Urusi imeingia kwenye 18 ya Marekani, dunia ijiandae kuona majimbo mapya ya Marekani katika ardhi ya Urusi

Urusi imeingia kwenye 18 ya Marekani, dunia ijiandae kuona majimbo mapya ya Marekani katika ardhi ya Urusi

Eti Russia anashambuliwa.
Duu!
Mkuu sasa hivi Putin ameshaandaliwa makazi ya kujificha huko chini ya udongo (handakini) maana kitachofatia baada ya Ukraine kuvuka boda itakuwa na habari mbaya kwa Putin na genge lake.
 
Umeandika ujinga ndugu..ni vizuri mnapoandika hizo makals...mseme kabisa.."Kwa maoni yangu..."
Mkuu kama unafikiri mimi natania basi subiri muda utaongea.
Tuombe uzima tu mkuu utakuja kuniambia.
 
Putin alitema mkwara kuwa ata deal na yeyote anaemsaidia silaha au mbinu za kivita M'ukraine.
Mmarekani amekuwa akimsaidia M'ukraine silaha na pesa, lkn Putin mpaka leo hajafanya kitu zaidi ya kulalamika tu kwamba Ukraine wanatumia silaha za hatari wanazopewa na Marekani kuyaangamiza majeshi yake.
Acha uongo mkuu! Putin alisema atakaye ingiza jeshi ukraine na sio atakaye msaidia ukraine.
 
yaan vita iliyoendeshwa miezibyote hyo hajakimbia!!… Kifupi siraha za iran hazijaleta impact kubwa kwene hii vita!!…Drone hata urusi anazo sema kuongeza washiriki!!
 
Za asubuhi ndugu zangu, kwema?

Kwa wale wanajamii forums wenzangu wafuatiliaji wa siasa za kibabe na za kimikakati za nchi za magharibi hasa Marekani. Bila shaka mtakubaliana na mimi kwamba sasa Russia (itake isitake) inakwenda kugawana baadhi ya majimbo yake ya mpakani na Marekani kupitia mgongo wa vita yake (Russia) na Ukraine.

Ni nani asiejua kwamba toka miaka mingi iliyopita, lengo kuu la Marekani na washirika wake lilikuwa ni kuigawanya Urusi vipande vipande ili iwe na eneo dogo, jeshi dogo na uchumi wa kawaida kwa ajili ya masilahi mapana ya kijeshi, kiuchumi na kiubabe kwa Marekani na washirika wake!

Hata kugawanyika kwa umoja wa nchi za Soviet pia kulikuwa na mkono wa Marekani na washirika wake, ambao wanataka kuiona Russia inakua nchi yenye kaeneo ka kawaida, jeshi la kawaida na uchumi wa kawaida kama ilivyo Iran, North Korea, Venezuela nk.

Sasa basi, kwa vile mkakati wa kuigawanya Urusi kwa njia ya kawaida ulishindikana, ndo ukatengenezwa mkakati wa kuanzisha zengwe katika mipaka ya Russia kwa kuitumia nchi ya Ukraine huku Marekani akiamini kwamba zengwe hilo lingeweza kuzaa matunda kwa kuishawishi Russia (bila kujua) iingie katika vita na Ukraine, na hatimae baadae Urusi itapoanza kuwa weak (kuelemewa) kutokana na vita hivyo.

Marekani na washirika wake waitumie nafasi hiyo kuitwanga Russia (kupitia jeshi la Ukraine) na hatimae kuingia mpaka Russia kama vile Russia ilivyoingia Ukraine. Ukraine itapoingia Russia, Marekani ataendelea kutuma silaha nzito nzito mno za kijeshi ili kuwapa nguvu zaidi wanajeshi wa Ukraine kuteka baadhi ya majimbo ya Russia yaliopo katika mpaka na Ukraine.

Ikumbukwe kwamba Marekani na washirika wake hawajaingia kwenye hii vita kijeshi, lkn wamekuwa wakituma silaha mbali mbali kwa jeshi la Ukraine ili kutimiza mipango yao, na kwa kiasi kikubwa zimeleta mafanikio makubwa kwa jeshi la Ukraine.

Mmarekani chini ya CIA yake sio mjinga wa kutuma tu mamilioni ya dola na silaha nzito nzito kwa Ukraine bila kujua hizo hela atazirudisha vipi. Bila shaka anajua anachokifanya, na huu ni mkakati wa muda mrefu ambao Putin bila kujua ameingia kichwa kichwa vitani asijue madhara yake ya baadae.

Vita hii ni kama mpira wa miguu ambapo timu iliyoanza kushambulia, sasa inashambuliwa huku wachezaji wake hadi wa akiba wakiwa hoi bint tabaani wasijue nini kifanyike ili kuzuia kufungwa.

Vita ilianza kwa Russia kuishambulia Ukraine na kuleta furaha kubwa huko Moscow hali iliyokuwa inapelekea Putin kuongea kibabe na kwa kejeli kubwa dhidi ya Ukraine na washirika wake (Marekani, UK)

Lakini sasa vita imegeuka, Russia sasa ndio inashambuliwa, furaha ya Moscow imegeuka majonzi, mpaka wanajeshi wa akiba wamepelekwa Ukraine, lkn kichapo ni kilekile.

Putin anataman ipatikane suluhu hata kesho ili Marekani asipate nafasi ya kukamilisha mission zake, ila ni kama vile amechelewa,,, na yeye kutafuta suluhu kupitia yeye mwenyewe hawezi, maana itaonekana ameshindwa vita alivyoanzisha, hivyo itakuwa aibu kwake, kwa jeshi lake na nchi yake.

Marekani anapokuwa na lengo la kuvamia nchi fulan kwa ajili ya masilahi yake fulan, basi huwa na njia nyingi tofauti tofauti za kukamilisha lengo hilo bila kujali itamchukua muda gani, na atapata kwanza hasara kiasi gani.

Tuliona alivyotumia mgongo wa Osama kuivamia Afghanistan, tuliona alivyotumia mgongo wa silaha sijui za sumu kuivamia Iraq chini ya Sadam Hussein, tuliona alivyotumia mgongo wa waandamanaji kuivamia Libya, na sasa anatumia mgongo wa jeshi la Ukraine kuivamia Russia.

Japo si kwa nchi yote, lkn kuna baadhi ya maeneo tutakuja kusikia yalivamiwa, kutekwa na kushikiliwa na jeshi la Ukraine (kumbe nyuma ya pazia) maeneo hayo yatakayotekwa yatakuwa chini ya usimamizi wa Marekani.

Hivi sasa Ukraine ishaanza kurudisha maeneo yao yaliotekwa, na kuyarudisha nyuma tena kwa kasi majeshi ya Russia. Ni swala la muda tu mtakuja kuona haya niliyoandika hapa yanatokea, na Putin hatothubutu kurusha bom la nyuklia hata 1, maana kwa vile Mmarekani atakuwa katika baadhi ya maeneo ya ardhi yake, basi akijaribu kurusha atajikuta anajiangamiza yeye mwenyew na watu wake.

Karibuni kwa uchangiaji zaidi, hasa kwa wale wenye uelewa mpana kuhusu malengo na mikakati ya vita hii.

Moderators najua kuna jukwaa la international, lkn nimeuleta uzi huu uku kwa sababu zangu 🙏

Nawatakieni siku njema.
wacha wapigane me nawatakia siku njema tu ya kupigana
 
Back
Top Bottom