Uchaguzi 2020 Upinzani watoe Ilani zao za Uchaguzi yaani “Election Manifesto" acheni porojo hazina Tija

Uchaguzi 2020 Upinzani watoe Ilani zao za Uchaguzi yaani “Election Manifesto" acheni porojo hazina Tija

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Ilani ya Uchaguzi au kwa kiingereza huitwa Election Manifesto ni kabrasha litolewalo na chama cha siasa ambalo limesheeni mawazo na sera zote.

Mara nyingi chama cha siasa kikishinda uchaguzi huweza kupimwa mafanikio yake kutokana na utekelezwaji wa ilani yake ya uchaguzi.

Kwa miaka mitano ilopita haitii shaka yoyote kwamba CCM imesimamia ilani yake ya uchaguzi na kuhakikisha inatekelezwa kwa asilimia 80 au zaidi.

Sasa bila kuoindapinda kona CHADEMA na vyama vingine vya upinzani wanatakiwa watoe ilani zao za uchaguzi kila mmoja kwa wakati wake.

Ilani ya uchaguzi huandaliwa na kundi la watu ambao wote hukaa pamoja na kwa lengo moja kushinda uchaguzi na kushika dola.

Dalili zote kwamba upinzani unaenda kwenye uchaguzi kupoteza viti vingi bungeni zajionyesha.

Ni makosa yaleyale ya miaka nenda rudi tangu sheria ya vyama vingi ipitishwe mwaka 1992.

Mpaka sasa Agustino Mrema ndie kiongozi pekee wa upinzani ambae alitoa ilani ya uchaguzi ya NCCR mageuzi na akatoa upinzani wa kutosha kwa mgombea wa CCM mwaka 1995 marehemu Benjamin Mkapa.

Sasa basi, mwaka huu hali si kama ile ya 1995 hali ni ngumu na ni vigumu kuishinda CCM, tusiwe wanafiki.

Ila bado CHADEMA ya Tundu Lissu na vyama vingine toeni ilani zenu za uchaguzi ili wananchi angalau waone mmejitahidi.

Hata kama ni mdahalo mnaouhitaji lakini kwenye mdahalo mtakinzana kwenye ilani zenu za uchaguzi na si shutuma za yule kafanza nini ama yule vipi.

Ndo maana ni vigumu kwa Tanzania kufanya midahalo kama hakuna sera kila upande.

Acheni porojo na blahbla za oh! mara jogoo kanunuliwa na kadhalika.

Karibu.
 
Ni kweli kabisa.
Naona CHADEMA are basking in the sunshine ya kumuona Lissu tena.
Wanasahau kuwa mwishowe Lissu atachusha na matatizo ya wananchi yako pale pale.
Hatujasikia siasa mbadala ambazo zimejengwa na sera zinazoeleweka.

Lissu si chakula cha kuliwa mezani.
 
Ni kweli kabisa.
Naona CHADEMA are basking in the sunshine ya kumuona Lissu tena.
Wanasahau kuwa mwishowe Lissu atachusha na matatizo ya wananchi yako pale pale.
Hatujasikia siasa mbadala ambazo zimejengwa na sera zinazoeleweka.

Lissu si chakula cha kuliwa mezani.
Hamna Chamaana alichozungumza Lissu mpaka Sasa ila blah blah ndo zimetawala kwake.
 
Ilani zimekuwepo miaka nenda rudi tangu 1960 hadi leo mmefanya nini?? Toa utopolo wako hapa.
 
Ilani zimekuwepo miaka nenda rudi tangu 1960 hadi leo mmefanya nini?? Toa utopolo wako hapa.

Mkuu, mimi najikumbusha nadharia za Karl Max na Friedrich Angels.

Vita vya matabaka, ubepari na mfumo wa uzalishaji mali wa kibepari.

Hawa mazee mwisho wa kitabu chao ndo walitoa hoja isemayo " "forcible overthrow of all existing social conditions",

Karibu sana.
 
Nadhani ilani ya chadema ni kuingiza wananchi barabarani na kutengeneza tshirts kali za chama.
Ndo walivyokwisha tuonyesha kila tulipohisi wanakuja na ilani.
 
Ilani ya uchaguzi au kwa kiingereza huitwa election manifesto ni kabrasha litolewalo na chama cha siasa ambalo limesheeni mawazo na sera zote.

Mara nyingi chama cha siasa kikishinda uchaguzi huweza kupimwa mafanikio yake kutokana na utekelezwaji wa ilani yake ya uchaguzi.

Kwa miaka mitano ilopita haitii shaka yoyote kwamba CCM imesimamia ilani yake ya uchaguzi na kuhakikisha inatekelezwa kwa asilimia 80 au zaidi.

Sasa bila kuoindapinda kona Chadema na vyama vingine vya upinzani wanatakiwa watoe ilani zao za uchaguzi kila mmoja kwa wakati wake.

Ilani ya uchaguzi huandaliwa na kundi la watu ambao wote hukaa pamoja na kwa lengo moja kushinda uchaguzi na kushika dola.

Dalili zote kwamba upinzani unaenda kwenye uchaguzi kupoteza viti vingi bungeni zajionyesha.

Ni makosa yaleyale ya miaka nenda rudi tangu sheria ya vyama vingi ipitishwe mwaka 1992.

Mpaka sasa Agustino Mrema ndie kiongozi pekee wa upinzani ambae alitoa ilani ya uchaguzi ya NCCR mageuzi na akatoa upinzani wa kutosha kwa mgombea wa CCM mwaka 1995 marehemu Benjamin Mkapa.

Sasa basi, mwaka huu hali si kama ile ya 1995 hali ni ngumu na ni vigumu kuishinda CCM, tusiwe wanafiki.

Ila bado Chadema ya Tundu Lissu na vyama vingine toeni ilani zenu za uchaguzi ili wananchi angalau waone mmejitahidi.

Hata kama ni mdahalo mnaouhitaji lakini kwenye mdahalo mtakinzana kwenye ilani zenu za uchaguzi na si shutuma za yule kafanza nini ama yule vipi.

Ndo maana ni vigumu kwa Tanzania kufanya midahalo kama hakuna sera kila upande.

Acheni porojo na blahbla za oh! mara jogoo kanunuliwa na kadhalika.

Karibu.
Porojo ndiyo wananchi tunazitaka. Election manifestos baadaye wakati wa utekelezaji kwani wakati huo hakutakuwa na porojo!
 
Tulia wewe tukutengenezee ajira M 10
IMG_20200805_225321.jpeg
 
Tulia wewe tukutengenezee ajira M 10View attachment 1528306

Safi sana ndo nataka watu kama wewe uje hapa na madini muhimu.

Sasa tuanze kuchambua, haki za walemavu hapana, kwa sababu tayari walemavu wanashirikishwa katika kila setka ikiwemo serikali kuu.

Tena hiyo ni pamoja na wazee, wastaafu na wasojiweza ambapo wazee sasa hivi hawalipi baadhi ya kodi na wana misamaha mingine mingi tu.

Pia wastaafu wanaweza kupata mikopo benki kwa riba ndogo sana hiyo ni sera ya mabekni kuwasaidia wastaafu.

Hata balozi mwenye ulemavu wa ngozi Dr Posi tunae nchini Ujerumani.

Kwa hii CCM itakushinda kwa hoja.

Nimeanzia chini kabisa ya jedwari lako.

Haya twende kazi.
 
Vyama vya upinzani hawana mpango wa kukamata dola wamepanga kumpa heka heka tuu magufuli

Tatizo jingine ni kwamba wapinzani wanashindwa kutofautisha kati ya harakati za mitandaoni na zile za ardhini kwenye eneo la tukio.

Kwa kiingereza tunasema hiyo yaitwa "asymmetrical warfare" yaani vita kati ya jeshi ambalo limekamilika kwa kila kitu linalopigana na waasi au wanamgambo wa kukusanya.

Hivyo chama tawala kina mbinu na mikakati ya ushindi wakati chama cha upinzani kinatumia mbinu ya kutafuta udhaifu wa chama tawala ilhali wanafahamu kwamba hawakiwezi kwa ubora , uzoefu na umakini.
 
Ilani ya uchaguzi au kwa kiingereza huitwa election manifesto ni kabrasha litolewalo na chama cha siasa ambalo limesheeni mawazo na sera zote.

Mara nyingi chama cha siasa kikishinda uchaguzi huweza kupimwa mafanikio yake kutokana na utekelezwaji wa ilani yake ya uchaguzi.

Kwa miaka mitano ilopita haitii shaka yoyote kwamba CCM imesimamia ilani yake ya uchaguzi na kuhakikisha inatekelezwa kwa asilimia 80 au zaidi.

Sasa bila kuoindapinda kona Chadema na vyama vingine vya upinzani wanatakiwa watoe ilani zao za uchaguzi kila mmoja kwa wakati wake.

Ilani ya uchaguzi huandaliwa na kundi la watu ambao wote hukaa pamoja na kwa lengo moja kushinda uchaguzi na kushika dola.

Dalili zote kwamba upinzani unaenda kwenye uchaguzi kupoteza viti vingi bungeni zajionyesha.

Ni makosa yaleyale ya miaka nenda rudi tangu sheria ya vyama vingi ipitishwe mwaka 1992.

Mpaka sasa Agustino Mrema ndie kiongozi pekee wa upinzani ambae alitoa ilani ya uchaguzi ya NCCR mageuzi na akatoa upinzani wa kutosha kwa mgombea wa CCM mwaka 1995 marehemu Benjamin Mkapa.

Sasa basi, mwaka huu hali si kama ile ya 1995 hali ni ngumu na ni vigumu kuishinda CCM, tusiwe wanafiki.

Ila bado Chadema ya Tundu Lissu na vyama vingine toeni ilani zenu za uchaguzi ili wananchi angalau waone mmejitahidi.

Hata kama ni mdahalo mnaouhitaji lakini kwenye mdahalo mtakinzana kwenye ilani zenu za uchaguzi na si shutuma za yule kafanza nini ama yule vipi.

Ndo maana ni vigumu kwa Tanzania kufanya midahalo kama hakuna sera kila upande.

Acheni porojo na blahbla za oh! mara jogoo kanunuliwa na kadhalika.

Karibu.
Mkuu unless sijaelewa..... Mbona kila chaguzi tokea 2005 CHADEMA wanatoa ilani za uchaguzi ama unaongelea kuisambaza/ kuifikisha kwa wananchi kupitia medium tofauti?

Nakumbuka ilani ya 2015 iliandaliwa na kina Dr Bashiru Ally na ilisheheni malengo kibao kama chama kingeshika dola. Hata ya 2020 imekua presented jana vizuri sana na Mrema, imechambua kila sekta kuanzia kilimo mpka Elimu na ina mashiko sana.
 
Back
Top Bottom