Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

“Binadamu wote ni ndugu zangu, Afrika ni moja”

Kwako Bernard Kamilius Membe

Nimekusikia muda mrefu toka wa wandani wako kua una mkakati wa kuingia magogoni 2020 iwe ndani ya CCM au nje ya CCM!

Binafsi sishangai wala kukukatisha tamaa kwakua umenuwia kuusaka Urais kwa njia halali kabisa yenye misingi ya kisheria.

Pili natambua umeamua kuwania ili Kumsaidia Rais wa sasa na mwenyekiti wako kwakua amekiri hadharani kuwa hii kazi ni ngumu mno kwake na haiwezi... alifika mbali zaidi kwakusema hii kazi alisukumiziwa tuuu.... aliibipu ikampigia hivyo kuleta picha kwamba aliingia huku hajui anakwenda kufanya nini. Hii imeonekana kwakuwa hadi sasa hana focus wala Vision!

Ushauri wangu: kama unataka urais wa nchi hii lazima ufanye patano la agano na Edward Lowassa!! Bila Lowassa 2015 leo hii Magufuli angekua anavua samaki Kwao Chatto!! Ni Lowassa aliyemfanya JK awe Rais 2005 na ni Lowassa aliyemfanya Magufuli awe rais 2015 na wewe ukakosa!! Sina sababu yakuelezea kilichotokea kwakua unafahamu!!


Mwenzako Mzilankende amejipanga!! Sasa anaileta Team Lowassa miguuni pale!! Akina Sophia Simba soon watawekwa kwenye hatamu na akina Ole Millya! Sasa kama hii team haikuungi mkono sahau kabisa urais iwe 2020 au 2025!! Mlifanya makosa sana kuhitilafiana vinginevyo leo ungekuwa kwenye first class!!

Narudia tena uwe wewe.. January Makamba ama Ridhiwani Kikwete bila kuunganisha nguvu na laigwanani katu hamtatwaa madaraka ya juu ktk nchi hii.


Hivyo fanya harakati muunganishe nguvu!! Huku akiwepo Maalim Seif kule Mbowe huku Lowassa nakuhakikishia hata Magu akimweka mtoto wa kumzaa awe mwenyekiti wa NEC na kujaza ndugu zake hatafua dafu kama alivyoshindwa Yahya Jammeh aliyeweka ndugu wote tume ya uchaguzi na akaangushwa vibaya.

NB: Huu ni ushauri halali hasa kwa kuzingatia kila raia ana haki ya kugombea... kuchagua na kuchaguliwa kuwa kiongozi yeyote kwamujibu wa katiba yetu.



MUNGU IBARIKI AFRIKA!
 
Aaahh kwa haraka haraka utagundua Vijana wa Lumumba upande wa Jiwe ndo hawahawa walofungua nyuzi zakujifanya wanampenda Membe ,ili mradi tu kujaribu kupenyezesha mpango wa membe alonao.

Hapo ndo tunarudi kulee ,jiwe alipopiga marufuku wanachama kuanza kuanza kupiga kampeni zao mapema.


Kwa ufupi..ukiwa na akili ya kawaida, utaona km ni Wafuasi wa membe...lkn kihalisia ni wafuasi wa JIWE ..namwisho Membe atajitoa mwenyewe..

Kimkakati, na Membe ni Mwanasiasa Nguli na mzito WALA HAWEZI KAA AANZISHE VIJIKAMPENI VYA KIPUUZI NAVYOVIONA HUMU .


Hata ivo Rais Ajaye ni Tundu Lissu .
Kula tano mkuu twende na tl
 
Mambo CCM huwa hayana tofauti na vikao vya kichawi, ili udumu na uendane na CCM inatakiwa uwe na tabia hizo za kichawi.
 
Mnazan mabadiliko aliyoyafanya na anayoendelea kuyafanya yatamruhusu membe hata kuchukua fomu?.... MARK MY WORD MAGUFULI KWA UBABE ATAPITA BILA KUPINGWA NDANI YA CCM,, HAKUNA MWANA CMM ATAKAE CHUKUA FORM
Hivi hizi kampeni zinazoendelea unadhani waliozianzisha wanasubiri hadi 2020 ndio mtu wao agombee?
 
Back
Top Bottom