Uraia pacha kwa taifa changa ni kifo kuliko faida

Uraia pacha kwa taifa changa ni kifo kuliko faida

sasa uraia pacha utazuia vipi hiyo kadhia unayisema> Uraia pacha utazuia vipi kukua kwa matabaka hayo? hamna hoja za maana aisei.
Watu wawe huru kwenda kusaka maisha ko kote wanakotaka bila kuogopa kupoteza uraia wao. Nchi kama Marekani kuna fursa nyingi sana huwezi kuzipata bila kuwa raia. Watajikomboa huko na wewe huku utakuwa umejipunguzia mzigo na nchi yako itapumua.

Kuwarundika tu hapa hao vijana huku hawana cho chote cha kufanya eti unaogopa wakienda huko sijui watakuwa magaidi ni mawazo finyu sana maana visababishi vya ugaidi vipo na vinajulikana.

1. Tupambane na ufisadi ili raslimali zetu ziwafaidie Watanzania wote. Hii ndiyo njia bora zaidi ya kuzuia ugaidi wa ndani (na hata wa nje)

2. Tuunde programu na mifumo mizuri itakayowasaidia vijana wetu kujiajiri na kufanikiwa (mf. Kuwafutia kodi kwa miaka miwili ya mwanzo wakianzisha kibiashara...)

3. Tuwaache waende huko nje wakatafute maisha bila kuogopa kupoteza uraia wao
 
Wakuu Tanzania hatuzungumzii uraia pacha bali hadhi maalum ( Non Resident Tanzanian)
 
Akikuletea magonjwa nayo ni haki.
Kama analiwa na wengine wasiolipia mahari ana tofauti Gani na Malaya wa kununua.
Mwanamke anaejua maana ya ndoa hawezi mvulia chupi mtu asiyemtolea mahari
mahari sio bei halisi ya mkeo. Mahari haiondoi haki za mwanamke, na ndio maana kwenye sheria kama mkeo ameliwa unachoweza kukifanya ni kumuacha la sivyo utatakiwa uonyeshe hasara uliyoipata kwa mkeo kuliwa ili ufidiwe. Mkeo akiliwa wewe unapata hasara gani? Onyesha...
 
Njia nzuri ni ukimaliza kuwa manamba huko, ukiona umezeeka na pesa unazo ukane uraia wa huku ili rudi huku uwe raia. hata hivyo utakuwa umetenda dhambi kubwa kwakuwa nguvu zako zote za ujana umezitumia kuijenga nchi nyingine ya ugenini sasa unarudi kula usichokipanda. Kodi yako imejenga barabara za marekani na kodi zetu sisi zimejenga barabara za tanzania, unarudi huku kufanya nini? fia hukohuko na uzikwe hukohuko ulikokujenga, hapo veepe??
Siyo kweli. Huna uelewa mpana wa jinsi uchumi wa dunia unavyofanya kazi. Na pengine unaongea tu ili kujifurahisha utafikiri wewe ndiyo mmiliki wa nchi hii.

Diaspora wetu hutuma mabilioni ya dola kila mwaka na wengi wao husaidia kuinua familia zao huku nyumbani (Data zipo BOT). Wanapaswa kuungwa mkono katika juhudi zao hizi ndiyo maana katika baadhi ya nchi zinazoongozwa na viongozi wanaoona mbali, ni rahisi sana kupata pasipoti ili uende huko unakokutaka maana ukifanikiwa huko mara nyingi na nchi yako pia itafaidika ama kwa remittances au kuinua familia yako (na hivyo kuipunguzia serikali ya CCM mzigo!)

Diaspora siyo adui wa taifa lako. Adui mkuu wa taifa lako ni viongozi wako ambao siyo wazalendo wanaofisadika kupindukia wao na familia zao na marafiki bila kujali Watanzania wenzao wanaishije. Hangaika na hao kama kweli unaitakia mema nchi yako. Hao ndiyo watakuletea ugaidi na siyo diaspora. Ukishindwa (ulishaambiwa) hamia Burundi ukachukue uraia pacha huko 😁
 
Wakuu Tanzania hatuzungumzii uraia pacha bali hadhi maalum ( Non Resident Tanzanian)
Why hadhi maalum? Yaani, mtu ameukana uraia wake hadharani ili aweze kuosha magari (car wash) marekani na wala hana fedha za kuwekeza tanzania na wala kodi yake haidaidii kuijenga tanzania kwa vyovyote vile kwanini apewe hadhi maalum? au ni nani mwenye sifa zipi za kupewa hadhi maalum? Kumbuka ni kodi za raia zinazotumika kuijenga na kulinda nchi, mtu ambae kodi yaKE haiji huku ataidikaje na tanzania? Labda kwa mwekezaji tu wa kuazia mtaji wa kiasi fulani
 
mahari sio bei halisi ya mkeo. Mahari haiondoi haki za mwanamke, na ndio maana kwenye sheria kama mkeo ameliwa unachoweza kukifanya ni kumuacha la sivyo utatakiwa uonyeshe hasara uliyoipata kwa mkeo kuliwa ili ufidiwe. Mkeo akiliwa wewe unapata hasara gani? Onyesha...
Akikupa ukimwi,mtoto wa nje ni faida ipi unapata
 
Unahisi wewe ndio mna Amani kuliko wengine wote? Jiranganye tu

Kinachokusumbua wewe ni wivu wa kijinga
wivu wa nn nami ningetaka ningebaki hukohuko ng;ambo au naweza kuja hata kesho kuchua uraia na kukana wa kwangu? kumbuka mm pia ninaajilika hukom pia
 
Akikupa ukimwi,mtoto wa nje ni faida ipi unapata
Kama hajafaanya hivyo? amekula tu bila kuacha ukimwi wala mtoto wewe umeingia hasara gani ili ulipwe? maana kutembea na mke/mume wa mtu ni kosa la madai sio jinai.
 
Hizo ni fikra na maoni yako
Kwanini wapitishe mali na nyie mmelala?
Unajua fika kuwepo au kusiwepo uraia pacha wizi ni kwa sababu za tamaa za wengi ambao wanakubali hata silaha ziingie au zitoke kwa thamani ndogo

Bila kupambana na Rushwa na kutokomeza nakuapia kuanzia maliasili atakula chake, uhamiaji atakugongea muhuri utoke na hata polisi atakula chake hata kama gari inaenda upande na imebeba watu 65

Uraia pacha una faida nyingi tu ila wewe umeona wizi tu wakati wizi umetamalaki hata bado hamna hata reserve za dhahabu wakati mnachimba dhahabu kila leo
Hao marais wote uliowataja ni wale wale tu
Kama watu wanachaguliwa kwa kuhonga halafu wanaenda kupiga magoti ya kinafiki makanisani unategemea nini

Nani aliehimiza katika wote hao pamoja na mawaziri wao wa fedha kuweka Dhahabu Bank kuu?
Algeria wanaongoza kwa gold reserves ya 174 metric tons ambayo ina thamani ya $10b
Sisi tuna nini cha kujivunia leo
Hela zinapigwa na hao hao viongozi na kuzipeleka China sio raia wa kawaida
Sasa hao wana uraia wa China?
 
Hizo ni fikra na maoni yako
Kwanini wapitishe mali na nyie mmelala?
Unajua fika kuwepo au kusiwepo uraia pacha wizi ni kwa sababu za tamaa za wengi ambao wanakubali hata silaha ziingie au zitoke kwa thamani ndogo

Bila kupambana na Rushwa na kutokomeza nakuapia kuanzia maliasili atakula chake, uhamiaji atakugongea muhuri utoke na hata polisi atakula chake hata kama gari inaenda upande na imebeba watu 65

Uraia pacha una faida nyingi tu ila wewe umeona wizi tu wakati wizi umetamalaki hata bado hamna hata reserve za dhahabu wakati mnachimba dhahabu kila leo
Hao marais wote uliowataja ni wale wale tu
Kama watu wanachaguliwa kwa kuhonga halafu wanaenda kupiga magoti ya kinafiki makanisani unategemea nini

Nani aliehimiza katika wote hao pamoja na mawaziri wao wa fedha kuweka Dhahabu Bank kuu?
Algeria wanaongoza kwa gold reserves ya 174 metric tons ambayo ina thamani ya $10b
Sisi tuna nini cha kujivunia leo
Hela zinapigwa na hao hao viongozi na kuzipeleka China sio raia wa kawaida
Sasa hao wana uraia wa China?
Huyu hajui anachokisema. Leo hii mtu ye yote akiwa na pesa anaweza kupata kitambulisho cha NIDA, cha utaifa na hata pasipoti kabisa. Kuna mtu ana uchungu na nchi hii? Wasomali wengi tu wanapata namba za NIDA na pasipoti. Yeye eti anahangaika na diaspora! Eti wataleta ugaidi 😁

Adui mkubwa wa nchi hii ni UFISADI na kukosa uzalendo!
 
Huyu hajui anachokisema. Leo hii mtu ye yote akiwa na pesa anaweza kupata kitambulisho cha NIDA, cha utaifa na hata pasipoti kabisa. Kuna mtu ana uchungu na nchi hii? Wasomali wengi tu wanapata namba za NIDA na pasipoti. Yeye eti anahangaika na diaspora! Eti wataleta ugaidi 😁

Adui mkubwa wa nchi hii ni UFISADI na kukosa uzalendo!
Nimemshangaa sana aisee
Labda haishi hapo
Watu masikini huwa wanajadili na kukataa vitu vya maana
Yaani hoja muflis ni mtu anaposema eti usalama wa nchi utakuwa matatani

Nimekaa nje ya bongo zaidi ya miaka 40 na ninaipenda nchi yangu
Ila nikirudi kutembea unaona kabisa unaweza ukapata chochote kwa hela yako tu
Watu wanapita wanaingia na siku 10 tu analetewa passport nyumbani
Sio Bongo tu hata iwe Egypt ni bure kabisa
Anahangaika na diaspora badala ya kuhangaika na hao anaowahonga mambo yake yanyooke

Diaspora ina faida nyingi na tutafaidi bila kuwa na uwoga wa kigaidi wala nini

Nimewahi kumiliki passports aina Tatu za halali katika maisha yangu na leo ninayo yenye hadhi na nguvu kubwa duniani
Ntarudi home na nitaishi kama mdigo na hakuna wa kunijua na ninaweza kukaa miaka
Sasa nirudi kufanya ugaidi ili iweje? Kwa ndugu zangu
Mawazo muflis kabisa hayo

Bro angehangaika na rushwa kwanza iliyoota mizizi mpaka Rais anasema wachukue za brush au wale kiasi
 
Naunga mkono.

Sikubaliani kabisa na suala la uraia pacha, hasara ni nyingi zaidi kuliko Faida.
Kamwe Serikali isikubali kuingia kwenye mtego wa uraia pacha.

Wewe kama raia wa Tz umeamua kuukana uraia wako baki hukohuko.
 
Hoja zenu za uraia pacha Tanzania hazina mashiko, unataka kufanya nini, kuleta nini na kuidia nini cha maana kama ukiwa na uraia pacha? una hela kiasi gani za kuwekeza huku zinazohitaji mpaka uwe na uraia pacha?

Mifumo yetu humu ndani ya nchi haisomani, sembuse huko nje ya nchi? Huku watu wana vyetu vya kuzaliwa na data zake, kitambulisho cha taifa na data zake, kitambulisho cha kupiga kula na data zake, driving license na data zake, NSSF na data zake kwa mtu huyohuyo, bank kuna data zake na kwa mwajili kuna taarifa zake kwa mtu huleyule. Msituongezee shida.
All that you have explained shows how narrow-minded you are about dual citizenship. Does a Tanzanian need to be solely Tanzanian for investment? How are you questioning the choices of those who have been able to travel and live in other countries? Who are you by the way?
 
Sasahv hilo lango la kupitia wezi limefungwa?
 
Kelele za kudai uraia pacha zinatokana na ulafi wa watawala. Hao ndiyo wanaopush hii ajenda ya urai pacha, wengine ni front tu, diaspora ni front tu, nyuma yao wapo hawa viongozi mafisadi.
 
Back
Top Bottom