Ups and down miaka 8 ya kubet (addiction) bila ya mafanikio

Ups and down miaka 8 ya kubet (addiction) bila ya mafanikio

Nashukuru kubet kumenipita kushoto.

Sina mzuka kabisa na kubet

Nachukia kupoteza Hela bila sababu ya msingi.

Niko tayari kupoteza hadi laki5 ila kwasababu ya msingi yenye mashiko.
Kama mimi tuu, yaani nitumie 10 milioni ziliwe kwenye kubeti, nitaumia kwa kipindi kirefu sana...
 
Hii kitu ainuke mtawala aipige pin nchini.

Huu ni ulevi kama tu WA kuangalia pornography au punyeto.

Betting ni laanatul!!
 
Ndugu zangu

Kwenye jukwaa hili nimeshuhudia hadithi na mikasa mingi watu waliyokutana nayo kabla na hata baada ya kujiunga mtandao huu mwaka 2014 hivyo kwanza nijipongeze kwa kufikisha miaka 10 kwenye hili jukwaa na miaka yangu hii kumi napenda kutoa stori fupi ya maisha yangu ambayo ni ya kusikitisha niliyaiga kutoka kwa Rafiki yangu mmoja mwaka23/3/ 2017.

MAISHA YA KUBETI

Watu wengi wanaoingia kwenye mikwamo ya ulevi hawaingii kwa kupenda ila mara nyingi huwa ni externally forcing huenda ni vichochezi vya marafiki,mitandao ya kijamii,dhiki na mengineyo.

Nakumbuka nilikuwa ni mtu safi ambaye nilijiapiza kutojihusisha na kamari pamoja utumiaji wa bangi ila la haula bahati mbaya iliyoje kote nimepakanyaga lakini nimeweza kuacha bangi ila siyo kamari ambayo imenicost muda,kuniathiri akili,fedha,magonjwa pamoja na tabia.

Kama hamutambui Magonjwa mengi ya akili,moyo na mabadiliko ya tabia huchochewa na kuanzisha tabia hizi mpya mimi nakumbuka 2016 nilimaliza masomo yangu ya kidato cha 6 kama mtahiniwa wa kujitegemea baada ya kushindwa kulipa ada,namshukuru mungu nilifaulu lakini ndiyo kipindi ambacho niliadapt tabia mbaya ya uchezaji kamari ambapo Rafiki yangu alikuwa ni mwenye kuicheza na kunishawishi sababu alikuwa anapata vishilingi na kwa bahati mbaya maisha yangu mimi toka udogoni ni mabovu pesa ni ngumu kushika hivyo nikasema acha nijitafutie bahati.

Lahaulaaaaa!!!nilijiunga na mtandao wa m-bet nilipigwa kila siku basi ikafika kipindi nikaanza kuhudhuria meridiani pale magomeni mkabala na mwendo kasi kwa siku ya kwanza niliweka 500 nikaweka odd ndogo nikala 4500 nikasema hapa mambo fresh,basi tangu hapo nilikuwa napigwa tu,kila navyopata pesa naenda kuongeza napigwa pesa yote na sikuwahi kuvuka hata kiasi cha 10,000.kuna siku nilibet PM bet nikala 15,000 ebwaa eeeh nikasema nicheze visual throne nikagongwa yote basi tangia hapo napigwa tu.


NIMEPATA KAZI YA KUUZA DUKA(2017)
Mwanzoni kabisa nilipata kazi ya kuuza duka xxxxxx basi ilitokea tu!bahati jamaa wa duka aliniamini sana,ila kwa bahati mbaya kamari ilivunja uaminifu nilikuwa kila usiku nikifunga duka hua naenda kubet thrown visual ya mpira nililiwa pesa ya watu mpaka nikawa najilaumu na kuapa viapo vyote kuwa nitaacha ila wapi!!.

Kibaya zaidi,nilikuwa natumia pesa ya dukani kila siku 20,000-30,000/= kuzani nitarejesha lakini wapi na mshahara wangu ulikuwa 90,000/= ilitokea siku nikafunga duka ili niende kufanya kitu fulani mkononi nilishika 60,000/= sijui ndiyo shetani akanipitia nikajiona naelekea thrown kucheza visual aiseee niligongwa yote yaaani unaweka mpira nyau nyau, dog hamna kitu,namba hamna daaaah toka siku hiyo nikajiapiza tena kuwa sitacheza ila wapi.

siku inayofata jamaa akaja dukani tukapiga hesabu kiasi kama cha 235,000/= kilipungua ndani ya siku chache tu, nikataka kupelekwa polisi ila huku na huku pesa ikalipwa..sikuwa mwenye kupata chochote ila nafsi yangu tu ni ngumu kuacha.

niliachishwa kazi,nilijutia ila niliendelea basi ilitokea home napewa pesa naenda kwenye kamari naliwa alafu nasingizia imepotea dah maisha yalikuwa ni ya kipumbavu sana.

Ukweli nikipiga hesabu ya pesa nilizotumia kwenye kamari naweza kupata 6,000,000/= mpaka kufikia sasa sina hata kiwanja wala chochote nipo nipo na bado nacheza tu.


WADAU MIAKA 8 BILA MAFANIKIO KATIKA KAMARI,MISUKOSUKO YA MAISHA KISA KAMARI


UKWELI BADO NACHEZA JAPO NIMEPEVUKA NIMEACHA MAMBO YA VISUAL ILA NINGELIKUWA RAIS NINGELIFUKUZIA MBALI HIZI KAMPUNI ZA KUBETI SIYO POWA VIJANA WANAKUWA WAGOJWA WA AKILI,MWILI N.K SABABU YA KAMARI


MWISHO UZI USIUNGANISHWE
Kwa huo upumbavu wako ni lazima wengi waone km michezo ya kubahatisha haifai.
Ndio,kwa watu wenye vichwa vidogo km wewe haifai. Kwani ulishindwa kusubiri kila upewapo mshahara wako utenge ijapo 20K kwa ajili ya betting na ikiisha unasubiri mwezi unaofuata?
 
Vipi tathmini yako betting imekutoa kimaisha au ndio majuto kama mleta uzi? Huko kitaa vijana huwaambii kitu kuhusu kubeti..
Binafsi kamari imekula hela zangu nyingi. Sio chini ya milioni 30.
Ila imenifanya niwe mtafutaji wa pesa.
Hata mjengo ninaomiliki ulitokana na juhudi za kusaka pesa baada ya kuliwa kwenye kamari.
Ninataka niache soon. I can do that
 
Betting ni Uraibu.. Ni Uraibu unaotibika.. Sijui kama hapa kwetu vipo vituo vya kutibu watu wenye Uraibu huu..

Ila mimi nilishindwa.. Kila anayebet unamsikia Dah Man U kanichania mkeka.. Nikajitahidi kuwatafuta wanaoshinda sikuwapata.. Nikajionea ujinga huu bora hela yangu nikavutie bangi..
 
Nafkir tabia ya betting kwa vjana una be caused by lack ya mchongo ktaaa

Kuacha kubet n jambo linaloezekana kbsa haswa kwa kjana kurdhka na kpato cha Kaz unayo fanya ila hata io Kaz ndg ukikosa Kuacha ndo bas tena😢
 
Kweli kabisa unavosema mtoa mada peer pressure kitu kibaya sana vichocheo vya marafiki.. mimi nilikua najua kabisa kamari sio kitu kizuri na nilikua sina shobo kabisa ila mshkaj wa karibu enzi tuko A level alipga hela akanunua Noka N series hizo tambo sasa..

Niliweka 2000 ya kwanza nikaliwa , siku ya pili nikaweka buku nikaliwa ndo ukawa mwisho wangu hadi leo! ila nakiri laiti ningekula ata elf 3 tu ningeendelea sana nashkuru kukosa mwanzoni
 
Dah we
Ndugu zangu

Kwenye jukwaa hili nimeshuhudia hadithi na mikasa mingi watu waliyokutana nayo kabla na hata baada ya kujiunga mtandao huu mwaka 2014 hivyo kwanza nijipongeze kwa kufikisha miaka 10 kwenye hili jukwaa na miaka yangu hii kumi napenda kutoa stori fupi ya maisha yangu ambayo ni ya kusikitisha niliyaiga kutoka kwa Rafiki yangu mmoja mwaka23/3/ 2017.

MAISHA YA KUBETI

Watu wengi wanaoingia kwenye mikwamo ya ulevi hawaingii kwa kupenda ila mara nyingi huwa ni externally forcing huenda ni vichochezi vya marafiki,mitandao ya kijamii,dhiki na mengineyo.

Nakumbuka nilikuwa ni mtu safi ambaye nilijiapiza kutojihusisha na kamari pamoja utumiaji wa bangi ila la haula bahati mbaya iliyoje kote nimepakanyaga lakini nimeweza kuacha bangi ila siyo kamari ambayo imenicost muda,kuniathiri akili,fedha,magonjwa pamoja na tabia.

Kama hamutambui Magonjwa mengi ya akili,moyo na mabadiliko ya tabia huchochewa na kuanzisha tabia hizi mpya mimi nakumbuka 2016 nilimaliza masomo yangu ya kidato cha 6 kama mtahiniwa wa kujitegemea baada ya kushindwa kulipa ada,namshukuru mungu nilifaulu lakini ndiyo kipindi ambacho niliadapt tabia mbaya ya uchezaji kamari ambapo Rafiki yangu alikuwa ni mwenye kuicheza na kunishawishi sababu alikuwa anapata vishilingi na kwa bahati mbaya maisha yangu mimi toka udogoni ni mabovu pesa ni ngumu kushika hivyo nikasema acha nijitafutie bahati.

Lahaulaaaaa!!!nilijiunga na mtandao wa m-bet nilipigwa kila siku basi ikafika kipindi nikaanza kuhudhuria meridiani pale magomeni mkabala na mwendo kasi kwa siku ya kwanza niliweka 500 nikaweka odd ndogo nikala 4500 nikasema hapa mambo fresh,basi tangu hapo nilikuwa napigwa tu,kila navyopata pesa naenda kuongeza napigwa pesa yote na sikuwahi kuvuka hata kiasi cha 10,000.kuna siku nilibet PM bet nikala 15,000 ebwaa eeeh nikasema nicheze visual throne nikagongwa yote basi tangia hapo napigwa tu.


NIMEPATA KAZI YA KUUZA DUKA(2017)
Mwanzoni kabisa nilipata kazi ya kuuza duka xxxxxx basi ilitokea tu!bahati jamaa wa duka aliniamini sana,ila kwa bahati mbaya kamari ilivunja uaminifu nilikuwa kila usiku nikifunga duka hua naenda kubet thrown visual ya mpira nililiwa pesa ya watu mpaka nikawa najilaumu na kuapa viapo vyote kuwa nitaacha ila wapi!!.

Kibaya zaidi,nilikuwa natumia pesa ya dukani kila siku 20,000-30,000/= kuzani nitarejesha lakini wapi na mshahara wangu ulikuwa 90,000/= ilitokea siku nikafunga duka ili niende kufanya kitu fulani mkononi nilishika 60,000/= sijui ndiyo shetani akanipitia nikajiona naelekea thrown kucheza visual aiseee niligongwa yote yaaani unaweka mpira nyau nyau, dog hamna kitu,namba hamna daaaah toka siku hiyo nikajiapiza tena kuwa sitacheza ila wapi.

siku inayofata jamaa akaja dukani tukapiga hesabu kiasi kama cha 235,000/= kilipungua ndani ya siku chache tu, nikataka kupelekwa polisi ila huku na huku pesa ikalipwa..sikuwa mwenye kupata chochote ila nafsi yangu tu ni ngumu kuacha.

niliachishwa kazi,nilijutia ila niliendelea basi ilitokea home napewa pesa naenda kwenye kamari naliwa alafu nasingizia imepotea dah maisha yalikuwa ni ya kipumbavu sana.

Ukweli nikipiga hesabu ya pesa nilizotumia kwenye kamari naweza kupata 6,000,000/= mpaka kufikia sasa sina hata kiwanja wala chochote nipo nipo na bado nacheza tu.


WADAU MIAKA 8 BILA MAFANIKIO KATIKA KAMARI,MISUKOSUKO YA MAISHA KISA KAMARI


UKWELI BADO NACHEZA JAPO NIMEPEVUKA NIMEACHA MAMBO YA VISUAL ILA NINGELIKUWA RAIS NINGELIFUKUZIA MBALI HIZI KAMPUNI ZA KUBETI SIYO POWA VIJANA WANAKUWA WAGOJWA WA AKILI,MWILI N.K SABABU YA KAMARI


MWISHO UZI USIUNGANISHWE
Dah pole sana mkamaria! We acha tu mi nimesumbuliwa na huu uraibu kwa takribani miaka kadhaa hv. Nilianza kama kimasihara hivi ..nilibeti 15000 nikala 48000 ...first day! Ndio ilikuwa ufunguzi rasmi. Nikaona hii ndio shortcut ya kutoboa ..aisee nikaja kupoteza pesa nyingi aisee. Kisaikolojia nikawa nimeharibikiwa, kiuchumi na mahusiano yangu kijamii yakawa hayaeleweki. Inafika kipindi unajilaumu sana kuijua kamari ila bado unashindwa kujinasua.

Ila namshukuru sana Mungu...kwasasa nina miezi kadhaa sijishughulishi na masuala ya kamari.

Niliamua kutoka moyoni nikamuomba Mungu kwa dhati aninasue. Nilifuta apps zote za mipira na live score, nikafuta apps zote za kubeti. Kila kampuni ya kubeti nilikuwa na account. Nimezifuta zote.

Na hiyo haitoshi nikafuta vitabu vyote vinavyofundisha mbinu mbalimbali za kubeti. Kifupi sijishughulishi tena na kamari. Na sas hivi naona afya yangu ya akili ikiimarika siku baada ya siku.

Kwani ilifika kipindi silali usiku mzima mimi nabeti mechi za akerica kaskazini n kusini, asubuhi nipo ligi za japan,australia,newzealand...mchana nipo ligi za china,iran,india,kazakhstan..jioni nipo ligi za uturuki,uarabuni, uingereza,ujerumani,n.k ndio ilikuwa cycle yangu.

Nilikuwa mtu wa kujitenga peke yangu tu, kazi kubwa ilikuwa ni kubeti tu.

Sasahivi namshukuru sana Mungu ,im clean from dat demon.
 
Back
Top Bottom