Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Kupitia hio mikakati ya kushughulika na vitisho ndivyo baadha ya mambo yakawa yanaichafuwa nchi ndani na nje.
 
Wote hovyo ni wachumia tumbo hamna mzalendo hapo. Uzalendo wao ni wa porojo tu
Wafanyakazi,wakulima na wafanyabiashara wamechoka,hawako tayari kusikiliza porojo hizo za uzalendo uchwara kutoka kwa watu wachache waliojimilikisha hatimiliki ya kufanya maamuzi.
 
Kwa JF hili haliwezi kupita hivihivi. Ni nani anaweza kupeperusha kwa ufasaha bendera ya CCM 2020. Tusizingatie kigezo cha kuwa na dola. Tuzingatie uwezo wa kuongoza na vision ya Tanzania tunayoitaka


Dr.Membe anayepigiwa chapuo kuleta mabadiliko ya makubwa kwa chama


Rais Magufuli
 
Na ndio itazidisha chungio la kuchekechea kuwa kali kwa watakaopitishwa kwenye CC na NEC, hapo ndio utajuwa hicho kitisho kilivyo cha juu sana
CC na NEC wakifanya hilo kosa la kushindanisha bwana mkubwa na wa gombea wengine hilo ndolitakua kosa la karne......
 
Legelege sana huyo amesha shindwa kabla haja anza
Uzee umemkubali haraka sana
 
Bora ccm watupe huyu membe kuliko huyu anayejiita kichaa maana najua upinzani tutaporwa ushindi
 
Kwa JF hili haliwezi kupita hivihivi. Ni nani anaweza kupeperusha kwa ufasaha bendera ya CCM 2020. Tusizingatie kigezo cha kuwa na dola. Tuzingatie uwezo wa kuongoza na vision ya Tanzania tunayoitaka
Unalinganisha mafi na dhahabu,

Membe for presidency
 
Ninaota na nitafuraha kama ndoto yangi itakuwa kweli. Na bila kuwa kweli kutatokea na mdororo wa kisiasa 2020.

Ninaota Membe kuitikisa CCM na kama CCM wakichulia hasira ya pata potea na Membe na Lowasa wakafuta tofauti zao wakawa pamoja katika chama cha ACT wazalendo (kwa maana Chadema wapo bizi na makesi na wamechoka kiana) Tanzania itainuka kwa nguvu na shangwe ya muelekeo wa utawala bora na kuondokana na matamko na udicteta uliopo.

Membe akigombea akiungwa mkono na Lowasa na wenzanke na akina Nape, Mwigulu na wengine wakishadidia, Kweli niwaambie 2020 patachimbika na watu wengine wanaojiona ni miungu watu watajua kuna watanzania.

Membe shime, Dedede kazia hapo hapo.

Wakati Mwingine tuseme Ukweli. kwa sasa bora kuwe na fisadi Membe kuliko tulivyo sasa (NB: Fisadi Membe kwa maana Yeyote agaist CCM ni Fisadi na Mwizi - Kwa mtazamo wa CCM wengi)
 
CC na NEC wakifanya hilo kosa la kushindanisha bwana mkubwa na wa gombea wengine hilo ndolitakua kosa la karne......

Hawataki kufika huko. Haya yanayoendelea ndio namna bora nadhani. Wakati utaamua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…