Usaliti ulivyogharimu maisha ya watu niliowapenda

Usaliti ulivyogharimu maisha ya watu niliowapenda

IMG_3954.jpeg
 
Inaendelea, No 2

Nilivyorudi home nikawa na mixed feelings, niliumia kumsaliti mpenzi wangu lakini pia nilienjoy show ya mtoto Lily nikawaza mbona hafananii? alionekana ni binti mpole sana asiye na hatia lakini kitandani kiboko, anyway nikamcall na kumwambia kilichotokea kiishe kisijirudie tena, akaitikia kinyonge sana na maisha yakaendelea, mawasiliano yalikuwepo ila nilikua namkwepa sana tusionane,
Siku moja ofisini kwetu kukawa na event Znz, tulialika watu na yeye nikamualika so akawa ni mgeni wangu, tulivyofika Zenji tukafikia hotel ila wageni walipewa pesa cash wajichagulie wao pakulala kama mtu ana ndugu ruksa au kama watashea room ni wao tu, basi Lily akaniomba ashee room na mimi ili asave pesa yake, nilijiwazia sana ila nikaona fresh huyu ni mwanafunzi acha asave pesa itamsaidia, usiku ulikua mrefu sana kwetu uvumilivu ulinishinda nikasaliti tena mahusiano yetu, tulikaa Znz for 3 days tuliienjoy each other, tulivyorudi Dar penzi likaiva, likawa shata shata,

About my babe, yeye alikua nje ya nchi kikazi, ndani ya Mwaka tulionana mwezi mmoja au mitatu, inategemea na likizo, ni kazi ambayo kwa pamoja tuliiridhia ili tufanikishe malengo yetu, ila hii sijaiweka kama kutetea usaliti wangu, bado nilikosea, mahusiano yetu yatafikisha miaka 10 huu mwaka,

Kupeleka story mbele, baada ya mwaka mmoja wa mahusiano yetu na Lily,
Mwaka 2021 September, babe wangu alikuja for my birthday katika vitu hawezi kumiss ni birthday yangu, so tukasafiri nje ya Dar, just kuenjoy pamoja, nikampanga Lily kua babe wangu amekuja na tunasafiri asinitafute mpaka nitakaporudi hapo ndio niliamsha a monster inside her, hakuweza kuvumilia kukaa bila mawasiliano, alipiga simu na kutuma meseji nonstop, kiufupi alichanganyikiwa alisema kila giza likiingia anawaza kuna mtu mwingine ananigusa basi anapata ukichaa, usumbufu ulikua mkubwa ikabidi nimblock kila sehemu, babe wangu nilimpanga ni simu za kazi anaelewa pia aliniamini sana,
Lily alipogundua nimemblock akatumia namba nyingine kupokea alikua ni yeye analia sana, niliumia hua sipendi kuona mtu analia hata awe nani, nikamtuliza akatulia nikapanga nikirudi Dar inabidi nimmwage haraka bila hivyo ataniharibia mahusiano yangu maana hakuweza kula na kipofu....

Itaendelea
Endelea kuishusha
 
Inaendelea No 3,
Nilirudi Dar na babe wangu aliondoka kurudi kazini, ndio nikapata nafasi ya kumpigia simu Lily na kumwambia tukutane kwenye mgahawa flani upo town, alifurahi sana akasema kwanini nisiende kwake amenimiss and stuff nikamwambia nope, tunahitaji kuonana pale basi jioni kweli tukakutana, alionekana mchangamfu kupita maelezo hadi nilimshangaa nikajiuliza kanywa pombe lakini hapana hua hanywi pombe basi nikajisemea labda alinimiss sana, ilikua ngumu sana kumwambia kua nataka kukatisha usaliti wangu nilizunguka sana hatimae nikampasulia ukweli, alitulia tuliiii, aliniangalia usoni kama dakika 2 hivi akacheka kidogo kisha akasema niende nyumbani atanitafuta baada ya siku 5, akaongeza kua sio akili yangu ni hiyo vacation imenichengua akili, ila nitarudi kua normal after sometimes kisha akaondoka haraka nikama hakutaka nimuone akilia, niliganda pale nikimtafakari nikaona isiwe shida nikamblock tena nikarudi home, alipiga akakuta block lakini mimi naona kua alinitafuta,
Baada ya siku 5 nikapokea simu kwenye namba ngeni akajitambulisha ni yeye na angependa twende Bagamoyo amesha arrange kila kitu, nikamjibu politely kabisa nimetingwa na kazi hadi wakati mwingine, akasema basi walau nimuone hata dakika 5 nikamwambia sina muda nikakata simu, baada ya muda mlango ukagongwa kutoka nje ni kijana anayetufanyia usafi anasema kuna mgeni wangu getini mmh nikapata wasiwasi kidogo sababu kwanza hua sileti mtu nyumbani kwangu akiwemo Lily hakuwahi kupajua kwangu, pili kwa wanaopajua hawawezi kuja bila kunipigia simu, nikamwambia kijana anisindikize, nafika nje namkuta Lily amebadilika sana, nywele zake ndefu na nzuri kazinyoa sijui kiduku sijui kijogoo, yule msichana mrembo mwenye uso usio na hatia alibadilika na kua kwenye muonekano wa kiume, alichora tattoo kubwa mkononi yenye jina langu, nilishangaa hadi nilitaka kudondoka, akavunja ukimya wa mshangao wangu kwa kunisalimia na kunitaka radhi kwa kuja bila taarifa, hapo ndio aliponizindua na kumuuliza amefikaje pale, akasema alikua anapajua maana alinifatilia siku nyingi kujua ninapoishi na mara kadhaa alifika pale bila kuniambia, kiufupi mchepuko alikua ananispy kama nachepuka dah😄
Nikamwambia aondoke haraka na asinisumbue nina kazi nyingi, wakati nataka kuondoka akanishika mkono kwa nguvu niliona moto mkali kwenye macho yake yaliyojaa hasira, nikasema kwa nguvu NIACHEEEE yule kijana akaingilia kati na kumtaka aondoke mara moja, mimi nikakimbilia ndani na kuwaacha nje, akasema nitakusubiri hapa hapa hadi utakapoamua kuondoka na mimi, geti lilifungwa na yeye alibaki nje.....

Itaendelea
 
Back
Top Bottom