Habari za kazi wakuu
Natanguliza shukrani kwa mungu kwa kutupa nafasi ya kuwa hai na kukutana kwa ajili ya mijadala mbalimbali kwenye uwanja huu.
Niende moja kwa moja kwenye point...
Nasumbuliwa sana na ugonjwa wa UTI(Urine Track Infection) na kiukwel nimetumia dawa nyingi sana na kwa kufuata masharti husika ya dawa, lakini kila ninapomaliza dose nikikaa siku kujisikilizia ili nikapime tena naanza kuhisi dalili za uwepo wa ugonjwa huu na mara nirudipo hospital kwa ajili ya vipimo ungojwa huwa bado upo na madaktari huamua kunibadilishia dozi.
Nimebadilishiwa dozi nyingi mpaka sindano lakini sijapona na huu ni mwez wa tatu sasa tangu ugonjwa huu uanze kunisumbua.
Ni matumaini yangu nitapata msaada japo wa mawazo na dawa nzur ya kutumia ili kutibu ugonjwa huu ambao sasa umekuwa sugu.Naomba msaada wenu kwa hili tatzo wakuu na mungu atawabariki.