Urusi yaanza mazoezi ya kijeshi ya siku kumi na Belarus

Urusi yaanza mazoezi ya kijeshi ya siku kumi na Belarus

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Urusi na Belarus zinaanza siku 10 za mazoezi ya pamoja ya kijeshi huku kukiwa na hofu inayoendelea ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

Belarus ni mshirika wa karibu wa Urusi na ina mpaka mrefu wa kusini na Ukraine.

Marekani imetaja mazoezi hayo - ambayo yanaaminika kuwa ndiyo makubwa zaidi ya Urusi kupelekwa Belarus tangu Vita Baridi kama hatua "ya kuongezeka kwa mvutano huo".

Urusi imekanusha mara kwa mara mpango wowote wa kuivamia Ukraine licha ya kuwa na wanajeshi zaidi ya 100,000 kwenye mpaka.

Lakini Marekani na nchi nyingine za Magharibi zimeonya kwamba shambulio linaweza kutokea wakati wowote.

Moscow inasema haiwezi kukubali kwamba Ukraine - jamhuri ya zamani ya Soviet yenye uhusiano wa kina wa kijamii na kiutamaduni na Urusi - siku moja inaweza kujiunga na muungano wa ulinzi wa Magharibi wa Nato na imedai kwamba hilo litakataliwa. Imekuwa ikiunga mkono uasi wa kutumia silaha mashariki mwa Ukraine tangu 2014.

Mazungumzo ya kidiplomasia yenye lengo la kutuliza mvutano huo yanatarajiwa kote Ulaya siku ya Alhamisi.
 
Urusi na Belarus zinaanza siku 10 za mazoezi ya pamoja ya kijeshi huku kukiwa na hofu inayoendelea ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

Belarus ni mshirika wa karibu wa Urusi na ina mpaka mrefu wa kusini na Ukraine...
Nipo nao huku kuna baridi kweli
 
Blaza yeye anafanya zoezi la kuzungusha koki
Ha ha haa Blaza na NATO kupigana na Urusi ni kujitoa mhanga.

Blaza analijua hilo na Eu wanalijua hilo,ambao kwa pamoja wanajiita Nato.

Vita pekee itakayopiganwa na mataifa haya ni kufunga koki na mambo kama hayo.

Unadhani Kuna nchi Iko tayari kurusha risasi kwa Urusi kisa Ukraine lazima ajiunge NATO?

Hakuna kitu kama hicho.
 
washirika wa Urusi hadi kichekesho.. Kampan lake nilatu-nchi twa hovyo hovyo tu kulingananisha na mshindini wake.
 
Mpaka sasa, Dikteta Lukashenko ndiye anayeonesha kuunga mkono Ukraine kuvamiwa. Nchi yenyewe [Belarus] haina utofauti sana na zile 'banana republics' za kusini mwa jangwa la Sahara.
 
Urusi na Belarus zinaanza siku 10 za mazoezi ya pamoja ya kijeshi huku kukiwa na hofu inayoendelea ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

Belarus ni mshirika wa karibu wa Urusi na ina mpaka mrefu wa kusini na Ukraine.

Marekani imetaja mazoezi hayo - ambayo yanaaminika kuwa ndiyo makubwa zaidi ya Urusi kupelekwa Belarus tangu Vita Baridi kama hatua "ya kuongezeka kwa mvutano huo".

Urusi imekanusha mara kwa mara mpango wowote wa kuivamia Ukraine licha ya kuwa na wanajeshi zaidi ya 100,000 kwenye mpaka.

Lakini Marekani na nchi nyingine za Magharibi zimeonya kwamba shambulio linaweza kutokea wakati wowote.

Moscow inasema haiwezi kukubali kwamba Ukraine - jamhuri ya zamani ya Soviet yenye uhusiano wa kina wa kijamii na kiutamaduni na Urusi - siku moja inaweza kujiunga na muungano wa ulinzi wa Magharibi wa Nato na imedai kwamba hilo litakataliwa. Imekuwa ikiunga mkono uasi wa kutumia silaha mashariki mwa Ukraine tangu 2014.

Mazungumzo ya kidiplomasia yenye lengo la kutuliza mvutano huo yanatarajiwa kote Ulaya siku ya Alhamisi.
Mbona hata Burundi inafanya mazoezi ya kijeshi? Mimi nikajua tayari kavamia Ukraine kumbe bado anajipigiza kichwa Chini kwa hasira ili aogopwe?

Tunasubiri Uvamizi kamili ndio nitakubali kweli Russia hatanii. Lakini akiishia kupiga Push-Up ni mwendelezo wa Mikwara TU.

Hata Marekani alifanya mazoezi ya Kijeshi kwenye Rasi ya Korea ili Kiduku aogope lakini wapi. Tena mazoezi ya Marekani yalichukua miezi 3 yakihusisha AIRCRAFT CARRIER 3 Kwenye Rasi ya Korea lakini hakuvamia na mwisho Pro-Russia mkasema Marekani ni PAPER TIGER.

Sasa nasema hivi!!!

Urusi isipovamia Ukraine awamu hi kwa Mikwara yake ya Mbuzi ya Kurundika wanajeshi laki moja Mpakani Basi kuanzia leo Urusi nayo itakuwa ni PAPER TIGER Kama Marekani tu.
 
Kwa kifupi Hana kampani Kali Kijeshi,lakini anawatesa kishenzi
Influence ya Russia duniani ilishaporomoka siku nyingi, kwa Ukraine lazima awe mkali kwani ni wazi NATO wanataka kumfuata mpaka chumbani. Mwanzoni USSR alikuwa anawazunguka adui zake, ila sasa Urusi ndiye anakaribia kuwekwa kati.
 
Mpaka sasa, Dikteta Lukashenko ndiye anayeonesha kuunga mkono Ukraine kuvamiwa. Nchi yenyewe [Belarus] haina utofauti sana na zile 'banana republics' za kusini mwa jangwa la Sahara.
Sidhani Kama ni sahihi nitafuatilia
 
Ha ha haa Blaza na NATO kupigana na Urusi ni kujitoa mhanga.
Blaza analijua hilo na Eu wanalijua hilo,ambao kwa pamoja wanajiita Nato
Vita pekee itakayopiganwa na mataifa haya ni kufunga koki na mambo kama hayo.
Unadhani Kuna nchi Iko tayari kurusha risasi kwa Urusi kisa Ukraine lazima ajiunge NATO?
Hakuna kitu kama hicho.
mzee hata hio koki haitafungwa EU itaendelea kuitegemea RUSSIA kwenye gesi mpaka labda itakapopatikana mbadala wake
EU hawamuwezi RUSSIA kwenye VITA zozote wangekua wanataka kufunga bomba kweli au kuanzish vita wasingeenda kulia lia MOSCOW mwenzao katulia anawachora tu naalivyo nakujiamini bwana VLADMIR watu wanaona kuna mgogoro mkuuubwa yeye anaenda kwenye kufungua olimpic[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Urusi na Belarus zinaanza siku 10 za mazoezi ya pamoja ya kijeshi huku kukiwa na hofu inayoendelea ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

Belarus ni mshirika wa karibu wa Urusi na ina mpaka mrefu wa kusini na Ukraine.

Marekani imetaja mazoezi hayo - ambayo yanaaminika kuwa ndiyo makubwa zaidi ya Urusi kupelekwa Belarus tangu Vita Baridi kama hatua "ya kuongezeka kwa mvutano huo".

Urusi imekanusha mara kwa mara mpango wowote wa kuivamia Ukraine licha ya kuwa na wanajeshi zaidi ya 100,000 kwenye mpaka.

Lakini Marekani na nchi nyingine za Magharibi zimeonya kwamba shambulio linaweza kutokea wakati wowote.

Moscow inasema haiwezi kukubali kwamba Ukraine - jamhuri ya zamani ya Soviet yenye uhusiano wa kina wa kijamii na kiutamaduni na Urusi - siku moja inaweza kujiunga na muungano wa ulinzi wa Magharibi wa Nato na imedai kwamba hilo litakataliwa. Imekuwa ikiunga mkono uasi wa kutumia silaha mashariki mwa Ukraine tangu 2014.

Mazungumzo ya kidiplomasia yenye lengo la kutuliza mvutano huo yanatarajiwa kote Ulaya siku ya Alhamisi.
 
Back
Top Bottom