DOKEZO URGENT: Binti wa miaka 16 ameozeshwa kwa lazima kama mke wa pili, huko Laela, Sumbawanga

DOKEZO URGENT: Binti wa miaka 16 ameozeshwa kwa lazima kama mke wa pili, huko Laela, Sumbawanga

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Ahsanteni sana Wadau wa JF kwa taarifa hii. Huu ndiyo ushirikiano wa jamii tunaohitaji. Tunashughulikia. Ahsanteni kwa mawasiliano ya namba ya simu.
Piga kazi mheshimiwa! Huyo binti atakuwa anatoka familia za kifugaji (Wasukuma) wanaozesha sana mabinti wadogo.
 
Niko hapa tayari, nimepokea, nampigia sasa hivi. Huwa napatikana binafsi kwa ujumbe kupitia simu namba 0765345777 na 0734124191. Pia siku hizi Wizara tumezindua JAMII CALL CENTER siku na saa za kazi simu na. 0734986503 na 026 2160250. Karibuni sana Wadau JF na jamii yote kwa ujumla. Umoja ni nguvu, ukatili wa kijinsia haukubaliki.
Shukran mheshimiwa kwa kulichukua hili
 
Niko hapa tayari, nimepokea, nampigia sasa hivi. Huwa napatikana binafsi kwa ujumbe kupitia simu namba 0765345777 na 0734124191. Pia siku hizi Wizara tumezindua JAMII CALL CENTER siku na saa za kazi simu na. 0734986503 na 026 2160250. Karibuni sana Wadau JF na jamii yote kwa ujumla. Umoja ni nguvu, ukatili wa kijinsia haukubaliki.
Kwani sheria ya ndoa ya serikali ya Tanzania inasemaje kuhusu ndoa kama wazazi wa binti wa miaka zaidi ya 14 wameridhia aolewe? Serikali si ilishindwa kwenye kesi ya Rebecca Gyumi kupinga ndoa za utotoni serikali ikakata Rufani ikashindwa tena ikashauriwa irekebishe sheria hiyo ya ndoa lakini mpaka hakuna muswada wowote wa wa mabadiliko ya hiyo sheria ya ndoa uliofikishwa bungeni.

Kama serikali haipendi hizo ndoa za utotoni kwanini walikata rufani waliposhindwa mahakamani na Rebecca Gyumi? Haya mnayotuambia hapa ni maigizo tu,kama kweli serikali inadhamira ya dhati a basi hiyo sheria ya binti wa miaka 14 kuolewa ibadilishwe mara moja vinginevyo serikali ikae kimya tu
 
Kwani sheria ya ndoa ya serikali ya Tanzania inasemaje kuhusu ndoa kama wazazi wa binti wa miaka zaidi ya 14 wameridhia aolewe? Serikali si ilishindwa kwenye kesi ya Rebecca Gyumi kupinga ndoa za utotoni serikali ikakata Rufani ikashindwa tena ikashauriwa irekebishe sheria hiyo ya ndoa lakini mpaka hakuna muswada wowote wa wa mabadiliko ya hiyo sheria ya ndoa uliofikishwa bungeni .Kama serikali haipendi hizo ndoa za utotoni kwanini walikata rufani waliposhindwa mahakamani na Rebecca Gyumi? Haya mnayotuambia hapa ni maigizo tu,kama kweli serikali inadhamira ya dhati a basi hiyo sheria ya binti wa miaka 14 kuolewa ibadilishwe mara moja vinginevyo serikali ikae kimya tu
Hapo shida sio umri pekee, shida ni kwamba binti mwenyewe hajaridhia na hayuko tayari kuolewa!
 
Niko hapa tayari, nimepokea, nampigia sasa hivi. Huwa napatikana binafsi kwa ujumbe kupitia simu namba 0765345777 na 0734124191. Pia siku hizi Wizara tumezindua JAMII CALL CENTER siku na saa za kazi simu na. 0734986503 na 026 2160250. Karibuni sana Wadau JF na jamii yote kwa ujumla. Umoja ni nguvu, ukatili wa kijinsia haukubaliki.
Asante sana mh waziri kwa wepesi wako wa kuzingatia matatizo ya wtz kwa haraka. Mungu akubariki sana.
 
Kwani sheria ya ndoa ya serikali ya Tanzania inasemaje kuhusu ndoa kama wazazi wa binti wa miaka zaidi ya 14 wameridhia aolewe? Serikali si ilishindwa kwenye kesi ya Rebecca Gyumi kupinga ndoa za utotoni serikali ikakata Rufani ikashindwa tena ikashauriwa irekebishe sheria hiyo ya ndoa lakini mpaka hakuna muswada wowote wa wa mabadiliko ya hiyo sheria ya ndoa uliofikishwa bungeni .Kama serikali haipendi hizo ndoa za utotoni kwanini walikata rufani waliposhindwa mahakamani na Rebecca Gyumi? Haya mnayotuambia hapa ni maigizo tu,kama kweli serikali inadhamira ya dhati a basi hiyo sheria ya binti wa miaka 14 kuolewa ibadilishwe mara moja vinginevyo serikali ikae kimya tu
Habari za jioni ndugu yangu katika JMT. Nadhani utakuwa umefuatilia mrejesho wa serikali kuhusu hoja uliyoleta. Mara kadhaa kumekuwa na mrejesho kuhusu hatua zinazochukuliwa na serikali juu ya ajenda hii. Hata hivyo, sidhani kama ni sahihi kutotoa msaada na ushirikiano kwa hoja iliyopo sasa dhidi ya manusura ambaye anahitaji msaada kwamba, tukae kimya tu kwa kuwa bado ile hoja ya awali haijafikia mwisho.

Sidhani kama kukaa kimya bila msaada ni sahihi. Hivyo, Kila jambo tutafanyia kazi katika kudhibiti ukatili wa kijinsia kulingana na lilivyo sasa kwa mazingira ya Sasa na wakati ujao nao utafanya kazi kwa mazingira ya wakati huo. Tumeshampata mtoa taarifa Ili kumsaidia manusura wetu. Ahsante Sana, ubarikiwe. usiku mwema,
 
Back
Top Bottom