafu nashangaa mvua inaweza nyesha mikoa mingine sana tu nani mvua ya nguvu lakini husikii watu wa mikoa hiyo wakilalamika jamani mvua jamani mvua, lakini watu wa mkoa wa dar kamvua kadoo tu basi dunia nzima itajua mvua imenyesha dar kwa kulalamika na kupicha picha mvua utadhani hawajawahi ona mvua, mi wananikera sana , kamvua ka jana kidogo tu basi watu wanalia lia sana utafikiri yatima
 
Kilatha,
Paragraph ya mwisho tu ndio nimeielewa mkuu,haaaa
Ila kama hujaona uzito wa wafanya maamuzi yaani wanasiasa walioshikilia mpini kwenye hili tutasubili sana na mambo yataendelea hivi hivi

Binafsi ningekuwa mkubwa kuanzia level ya katibu mkuu,waziri and above jambbo la kwanza kulishikia bango lingekuwa la kuunda mamlaka au tume ya ardhi na mipango miji ili kupata fedha na kudhibiti ujenzi holela hii ya kuwaachia serikali za mitaa imeshashindwa kitambo
 
Tokyo massive flood protection facility
View attachment 1295951View attachment 1295952View attachment 1295953Mnaweza kwenda YouTube weyewe mjionee sina cha kuongeza mtoa mada
Hizo nyumba za Dar ebu fanya kama unaziwekea hiyo massive flood protection.
Issue sio Civil Engineering, issue ni Mipango Miji na sisi wenyewe kujenga nyumba zetu pasipo ushauri wa kitaalamu,lakini pia tukiambiwa tuhame tupishe uboreshaji wa miji hatutaki tunataka kuishi mjini.
75% ya wakazi wa Dar hasa mjini kati inabidi waamishwe ili kujenga miundombinu imara.
 
Hivi hili swala la mafuriko limeshashindikana kabisa hapa Dar es Salaam?
 
Hivi hili swala la mafuriko limeshashindikana kabisa hapa Dar es Salaam?
 
Hivi hili swala la mafuriko limeshashindikana kabisa hapa Dar es Salaam?
 
Back
Top Bottom