Upinzani watangaza mapambano 2008

Upinzani watangaza mapambano 2008

dah bubu leo unampatia jamaa kweli...ila nae hakomi naona leo katuamulia
 
Tumempa Mh Rais wiki mbili unusu atoe ripoti la sivyo mapambano yatachukuliwa to the next level!
 
Inawezekana Mtu Akishakuwa Mpinzani Katika Nchi Ya Tanzania Basi Anabatizwa Moja Kwa Moja Kuwa Mwokozi , Yeye Hawezi Kufanya Makosa , Hakosei Na Hastahili Kusahihishwa Kila Mtu Amsikilize Yeye Hata Kama Hajui Asemalo Na Atendano

Basi Kama Mawazo Ya Wapinzani Wengi Yako Hivi Kama Ninavyoona Hapa , Kuna Safari Ndefu Sana Ya Kupata Mapinduzi Ya Kweli , Yaani Nafananisha Upinzani Sawa Na Kupita Barabarani Kichaaa Akawa Upande Wa Kushoto Na Mimi Kukaa Mkono Wa Kulia

Saa Zote Namwangalia Yule Kichaa Asije Akapita Barabarani Agongwe Na Gari . Lakini Si Kichaa Hata Madereva Wanajua Yeye Ni Kichaa Hawana Wasi Wasi Nae Kabisa Wanajua Atafika Pale Apige Kelele Wee Alale Kisha Jioni Arudi Zake Kwao
 
Mumeongea yote lakini hamjajibu hoja ya Shy; Shy ni mwananchi wa Tanzania, wazo lake linahitaji kujadiliwa, na huenda akawa anawakisha mawazo ya Watanzania wengi;

Binafsi; Nawashukuru sana vyama vya upinzani kuanika uozo wa nchi yetu;lakini kwa kuwa pia wanataka tuwapatie mikoba ya nchi basi pia waonyeshe mengine zaidi ya hao... kuweza kukosoa sio qualification ya kuweza kuongoza... yawezekana wanaweza tu kosoa lakini hawawezi kuongoza.

Chukua mfano wa Mshabiki wa soka na Mchezaji, Shabiki anauwezo mkubwa kukosoa lakini kwa hakika hawezi cheza...

Sina hakika kama CUF wanaweza kuwa katika mgao wao wa fedha wamejaribu kutenda hata 10-20% kuweka kwenye miradi ya kuwasaidia wananchi... kufungua hata pampu ya maji at least moja... au kusaidia wanabuguruni (makao makuu ya CUF yalipo) kuzibua mifereji ya majumbani mwao ili wasipate kipindupindu. Au hata kutoa kwa ajili ya kampeni ya kusaidia wananchi kujali usafi.

Yet hawa ndio tunawaona wameshikilia mstakabali wa Taifa letu; wanaendelea kuwaambia wananchi kwamba siasa za vyama vingi ni mikutano, maandamano na press conferences...!!!

Kwa hakika wananchi kama hatulioni hili.... tumekwisha... na hiyo ndio hoja ya SHY
 
Tatizo letu hatupati muda mwingi na mahali kwingi kutoa machungu yetu ya maisha na fikra,ndiyo maana wakati mwingine hoja nyingi humu ndani huwa zinajadiliwa kishabiki sana.

Sikubalini na mambo mengi yanayosemwa na kutendwa na CCM lakini siyo kwamba sikubalini nao kwenye kila kitu,na pia napenda nguvu ya Upinzani ikue na kukomaa nchini kwetu,lakini sikubaliani na mbinu zao nyingi ambazo naziona butu

kwa mfano wapinzani wamejikita kwenye mikutano na waandishi wa habari pale kwenye ukumbi wa maelezo Dar es salaam, bila ya kuwa na mikakati mbinu ya kuhakikisha kwamba na wao wanajenga Oganaizesheni imara kuanzia ngazi ya taifa hadi mitaani kwetu.

Ingawa wengi wetu tunashindwa kuangalia au kukubali kwamba kuna tofauti kubwa sana kati ya nadharia (Theory) na mkakati mbinu (Strategy) katika kujenga chama. Vyama vingi vya upinzani vimejikita katika kupambanua nadharia zao bila ya kujenga mikakati imara ya kuzitekeleza nadharia hizo

CCM ni dhaifu lakini uimara wake unatokana na yenyewe kumiliki dola la Tanzania,kuitoa CCM hakutafanikiwa kwa kusema tuu kwamba fulani ni fisadi,inatakikana mikakati ya uzamivu kubadili fikra za watu waliotawaliwa na CCM kwa zaidi ya miaka 30, siyo kupiga domo tu kila siku

Mfano halisi ni Mwalimu. Aliijenga TANU kwa kufika kwa watu akiwa anafanana nao na anaongea lugha yao,aliwajaza matumaini chanya na wao walimpa dhamira zao. Wapinzani wa sasa wananchi wanasema "hata wao tukiwapa nchi watakula kama CCM,tena heri CCM wameshaanza kuvimbiwa!
 
Hii thread inanichekesha sana. Halafu kuna watu wanalalamika kuhusu seriousness

with threads like therese who needs one? Its pure comedy sasa kwa nini isiunganishwe na ile nyingine au ndio kuchangamsha "barza"
 
Shy,

Afadhali kumbe huwa unaamini Tanzania inahitaji mapinduzi eeh? Sasa tafadhali acha kuwa kikwazo cha mapinduzi hayo.Kumbuka wewe ni kijana ambae taifa linakutegemea ili uwe chachu ya mabadiliko.

Kwanza nani kakuambia huwa wapinzani hawakosei?manake naona wewe ni mtu unayeongozwa na hisia tu.
 
Niu kweli kabisa sio kila kitu kinachofanywa na CCM ni kibovu lakini katika kipindi cha hivi karibuni imeonyesha uozo mkubwa sana.

Wapinzani hatuwezi kila siku tukawabatiza kuwa bado wachanga, mfumo wa chama kimoja umenza kwa miongo miwili sasa kwahiyo hatuwezi kusema wapinzania bado wachanga kwani kama ni mtoto ni mkubwa kabisa, je kwanini wanaonekana kana kwamba hawana Strategy sahihi ya kuwafikia wananchi walio wengi hasa vijijini?

Hili nafikiri hata wao wanaweza wasiwe na jibu sahihi zaidi ya kukwambia pesa hakuna, lakini ninachofahamu ni kuwa pesa sio msingi wa maendeleo, kwanini vijijini wananyanyaswa na serikali yu CCM lakini bado wanawapigia kura, ni kwakuwa wapinzania hawana mkakati sahihi wa kuwasiliana na wananchi hasa wa vijijini.

Hili sio la vyama vya upinzani pekee even NGO's zote zipo mijini zinafanya kazi mijini hata kama hile kazi inatakiwa ifanyike vijijini, unakuta NGO zinapigana vikumbo kutoa misaada kwa watoto yatima mijini lakini hawa watoto wanapata tabu sana vijijini hata blanket hana hacha nguo ya kuvaa.

Vyama vya upinzania vinatakiwa viungane na asai zisizo za kiserikali na kwenda vijijini kuwasaidia wananchi na kuwaelimisha kuwa kuuza kura yako siku ya kupiga kura ni sawa na kuuza uhuru wako, mfano mzuri ni zimbabwe ambako NGO ziliungana na kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kupiga kura na matokeo yake tumeyaona.

CCM wana base kubwa sana vijijini na wanajua wanachofanya ndo maana wanaendelea na ufisadi kwa kuwa wanajua kuwa mwaka 2010 watakwenda na pea ya kanga na chupa ya gongo kwa wananchi vijijini na wananchi hawatawaangusha watawapigia kura.
 
I think SHY is ashamed after having read comments given against his thread.

Shy najua unatoa maoni yako kutokana na jinsi unavyotaka kuwafurahisha waajiri wako. Usijali sana mwanangu endelea kufanya kazi kwa kuwa huna njia nyingine ya kipato.

Lakini kwa ajili ya kutunza utu na heshima yako na ya utaifa wako pitia hoja zake tena na tena.

Yenyewe
 
Ni jambo zuri kuwa na viongozi wenye veyti vya kughushi?

Kiongozi gani mwenye cheti cha kugushi?
Maana mi namkumbuka Kihiyo!
Ama mwenzetu una brekin nyuzz kama za ndugu yetu GT?
 
Kuna hoja za msingi kama za wapinzani to do more than maelezo .Hili nadhani waliangalie sana .Sera zao ziende vijijini .Waendee kwa kusambaa na si kuwangija viongozi wa Kitaifa kuwa katika maeneo yao .Wachaguliwe watu wao kubalika katika ngazi zote ili waweze kukisemea Chama si kishabiki ila nini wanataka kuwafanyia Watanzania .

Mwisho nyie mnao biashana na shy naona mna muda wa kuuza bure .Huyu yuko kazini .Ila kuna siku atanasa tu .Maana kila muosha maiti ataoshwa pia .
 
Tatizo letu hatupati muda mwingi na mahali kwingi kutoa machungu yetu ya maisha na fikra,ndiyo maana wakati mwingine hoja nyingi humu ndani huwa zinajadiliwa kishabiki sana.

Sikubalini na mambo mengi yanayosemwa na kutendwa na CCM lakini siyo kwamba sikubalini nao kwenye kila kitu,na pia napenda nguvu ya Upinzani ikue na kukomaa nchini kwetu,lakini sikubaliani na mbinu zao nyingi ambazo naziona butu

kwa mfano wapinzani wamejikita kwenye mikutano na waandishi wa habari pale kwenye ukumbi wa maelezo Dar es salaam, bila ya kuwa na mikakati mbinu ya kuhakikisha kwamba na wao wanajenga Oganaizesheni imara kuanzia ngazi ya taifa hadi mitaani kwetu.

Ingawa wengi wetu tunashindwa kuangalia au kukubali kwamba kuna tofauti kubwa sana kati ya nadharia (Theory) na mkakati mbinu (Strategy) katika kujenga chama. Vyama vingi vya upinzani vimejikita katika kupambanua nadharia zao bila ya kujenga mikakati imara ya kuzitekeleza nadharia hizo

CCM ni dhaifu lakini uimara wake unatokana na yenyewe kumiliki dola la Tanzania,kuitoa CCM hakutafanikiwa kwa kusema tuu kwamba fulani ni fisadi,inatakikana mikakati ya uzamivu kubadili fikra za watu waliotawaliwa na CCM kwa zaidi ya miaka 30, siyo kupiga domo tu kila siku

Mfano halisi ni Mwalimu. Aliijenga TANU kwa kufika kwa watu akiwa anafanana nao na anaongea lugha yao,aliwajaza matumaini chanya na wao walimpa dhamira zao. Wapinzani wa sasa wananchi wanasema "hata wao tukiwapa nchi watakula kama CCM,tena heri CCM wameshaanza kuvimbiwa!

Hayo uliyosema ni ya msingi kidogo lakini hebu tujiulize hakuna mtu ambaye ni msafi moja kwa moja na pia hatuwezi kuisema CCM moja kwa moja nionavyo mimi anayekosa ni mtu na wala sio chama hata nyumbani kwako kunaweza kukatokea mtoto mwizi atakayekamatwa ni yeye mtoto na wala hahukumiwi baba eti kwa sababu amemzaa huyo mtoto haiwezekani hata kidogo hilo nakataa
 
Ni jambo zuri kuwa na viongozi wenye veyti vya kughushi?

BABU ATAKA KUSEMA acha mambo ya uzushi ni viongozi gani ambao wewe unaeleza kuwa wana vieti vya kugushi usilete habari za uzushi hapa unatkiwa utoe ushahidi ili wapelekwe mahakamani ili kama ilivyokuwa kwa kihiyo
 
Niliwahi kuona tangazo katika mtandao wakati Fulani , mmoja wa wabunge wa upinzani Tanzania ameacha namba yake ya simu atakayotumia atakapofika marekani , kwa wale ambao hawako busy wanapenda kuonana nae na vijana wengine wengi wenye muelekeo wa kipinzani .

Sitaki kubisha inaonekana wapinzani wamewashika sana vijana wa kitanzania walio nchi za nje haswa marekani kiasi kwamba zitto anapokanyaga huko wanaona mwokozi wao kafika watu wanasongamana wanataka kumwona kupiga nae picha na vitu kama hivyo .

Pamoja na kuacha hizo namba za simu na watanzania kujitokeza kuonana nae , sera na mambo anayoongea katika mikutano hii ni zile zile , za ufisadi ambazo sasa hivi ni zilipendwa , yale yale ya epa na mambo mengine ambayo kwa hakika sio ya kujenga upinzani sio ya kujenga nchi ni ya kupasua hadhi ya nchi na watu wake nje ya mipaka yake .

Namheshimu Nyepesi na Wenzake wengi kama watanzania lakini siwezi kuheshimu na kuendelea kusikiliza watu wenye mawazo ya kuvuruga wananchi wakiwa nje ya mipaka yao huwa nashangaa kama hawana masuala mengine ya kuongea zaidi ya haya .

Hao ni chadema ndio wameshikilia Epa , Ufisadi na Usalama wa Taifa , ukirudi kwa upande wa baba zako chama cha wananchi CUF , ningekuwa mimi ni mwanachama wa CUF ningehoji kwanini hao viongozi wawili wa CUF wako pale walipo mpaka sasa hivi

Tangia upinzani umeanzishwa ni viongozi wale wale wa CUF wanaowashika masikio baadhi ya wanachama wao , ni viongozi wale wale wakorofi wako madarakani katika chama hicho mpaka sasa hivi , sijui CUF hawana viongozi wengine ni lazima wawe hawa hwaw ?

Mtihani wao wa kwanza wameshaushindwa wa kuleta maelewano huko visiwani , kwa sababu wameshashindwa jaribio hilo , sioni sababu ya kwanini wasiache nafasi hizo wazi waje watu wengine wenye utashi zaidi yao , watu wanaopenda kukaa mezani na kumaliza tofauti zao .

Niliangalia hata wakati wa maandamano ya CUF visiwani wiki iliyopita mmoja wa washairi aliposema kwamba anaweza kujilipua kama mambo yataendelea kuwa hivyo , wengine wakawaambia wenzao wasipeleka bidhaa katika kisiwa kingine wakipeleka basi wao ni halali yao .

Yote hayo yanasemwa viongozi wa CUF wamekaa katika viti wanasinzia wengine wanacheka na kufurahia kwa madaha kama vile ile ni halali yao kusema vile na hakuna chochote kile mbele yake .

Nilitegemea mmoja wa viongozi hawa au msemaji wa CUF aje mbele na kusema kile kilichosomwa na yule mshairi sio msimamo wa CUF lakini hakikutokea kitu kama hicho kwahiyo tuchukulie basi kuanzia sasa hivi na mpaka hapo viongozi wa CUF watakapoamua baadaye

Kwamba sera za CUF kuanzia sasa hivi ni KUJILIPUA , KUKATAZA BIASHARA NA UNGUJA NA KUPUNGUZA UNDUGU WAO kwa sababu hawa wengine sio wanachama wao , wao ni CCM.

The author of this article is a victim of numb thinking..... a condition which makes brain vunarable to stupidity and ignorant .... as a result a victim always do something he/she know (or he/she should know) he/she shouldn't be doing but he/she do it anyway

"Nothing in the world is more dangerous than sincere
ignorance and conscientious stupidity."
-- Martin Luther King Jr.
 
Last edited by a moderator:
The author of this article is a victim of numb thinking..... a condition which makes brain vunarable to stupidity and ignorant .... as a result a victim always do something he/she know (or he/she should know) he/she shouldn't be doing but he/she do it anyway

Humu ndani watu kwa kujilipua, utadhani wako kambi moja na Osama Bin Laden!
 
Last edited by a moderator:
Shy,
Naweza kukubaliana na wewe kwa kiasi kikubwa, kweli kitendo cha wapemba kusema wanaweza kujilipua si wazo jema ktk jamii yetu hii, ila sasa tusiwashangae wale wanaomuunga mkono Zitto, hizi yote ni harakati za kujikomboa toka kwenye fikra butu za wakongwe ccm, tunajua Shy mawazo yako ni hai na kila mara umekuwa ukisema kweli, ukiishawishi jamii yetu sasa tunaomba muongozo tufanye nini ili tujikwamue kwa haya unayodhani vyama vya upinzani vinatuhadaa?
 
Wana JF tumeshupalia kuikosoa serikali hii ambayo ni failure seriksli kichwa ngumu.
Je hawa vyama vya upinzani wamefanya nini katika ku capitalize failure ya hii serikali?......NOTHING.
Je wameenda vijijini haswa sehemu ambazo ni stronghold ya CCM,Songea Mtwara Sumbawanga Mbeya n.k?.........HAPANA

Wameshupalia sehemu za madini na mikoa ya North East tu....Tanzania sio madini tu na sio North East tu na mjue hizo mikoa mnayoenda kila mara hakuna shida sana kama sehemu zingine...nendeni vijiji ambavyo vimepigwa chini kiuchumi.

Je mwaelimisha wananchi kuhusu ufisadi?....HAPANA
Mnakaa mnafanya ma press conference tu je mnajua ni watanzania wangapi wanasoma magazeti au wana ma TV?
Mnaongea lugha ambayo ya kitaalam badala ya kurahisisha kwa mfano ukimweleza mwanakijiji EPA,Twin Towers,n.k... anaelewa nini?.......ZERO.

Lakini ukiwaambia serikali yetu ya CCM imepoteza mabilioni 133 ya pesa ambazo ziingetujengea shule kadhaa,hospitali kadhaa,barabara kadhaa n.k...

Ninachowaomba nyie Vyama Vya upinzani muamke angalieni mapinduzi ya Iran enzi ya Aytollh au Chiluba na MMD simaanishi hawa walikuwa viongozi bora bali waliitumia ubovu wa serikali zao kuingia kwenye power.
 
Sijui kama vyaupinzani kama vinakusanya ushahidi chungu nzima wa ufisadi unaofanywa na viongozi wa chama na sirikali ili vitumie ushahidi huo kuimaliza kabisa CCM kila kona ya nchi. Wizi wa KCM uliofanywa na fisadi Mkapa na Yona, mabilioni ya shilingi yaliyochotwa toka BOT (155 billioni zilizoingia eremeta na 133 billioni zilizoingia katika makampuni ya kifisadi na mafisadi).

Pia pamoja na Watanzania wengi kushauri vyama vya upinzani kuungana ili kuunda chama kimoja chenye nguvu, hadi hii leo ushauri huo wa Watanzania umedharauliwa na hivyo kutofanyiwa kazi.

Sasa hivi ingekuwa ni wakati mzuri sana wa viongozi hao kupita kila kona ya nchi hasa vijijini ili kuwaambia Watanzania kuhusu ufisadi unaofanywa na CCM na sirikali na pia kuanza kuweka utaratibu wa kuungana kabla ya uchaguzi mkuu wa 2010. Tutapiga kelele za ufisadi mpaka tuchoke lakini kama vyama vya upinzani havifanyi lolote ili kufuata ushauri wa Watanzania walio wengi wa kuunda chama kimoja chenye nguvu na kutembea Tanzania nzima hasa vijijini ili kuwafahamisha wananchi kuhusu ufisadi, basi chama cha mafisadi kitaendelea kuwa madarakani miaka nenda miaka rudi. Wakati sasa umefika wa Watanzania kuwageukia vyama vya upinzani na kuwauliza kulikoni? Je, mmesikia ushauri wetu kwenu? Je, mnaufanyia kazi? Kwanini mkubali kuweka ubinafsi mbele na kushindwa mwaka nenda mwaka rudi pamoja na kuwa CCM sasa imekuwa ni chama cha mafisadi na ushahidi wa kutosha upo? Mikakati yenu ya kuing'oa CCM madarakani kamwe haitafanikiwa kama hamuwasikilizi Watanzania na pia kubadilisha mikakati hiyo kutokana na ushauri wa bure mnaopewa na Watanzania.
 
Back
Top Bottom