Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wamechelewa Sana, bado UK Aid, DANIDA, KOICA na NORAD, hii misaada imetufanya tuwe maskini, tunalala na kuzaliana kusubiri tuletewe mipira ya uzazi, chanjo, kukatwa mikono sweta na USA kwa msaada wa watu wa Marekani.Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) limetangaza kusitisha utoaji wa fedha mpya na usambazaji wa fedha chini ya makubaliano ya malengo ya maendeleo (DOAGs) hadi uhakiki wa programu za msaada wa nje zinazofadhiliwa na USAID utakapokamilika.
Wakati mchakato wa kuhakikisha msaada wote wa nje unalingana na ajenda ya sera ya nje ya Rais Donald Trump ukitarajiwa kutolewa ndani ya siku 30, uhakiki huu unatarajiwa kukamilika ndani ya siku 85 kuanzia Januari 24, 2025.
Kutokana na hilo, USAID imewaagiza maofisa wote kusimamisha kazi, mishahara, na safari kwa asasi na taasisi zote zilizopokea misaada kupitia shirika hilo.
Hayo yamebainishwa kupitia barua rasmi kwa maofisa wa mikataba na makubaliano ya USAID na washirika wake, iliyotolewa na shirika hilo Januari 24, 2025.
Barua hiyo, iliyosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Manunuzi wa USAID, Jami J. Rodgers, imeeleza uamuzi huo unatokana na utekelezaji wa agizo la Rais Trump la kurejelea na kurekebisha misaada ya nje ya Marekani.
Soma kwa undani katika tovuti ya Mwananchi.
View attachment 3215692
Kwa msaada wa watu wa Marekani.
TRump kishateua Administrator wa USAID, shirika linazikwa hilo.Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) limetangaza kusitisha utoaji wa fedha mpya na usambazaji wa fedha chini ya makubaliano ya malengo ya maendeleo (DOAGs) hadi uhakiki wa programu za msaada wa nje zinazofadhiliwa na USAID utakapokamilika.
Wakati mchakato wa kuhakikisha msaada wote wa nje unalingana na ajenda ya sera ya nje ya Rais Donald Trump ukitarajiwa kutolewa ndani ya siku 30, uhakiki huu unatarajiwa kukamilika ndani ya siku 85 kuanzia Januari 24, 2025.
Kutokana na hilo, USAID imewaagiza maofisa wote kusimamisha kazi, mishahara, na safari kwa asasi na taasisi zote zilizopokea misaada kupitia shirika hilo.
Hayo yamebainishwa kupitia barua rasmi kwa maofisa wa mikataba na makubaliano ya USAID na washirika wake, iliyotolewa na shirika hilo Januari 24, 2025.
Barua hiyo, iliyosainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Manunuzi wa USAID, Jami J. Rodgers, imeeleza uamuzi huo unatokana na utekelezaji wa agizo la Rais Trump la kurejelea na kurekebisha misaada ya nje ya Marekani.
Soma kwa undani katika tovuti ya Mwananchi.
View attachment 3215692
Kuna watu wengi sana wamegeuza huu ugonjwa mtaji, ile barabara ya mikocheni kuna vi NGO kibao vinapiga pesa kwa kisingizi cha awareness, hakika nawahakikishia, huu ugonjwa ukinyimwa funding, utapotea wenyewe moja kwa moja..Yale ma deals ya TACAIDS ndio basi tena.......Kumaanisha!!![]()
Ss kuna Vi NGO vitakufa kifo cha mende..vile vilikuwa vinasurvive kwa ajili ya ukimwi vitapata mhaho..Kuna watu wengi sana wamegeuza huu ugonjwa mtaji, ile barabara ya mikocheni kuna vi NGO kibao vinapiga pesa kwa kisingizi cha awareness, hakika nawahakikishia, huu ugonjwa ukinyimwa funding, utapotea wenyewe moja kwa moja..
Ni kama Corona, ukileta tu funding, unashangaa ugonjwa unalipuka upya!!
Hatariiiiiizzzzz......Umasikini na ugonjwa ni vitu viwili tofauti.., hiyo lishe unatoa wapi wakati hata milo miwili tu ya makande kwa siku ni shida?
- Hivi unafahamu kwamba Ukimwi (AIDS) sio ugonjwa, bali ni mkusanyiko wa magonjwa yanayosababishwa na kushuka kwa kinga mwilini? Mfano T.B
- Unafahamu kwamba magonjwa hayo yote yana tiba kamili zinazofahamika?
- Unafahamu kwamba mtu anaweza kupata magonjwa hayo bila hata kuwa na upungufu wa kinga mwilini? (Ukimwi?)
- Unafahamu kwamba magonjwa mapya yaliyo ndani ya kundi hilo yalipngezeka baada ya matumizi ya ARVs, nayo ni Kufeli ini, kufeli figo, na kufeli Moyo?