Updates: Misri vs Tanzania [Michuano ya makundi kufuzu AFCON 2017]

Updates: Misri vs Tanzania [Michuano ya makundi kufuzu AFCON 2017]

TBC mnangoja kuonesha misiba tu hata timu yetu ya taifa mnapata kinyaa cha kuionesha kweli?
 
Hivi mechi hii itaonyeshwa vituo gani vya TV??

unataka uangalie jinsi tunavyofungwa mkuu? mimi naona ni bora hatuonyeshwi kwani kwa upoyoyo wa timu yetu tungepandishana tu presha bure halafu tufe! utampangaje mkude acheze kiungo ya pembeni na kumwacha erasto nyoni akicheza kama holding midfielder? labda wao kwa wao wawe wajanja wafanye switching na nadhani mkude is more comfortable akicheza mbele ya beki 4 na 5 na nyoni ni mzuri sana kulia na amekuwa effective sana akiwa anachezeshwa upande huo. wachezaji wetu na wao wanatakiwa mambo mengine waamue wao kwa wao wakiwa in the field of play na si kila wakati kumsikiliza ( chuck norris ) kocha wetu mart noij.
 
Viungo wa Tanzania Kiemba, Kazimoto na Mkude ni kama hawapo...

Hadi sasa sijamuona Samatta wala Ulimwengu wamegusa mpira...
 
Dk 20

Misri 0 - 0 Tanz
 
Kwa tabia hii ya timu ya Taifa inacheza nje huku tv zote watanzania hatuna uhakika Wa kurushiwa mechi safari yetu bado ni ndefu sana kwasababu katika hari ya kawaida mpaka sahivi hata kabla hatujaangaika kuuliza tulitakiwa kuwa tushaambiwa ni kituo gani kinarusha ila mpaka sahivi hamna, watanzania uzalendo umeisha kabisa

tivii zote sasa zinachanja mbuga na watangaza nia hivyo mtatusamehe sana na tuvumiliane tu watanzania wenzangu. siasa kwanza!
 
Hadi sasa Dida ndiye anayetutoa...
 
Dida anaumia tena baada ya kuangukiwa na mchezaji wa Misri...

Inaonekana kaumizwa bega na sasa anagangwa...
 
Back
Top Bottom