Usafiri wa Anga Tanzania chini ya ATCL ni ghali kuliko hata usafiri kutoka Bara moja kwenda lingine kwa mataifa mengine

Nadhani moja ya sababu ni " ECONOMIES OF SCALE. Mifano uliotoa wanatumia ndege zinazibeba watu zaidi ya 250 and almost full booked. But still, Atcl na wenzake, nauli zipo unfairly high.
ujinga ni kutumia ndege za kurushwa masafa ya kimataifa kwa safari za ndani. kingine pale atcl kuna lundo la wafanyakazi waliajiriwa kiholela bin kujuana bado ufisadi. ukiwaza mambo ya ukimani utachanganyikiwa.
 
Ni wapi ulisoma kuwa sababu za kuanzisha upya Air Tanzania zilikuwa ni kushusha bei za nauli ya ndege?
 
Kufariki kwa Magufuli lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa nchi hii
 
Sema hapa kwenye magari hata JPM alifeli, yaani aliendelea kuifurahia kodi kubwa. Magari kodi ilitakiwa iwe sio zaidi ya 1/3 ya bei ya manunuzi. Punguza kodi, wengi wanunue magari upate kodi nyingi na maduka ya vipuri yaongezeke, unakua umekuza na ajira.
 
Fastjet si alikimbizwa ili watunyonye vizuri. Kutoka kumlaani kabaila mpaka kuwa kabaila.

Hapa tatizo serikali huwa hailipi ghalama zake, viongozi wanasafiri Bure tu bill zikija zinatupwa kabuni, inabidi wewe msafiri tukunyonye kufidia hasara ya viongozi.

Kumbuka mdaiwa sugu ni serikali, Hata World Bank and IFM wanalijua hili.
 
Inasikitisha sana flights hazigusiki ndani ya nchi – zinaonekana ni kwa ajili ya watu baadhi.

Leo hii wakipunguza gharama na kuongeza flights, kuna faida kubwa shirika litaingiza na kuchagiza uchumi.
Kweli kabisa, kuna abiria wengi tu hawajawahi kupanda tena ndege baada ya Fast Jet kufurumushwa. Yaani ATCL wangezidiwa na abiria.
 
Hii ndiyo shida ya monopoly, ATCL hakutaka ushindani zikafanywa figisu kuwatoa players wengine kwenye soko ili abaki mmoja tu atawale

Huko ulipotolea mifano unakuta mashirika yapo mengi kwa hiyo bei itakuwa nafuu maana watakuwa wanashindana kwenye bei ili kupata wateja hapa kwetu huna option aliyepo atapanga bei atakayo, hutaki ni mwendo wa magufuli pale ukachague ally's, kisbo, maning nice nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…