Ushabiki wa Simba na Yanga umewapumbaza Watanganyika

mtoa hoja akili ndogo sana, huu ni ujinga tu ulioandika hapa
 
Heshima kwako Mkuu

Hoja zako zinaelezea vile u-mgeni hapa Tanzania.

Kifupi sana, Yanga na Simba zilikuwepo kabla ya TAA, TANU, ASP na CCM, kabla ya uhuru wa Tanganyika, kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar,kabla ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Maana yangu ni kuwa, watu walizijua Yanga na Simba kabla hawajawa huru. Shida ipo wapi kupenda vitu walivyoanzisha miaka 80+ iliyopita?
 
Wewe unamatatizo ya akili kwani nani kakuambia anataka nchi iendelee kwani tutaishi milele hapa
 
Yaani leo vijiweni ni habari ya yanga na simba na hawajuwi kesho yao ....hata diko la mchana ni shida aiseeeh Ujinga umetukuka..
 
Pole! Sikujua naongea na mtoto. Yawezekana umasikini wako mechanical na ushabiki wa kidwanzi...
Anyway, jana niliona Mama Samia anawapigia simu mkiwa uwanjani basi mkaridhiiika mwenyewe kumbe nyuma ya pazia anawapiga tu Malimbukeni nyie
 
Kabla ya simba na Yanga kuongeza ushawishi nyie wazee mlifanya nini enzi zenu ? Kwanini msingetuunganisha na Rwanda badala ya Zenji hamkuona hata ni jinsi gani Rwanda ina mademu wakali?
 
Pole! Sikujua naongea na mtoto. Yawezekana umasikini wako mechanical na ushabiki wa kidwanzi...
Anyway, jana niliona Mama Samia anawapigia simu mkiwa uwanjani basi mkaridhiiika mwenyewe kumbe nyuma ya pazia anawapiga tu Malimbukeni nyie
Mpira na siasa kwa Tanzania huwezi kuvitenganisha. Wanasiasa wanalijua hilo na SSH keshaanza kampeni zile pana za kutafuta kura za 2024-25.

Sio mtoto mdogo, nazielewa sana siasa za nchi hii kwa miaka 43 sasa. Sipendi hulka za kishamba za kudhani kuwa michezo inahusika moja kwa moja katika kukuongezea umaskini wako binafsi.
 
Watanzania wanachotaka ni amani tu ili wafanye shuhuri zao,

Sasa nyie na chuki zenu sababu mtawala ni muislam mnataka kila mtu awafuate nyie mnaoendeshwa na chuki, nyie jazaneni ujinga huko kwenye makanisa yenu ya kilanguzi na utapeli,serikali itahakikisha ulinzi na usalama unaimalika ipasavyo, mara chache serikali na vyombo vya ulinzi vitaingilia kuwakoa nyie mazuzu dhidi ya hao wachungaji matapeli wanaowafirisi, mfano nabii wenu kiboko ya wachawi keshafukuzwa nchini,

Amani ndio jambo la msingi,sio izo chuki zenu kwa viongozi zenye mlengo wa kidini, mngekuwa na akili na ufahamu msingekuwa mnatapeliwa na hao manabii na wachungaji kila siku.
 
Tanzania ni nchi kamili tangu mwaka 1964, wewe ukiwa mtoto wa 2000 hayo ni matatizo yako binafsi. Tambua hivyo mleta mada.
 
Yaani leo vijiweni ni habari ya yanga na simba na hawajuwi kesho yao ....hata diko la mchana ni shida aiseeeh Ujinga umetukuka..
Hii ni ajabu sana,ghafla Mzee Magoma ndio habari kubwa.
 

Umepita kwenye majukwaa ya MMU kujiridhisha?
 
Kushabikia hizi timu sioni shida shida nayoiona muda wa kuzizungumzia timu hizi umekuwa kero iwe makazini au kwenye biashara.
Jitu tangu asubuhi hadi jioni hana stori zingine za kijiongezea kipato kakalia Simba na Yanga akitoka hapo anaanza kulalamika maisha magumu.
 
Hakuna kilichouzwa wala kitakachouzwa, tujilaumu sisi wenyewe na tabia zetu za uvivu na wizi mkubwa kila tunapopewa kuendesha mashirika. Hatuna kabisa nidhamu ya uendeshaji halafu tunakuwa wepesi kunyooshea vidole viongozi wenye maono ya kutaka kuyatoa haya mashirika kwenye hatua mmoja na kuyasogeza mbele zaidi.

Hiyo bandari ilijaa wizi na ufisadi mpaka Paul Kagame akamkejeli Kikwete kwamba anao uwezo wa kuiendesha Tanzania kwa kutumia bandari peke yake!, Leo kaja SSH mwenye utayari wa kufanya kile alichokiongea Kagame na wanaibuka wapumbavu wa humu JF na kuanza kusema eti kauza bandari!.

Pale Airport kuna kampuni ya Swissport ipo kwa miaka karibu 30 inafanya kazi, ina maana tumeuza pia uwanja wetu wa ndege wa Dar kwa wazungu?.

Tuchangamke vichwani, tuchangamkie elimu za mashuleni, uwepo utayari wa dhati wa kubadilisha mifumo ya elimu ili tuweze kwenda sambamba na ushindani wa kidunia, hii dunia kwa bahati mbaya huwa haimsubiri mtu aamke yenyewe inakwenda kwa kasi siku zote.

Kuipenda Simba au Yanga ni masuala binafsi tukizingatia hii ni dunia ya simu janja za viganjani. Kila mtu anao uhuru wa kuipenda Real Madrid, Barcelona, Manchester United au Arsenal, huwezi kumpangia mtu cha kufanya ni upuuzi na ukosefu wa elimu na ustaarabu pia.
 
Huu upumbavu umedumaza akili za vijana wa Tanganyika kabisa, hawafikirii maendeleo ya nchi yetu, changamoto gani zipo wazijadili namna ya kuzitatua, midahao vyuo vikuu haipo kutwa kucha wanaongelea Yanga, Simba na kubeti lakini general knowledge hawana. Tunatengeneza taifa la kipumbavu kabisa lisilokuwa na muelekeo wowote. Nchi yetu bado kuna maeneo mengi hayana barabara tena mbaya zaidi yapo katikati ya majiji kama vile barabara ya kutoka Mkuyuni kupitia Mahina Kanyerere Nyangulugulu hadi Mwatex Jijini Mwanza, huduma za maji safi maeneo ya Nyegezi, Mkolani, Igoma, Kisesa Jijini Mwanza. Huduma ya upatikanaji wa madawa mahospitalini ni changamoto kubwa pia lakini vijana hawayajadili hayo wamekalia Simba Day, Wiki ya Mwananchi, magoli ya mama hadi wengine wanataka kutoana roho kwa ushabiki wa kijinga usiokuwa na tija.
 
Na sasa tuna Mpango wa kuwapa wewekezaji wa kuwa saidia , ili timu ziweze kufanya vizuri zaidi.
 

Napishana na coaster nyingi zinaelekea Dar eti Simba Day.


Hizo timu ni project ya CCM ndiyo maana mchakato wa mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji yanasusua


Uchawi wa CCM/Mafisadi wa mali za umma upo kwenye muvi, Simba & yanga na Mwenge.


Umeniwahi nilitaka kuanzisha uzi kama huu huu!

Nadhani pia kinachosababisha wengi hasa vijana kutojua lolote linalowahusu ni ELIMU vijana Wakenya ni wasomi! wanajua Generation Z tulitakiwa tutendewe nini kitaifa, sisi tunajua ubaya ubwela

Juzi nimewapa makavu live kwenye gari wakapanic.Walianzisha mjadala kwenye daladala ujinga tu


Ukitaka kuwatawala watu wa kawaida,wape mkate na michezo.Yaani wakila mikate na kushiba,wape michezo waburudike,hawata jadili mambo ya msingi ya taifa lao.

Sio vijana tu, hata watu wazima wakiweko wabunge.
Ningekuwa na Mamlaka mimi ningezifutilia mbali hizo Yanga na Simba
Inaumiza na inakera sana. Juzi niliona JamiiForums uzi kuhusu Russia na Ukraine una trend sana. Nikauliza mbona hatujali yanayoendelea kwetu tunajadilo ya watu tu. Niliishia kukejeliwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…