Usafiri wa Anga Tanzania chini ya ATCL ni ghali kuliko hata usafiri kutoka Bara moja kwenda lingine kwa mataifa mengine

Usafiri wa Anga Tanzania chini ya ATCL ni ghali kuliko hata usafiri kutoka Bara moja kwenda lingine kwa mataifa mengine

Nahisia kali sana juu ya hili suala ndani ya nchi, kuna mifumo engineered kuwafanya watu wakakaa na kuona umaskini, ukosefu wa standard nzuri ya maisha ni hali ya kawaida.

Hili halikubaliki!
Shida ya Tatizo hili inaanzia mbali:
1.SERA zilizopo zimeshindwa kutafsiri mabadiliko ya Dunia(Tulitoka kwenye ujamaa kuja soko huria, mfano kuagiza gari,kodi na tozo ni sawa na kununua gari 2,ni kama vile ni anasa kumiliki gari).
2.Mamlaka za usimamizi kushindwa kudhibiti anguko la thamani ya shilingi.
3.Mamlaka za upangaji wa bei na tozo mbalimbali kupanga bei kuongezeka hakuna siku wamekaa kushusha gharama(mfano Nauli ya daladala na mabasi,hata bei mafuta kwenye soko la dunia ikipungua,Mamlaka husika hazipunguzi bei) ,ni kama vile haya mambo yanafanywa kuwanufaisha wachache.
4.Mwekezaji akipanga bei ndogo ya huduma na bidhaa anajikuta anapigwa vita(mfano FastJet,),badala ya kujifunza kwa wenye uwezo wa kusha bei tunaleta zengwe na kuwakatisha tamaa.
5.Bado sheria za kodi hazina mtazamo wa "viwango vidogo vya kodi,wengi ili walipe "
 
Mambo haya yote na mengine mengi ambayo hujayaandika yamesababishwa ccm
Wanaiba sana pesa za uma. kupanda ndg kwenda na kurudi mara4 ni mtaji mjubwa kabisa wakuanzia biashara
ndogondogo na hii ccm wanajua tukitajirika wengi hatuta wasikiliza kwa porojo zao
 
Ni kweli kabisa kuna safari za mashirika mengine ya ndege Afrika kutoka nchi moja kwenda nyingine ambayo inachukua takribani masaa 4 angani lakini nauli yake ni cheap sana si zaidi ya dollar 150.

Na mara nyingi ndege za ATCL kwa viwango hivyo vya nauli seats nyingi zinakuwa wazi. Ndege ina siti zaidi ya 120 badala yake abiria wanakuwa ni 44 tu.

Naona kabisa hasara ni kubwa mno.
 
Usafiri wa anga nchini Tanzania ni usafiri ghali na wa gharama ya juu hadi kufikirisha ukilinganisha na mataifa mengine yakihusisha na safari kutoka bara moja hadi bara jingine.

Usafiri wa anga chini ya Air Tanzania kwa kiasi kikubwa ukisaidiana na Precision Air unaonekana kama umewalenga wanasiasa na wafanyabishara wakubwa.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Caracas, Venezuela hadi Madrid, Uhispania ni takriban $290 sawa na TZS 864,311 - hiyo ni nchi hadi nchi kwenye mabara mawili tofauti.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Bukoba, Tanzania hadi Dar es Salaam, Tanzania ni takriban TZS 631,000 sawa na €212 - hiyo ni mji hadi mji ndani ya nchi.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Fort Lauderdale, USA hadi Cartagena au Barranquilla, Colombia ni takriban $69 sawa na TZS 189,000 - hiyo ni nchi hadi nchi.

Safari ya ndege ya unganisho kutoka Mbeya, Tanzania hadi Mwanza, Tanzania ni takriban 1,100,000 sawa na $403 - hiyo ni jiji hadi jiji ndani ya nchi.

Hii ni mifano midogo sana maana kuna safari za kutoka Seoul, Korea Kusini hadi Barcelona kwa TZS 1,023,000.

Swali langu ni kwanini ATCL na washirika wake ndani ya nchi wana gharama kubwa katika usafirishaji! Je wanatumia teknolojia na mifumo tofauti na ghali ukilinganisha na mataifa mengine?

Ni sababu zipi za msingi zinazofanya flights za ndani ya nchi kuwa ghali maradufu kiuhalisia na hata ukilinganisha na mataifa mengine?

Ni maelekezo kutoka juu kuendelea kuwafinya watanzania wazidi kuishi kijamaa?

JamiiForums naomba msaada wa kuwatafuta ATCL, Mamlaka ya Anga na Wizara ya Uchukuzi watupatie ufafanuzi na statistics zinazohalalisha gharama za usafiri wa anga.
Nchi hizi za ulimwengu wa 3 Bado zimejenga Uchumi wa kikoloni na unyonyaji.

Harafu sio Tzn pekee ni African yote.

Ukitaka kwenda Lagos kutoka Dar gharama ni kubwa Bora utoke Dar Hadi London.
 
Wanasema kodi ya viwanja vya ndege Tanzania ipo juu sana ndio maana wageni wengi wanashukia Nairobi harafu wanaletwa na Coaster kutoka Nairobi au mwenye kampuni ya Utalii anapeleka gari lake Nairobi nadhani tuna shida sehemu sio bure ukishakata hiyo Tiketi ukaangalia hiyo kodi na bei ya nauli zimetofautiana kidogo sana..
 
Sasa hapo utashangaa Fast Jet alifanya kazi nchi hii hii lakini bei ilikua chini na hakuendesha shirika kwa hasara. Watu walikula sana mwewe Mwanza Dar kwa siku zilikua safari 4 hivi kwenda na 4 kurudi na zote ndege zinajaa abiria
Kuna mda ukitafakari hupati majibu kabisa kuna mambo mengi ya hovyo sana
 
Kuna risk kubwa sana kwa pilots unaendesha ndege mbovu, au zisizo brand za abiria za made in Korea au China etc roho mkononi

Compensation ya mshahara lazima iwe kubwa kwa pilots na cabin staff
Acha uongo china wameanza kuzalisha ndege za majaribio recently wapo kwenye majaribio tena bado hawajaanza kufanya mass production acha uongo

Ndege nyingi za abiria zinanazalishwa na boeing au airbus
Mfano korea hawana historia yeyote ya kuzalisha ndege
 
Nauli ya ndege Dar mwanza ni kama Dar Dubai. Tanzania shida iko kwenye idadi ya ndege.

Tuko Milioni 65+ lakini ndege hazizidi 28, hizo hizo zitumiwe na viongozi wa serikali, hizo hizo wananchi wa kawaida.

Shida iko kwenye idadi ya ndege zilizopo na mahutaji ya ndege kua makubwa sana lakini fleet yetu bado haikui kuendana na mahitaji makubwa ya usafiri wa anga.
 
Usafiri wa anga nchini Tanzania ni usafiri ghali na wa gharama ya juu hadi kufikirisha ukilinganisha na mataifa mengine yakihusisha na safari kutoka bara moja hadi bara jingine.

Usafiri wa anga chini ya Air Tanzania kwa kiasi kikubwa ukisaidiana na Precision Air unaonekana kama umewalenga wanasiasa na wafanyabishara wakubwa.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Caracas, Venezuela hadi Madrid, Uhispania ni takriban $290 sawa na TZS 864,311 - hiyo ni nchi hadi nchi kwenye mabara mawili tofauti.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Bukoba, Tanzania hadi Dar es Salaam, Tanzania ni takriban TZS 631,000 sawa na €212 - hiyo ni mji hadi mji ndani ya nchi.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Fort Lauderdale, USA hadi Cartagena au Barranquilla, Colombia ni takriban $69 sawa na TZS 189,000 - hiyo ni nchi hadi nchi.

Safari ya ndege ya unganisho kutoka Mbeya, Tanzania hadi Mwanza, Tanzania ni takriban 1,100,000 sawa na $403 - hiyo ni jiji hadi jiji ndani ya nchi.

Hii ni mifano midogo sana maana kuna safari za kutoka Seoul, Korea Kusini hadi Barcelona kwa TZS 1,023,000.

Swali langu ni kwanini ATCL na washirika wake ndani ya nchi wana gharama kubwa katika usafirishaji! Je wanatumia teknolojia na mifumo tofauti na ghali ukilinganisha na mataifa mengine?

Ni sababu zipi za msingi zinazofanya flights za ndani ya nchi kuwa ghali maradufu kiuhalisia na hata ukilinganisha na mataifa mengine?

Ni maelekezo kutoka juu kuendelea kuwafinya watanzania wazidi kuishi kijamaa?

JamiiForums naomba msaada wa kuwatafuta ATCL, Mamlaka ya Anga na Wizara ya Uchukuzi watupatie ufafanuzi na statistics zinazohalalisha gharama za usafiri wa anga.
Dar - Kigoma round trip 750,000/=. In short tuna nchi la hovyo sana! Viongozi wetu wote ni average people wala hawana tifauti na mwananchi wa SangaMwalugesha! Au Itongolyangamba! Fast Jet alitaka kuleta mabadiliko akapiga spana!
 
Usafiri wa anga nchini Tanzania ni usafiri ghali na wa gharama ya juu hadi kufikirisha ukilinganisha na mataifa mengine yakihusisha na safari kutoka bara moja hadi bara jingine.

Usafiri wa anga chini ya Air Tanzania kwa kiasi kikubwa ukisaidiana na Precision Air unaonekana kama umewalenga wanasiasa na wafanyabishara wakubwa.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Caracas, Venezuela hadi Madrid, Uhispania ni takriban $290 sawa na TZS 864,311 - hiyo ni nchi hadi nchi kwenye mabara mawili tofauti.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Bukoba, Tanzania hadi Dar es Salaam, Tanzania ni takriban TZS 631,000 sawa na €212 - hiyo ni mji hadi mji ndani ya nchi.

Safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Fort Lauderdale, USA hadi Cartagena au Barranquilla, Colombia ni takriban $69 sawa na TZS 189,000 - hiyo ni nchi hadi nchi.

Safari ya ndege ya unganisho kutoka Mbeya, Tanzania hadi Mwanza, Tanzania ni takriban 1,100,000 sawa na $403 - hiyo ni jiji hadi jiji ndani ya nchi.

Hii ni mifano midogo sana maana kuna safari za kutoka Seoul, Korea Kusini hadi Barcelona kwa TZS 1,023,000.

Swali langu ni kwanini ATCL na washirika wake ndani ya nchi wana gharama kubwa katika usafirishaji! Je wanatumia teknolojia na mifumo tofauti na ghali ukilinganisha na mataifa mengine?

Ni sababu zipi za msingi zinazofanya flights za ndani ya nchi kuwa ghali maradufu kiuhalisia na hata ukilinganisha na mataifa mengine?

Ni maelekezo kutoka juu kuendelea kuwafinya watanzania wazidi kuishi kijamaa?

JamiiForums naomba msaada wa kuwatafuta ATCL, Mamlaka ya Anga na Wizara ya Uchukuzi watupatie ufafanuzi na statistics zinazohalalisha gharama za usafiri wa anga.
FAST JET warudi haraka sana
 
Hili ni ukweli kabisa.

Haya mashirika ya ndege ATCL na Precision Air yana wafanyakazi wengi sana.

ATCL kila mtu anajikuta bosi.

Precision Air ina ndege nne tu zinazo operate. Lakini ina wafanyakazi wengi sana.

Sasa kwa hali kama hii, Lazima tu watapandisha gharama ya nauli.
Wengi wangapi? Malizia
 
Hii
Wakifanya laki 3 iwe ni gharama za wastani za kusafiri miji mikubwa Tanzania nadhani watapata wateja wengi na faida kubwa baada ya muda fulani.

Hata kama wanasema booking ya mapema ina gharama lakini hizo gharama ni kubwa sana, haijulikani kama wameakisi uchumi wa mtanzania mwenye maisha ya kawaida au kulenga mafisadi wenzao hiko serikalini.

Halafu unaambiwa hizo ndege zimenunuliwa kwa pesa ya mlipa mkodi 😂, mlipa kodi mwenyewe anaiona ndege pichani tu 😂.

Hii nchi watu hawajagundua wana haki gani na wanapaswa kuishi maisha ya aina gani, siku wakijitambua watapambana kwa nguvu kupata haki zao. Halafu watajiona wajinga walikuwa wapi kuteseka miaka yote na kujihisi walirogwa.
Hii inch imejaa wezi, Ina viongoz wa ajabu sana, rushwa, ufisadi na Kila Haina ya uhuni, na wanainch hawana habari
 
Back
Top Bottom