Anza kwa kusoma hiyo mistari michache ya Qur'an niliyokuwekea hapo juu. Na kila unapoiona rangi ya blue ni link itayokufikisha uisome zaidi Qur'an.Kwanza hongera kwa kuwa msomaji. Tushawishi na wengine ambao hatujawahi kuisoma, tutufaikaje? Ungetupa alau shuhuda zako binafsi au za watu wengine za wdliosaidika kupitia Qur'an.
Anza kwa kusoma hiyo mistari michache ya Qur'an niliyokuwekea hapo juu. Na kila unapoiona rangi ya blue ni link itayokufikisha uisome zaidi Qur'an.
Jionee "ushuhuda" wa muujiza wa Qur'an:
Hatushindanishi bali kinachotakiwa kueleweka kama tunaloliongelea ni "neno la Mungu" kweli?Nafikiri si busara kuvishindsnisha Vitabu vya dini, lakini tunaweza kuelezana vinavyopatikana humo ili mtu akiona anavihitaji avisome kwenye Vitabu husika.
Binafsi, nimeshaisoma Biblia mara kadhaa lakini sijabahatika kuisoma Qur'an, kwa hiyo nikicomment kuhusu Qur'an nitakuwa nasema uongo.
Labda ungefafanua na wewe jinsi ulivyosaidika nayo, huenda kuna mtu anahitaji ulichokigundua kupitia usomaji wa Qur'an.
Asante sana!Hapa ninazungumzia Neno la Mungu la kwenye Biblia.
Wanasaikolojia wanakiri kuwa maneno yana uwezo mkubwa sana wa kumwathiri mtu. Ikiwa maneno ya kawaida yanaweza kusababisha mabadiliko, ni kwa kiwango gani Neno la Mungu linaweza kuleta matokeo yaliyoahidiwa na Mungu Mwenyewe? Kama unataka kusikia jibu, basi ujue ni kwa asilimia mia moja. Halijawahi kushindwa, na haitatokea lishindwe.
Ushauri nasaha unaweza ukashindwa. Sayansi inaweza ikakwama. Hata maombi yanaweza yakakwama, lakini si NENO LA MUNGU. Halijawahi kushindwa, halitakaa lishindwe.
Lakini nimeshawahi kuwasikia watu, tena wengi tu, wakikalamika kuwa Neno la Mungu halitendi kazi kwao. Hata mimi nilishawahi kupitia hiyo hali. Nilikuwa nikishangaa kwa nini pamoja na jitihada zote nilizokuwa nikizifanya, sikuwa nikipata matokeo! Kumbe ulikuwa ni ujinga wangu ndiyo uliokuwa ukinikwamisha kupata matokeo niliyoyatamani sana. Mungu hakuwa tatizo, tatizo lilikuwa kwangu, ujinga.
Niliugua vidonda vya tumbo kwa muda mrefu. Nilitibiwa hospitali mbali mbali bila mafanikio. Niliomba na kuombewa lakini bado vidonda viliendelea kuling'ang'ania tumbo langu. Lilionekana kama vile ni tatizo ambalo ningedumu nalo siku zote za maisha yangu.
Niliendelea kutumia dawa na kufuata maelekezo ya madaktari, yakiwemo ya kutokula vyakula fulani. Niliendelea pia kuomba, na hata kuombewa ilipopatikana fursa ya aina hiyo, lakini ilikuwa kama kutimiza wajibu tu. Sikutarajia kama ningeweza kupona tena. Ilikuwa kama vile nilikuwa nimekata tamaa, japo nilitamani sana kuondokana na hayo mateso. Lakini kwa sababu ya kuomba na kuombewa mara nyingi bila mafanikio, kulinifanya nikate tamaa ya kupona.
Mambo yalibadilika nilipoamua kujikita kwenye Neno la Mungu. Baada ya muda, niliyekuwa mateka wa vidonda vya tumbo, niligeuka kuwa mbabe dhidi ya magojwa. Vidonda vya tumbo havikuweza tena kuendelea kulifanya tumbo langu makazi yake. Viliisha kabisa. Ni miaka kumi sasa tangu nipone vidonda vya tumbo kwa imani. Sikuomba wala kuombewa. Neno la Mungu liliumbika moyoni mwangu, nikaamini nimeshapokea uponyaji, nikatenda kama aliyeponywa, na ikawa hivyo. Kesi ikawa imefungwa. Vilianza kunisumbua kwenye mwaka 2002 hivi, nikapona kwa imani mwaka 2013. Hatimaye vidonda vya tumbo kwangu vikawa Historia.
Neno la Mungu ni kama gari. Ni usafiri ulio wazi kwa kila msafiri. Litakufikisha kule alikosema Mmiliki Wake, Mungu. Lakini ni mpaka tu ulipande ndiyo utaweza kufika huko. Nje na hapo, utakuwa mtazamaji na msindikizaji .
Alichosema Mungu ndicho alichomaanisha.
Neno Lake linaponya, linafanikisha, ni ulinzi, ni hekima, ni kila kitu ilichosema.
JINSI GANI UNAWEZA KULIPANDA HILI GARI LIITWALO NENO?
Nitakueleza njia mojawapo ninayoifahamu! Ni kwa kulipa muda.
Kitu chochote cha thamani kinahitaji kupewa muda. Ndivyo ilivyo pia kwa Neno la Mungu. Ni muhimu kulisoma, lakini haitoshi kulisoma tu, ikiwa unataka kuona uthihirisho Wake katika maisha yako. Ni lazima kulitafakari.
Yoshua 1:8 inasemaje?
KITABU HIKI CHA TORATI KISIONDOKE KINYWANI MWAKO, BALI YATAFAKARI MANENO YAKE MCHANA NA USIKU, UPATE KUANGALIA KUTENDA SAWASAWA NA MANENO YOTE YALIYOANDIKWA HUMO; MAANA NDIPO UTAKAPOIFANIKISHA NJIA YAKO, KISHA NDIPO UTAKAPOSITAWI SANA.
Litafakari Neno. Hilo ni la muhimu sana, tena sana, kama shauku yako ni kuyapata matokeo iliyoyaahidi. Kusoma haitoshi! Kulifundisha haitoshi! Ni lazima na ni muhimu sana kulipa muda kwa kulitafakari
Ukifanya kiusahihi kama ilivyoelekezwa na Yoshua 1:8, utapata matokeo sahaihi. Mungu anamaanisha anachosema.
Kwa hiyo basi, chukua Andiko lenye Ahadi ya Mungu na uanze kulitafakari usiku na Mchana. Unachokihitaji kimo ndani ya Hilo Neno. Kadiri unavyolitafakari, ni kama vile unalifyonza kuingia rohoni mwako. Likiingia vya kutosha litajidhihirisha katika mazingira yako ya nje. Kama ni ugonjwa utayeyuka. Kama ni hofu itaondoka bila kuaga. Chochote kile unachokihitaji unaweza kukipata kwenye Neno. Kama imeahidiwa na Mungu, ni kwa ajili yako. Inakusubiria uichukue.
Na kutafakari Neno la Mungu kwa mujibu wa Biblia, ni pamoja na kulitamka. Usilitafakari kimya kimya tu, bali, ulitamke kwa sauti ya chini kwa kulirudia rudia mara nyingi sana kadiri iwezekanavyo. Hiyo ndiyo tafakari mojawapo ya Kibiblia.
Labda ni mgonjwa? unaweza ukatumia Isaya 53:5 kwa kujisemea kwa sauti, KWA KUPIGWA KWAKE YESU KRISTO NIMEPONA... Tuchukulie, kwa mfano, una mafua. Unaweza ukasema, KWA KUPIGWA KWAKE YESU, NIMEPONA MAFUA.
Unapata upinzani kwenye shughuli zako halali? unaweza ukatumia Zaburi 1:2-3 kwa kujisemea mara kwa mara kila siku, NINAPENDEZWA NA SHERIA YA BWANA, KWA HIYO KILA NINALOLIFANYA LINAFANIKIWA. Au 1Yohana 4:4; HAKUNA AWEZAYE KUNIKWAMISHA KWA SABABU ALIYE NDANI YANGU NI MKUU KULIKO YEYE ALIYE KATIKA DUNIA HII.
Unafanya kazi halali, labda umeajiriwa au unafanya biashara, lakini hupigi hatua kimaendeleo? Tumia Wafilipi 4:19. Jisemee mara nyingi kila siku, MUNGU AMENIJAZA KILA NINACHOKIHITAJI KWA KADIRI YA UTAJIRI WAKE KATIKA UTUKUFU NDANI YA KRISTO YESU.
Nisikuchoshe! Itoshe kusema kuwa NENO LINATENDA. Lilitenda kwa wengine, litatenda na kwako pia.
Kumbuka, MUNGU HANA UPENDELEO; Matendo 10:34.
Naam, ni ishara mojawapo tena ni muujiza.Kwa hiyo kuhifadhiwa na watu ndio ishara ya neno la Mungu?
Amina!Uhai wa Neno la Mungu uko wazi kabisa, lakini bado kuna watu wanaojitahidi kuwashawishi wenye imani haba wasiliamini.
Kwa ushuda kama huu sijui watakuja na hadithi gani tena!
Ubarikiwe sana kwa ushuhuda wako. Naamini na wengine wamepata cha kuwasaidia kama nami nilivyopata.
Ni sahihi kabisa!Nguvu ya neno ni hali ya kuita usaidizi wa ya asili either kutoka chini au juu.
Ndo maana ukitamka kwa jina la Yesu hakuna jinni Wala mchawi anaendelea kuwepo hapo kinachowakimbiza ni ile nguvu ya ule moto wa gesi unawachoma.
Na unapomtukana mtu unakuwa umeita nguvu ya uharibifu toka kwa mapepo ya kuzimu yaje yamdhuru uliyemtusi.
Ndo maana mtu akitukanwa anaumia kiletacho maumivu ni zile roho chafu toka kuzimu ulizoziita kupitia maneno uliyoyatamka zimuumize mhusika.
Kutukana ni kitendo Cha kuvuta roho chafu toka kuzimu.
Ndo maana kabla ya watu kupigana kwanza ni lazima watukanane yaani kuziinua zile roho chafu hizi uchochea hasira na mauti.
Kubariki au kuomba ni kitendo Cha kuvuta uwepo wa Mungu katika maisha yako.
Wewe hujengi hoja ila una tetea dini yako ya uislamu.Tatizo kubwa biblia ni mkusanyiko wa vitabu vilivyoandikwa na watu. Neno la Mungu halipo tena kwenye biblia, kama lipo ni asilimia ndogo sana iliyobaki nayo imechakachuliwa.
Neno la Mungu kwa (asilimia mia moja) 100% linabaki kuwa Qur'an peke yake. Imeteremshwa kuweka sawa kulipochakachuliwa neno la Mungu na kupotezwa zamani.
Soma Qur'an ujionee muujiza wake.
Kwa miaka zaidi ya 1,400 sasa kimebaki kuwa kitabu pekee kilichohifadhiwa mioyoni mwa watu wengi zaidi duniani nukta kwa nukta (to the dot).
Mumzibe mdomo nani?Asante sana mtu wa Mungu kwa somo zuri.Masomo km haya yaendelee kutolewa kwa kasi ili kuwaziba midomo wale wasemao hakuna Mungu.
Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Kwa ufupi ni kuamini kisemwacho katika Biblia kuhusu sisi. Mathalani, Zaburi 103:3: "Akusamehe maovu yako yote,Funguka zaidi mkuu, wengi tunafaike na hii elimu tusiyoifahamu bado.
Kutubu kwa binadamu na sio kwa Mungu ni aina gani ya kutubu?Kwa ufupi ni kuamini kisemwacho katika Biblia kuhusu sisi. Mathalani, Zaburi 103:3: "Akusamehe maovu yako yote,
Akuponya magonjwa yako yote."
Ukitubu dhambi zako kwa Mungu (si kwa wanadamu), kwanza anakusamehe na pili anakuponya pia. Double blessings!
Una uthibitisho yupo?Neno la Mungu linaponya,Neno la Mungu linaokoa ukiamini Mwenyezi Mungu atakupatia hitaji lako.Binafsi nina ushuhuda na neno la bwana amenitendea miujiza ambayo kibinadamu ilionekana ngumu.Ambao hawaamini katika uwezo wa Mwenyezi Mungu au uwepo wake hunisikitisha sana.Maana baada ya haya maisha ya duniani watapatwa na majuto pale ambapo waliyedhani hayupo YUPO.
We nawe jitu zima hovyo, hyo promo yako ushafeli. Kwani hicho kitabu chako si kimeandikwa na wanadamu?? Acha dharauTatizo kubwa biblia ni mkusanyiko wa vitabu vilivyoandikwa na watu. Neno la Mungu halipo tena kwenye biblia, kama lipo ni asilimia ndogo sana iliyobaki nayo imechakachuliwa.
Neno la Mungu kwa (asilimia mia moja) 100% linabaki kuwa Qur'an peke yake. Imeteremshwa kuweka sawa kulipochakachuliwa neno la Mungu na kupotezwa zamani.
Soma Qur'an ujionee muujiza wake.
Kwa miaka zaidi ya 1,400 sasa kimebaki kuwa kitabu pekee kilichohifadhiwa mioyoni mwa watu wengi zaidi duniani nukta kwa nukta (to the dot).
Hii dini siiamini kabisa aisee.Qur'an 20:
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0
1. T'AHA! 1
2. Hatukukuteremshia Qur'ani ili upate mashaka. 2
3. Bali ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea.3
4. Materemsho yatokayo kwa aliye umba ardhi na mbingu zilizo juu. 4
5. Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliye tawala juu ya Kiti cha Enzi. 5
6. Ni vyake vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, na viliomo baina yao, na viliomo chini ya ardhi. 6
7. Na ukinyanyua sauti kwa kusema...basi hakika Yeye anajua siri na duni kuliko siri. 7
8. Mwenyezi Mungu! Hapana mungu isipo kuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri kabisa. 8
9. Na je! Imekufikia hadithi ya Musa? 9
Soma zaidi: Al Baqara
Kimehifadhiwa mioyoni mwa binadam.We nawe jitu zima hovyo, hyo promo yako ushafeli. Kwani hicho kitabu chako si kimeandikwa na wanadamu?? Acha dharau
Safi sana, na Uislam hautaki yeyote aamini tu kama kipofu, unatakiwa ujiridhishe.Hii dini siiamini kabisa aisee.
Mungu anaepiganiwa na wanadam badala ya kujipigania mwenyewe.