Uraia pacha kwa taifa changa ni kifo kuliko faida

Uraia pacha kwa taifa changa ni kifo kuliko faida

Uoga wenu ndio maana ya huu umaskini

We fanya kazi kwa bidii Sana, kuwa muungwana, kuwa mstaarabu, kuwa mkweli acha unafiki utafanikiwa bila kuogopa sijui taifa changa sijui matakataka gani.

Yaani unaogopa raia pacha kwa watanzania wasiozidi 5000 dunia nzima wakati unaiba kura, unaiba mali ya umma, unafisadi hadi hela ya dawa vijijini, wanyama wanauzwa wazima wazima kwenda Dubai na kuuwa mimamba ya mita 10 una akill kweli?

Mwambie huyo. Hapa kwenyewe hatuna uraia pacha ila watu wanaiba kama kawa
 
Hiyo ni kidogo sana, ugaidi unazaliwa na mataifa ya magharibi na marekani pale yanapotaka rasilimali zenu. Mkigungua rasilimali nyingi ambazo wao hawazifaidi basi jiandaaeni ni ugaidi wa kupandikiziwa. Osama, Sadam, Gadaffi na wengine kule DR Congo, Niger, Afrika ya kati, Sudan kusini, sudan, Msumbiji, Nigeria na kwingine kote kwenye mali nyingi wazungu watapandiza magaidi. Na sifa kuu ya mtu anaefaa kutumiwa kuwa gaidi lazima awe na uraia wa nchi husika na uraia wa nchi nyingine ya wanaomtuma. yaani ni rahisi kuingia kwenye nchi husika kwakuwa anaifahamu vizuri na hamna mashaka nae. Wanaoeneza ushoga huku kwetu ni raia wenzetu wenye passport za kwetu ambao wamerahisishiwa kuingia mataifa yanayodhamini ushoga. Yaani wao ni rahisi kupewa visa za nchi hizo na saa nyingine wamepewa passport za siri za nchi hizo.
Chunguza sana,wenye uraia pacha ndio wengi ni magaidi,wacha hawa wanaotumiwa kutekeleza ugaidi,kuna wanaoingia kutoka nje,wana uraia pacha au ni raia wa nchi husika,lakani ana passport ya UK au Amerika au kokote,imeandikwa kazaliwa Somalia,wakati ni mtanzania,hata kisomali hajui,wapo mpaka the wanawake,kutafuta wenyeji wafanye ugaidi kwa kuwashawishi,kuwalipa pesa,wafanye ugaidi.
 
Hapo tatizo sio uraia pacha wala uchanga wa nchi bali tatizo liko kwa wale waliopata dhamana yakuongoza hii nchi toka mkoloni hadi leo bado wameshindwa kuweka mifumo thabiti yakuondoa hizo kasoro ulizozianisha.Na hizo akili kamwe hawawezi kua nazo ndio maana option kwao ni kukwepa hiyo hoja badala yakutafuta ufumbuzi.Mapungufu yote uliyoyataja yanarekebishika.Sasa tunatakiwa tusubiri miaka mingapi ili tuje tupate serikali itakayolinda rasilimali za nchi na mambo mengine yenye manufaa?..
 
Kuna sababu dhaifu sana za kuhalalisha uraia pacha. Nchi zetu hizi zina mifumo legelege sana ya kudhibiti uhalifu na wizi wa mali na rasilimali za taifa.

Hata bila uraia pacha mali zetu zinaibwa na watanzania na viongozi wetu na kwenda kufichwa nje ya nchi (ulaya, marekani na Asia (Dubai, oman, Singapole, Malaysia, nk) itakuwaje kama wezi hawa watakuwa na fursa ya kuwa na uraia pacha?

Hata nchi ndogo/changa zenye uraia pacha hatuoni faida za maana wanazozipata kwa kuwa na uraia pacha zaidi ya kuongezeka kwa wizi na utapeli ndani ya nchi zao tu. hata nchi zilizoruhusu uraia pacha (diaspora) naazo ni masikini pia, zinapigana, na wizi mwingi na mkubwa wa rasilimali zao. hatuna cha kujifunza kutoka kwa nchi hizo.

Faida tutakayopata kama tutaruhusu uraia pacha ni ndogo sana by far kuliko hasara tutakayoingia. Sababu ziliwafanya Nyerere, karume, mzee Mwinyi, Mkapa, Kikwete na magufuli kuukataa Uraia wa nchi mbili bado zipo hadi kesho.

Kuna watu wanatoa sababu dhaifu sana za kuruhusu uraia pacha za kupata wachezaji wa mpira na wawekezaji, ni za kipuuzi kabisa. Tutapanua lango la kupitia wezi wa mali zetu na kutumia barabara pana kuzisafirisha huko Swiss na visiwa vya Jersey kwa urahisi kabisa mchana kweupe.

Siungi mkono upuuzi huu.
Wewe ni mjinga katika wajinga wa Tanzania wewe ni mpumbavu hasa huna uelewa wala huna vision .Uraia pacha haukimbiliki lazima watafanya tu kwa sababu Tanzania siasa zake zinaendesha na Bwana wake Kenya .Kenya ikifanya kitu lazima TZ watafanya tu hata kama watachukua muda hizo fikra ni za kimasikini.
 
Kwenye hii thread kuna watu wako serious sana. Unfortunately mwenye thread yake either hayuko serious or haelewi 😂 😂
 
Mifumo gani kaka. Taifa makini haliwezi kutengeneza mifumo inayowarahisishia vijana wake wenye nguvu, ujuzi Na maarifa (nguvukazi) iondoke nchini. Mtawala kama huyo atakuwa ni mpumbavu mkubwa. Mchi inajengwa Na vijana wake sio wazee. Tunahitaji vijana wetu jeshini, kwenye kilimo, uvuvi, ufugaji, viwandani Na kwenye huduma mbalimbali Na hatimae walipe kodi kwa maendeleo ya taifa lao.
Sawa bosi!

Endeleeni kufyatua maelfu ya wahitimu na kuwarundika mitaani bila ajira wala misaada yo yote ya kimfumo huku mafisadi yasiyozidi 50 yakiiba raslimali zote na kujirundikia mali bila huruma. Siku moja mtakipata tu mnachokitafuta.

I am out 🙏🏿

 
Uchanga upo ukilinganisha na nchi km UK, USA n.k. nchi iliyopata uhuru mwaka 1013 utalinganisha vp na ya 1961? Tofauti ipo wazi ukizingatia hao waliokutangulia hakupi fursa zaidi ya kukukandamiza
Hata kama ikiisha miaka elfu moja kwa akili hizo hizo bado tutajihesabu ni wachanga maana nchi hizo ulizozitaja zilitutangulia kupata uhuru.Umri wa mtu mzima ni miaka Ishirini,kama miaka yetu ilishavuka huo umri hakuna uchanga hapo tatizo ni kujipanga.
 
Niambie mfano wa taifa dogo kama letu ambalo linafaidika sana na uraia pacha kiasi cha kutamani kuiga maisha na hali yao kiuchumi, kijamii na kisiasa. Mnatafutia majizi njia nyepesi ya kutoroshea nje mali zetu.
Tatizo huna exposure ... nenda ghana ukaone diaspora wanavyofanya mambo makubwa

Wanajenga malls, wana viwanda , migahawa na wamewekeza heavily kwenye kilimo

Ukienda ghana especially accra utaona expensive cars kila sehemu unayoenda hao ni diaspora wamechangamsha uchumi na kutoa ajira kwa watu wengi sana

Sasa nyie endeleeni na ujima wenu wa kukataa uraia pacha huku nchi ikiendelea kuwa maskini wa kutupwa.
 
Kuna sababu dhaifu sana za kuhalalisha uraia pacha. Nchi zetu hizi zina mifumo legelege sana ya kudhibiti uhalifu na wizi wa mali na rasilimali za taifa.

Hata bila uraia pacha mali zetu zinaibwa na watanzania na viongozi wetu na kwenda kufichwa nje ya nchi (ulaya, marekani na Asia (Dubai, oman, Singapole, Malaysia, nk) itakuwaje kama wezi hawa watakuwa na fursa ya kuwa na uraia pacha?

Hata nchi ndogo/changa zenye uraia pacha hatuoni faida za maana wanazozipata kwa kuwa na uraia pacha zaidi ya kuongezeka kwa wizi na utapeli ndani ya nchi zao tu. hata nchi zilizoruhusu uraia pacha (diaspora) naazo ni masikini pia, zinapigana, na wizi mwingi na mkubwa wa rasilimali zao. hatuna cha kujifunza kutoka kwa nchi hizo.

Faida tutakayopata kama tutaruhusu uraia pacha ni ndogo sana by far kuliko hasara tutakayoingia. Sababu ziliwafanya Nyerere, karume, mzee Mwinyi, Mkapa, Kikwete na magufuli kuukataa Uraia wa nchi mbili bado zipo hadi kesho.

Kuna watu wanatoa sababu dhaifu sana za kuruhusu uraia pacha za kupata wachezaji wa mpira na wawekezaji, ni za kipuuzi kabisa. Tutapanua lango la kupitia wezi wa mali zetu na kutumia barabara pana kuzisafirisha huko Swiss na visiwa vya Jersey kwa urahisi kabisa mchana kweupe.

Siungi mkono upuuzi huu.
Bro umeongea fact ila bado haujatupatia mofano halisi ya hizo nchi
 
Kuna sababu dhaifu sana za kuhalalisha uraia pacha. Nchi zetu hizi zina mifumo legelege sana ya kudhibiti uhalifu na wizi wa mali na rasilimali za taifa.

Hata bila uraia pacha mali zetu zinaibwa na watanzania na viongozi wetu na kwenda kufichwa nje ya nchi (ulaya, marekani na Asia (Dubai, oman, Singapole, Malaysia, nk) itakuwaje kama wezi hawa watakuwa na fursa ya kuwa na uraia pacha?

Hata nchi ndogo/changa zenye uraia pacha hatuoni faida za maana wanazozipata kwa kuwa na uraia pacha zaidi ya kuongezeka kwa wizi na utapeli ndani ya nchi zao tu. hata nchi zilizoruhusu uraia pacha (diaspora) naazo ni masikini pia, zinapigana, na wizi mwingi na mkubwa wa rasilimali zao. hatuna cha kujifunza kutoka kwa nchi hizo.

Faida tutakayopata kama tutaruhusu uraia pacha ni ndogo sana by far kuliko hasara tutakayoingia. Sababu ziliwafanya Nyerere, karume, mzee Mwinyi, Mkapa, Kikwete na magufuli kuukataa Uraia wa nchi mbili bado zipo hadi kesho.

Kuna watu wanatoa sababu dhaifu sana za kuruhusu uraia pacha za kupata wachezaji wa mpira na wawekezaji, ni za kipuuzi kabisa. Tutapanua lango la kupitia wezi wa mali zetu na kutumia barabara pana kuzisafirisha huko Swiss na visiwa vya Jersey kwa urahisi kabisa mchana kweupe.

Siungi mkono upuuzi huu.
Yaani umeniacha kapa la kuongeza. Umeeleza vizuri sana..heko mkuu
 
Aliyewaambia watanzania ni matajiri sana, kila mtu anawaonea wivu na anataka kuwaibia aliwajaza ujinga wa kiwango cha lami. Mmekua mazuzu na woga kama kunguru. Kila kitu mnaogopa
Kama watanzania ni masikini unataka uraia pacha wa nini? kaa na uraia wa sehemu tajiri. Sisi huku ni masikini jeuri. Ukifungua mlango wako wataingia wema na wezi, na shida yetu sio wema bali wale wezi wa ndani na nje. Ukikarbisha mgeni nyumbani hakikisha kuwa mwenyeji unakuwa wa mwisho kwenda chumbani kulala na funga mlango na nenda chumbani na ufunguo wa milango ya kutokea ili kuhakikisha kuwa mgeni hakuibii na kutoroka. Hatuwezi kuruhusu uraia pacha eti ili tupate read made wachezaji mpira wa timu yetu ya taifa (non sense) badala ya kuwekeza kwenye soka la watoto na vijana.
 
Serikali iko tayari kuruhusu wadada kwenda kufanya kazi za ndani nje, kuliko kutoa uraia pacha. By the way Nikipata gape siwezi kuishi bongo, imagine unasoma huku unawaza kama utaweza kuishi maisha ya standards, maana no ajira, no mitaji🚶🚶
 
Amani iliyoko Tanzania hats marekani haiko Na haipatikani. Hakuna amani kabisa kufa ni kitu cha kawaida kabisa, upweke (loneliness) mkubwa, madeni mengi, homeless mengi, wenye stroke na stresses wengi, kila kitu ghali sana.
Unazungumzia amani au maisha bora au nini hasa unachozungumzia maana nimeshindwa kukuelewa?
 
Huna akili.

Nimejisikia vibaya sana kukwambia “huna akili”
Ila nilikuwa sina jinsi.
jizi ni jizi tu, haliwezi kujibu hoja kwa hoja hiyo inafahamika. Sababu ziliwafanya Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli wasiruhusu uraia pacha wala hata kuujadili zingali zipo valid mpaka leo. Wahindi wengi hapa wana uraia pacha, fedha zao nyingi zinachumwa Tanzania na kwenda kujenga nchi za canada, uingereza, marekani kwasabu ya urahisi wa kuingia na kutoka kama raia. Wanahodhi ardhi yetu hapa na kwenda kuikopea canada.
 
Aliyewaambia watanzania ni matajiri sana, kila mtu anawaonea wivu na anataka kuwaibia aliwajaza ujinga wa kiwango cha lami. Mmekua mazuzu na woga kama kunguru. Kila kitu mnaogopa
Kuna huu ujinga wa kukaririshwa amani kana kwamba dunia nzima ipo kwenye vita kama Ukraine au Gaza ila Tanzania tu ndio ina amani.
 
Back
Top Bottom