Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Tunataka mkali + hapana asiwe mkali + tunataka anayesafiri + hapana hatutaki Vasco dagama + tunataka anayecheka + hapana hatutaki anayecheka cheka = ?

Hii ndiyo Tanzania bwana.
Lakini amini nakwambia wote wanaopiga kelele humu ni waathirika tu wa JPM. Ila siku moja watakuja elewa wale watakaosalia. A matter of time
 
Kazi gani gadamn! Naona mmekariri kazi! Kazi mnazungumzia. Tumekuwa na uwezo mdogo kupambanua mambo wafrica.
Tatizo unapokuwa na uwezo Mdogo huoni kitu kama wewe hapo.Unaangalia maslahi yako sisi tunaangalia nchi.
 
Hii agenda ya kumpromote huyu Membe ilioanza mwezi uliopita dhamira yake ni ipi hasa?
 
Hawakupata maendeleo kwa kutumia usanii wa kujifanya unapiga vita ufisadi huku ukirundika kwenu "White elephant projects" ambazo kila unapohubiri maendeleo unaona aibu kuzitaja kama sehemu ya ufanisi wako.

What are the black elephant projects ambazo ndio zafaa kuhubiriwa?
Hebu tutajie hata moja unayoijua wewe then tuanzie hapo...
 
Hivi Tanzania imishiwa kabisa watu wenye uwezo wa kuongoza mpaka mnafanya 'recycling' kiasi hiki? majina yale yale.
 
Ninawaza tu ikiwa BM ni jasusi na kada mzoefu...huenda kajenga mnyororo wa thamani mkubwa na hatari kwa mwenyekiti ukizingatia mwenyekiti wangu sidhani kama alishawahi hata kuwa informer wa idara ile au mwenyekiti wa shina la CCM!!
 
Tatizo unapokuwa na uwezo Mdogo huoni kitu kama wewe hapo.Unaangalia maslahi yako sisi tunaangalia nchi.
Sasa hapa kati yangu na wewe nan mwenye narrow mind, wewe umekalia kusema kazi wakt watu tunapiga kazi kila mwez tunafanya yetu kweny kodi alaf kweny mafao unasubiria kupewa 25. Mimi huyohuyo nafanya biashara ya mazao ambayo ni ngumu kwasasa ushahid ninao mimi mwenyewe, biashara ndogondogo kodi hazina uhalisia. Mnazungumzia kazi gani nyie watu.
 
Sasa hapa kati yangu na wewe nan mwenye narrow mind, wewe umekalia kusema kazi wakt watu tunapiga kazi kila mwez tunafanya yetu kweny kodi alaf kweny mafao unasubiria kupewa 25. Mimi huyohuyo nafanya biashara ya mazao ambayo ni ngumu kwasasa ushahid ninao mimi mwenyewe, biashara ndogondogo kodi hazina uhalisia. Mnazungumzia kazi gani nyie watu.
Fanya kazi acha kelele jiwe halipigwi konzi.
 
sasa hivi hata sisi wana ccm tunajuta sema ni kimyakimya hakuna anayesema kiukweli mwenyekiti ana kasoro nyingi .tunaongozwa kwa "mkono wa chuma"
Ccm ndo tunaoumia Sana. Makusanyo ya kodi za vibanda yote yanaenda makao makuu, slow slow na wenzake wanayainjoi. Kwenye ofisi za ccm wilaya na Mkoa njaa kali Sana. Tunajuta kumweka huyu jamaa kiukweli hali ni mbaya kuliko ile miezi 18 ya kufunga mkaja wakati wa Nyerere.
 
Mkuu yani hapa kinachofanyika Upinzani wanaamsha presha ili Membe asimamishwe na CCM lakini target yao wanajua Membe wanauwezo wa kumchezesha dele mpoaka wamshinde lakini JPM hawamuwezi kamwe! kwaiyo ndiyo gia yao wamjaze membe alete vurugu ndani chama chake kipasuke wao iwe faida kwao.
Hivi aliyeibua mambo ya Membe ni upinzani au Katibu Mkuu wa Jiwe, Bashiru Ali na yule punguwani mwingine waliyemtuma kabla?
 
Hii ndiyo Tanzania bwana.
Lakini amini nakwambia wote wanaopiga kelele humu ni waathirika tu wa JPM. Ila siku moja watakuja elewa wale watakaosalia. A matter of time
We jidanganye na jivike upofu hivyohvyo
 
katibu mkuu wa chama cha mapinduzi ameonekana kukerwa na mtu katika mtandao wa twitter anayejiita membe.

hii imesababishwa na mtu huyo kutoa masharti ya kukutana nae yeye kama katibu mkuu wakati akijua kwamba yeye ni mwanachama wa kawaida kama walivyo wanachama wengine

dk bashiru amemtaka mtu huyo anayejiita membe aseme wazi kama yeye sio mwanachama tena wa chama cha mapinduzi

chanzo ni gazeti la mwananchi : Alichokisema Bashiru Ally baada ya majibu ya Membe

HBARI KAMILI.

Dar es Salaam. Ni vita mpya kati ya Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally na Bernard Membe.
Ndivyo unavyoweza kusema kutokana na Dk Bashiru kutumia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter kuhoji kitendo cha kusambaa kwa ujumbe katika mitandao ya kijamii ulioandikwa na mtu aliyejiita Bernard Membe, akijibu wito wa katibu mkuu huyo.
Juzi Desemba Mosi, 2018 Dk Bashiru alirejea kumtaka Membe, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kwenda ofisini kwake, akidai mbunge huyo wa zamani wa Mtama anatuhumiwa kuandaa mpango wa kumkwamisha Rais John Magufuli katika uchaguzi wa Rais, kwamba lengo la wito wake huo ni kumueleza kama anayoyasikia ni kweli au si kweli.
Katika kile kinachoonekana kuwa majibu ya mtu anayejiita Membe katika mitandao ya kijamii baada ya wito huo wa Dk Bashiru yamemtibua katibu mkuu huyo, kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twitter amesema;
“Nakuita ofisini unanijibu Twitter na kunipa masharti. Ninapokuita nafanya hivyo kama Katibu Mkuu wa chama chako. Kama wewe si mwanachama ni vyema ukasema rasmi,” amesema Dk Bashiru kupitia ukurasa wake huo.
Katika majibu ya wito huo, mtu anayejiita Membe amesema amempelekea Dk Bashiru ujumbe wa kukubali kumuona mara atakaporejea Tanzania kutoka nje ya nchi.
Amesema ameshangazwa na utaratibu uliotumika kumuita, lakini kwa sababu ya ugeni kazini na kwa sababu anamheshimu (Dk Bashiru) atakwenda kumuona ofisini kwake.
Katika ujumbe huo, ‘Membe’ huyo anasema atakapokwenda ofisini kwa Dk Bashiru, mtu anayemtuhumu kuandaa mkakati wa kumng’oa Rais Magufuli, naye awepo ili kuthibitisha tuhuma hizo.
 
katibu mkuu wa chama cha mapinduzi ameonekana kukerwa na mtu katika mtandao wa twitter anayejiita membe.

hii imesababishwa na mtu huyo kutoa masharti ya kukutana nae yeye kama katibu mkuu wakati akijua kwamba yeye ni mwanachama wa kawaida kama walivyo wanachama wengine

dk bashiru amemtaka mtu huyo anayejiita membe aseme wazi kama yeye sio mwanachama tena wa chama cha mapinduzi
Ndiisi ameenye kyala
 
Back
Top Bottom