Usafiri wa basi na kero ya kelele za muziki

Usafiri wa basi na kero ya kelele za muziki

The golden

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2018
Posts
1,382
Reaction score
2,582
Kutokana na hali mbaya ya uchumi, watu wengi tunatumia usafiri wa basi kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine. Mabasi ya siku hizi yanakuja na Tv set. Wamiliki wa mabasi haya wana tabia ya kufungua mziki kwa sauti kubwa sana wakidhani labda ni burudani kwa abiria wote waliomo ndani ya basi husika.

Kiwango cha sauti kinapokuwa kikubwa hugeuka kuwa kero hasa unapokuwa na safari ndefu mfano kutoka Dar mpaka Mwanza. Siyo kila mtu anahitaji kelele hizo. Wapo watu wanasafiri na Tablets au vitabu wangependa kujisomea ndani ya basi wakiwa wanasafir safari ndefu kama hiyo. Wapo watu wanaopenda utulivu na ukimya ili watafakari mambo yao wakiwa safarini, hivyo mziki wa sauti ya juu ni kero kwao.

Ningependa kushauri wamiliki wa mabasi kuweka headphones kwenye kila siti ili anayependa kusikiliza mziki afanye hivyo kwa manufaa yake binfsi. Mazingira ya chombo cha usafiri yasigeuke kero.

Napenda kumaliza kwa kusema kelele ina uhusiano mkubwa sana na umasikini, ujinga.

Jiulize maswali haya:

1. Kwa nini kwenye usafiri wa ndege hakupigwi mziki mkubwa? Halafu Angalia aina ya watu wanaopanda ndege.

2. Kwanini maeneo wanaoyoishi watu wenye mafanikio hayana makelele? Angalia Masaki, Osterbey au Upanga halafu linganisha na maeneo wanaishi watu masikini.

3. Kwanini baa au sehemu za kupumzika wanazoenda watu waliofanikiwa hazina mziki mkubwa? Halafu linganisha na baa za makabwela.
 
Ni keroo kama haya mabus ya nyanda za juu kusini yamegeuka vibanda umiza wanaweka movies zilizotafrisiwa mara za mkojani mara nyimbo za Wasafii ni keroo tupu mamlaka husika angalieni hili.
 
Nacho uliza vipi kuhusu haki za wale wajinga na maskini walio wengi wanaopenda hizo movie na makelele? Na wao si wamelipa nauli sawa na wale wa masaki ili wasafiri? Binafsi sipendi yale mamuvi bora hata muziki tena ukute pembeni nakolezea safari na kasavana au karedds ndo dahh
 
Point kubwa sana umetoa mkuu. Kuna mambo ya miziki au movie za kina Mkojani. Unakuta movie moja inarudiwa safari nzima tena kwa sauti kubwa.

Basi lenye abiria takriban 65 haliwezi kuwa na taste moja ya aina ya movie/music na level ya kelele/sauti ya vitu hivyo vikichezwa. Lakini unakuta kwa utashi wa dereva na utingo wake wanaweza fululiza kuweka nyimbo za kwaya/kaswida safari yote kusahau kuwa basi linabeba watu wa imani tofauti.
 
Point kubwa sana umetoa mkuu. Kuna mambo ya miziki au movie za kina Mkojani. Unakuta movie moja inarudiwa safari nzima tena kwa sauti kubwa.

Basi lenye abiria takriban 65 haliwezi kuwa na taste moja ya aina ya movie/music na level ya kelele/sauti ya vitu hivyo vikichezwa. Lakini unakuta kwa utashi wa dereva na utingo wake wanaweza fululiza kuweka nyimbo za kwaya/kaswida safari yote kusahau kuwa basi linabeba watu wa imani tofauti.
Hawa jamaa acha atu.
 
Nacho uliza vipi kuhusu haki za wale wajinga na maskini walio wengi wanaopenda hizo movie na makelele? Na wao si wamelipa nauli sawa na wale wa masaki ili wasafiri? Binafsi sipendi yale mamuvi bora hata muziki tena ukute pembeni nakolezea safari na kasavana au karedds ndo dahh
Ili kulind haki yao, ndio maana tumeshauri wamiliki wa haya mabasi waweke Headphones kwenye kila siti ili kila mtu apate haki yake bila kumkera mtu mwingine.
 
Kuna Basi la IMANI Dar - Mbeya , sikutegemea kuwa na nyie mnaweka sauti kuuubwa hivyo, basi lenu la kiistaarabu,
rekebisheni sauti, yaani kadiria kwamba mtu anasikia kitu kinachoendelea ila hakereki. yaani hata akitaka kuongea na simu isiwe shida, sasa unakuta unaongea na simu mpaka mtu anakuuliza '' uko wapi hapo ? "
 
Kutokana na hali mbaya ya uchumi, watu wengi tunatumia usafiri wa Basi kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine. Mabasi ya siku hizi yanakuja na Tv set. Wamiliki wa mabasi haya wana tabia ya kufungua mziki kwa sauti kubwa sana wakidhani labda ni burudani kwa abiria wote waliomo ndani ya basi husika.
Hili ni tatizo Kwa kweli
 
Kutokana na hali mbaya ya uchumi, watu wengi tunatumia usafiri wa Basi kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine. Mabasi ya siku hizi yanakuja na Tv set. Wamiliki wa mabasi haya wana tabia ya kufungua mziki kwa sauti kubwa sana wakidhani labda ni burudani kwa abiria wote waliomo ndani ya basi husika.

Kiwango cha sauti kinapokuwa kikubwa hugeuka kuwa kero hasa unapokuwa na safari ndefu ya kutoka Dar mpaka Mwanza. Siyo kila mtu anahitaji hizo kelele. Wapo watu wanasafiri na Tablets au vitabu wangependa kujisomea ndani ya basi wakiwa wanasafir safari ndefu kama hiyo. Wapo watu wanaopenda utulivu na ukimya ili watafakari mambo yao wakiwa safarini, hawa mziki wa sauti ya juu ni kero kwao.

Ningependa kushauri wamiliki wa mabasi waweke Headphones kwenye kila siti ili anayependa kusikiliza mziki afanye hivyo kwa manufaa yake binfsi. Mazingira ya chombo cha usafiri yasigeuke kero.

Napenda kumaliza kwa kusema kelele ina uhusiano mkubwa sana na umasikini, ujinga. Jiulize maswali haya:
1. Kwa nini kwenye usafiri wa ndege hakupigwi mziki mkubwa? Halafu Angalia aina ya watu wanaopanda ndege

2. Kwanini maeneo wanaoyoishi watu wenye mafanikio hayana makelele? Angalia Masaki, Osterbey au Upanga, halafu linganisha na maeneo wanaishi watu masikini.

3. Kwanini baa au sehemu za kupumzika wanazoenda watu waliofanikiwa hazina mziki mkubwa? Halafu linganisha na baa za makabwela.
Ni ukweli usiopingika. Tafadhali Mamlaka inayohusika ifuatilie kero hii. 'Noise pollution' inayosababishwa na sauti iliyopitiliza kiwango ndani ya baadhi ya mabasi yetu inakera na kuathiri 'comfortability' na afya za abiria.

Sababu mojawapo ya kufunguliwa sauti kubwa ndani ya mabasi haya ni kuhakikisha 'speed limit alarm' haisikiki wakati imefikiwa, hivyo kukuta dereva anaendesha mwendo wa kasi uliopitiliza kiwango kilichotegeshwa i.e. 80Km/hr
 
Sio muziki tu na zile movie zao za kina Mkojani na Tin white, yaani inakera sana au wanaweka movie za kutafsriwa!
Mkuu kwa upande wa movie hapo kidogo unataka kupotoka ile ni comedy ya kibongo ifike mahali tupende vya kwetu bongo movie mmediss sasa hata comedy mkuu?
 
Sauti kubwa,muvi au nyimbo zinarudiwarudiwa hovyo
 
Back
Top Bottom