Urembo wa vikuku, vishaufu na cheni (shanga) kiunoni kwa wadada

Urembo wa vikuku, vishaufu na cheni (shanga) kiunoni kwa wadada

Katika mavazi au mapambo yeyote kuna wale wanaovaa kwa kujifurahisha wao au wenzao na wale wanaovaa ili kutuma ujumbe kwa wale wanaoelewana lugha. Ubaya ni kuwahukumu wote kwa matendo ya wachache. Mwanamke ana uhuru wa kuvaa anavyotaka na kujipamba atakavyo ili mradi conscience yake haimshtaki. Sisi wengine inabidi tuangalie na kushukuru Mungu kuwa ameumba watu wa jinsia tofauti. Kama tunaona wafanyavyo hakutufurahishi, basi tugeuze macho na kupitia kwengine. Mimi sijali hizo maana zinazosemekana bali nafurahi kuona mguu ulioumbika umerembwa ipasavyo. Hayo mengine nawaachia nyie.
Amandla.....

I salute you!
Kama tutaendekeza kujali nani atasema nini basi maisha yatakuwa ya tabu sana maana kila mtu afanyacho kinaweza kutafsirika vibaya.
Afterall who has the right to judge others?
Kama ni suala la secret societies na secret symbols basi "WAHUSIKA" waachiwe wajitafsiri na kuelewana wenyewe kwa wenyewe kuliko kudhani kila mtu ana maana hiyo hiyo mbaya.
 
I salute you!
Kama tutaendekeza kujali nani atasema nini basi maisha yatakuwa ya tabu sana maana kila mtu afanyacho kinaweza kutafsirika vibaya.
Afterall who has the right to judge others?
Kama ni suala la secret societies na secret symbols basi "WAHUSIKA" waachiwe wajitafsiri na kuelewana wenyewe kwa wenyewe kuliko kudhani kila mtu ana maana hiyo hiyo mbaya.

Ni kweli unachokisema WOS, lakini kwa hulka za Binadamu, wote wenye nia ya kuvaa vikuku na vibata kama urembo na wale wanaotaka kufikisha ujumbe maalum watawekwa kwenye kapu moja tu, kwamba wanafikisha ujumbe maalum na pia kwenye kadamnasi hawana luxury ya kujitafsiri kwamba ule ni urembo tu au una ujumbe wake maalum. Watu, ukiondoa wale wanaokufahamu kwa karibu, wakishaona hicho kikuku au kibata 😉 tayari wameshaform their own opinion. Huu ndiyo Ulimwengu tuliokuwa nao sasa.
 
Hawa bado wanafuata mila zao za kuvaa hizo shanga miguuni. Hakuna ujumbe wowote wanaopeleka zaidi ya kufuata mila zao walizorithi kwa mababu na mabibi zao.

Unajuaje kama hawana ujumbe wowote? Na kama ni kufuata mila zao walizorith kwa mababu na mabibi zao, basi hata wengine wanaweza kuwa wanafuata fashion na sio kutoa ujumbe wowote.
 
the bottom line is what is good for you na kama haijamuathiri mwingine vibaya so what!?
Nasema hivi.... kuvaa vikuku,vibata,vipuri na mapambo mengine yote ruksa alimradi havimuathiri mtu.This is a free country... iweje watu waishi kwa woga??
 
the bottom line is what is good for you na kama haijamuathiri mwingine vibaya so what!?
Nasema hivi.... kuvaa vikuku,vibata,vipuri na mapambo mengine yote ruksa alimradi havimuathiri mtu.This is a free country... iweje watu waishi kwa woga??
 
the bottom line is what is good for you na kama haijamuathiri mwingine vibaya so what!?
Nasema hivi.... kuvaa vikuku,vibata,vipuri na mapambo mengine yote ruksa alimradi havimuathiri mtu.This is a free country... iweje watu waishi kwa woga??

Kila jamii ina mambo yake. Ndiyo yanoifanya iwe tofauti na nyingine. Sasa iwapo jamii yako inatafsiri kwamba vikuku vikivalikwa kote kote maana yake "kote kote", basi ni hiari yako kama unavyosema. Tatizo ni pale ambapo hata famili yako, wakiwemo watoto wako wakiwa wanajua hizo tafsiri za vikuku kama zilivyo mitaani na wakati huo huo kukuona wewe kama mama yao umevitundika miguuni!!
 
Unajuaje kama hawana ujumbe wowote? Na kama ni kufuata mila zao walizorith kwa mababu na mabibi zao, basi hata wengine wanaweza kuwa wanafuata fashion na sio kutoa ujumbe wowote.

Katika moja ya makabila nchini mwetu mbayo yamedumisha mila zao miaka nenda miaka rudi ni wamasai.

Pamoja na kuwa kuna wachache walioziweka pembeni mila zao walizorithi toka kwa mababu na mabibi zao, lakini ukimuona mama wa kimasai kanyoa upara na shanga kibao shingoni, katoboa masikio ile style ya kimasai na hereni kubwa za kimasai masikioni na amevaa vazi lao la kikabila ile rubega na ana shanga mguuni au miguu yote miwili kweli hapa unadhani huyu mmasai anapeleka ujumbe maalum kwa muangaliaji wa ushanga huo ulivaliwa mguuni/miguuni!? Au anadumisha mila yake aliyoirithi?

Sikatai kama wengine wanafuata fashion, lakini kadri ya wengi wanaovaa hivyo vikuku watapofahamu vinapeleka ujumbe gani kuna baahi wataacha kuvivaa kwa kuwa wao hawapeleki ujumbe wowote zaidi ya kuwa ni urembo na wengine wataendelea kuvivaa kwa kuwa ama wanapeleka ujumbe maalum au wanavivaa kama urembo.
 
Mkuu, Bubu! Katika avatar yako jamaa kavaa hereni. Nakumbuka kuna wakati tuliamini kuwa wanaume wanaovaa hereni wanatuma ujumbe kuwa wao ni mashoga. Leo wengi wa wanaume wetu ( naamini hata baadhi ya wana JF) hawavai hereni tu bali hata nywele wanasuka. Mbona tumewakubali baada ya kugundua kuwa tafsiri yetu ya mwanzo ilikuwa na walakin? Kwa nini isiwe hivyo kwa binti zetu, dada zetu na mama zetu? Au kwa vile wao ni wanyonge basi tunang'ang'ania tafsiri hizi ili zitupe kinga tukiwafanyia ubaladhuli?
 
It is obvious that in our times vikuku kwa maana ya kuiga watu wa magharibi vina maana yake iliyowazi yaanni kwenda kinyume na maumbile, kwa watu wanaowaiga wa magharibi basi maana ni hiyo hiyo. Hakuna ugomvi kwa watu kwenda kinyume na maumbile kama hilo ni chaguo lao, wawe waheshimiwa au wawe walala hoi, na hakuna ugomvi kwa wao kujitangaza kuwa ni watu wa namna hiyo. Tatizo ni kuwa unapokuwa public figure tunategemea uwe ni mtu mwenye high moral standards of the community you are living in, hapa kwetu ukweli sio huo. Public figures wengi na hata walio kwenye nyadhifa za juu ni watu ambao ni very corrupted.

Ukiangalia hata wazungu nao wana historia zao, kuna kipindi nao walitembea bila viatu, kunakipindi nao walivaa shanga na kengele, kuna kipindi nao walikuwa wanaiga kutoka kwa watu wengine, kwa hiyo ni safari ndefu imewafikisha walipo, huenda na hawa wenzetu hapa Tanzania nao wanaiga watu wa aina yao wa huko magharibi.
 
Katika moja ya makabila nchini mwetu mbayo yamedumisha mila zao miaka nenda miaka rudi ni wamasai.

Pamoja na kuwa kuna wachache walioziweka pembeni mila zao walizorithi toka kwa mababu na mabibi zao, lakini ukimuona mama wa kimasai kanyoa upara na shanga kibao shingoni, katoboa masikio ile style ya kimasai na hereni kubwa za kimasai masikioni na amevaa vazi lao la kikabila ile rubega na ana shanga mguuni au miguu yote miwili kweli hapa unadhani huyu mmasai anapeleka ujumbe maalum kwa muangaliaji wa ushanga huo ulivaliwa mguuni/miguuni!? Au anadumisha mila yake aliyoirithi?

Sikatai kama wengine wanafuata fashion, lakini kadri ya wengi wanaovaa hivyo vikuku watapofahamu vinapeleka ujumbe gani kuna baahi wataacha kuvivaa kwa kuwa wao hawapeleki ujumbe wowote zaidi ya kuwa ni urembo na wengine wataendelea kuvivaa kwa kuwa ama wanapeleka ujumbe maalum au wanavivaa kama urembo.

Tafsiri ya vitu sio static. Ni lazima tafsiri iende na wakati. Ni kupotosha ukweli kuwa wamasai wamedumisha mila zao.

Nguo wanazoa wamasai zimetengenezwa kwa pamba. Na sijaona mmasai yoyote mwenye ujuzi wa kutengeneza nguo. Hivyo miaka mia moja iliyopita walikuwa wanavaa ngozi, magome ya miti au nyasi.

Pia sijaona mmasai mwenye ujuzi wa kufua shaba au chuma. Hivyo wanavyovaa wamasai ni sehemu ya interaction yao na jamii zingine.

Tukirudi kwenye mada. Dunia inakwenda inabadilika. Na njia moja ya kuonyesha jamii inabadilika kuwa ya kimjini au kuongeza kwa pato, ni kuonekana kwa decoration za fashion za majumba na miili. Kuna watu watakuwa na ziada ya kipato na watakitumia katika vikuku, majumba or whatever.

Na jinsi urbanization inavyoendelea kukua na vipato kuongezeka; tafsiri zingine zinakuwa pure crap.
 
Vishaufu....ha ha haaa...nadhani waliodesign magari ya Mkonga nje walichukua hii technolgy kutoka kwa dada zetu wenye vishaufu!!!!!!!
 
Vishaufu....ha ha haaa...nadhani waliodesign magari ya Mkonga nje walichukua hii technolgy kutoka kwa dada zetu wenye vishaufu!!!!!!!

Hii kali!
Vishaufu na mkonga.. wapi na wapi?Hii analogy yako inatisha!
 
Kama ambavyo binadamu tunavaa pete zinazoonyesha kwamba msichana yuko engaged au Mwanaume au Mwanamke ameowa au kuolewa.

Nimeona katika baadhi ya nchi hivi vikuku wameviwekea maana maalum inayokubalika.

Nakumbuka nilikuwa na email inayoonyesha maana ya hivi vikuku vinavyovaliwa miguuni (kuna maana tofauti kati ya kuvaa mguu wa kushoto na mguu wa kulia na kuvaa miguu yote) vina maana gani lakini bahati mbaya inaelekea niliifuta.

Kwa Tanzania miaka ya nyuma wengi walikuwa wanavaa kama urembo tu lakini kwa miaka ya karibuni baadhi ya wavaaji hukusudia pia kupeleka message fulani kwa wale waangaliaji wa hivyo vikuku na vibata 😉

Tukiachana na vikuku/vishaufu
hebu tuangalie pete.Hivi kwa siku hizi pete ina maana ileile iliyokuwepo zamani?Nimeshaona kwa mfano wanawake ambao hawajawahi hata kuchumbiwa wala kuolewa wakijisheheni mapete - kuanzia yenye kito ikimaanisha uchumba hadi ya mviringo ikimaanisha ndoa.Hapa tunaona maana zinavyoweza kupotoshwa kwa malengo ya mvaaji.Kwa mantiki hii basi nadhani si sahihi kutoa maana moja kwa kila umuonaye amevaa pambo iwe ni vikuku au pete.
 
Duuh !! Ipo siku pete itavaliwa kwenye dole gumba !!
 
Hii kali!
Vishaufu na mkonga.. wapi na wapi?Hii analogy yako inatisha!

WoS
Just check gari zenye mkonga utaona ufanano...infact every time i meet a lady with kishaufu i say mkonga nje!!!!!

By the way vikuku/vishaufu kama ndo asili yetu basi turudi kwenye asili tuvae nguo zinazotokana na magame ya miti au km vipi tutembee naked...kitu gani kwan!? Naamini hata wewe usingependa urudi kwenye asili hiyo na hata hapo ulipo unajitahidi kuwabadilisha wamasai na wamangáti ili wawe modernized kama wewe!!!

Mimi sifagilii kikuku/vikuku/vishaufu maana ni moja kati ya upotofu tulionao waafrika kwa kuiga!!!

Pili hata wale wabongo wanaume wanaovaa hereni etc!! Sipendi maana iliyopo na nawashangaa sana kwani wengine huvaa kwa sababu ni urembo, they put me off kabisa!!!!

Enewei hii ni nchi huru na kila mtu anastahili kufanya kimfurahishacho bila kuvunja sheria then enjoy urselves...ila usiombe kurudi enzi zetu zile Stone age, Iron age etc!!!
 
Jamani hayo ya vikuku tuachieni sisi tunaovipenda.....ni urembo tu,,, kama urembo mwingine. tafsiri ni za muonaji....lakini mvaaji ana ya kwake na sidhani kama ni zaidi ya urembo,,,,sisi wengine tukiviona mshipa wa fahamu unashtuka....ebo!
 
Vipi heleni? Au kusuka nywele? Hivi leo tutaweza kusema kweli hivyo ni vitu vya wakina mama tuu?

Au tuangalie ndonya ya wamakonde. Hii mbona baada ya muda wake kupita imepotea. Lakini naamini mjanja ukii-market ulaya ambako vijana wanajitoboa kila sehemu,, unaweza kupata market! Na wakianza wao basi na sisi tutawaiga.

Amandla....
 
Lakini naamini mjanja ukii-market ulaya ambako vijana wanajitoboa kila sehemu,, unaweza kupata market! Na wakianza wao basi na sisi tutawaiga.

Amandla....
Kumbe shurti waanze wao! au kwa kuwa waliita utamaduni wetu ni wa kishenzi?
 
Kumbe shurti waanze wao! au kwa kuwa waliita utamaduni wetu ni wa kishenzi?

Naam! Hata kama ni cha kwetu shurti kwanza kikubaliwe nao ndiyo sisi tunakiheshimu! Hatuheshimu cha kwetu hadi kipate barka yao! Ngoja watuige kwenye ndonya kama vijana wetu nao hawataanza kuiga wakisahau kuwa mwanzilishi alikuwa mmakonde!
 
Naam! Hata kama ni cha kwetu shurti kwanza kikubaliwe nao ndiyo sisi tunakiheshimu! Hatuheshimu cha kwetu hadi kipate barka yao! Ngoja watuige kwenye ndonya kama vijana wetu nao hawataanza kuiga wakisahau kuwa mwanzilishi alikuwa mmakonde!

Na kwa kuongezea tu,
Hizi tafsiri mbaya za hereni na vikuku hao wa magharibi ndio waliotupatia... maana kwa jadi zetu vikuku na vishaufu ni utamaduni wa makabila mbalimbali ya kiafrika! Inachekesha jinsi tulivyo wepesi kuiga hata kama ni kujidhalilisha!
 
Back
Top Bottom