jiwe angavu
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 20,419
- 39,217
Huu uwekezaji mkubwa..sana hongera sana..Niko mbali na shamba hivyo picha wakati wa kumwagilia kwa sasa sina isipokuwa mfumo niliotumia wa umwagiliaji ni very simple. Umwagiliaji kwa sasa haifanyiki cause mahindi yamekomaa yakiendelea kukauka tayari kwa kuvunwa. Shamba linapakana na mto mkubwa usiokauka mwaka mzima hivyo nachofanya ni kulekeza pipes mtoni na kuchukua maji na kumwagilia kwa mashine inyorusha juu na kufanya mazao kama yananyeshewa mvua. Mashine hii kwa Tanzania inauzwa around milioni 40. Haina complication. Ni simple kabisa.
Hata Iringa hali ya mahindi si nzuri saana...Kwa mkoa wa Iringa hali ya mavuno hasa ya mahindi nakadiria kuwa 70%. Kuna maeneo mavuno ni mazuri na mengine ni wastani. Ila kwa zao la Alizeti halijaathirika na upungufu wa mvua uliojitokeza.
Kwa mkoa wa Mbeya kuna mtu kaniambia hali si nzuri sana kwa baadhi ya maeneo japo watavuna.
Ufuta bei gani? Na una uwezo wa kusuply tani ngapi?Kwa wadau watakao hitaji mazao kama mahindi, ufuta, mbaazi na soya na wako serious tuchekiane ... nipo mgodini kwa bei nafuu sanaa
Hiyo pump haitendei haki ukilinganisha na ukubwa wa Shamba; labda kama aliipata bureHuu uwekezaji mkubwa..sana hongera sana..
#MaendeleoHayanaChama
Hali ni mbaya, kwa kifupi wakulima tunatakiwa kubadilika hasa kwenye swala la matumizi ya Mbegu, inatakiwa tutumie Mbegu ambazo zimefanyiwa utafiti, kwani siku hizi mabadiliko ya Tabia ya nchi yameathiri kilimo kwa kiasi kikubwaHata Iringa hali ya mahindi si nzuri saana...
Naunga mkono hoja..mpunga haishikiki kaliua guni ni 80k..na ndio wameanza kuvuna.Mwaka huu2022 Hadi2023,Hali ni mbaya watakafaidi sanasana wanaomwagilia.
Phased investment. 25(trials) then 100 then 200 lengo ni acre 500 ambapo ndio ukubwa wa eneo lote. Tahadhari ni muhimu sana katika kilimo maana risk ni nyingi sana.Hiyo pump haitendei haki ukilinganisha na ukubwa wa Shamba; labda kama aliipata bure
Ni wap huko mkuuNilipo mimi kwa sasa alizeti ni 9000 debe ila mahindi wamekula za kichwa
Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Vipi ufuta umeanza na bei gani na mfumgo wa ununuzi Uko je? Au ndio mpaka upitie Amcos?Kwa sasa baadhi ya mazoa kwa SONGEA -Ruvuma yameanzwa kuvuna ikiwemo ufuta,soya , mpunga na mahindi.Kwa upande wa maharage kwa soko la sodeko yanaonekana yapo mengi na kufanya Bei Hadi wiki iliyopita unaweza pata kwa Tsh 1000
Nadhani Hivyo mpaka Amcos niliona Kijiji flani wanapeleka ktk magodauni,Bei sikuulizaVipi ufuta umeanza na bei gani na mfumgo wa ununuzi Uko je? Au ndio mpaka upitie Amcos?
Afadhali ya nyie kama mtavuna kidogo wengne kwenye mpunga tumekula za kichwa mazima aisee... alaf ndio bei ya mpunga kubwa hatar.
Ngoja tukanunue tu alzeti ili tufidie hasara japo nao mwaka huu wameanza na bei kubwa balaa.
Kwa alizeti debe saba ndiyo kilo 100. Chini ya hapo haifiki
Morogoro, shamba ni la kwangu nilinunua takribani miaka takribani 15 iliyopita. Ila cheki na waliopo mikoa ya pwani along Rufiji River. Unaweza kubahatisha good deal. Na mimi nikisikia nitakucheki pia.
Mwaka huu sikuwaza kuingia shambani kabisa,ila zile mvua za May nilizitumia ipasavyo nilipanda milimao size ya kati mpaka muda huu yote imeshika na naomba naomba mvua za Vuli zianze mapema ishamili zaidi ili mwakani ikimpendeza Mnyazi niipige kisu.Habari wakulima na wafugaji wenzangu, kutokana na hali ya hewa kubadilika na mvua kuwa chache nimeona ni bora tupeane updates za maendeleo ya Mazao hapa nchini ili watu wajipange kwa kununua Mazao sehemu yatakapopatikana kwa wingi
Huku maeneo ya Tanga hasa maeneo ya Muheza naona kama mvua ishakimbia na Mahindi yameachwa stages ambayo si Rafiki, yameachwa mengi yakiwa na umri wa mwezi mmoja na wakulima wengi wamepanda Mbegu za kienyeji ambazo zinachukua mpaka siku 120 mpaka kukomaa
Vip eneo lako Mazao yanaendaje?