Uchaguzi 2020 US Ambassador to Tanzania: I am concerned, if election officials do not take necessary steps, country's democracy will lose credibility

Uchaguzi 2020 US Ambassador to Tanzania: I am concerned, if election officials do not take necessary steps, country's democracy will lose credibility

Mmebaki na propaganda uchwara tu hamna jipya!!Kuna wasaliti zaidi ya wanaiongiza nchi katika mikataba ya siri kwa manufaa yao?!
Kwani wewe kamanda, mkataba wa lile lipagala la pale ufipa ulishawai kuona[emoji23][emoji23][emoji23] wasaliti .
 
Hakuna jambo ninalolichukia...kama kutegemea Misaada ya hao Mabwana zenu

Ifike wakati
Tunapozungumza kuhusu Taifa,Tuzungumze namna ya kujikomboa na kujikwamua sisi kama sisi bila ya kumshirikisha hata Jirani

itakuwa jambo jema sana

Tz bila ya Misaada,inawezekana
Lkn...ni lazima tufunge mikanda
Na tuache kabisa kusikiliza Propaganda zao Hayawani weupe
Unatukana huku kila siku mnategemea misaada kutoka kwa hao hao.Ungekuwa na hoja kama misaada tungekuwa tumeikataa miaka 59 baada ya uhuru.MATAGA hamna akili kabisa!
 
Unatukana huku kila siku mnategemea misaada kutoka kwa hao hao.Ungekuwa na hoja kama misaada tungekuwa tumeikataa miaka 59 baada ya uhuru.MATAGA hamna akili kabisa!
Miaka 59 watu bado wanaishi kwenye nyumba za nyasi alafu bado wanajiona wanaweza leta mabadiliko ndani ya miaka mitano,ni mjinga tu ndo anayeweza kuwaamini CCM
 
Kateni misaada na mikopo vinginevyo mambo haya kamwe hayatakoma.

Sijui kwanini nchi wahisani wanashindwa kuweka shariti la kutoa misaada na mikopo kuwa ni lazima nchi husika iwe na Tume Huru ya Uchaguzi inayokubalika na makundi yote.
unadhani yakifanyika hayo ndio utamkomoa Magufuli na Mambo ndio yataenda sawa... Swala hapa ni maridhiano ya kitaifa
 
Ila CCM ukiwatafakari unabaki unacheka tu-Jamaa pamoja na kusifia kote mitishamba ya madagascar na kutumia gharama kubwa kuileta kwa usimamiz wa Proffesor kwa ajili ya kinga ya Corona mwisho haikutumika,kwa mtu mwenye akili timamu lazima ujiulize swali,inakuwaje mtu anakuuzia dawa ya Corona wakati yeye mwenyewe kavaa mask na kaweka watu wake lockdown na wanachangamoto kuikabili?Ndo maana Trump huwa anadharau sana mambo yetu Waafrica-unapambanaje kumweka mtu korokoroni just because mmetofautiana ideas?
 
Kabla hiyo miaka 5 haijaisha,ipo siku, panapo majaliwa,utakuja hapa kulalamika kwanini Magu alipita tena iwapo atapita kama unavyotaka.

hahaha sasa akizingua si tunamtoa, ingawa jamaa utendaji wake ni ule ule toka akiwa waziri, sasa na nyie mnatakiwa mjenge chama akizingua wananchi wanakua kazi ni rahisi, sasa uku magu akizungua ukigeuka upande wa pili ndo matatizo juu ya shida, kampeni nzima ni matusi juu ya matatizo, sasa ni bora tu aendelee, we unadhan watu hawajui lissu kapigwa risasi, we unadhan watu hawajuui mmenyimwa kufanya siasa miaka minne, mfano mm nalipa leseni 1.3M kila miaka mitatu tcra kuendesha youtube channel tu, unadhan hatupitia hizi changamoto?

- lakini sasa tufanye nn? upande wa pili ndo huyu kila saa utaskia dunia inaskiliza, mara hakuna kilichofanyika, kidogo jukwaani utaskia kikundi kishaiitwa majinga, polisi ndo wamechezea matusi mpaka washazoea, sasa tunaona bora tu tuendelee na huyu huyu, tutafanya nn sasa? tukiwapa ushauri uku tafuteni hoja nzito, mfano magu kasema anashusha bei ya umeme, nyie tafuteni namna muonekane better, iwe win win situation! lakini ona anchoongea sasa jukwaani, sjui haki, kidogo tusi, haki sio kwamba wananchi hawana wanaoshikwa kwenye hili kundi ni nyie vyama vingine, na ndo mkono unawakuta ila sasa tutafanya nn mgombea kidogo tusi, badala atuonyeshe nafuu yeye anjibizana na magufuli, hajui wananchi wana matatizo nn
 
To my dismay, I have seen and heard reports of government and security representatives disrupting and preventing candidates’ ability to campaign freely. As we get closer to election day, the pace and severity of these disruptions is quickening and deepening. We have seen political violence, restrictions on media, and a candidate certification process that, by all appearances, gave a clear advantage to the ruling party. Already, we are hearing reports of officials denying poll watchers the ability to do their jobs. Taken together, these developments paint a picture of an electoral process that does not provide a level playing field.

Mr. Ambassador, for all that matters you might just choose to sing melodies to goats. It will probably be a more worthwhile gesture that could get someone more milk!
 
Hayo yangesemwa na Magufuli watu wangeelewa ni kwa kuwa hajui lughà kama wewe aliyotumia Balozi bali yangekuwa si maneno ya kupuuza kwa kuwa ni Rais lakini yakisemwa na vilaza wa bure elimu ya Magufuli hata Balozi apuuze tu maana bado mgeni ataona na kusikia mengi.
Ulitaka aseme mara ngapi, huo ndio upimbi wenyewe. Wewe endeleza ukasuku wako lakini kwa JPM wamegonga mwamba.
 
Kateni misaada na mikopo vinginevyo mambo haya kamwe hayatakoma.

Sijui kwanini nchi wahisani wanashindwa kuweka shariti la kutoa misaada na mikopo kuwa ni lazima nchi husika iwe na Tume Huru ya Uchaguzi inayokubalika na makundi yote.

Ningekuwa na ushawishi, ningeanzisha movement ya kuzitaka nchi tajiri na mashirika ya fedha ya kimataifa kuweka shariti kwamba, kila nchi inayotaka msaada au mkopo, ni shariti nchi hiyo iwe na Tume Huru ya Uchaguzi inayokubalika na wadau wote wa uchaguzi katika nchi hiyo.

Au kama hili gumu,basi movement yangu nyingine ingekuwa ni kuzishawishi nchi hizi kuweka shariti linaloweza kuwa kama incentive ambapo nchi yenye kuonyesha demokrasia ya kweli, kwa kuwa na Tume Huru na Katiba inayokubalika na makundi yote katika nchi, inakuwa ni moja ya kigezo kwa nchi husika kupunguziwa au kufutiwa madeni.

Jitihada za nchi wahisani na mashirika ya fedha ya kimataifa za kuondoa umasikini katika mataifa yanayoendelea, hasa Afrika, haziwezi kufanikiwa iwapo katika nchi hizi hakuna demokrasia ya kweli, hivyo kuna ulazima wa kulazimisha nchi hizi kuwa na demokrasia vinginevyo maendeleo yatachukuwa muda mrefu kufikiwa katika nchi hizi.

Demokrasia ya kweli inafanya watawala wawajibike kwa watu wao na nchi zao na hivyo kuwezesha maendeleo kupatikana kwa haraka zaidi.
Hama nchi
 
Back
Top Bottom