Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Hii mbinu ya UPINZANI kumchokonoa Yohana na kufarakanyisha Chama Tawala kitoke katika malengo yao ni ya aina yake!

Chama tawala kilianza kuwafarakanyisha CHADEMA humu kwa nyimbo za kumtia Mbowe katika Kiti, na kushindwa jamaa nao wamejibu kwa njia ile ile kuwafarakanyisha CCM na Mwenyekiti.

Wanajua Chair hana uvumilivu, atajibu na wao watakula alama!

Siasa bwana!....piga nikupige
 
Hiyo heshima imepotelea wapi au imetoweka kwenda wapi hadi airudishe huyo membe.

#histimehadpassedaway
 
Huyo jamaa sijawahi mkubali kuwa kiongozi wa nchi hata siku moja....nafikiri amekuwa over_rated mno
Amekuwa overrated kivipi? Kwani nafasi alizotumikia hakuzitendea haki?
 

Hivi hizi Hela / Pesa ambazo Membe na Kikundi chake cha ' Propaganda ' anazowapeni hadi tokea juzi, jana na leo naona kila mara mnafurika tu hapa Kumuanzishia ' Threads ' kwanini asizikusanye zote na awarudishie Familia ya Hayati Rais wa Libya Muamar Gadhaffi? Mwambieni kabisa kwamba ile ' laana ' ya yule Balozi wa Libya nchini Tanzania aliyefia Ubalozini haitomuacha salama na ni bora aanze ' Kutubu ' kama siyo ' Kuungama ' mapema. Hata afanye vipi na aende wapi Bernard Camilius Membe hawezi na hana uwezo wa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ikitokea akawa basi kwa mara ya Kwanza Tanzania jiandaeni kushuhudia Kundi la Waasi litakaloongozwa na ' Shadow General ' au ' Warlord ' aitwae GENTAMYCINE na nina uhakika ' Utawala ' wake hautokaa / hautodumu / hautochukua muda mrefu na hatimaye sasa Watanzania wote mtakuwa chini ya Uongozi wa muda wa GENTAMYCINE ambapo nitaitisha Uchaguzi mpya na halali na Mshindi ambaye nitaona anafaa Kuwaongozeni Watanzania nitamkabidhi nchi na Mimi kurejea zangu Kutiririka na Kuserereka hapa Jamvini JamiiForums kama kawaida.
 
Hata Membe mwenyewe akiiona hii thread atashangaa ulikoyatoa haya! Anyway, kwa sisi tuliomo humu JF muda mrefu, hatushangazwi na hizi
Hata Membe mwenyewe akiiona hii thread atashangaa ulikoyatoa haya. Anyway, kwa sisi tuliomo humu JF muda mrefu, hatushangazwi na hizi "White Elephant Inventions" zenu.Mwaka2000 mlisema humu humu kuwa Mkapa atatolewa. Haikuwa!
Mwaka 2010 mlisema Kikwete atatolewa. Haikuwa!
Hivyo, tuna haja gani ya kushangaa mnaposema mwaka 2020 hatatolewa? Tuna haja gani ya kutoamini kuwa Rais Magufuli ataendelea hadi 2025 na zaidi ikibidi?
 
umeona jina membe tu umewashwawashwa. Tulia hii game haiitji hasira.
Wewe ndio unaleta hasira hili game kwangu la kitoto. Unajificha kwenye ujinga IQ hata unajifanya great thinker wakati ni mpuuzi kama mchuzi.
 
Amekuwa overrated kivipi? Kwani nafasi alizotumikia hakuzitendea haki?
...kwa hiyo wewe na akili zako kabisa unaamini Membe anaweza kuwa rais wa nchi hii mzuri ?!!.....hizo nafasi alizobebwabebwa ndio kipimo mnachompimia..?
....hamko serious kabisa
 


Labda kupitia CUF,ACT-Wazalendo au CDM
 
Sawa tumezpokea

Japo sielewi hii morale ya kumsifia Membe kwa kasi huku mitandaoni mnaitoa wapi, naamini sio bure kuna cha ziada
Mkuu Korosho ndiyo imeiua haya yote! Yamkini kuna kitu kweli kafanya nyuma ya pazia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…