MJUE KAMANDA MPYA WA OPERATIONS UKRAINE.
Ni mwanajeshi mwenye uzoefu
Baada ya mambo kuwa magumu huko Ukraine, Rais Putin amemteua ndugu Dvornikov kuwa kqmqnda wa opérations.
Dvornikov alijiunga na jeshi la Usovieti katika mwaka 1978 baada ya kuhitimu kutoka shule ya kijeshi iliyoko mashariki mwa Urusi.
Alianza kazi yake kwa kupanda cheo haraka baada ya kupata cheo kama platuni kamanda katika mwaka1982.
Alipata diploma ya masuala ya kijeshi katika chuo cha jeshi cha Frunze katika mwaka 1991, katikati ya kuvunjika kwa Muungano wa Usovieti.
Katika miaka ya 2000, Dvornikov alipigana katika vita ya pili nchini Chechnya na kushikilia vyeo vya juu kadhaa kabla yar ais wa Urusi Vladimir Putin kumteua kuwa mkuu wa majeshi ya Urusi nchini Syria katika mwaka 2015.
Dvornikov alihudumu kama kamanda wa kwanza wa jeshi la Urusi katika operesheni za nchi ya kiarabu, baada ya putin kutuma vikosi huko mwezi septemba 2015 , kuiunga mkono serikali ya rais wa Syria Bashar al - Assad.
Urusi ilimpatia Al-Assad, ambaye alikuwa anahofia kupinduliwa, msaada wa ndege za kijeshi na kumsaidia kumaliza vita lakini kwa kwa garama kubwa.
Chini ya amri ya Dvornikov, vikosi vya Urusi nchini Syria viliripotiwa kukabiliana na wenyeji na na kuangamiza miji kwa kupiga makombora, kutumia silaha zilizopigwa marufuku kimataifa yakiwemo mabomu.
Alipochukua uongozi, Dvornikov alianzisha haraka sana ngome ya majeshi ya anga karibu na mwambao wa Kusini mashariki mwa Syria na kutoka kule aliangamiza miji na jiji katika jimbo la Idlib.