Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Urusi na Belarus zinaanza siku 10 za mazoezi ya pamoja ya kijeshi huku kukiwa na hofu inayoendelea ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Belarus ni mshirika wa karibu wa Urusi na ina mpaka mrefu wa kusini na Ukraine.
Marekani imetaja mazoezi hayo - ambayo yanaaminika kuwa ndiyo makubwa zaidi ya Urusi kupelekwa Belarus tangu Vita Baridi kama hatua "ya kuongezeka kwa mvutano huo".
Urusi imekanusha mara kwa mara mpango wowote wa kuivamia Ukraine licha ya kuwa na wanajeshi zaidi ya 100,000 kwenye mpaka.
Lakini Marekani na nchi nyingine za Magharibi zimeonya kwamba shambulio linaweza kutokea wakati wowote.
Moscow inasema haiwezi kukubali kwamba Ukraine - jamhuri ya zamani ya Soviet yenye uhusiano wa kina wa kijamii na kiutamaduni na Urusi - siku moja inaweza kujiunga na muungano wa ulinzi wa Magharibi wa Nato na imedai kwamba hilo litakataliwa. Imekuwa ikiunga mkono uasi wa kutumia silaha mashariki mwa Ukraine tangu 2014.
Mazungumzo ya kidiplomasia yenye lengo la kutuliza mvutano huo yanatarajiwa kote Ulaya siku ya Alhamisi.
Belarus ni mshirika wa karibu wa Urusi na ina mpaka mrefu wa kusini na Ukraine.
Marekani imetaja mazoezi hayo - ambayo yanaaminika kuwa ndiyo makubwa zaidi ya Urusi kupelekwa Belarus tangu Vita Baridi kama hatua "ya kuongezeka kwa mvutano huo".
Urusi imekanusha mara kwa mara mpango wowote wa kuivamia Ukraine licha ya kuwa na wanajeshi zaidi ya 100,000 kwenye mpaka.
Lakini Marekani na nchi nyingine za Magharibi zimeonya kwamba shambulio linaweza kutokea wakati wowote.
Moscow inasema haiwezi kukubali kwamba Ukraine - jamhuri ya zamani ya Soviet yenye uhusiano wa kina wa kijamii na kiutamaduni na Urusi - siku moja inaweza kujiunga na muungano wa ulinzi wa Magharibi wa Nato na imedai kwamba hilo litakataliwa. Imekuwa ikiunga mkono uasi wa kutumia silaha mashariki mwa Ukraine tangu 2014.
Mazungumzo ya kidiplomasia yenye lengo la kutuliza mvutano huo yanatarajiwa kote Ulaya siku ya Alhamisi.