Hivi kuna mtu yeyote anaefuatilia Olimpic games na kumuona huyu Usain Bolt anachokifanya?
hivi inawezekana binadaamu wa kawaida akafanya hivi?
yaani mtu akimbie hadi kuamua kukimbia huku anawatazama wenzie tu wasimzidi
nikama vile yuko mazoezini na watoto wa chekechea...
is this normal?
binafsi nakataa kuamini
hasa baada ya kusoma historia ya Carl Lewis....
ambae nae alikuwa anavunja rekodi za kila aina
kumbe alikuwa anatumia drugs na hakuwahi kukamatwa hadi ana staafu
kuna kipindi alishinda shindano la mbio huku aliowashinda wengine saba wote walikuwa wanatumiaL
madawa.....aliekuja kukamatwa alikuwa Ben Johnson wa Canada....
Karl Leewis alikuwa wa pili huku wengine saba wote ni drugs tupu....
Binafsi naamini Usain Bolt hana tofauti na Lance Armstrong ...
only time will tell.......
Mkuu umezungumza kitu kilicho kuwa moyoni mwangu kwa muda mrefu, kuna vitu mwanadamu anaweza kufanya ambavyo vinaonekana ni natural, lakini vitu vingine vinakuwa beyond human endurance na ngumu ku comprehend kama unacho ona kina ukweli wowote au kuna udanganyifu wa kibaiolojia wa ku tax mwili - kisa, ushinde medali by all means - ujali long term madhala ya ku abuse madawa.
Kimaumbile binadamu kadri miaka inavyo kwenda na wewe stamina inapungua hata ufanye mazoezi ya kufa mtu aisandii kitu - sasa huyu Usain Bolt awezi akawa na uwezo wa kushinda tuu kwa muda wote wa miaka kumi na mbili - hii aingii akilini hata kidogo, Usain Bolt angekuwa ni Mrusi basi Waingereza na Wamerikani wangelazimsha achukuliwe samples za damu na urine kwa mara ya pili ili zifanyiwe uchunguzi wa kina au hata kudanganya kwa kuzi- contaminate aonekane ni mdanganyifu.
Nashukuru kwa kunikumbusha visanga vya Lance Amstrong na Karl Lewis na wenzake, nikiona America inawakomalia Warusi mpaka kufikia hatua ya kumlahumu Putin, ndiyo nawaona walivyo wanafiki -niliangalia michezo ya Olympic ya 1988, mpaka leo hii na amani kwamba hata kama Johnson asingetumia dawa angeweza kumshinda Lewis kirahisi - baada ya Lewis kushindwa alitoka pale uwajani anafoka foka kuhusu ushindi wa Johnson kwamba ushindi wake unatokana na matumizi ya madawa - suala hilo alilivalia njuga kweli kweli mpaka anafikia kuonekana kero! Kumbe shutuma anazo msema mwenzake kumbe na yeye ni teja mzuri tu!!
Haya tuje kwa Lance Amstrong, yeye alikuwa anashinda tu mbio za baiskeli miaka nenda rudi mpaka wezake wanashangaa, katumia madawa kwa muda mrefu mpaka yakamsababishia ugonjwa wa cancer, cha ajabu ni kwamba wasimamizi wa mbio za baiskeli walikuwa awajui kwamba Amstrong alikuwa atumia dawa za kuongeza nguvu/stamina - walijua sana lakini walikuwa wanamfuchia siri, sijui nani alifichua siri yake.