Urusi sasa amecharuka, ni mvua za makombora kaskazini na magharibi ya Ukraine. Boris amekubali yaishe

Urusi sasa amecharuka, ni mvua za makombora kaskazini na magharibi ya Ukraine. Boris amekubali yaishe

Mkuu aya mambo ni mapana sana, tatizo ni kwamba ulaya na marekani tangu enzi na enzi wanaona wao ndo wana haki na kila kitu duniani, fatilia mifumo yao ya biashara za kinyonyaji, ukoloni, utumwa na mengine mengi waliyofanya kwa kuona binadamu wengine hawana haki na uhuru na rasilimali zao.
Icho ndo kitu wanataka kukifanya kwene mataifa tajiri ya rasilimali kama urusi na china... huku kwetu walishatuweza, urusi analinda mipaka yake kwa maana ya rasilimali zake na watu wake, ajenda zilizo nyuma ya utanuzi wa nato sio rafiki kwa ustawi wa taifa lake, kwa nini asizuie?
Khidego asante kutukumbusha kuhusu ubaya wa ukoloni lakini tafadhali usimsahau mkoloni mkubwa duniani - ambaye ni Urusi!
Urusi kiasili ni eneo katribu na Moscow. Katika karne zilizopita ilifaulu kutwaa nchi nyingi na kuzifanya koloni zake. Ni kweli, haikufika Afrtika. Sanbabu yake ni ilikuwa na kazi kushambulia nchi za Asia ya Kati na Asia Kaskazini-Mashariki. Sehemu zilifaulu kupata uhuru mwaka 1991. Sasa Putin anajaribu kurudisha ukoloni Ukraine.
Uingereza ilipaswa kuachana na koloni zake.
Urusi bado. Hata ndaniya mipaka ya leo kuna koloni nyingi.
Ona ramani ya upanuzi wa Urusi:
1656617053819.png
 
Wewe ndo hujui tuendako. Hujui ukrein ni mzalishaji mkubwa wa chakula na mafuta ya alzeti duniani na ulaya inamtegemea yeye kwa mahitaji yao ya chakula, hasa eneo laliloteka Mrusi. Duniani inahitaji nini zaidi ya chakula⁉️ ukiwa na madini utakula hayo madini. Loh wewe utakuwa bado unaishi kwa shemeji
SSH aliwahi tudanganya hili... Nchi gani afrika inategemea chakula Ukraine?😁
 
Back
Top Bottom