USHAURI: Binti mwanafunzi wa miaka 18 apata ujauzito, tufanye nini?

USHAURI: Binti mwanafunzi wa miaka 18 apata ujauzito, tufanye nini?

Uzoefu unaonesha kwamba mchakato wenye Tija zaidi nzuri zaidi ni (a) Kwanza Binti mwanafunzi amtambue fika Mhusika i.e. awaambie ni nani mwanaume mhusika, halafu ndo: 1. wasilianeni kwanza na Mwanaume mhusika kama anakubali Mzigo wake, 2. Wasilianeni na Wazazi wa mwanaume mhusika na mkubaliane nini cha kufanya hususan malezi ya mimba hadi mtoto-mtarajiwa akizaliwa salama. 3. Msijaribu/Msikubali kamwe hoja ya kutoa mimba (Mnaua kitoto kisicho na hatia na hakiwezi kujitetea- Ni dhambi kubwa mno).
Aidha katika majadiliano yenu pande zote mbili zingatieni kwamba suala/Hoja ya Uanafunzi, binti anaweza kuahirisha masomo kama ni chuo, kubadilisha shule (Sekondari)baada ya kujifungua au binti anaweza kuhiari kuachana na masomo na kuolewa Rasmi i.e. kuanza maisha ya Ndoa yaani kuwa na Familia.
Mwisho nakushauri kwamba Hoja ya Hatua za Kisheria mara zote hazinaga Tija kwani utapoteza JUMLA (Hakuna maslahi yoyote kwako wala kwa binti wala kwa Kidume-husika) e.g. kwani Kidume mhusika akifungwa miaka 30 ww mzazi utapata nini? Kidume mhusika kama ni mtumishi atafukuzwa kazi mazima na kwenda kutumikia 30yrs na hivyo Hataweza tena kutoa msaada wowote kwa binti wala kwako ila ww utalazimika kulea mimba & mtoto(Mjukuu) hadi hapo baba yake atakapotoka Jela. Kwa kifupi kwenye Sheria, Binti atapoteza masomo kwa kufukuzwa shule, Ww mzazi wa binti utapoteza kwa kuingia gharama kubwa ya kulea, Kidume atapoteza kwa kufungwa 30yrs. Ila kama ww unataka kutoa Adhabu kali, basi nenda kwenye Sheria. Lakini kama nia yako ni njema au ni kuweka njia muafaka kukuza na kudumisha mahusiano kati ya familia za pande mbili - yamalizeni nje ya Mahakama.
Asante sana boss kwa ushauri mzuri. Kijana kakubali mzigo na tunaangalia taratibu nzuri waende zao wasitusumbue tena.
 
Ni mwanao au? ., ila we elewa 2 kwamba alipenda mwenyewe coz vibinti vya ck hz ivyo viwanafunzi inabd wazaz wao pia wawe na uhusian mzur na watt lakn pia huyo mzaz hajamfunza maadili mazur toka mdg coz me naamin kwamb alikua hachungwi af isitoshe kuwapa watt cm wakiwa wadg ndo tatz kubwa ktk mikoa eti mtt wa la 5 anatembea na smatphone unategemea nn ka mzaz
Lawama za kumchunga au malezi usizitoe wakati huu. Pengine hujawahi kuwa na watoto katika kizazi hiki.
 
Ndio hapa tungependa kujua kisheria kipi kinahesabika kikubwa kati ya uanafunzi au utu uzima wa miaka 18
Sheria inasema ukimpa mimba mwanafunzi ni miaka 30 ndani.

Swali ni...

Je mkienda mahakaman alafu binti akawageuka? Yaani akasema huyo sio baba!

Je mkimfunga huyo jamaa huoni kama mtoto atalelewa bila baba?

Hali kama hii wanavyo fanya watu ni kichukua mahari na kuwafungisha ndoa.. ila ujue ukifanya hivyo shule ndio imeishia hapo na kama huyo baba mtarajiwa hajielewi mtakua mnasovu kesi kila siku! Kwa kifupi kama huyo jamaa hampendi binti (kuna uwezekano mkubwa ikawa hivi maana tayari kesha mbebesha mimba) mjiandae kwa vimbwanga!
 
Mwanafunzi wa shule ya msingi, sekondari au chuo?.

Kama ni wa msingi au sekondari hizo ni jinai na jinai zinaripotiwa kwa vijana wa IGP N. Sirro

Ila kama ni wa chuo, mkazanieni kuwahi clinic kwanza mengine yataji sort tu baadae.
Huyu ni kidato cha tatu. Hii njia ya kwa Siro sioni kama inakuwa na tija kwa yeyote.
 
Sheria inasema ukimpa mimba mwanafunzi ni miaka 30 ndani.

Swali ni...

Je mkienda mahakaman alafu binti akawageuka? Yaani akasema huyo sio baba!

Je mkimfunga huyo jamaa huoni kama mtoto atalelewa bila baba?

Hali kama hii wanavyo fanya watu ni kichukua mahari na kuwafungisha ndoa.. ila ujue ukifanya hivyo shule ndio imeishia hapo na kama huyo baba mtarajiwa hajielewi mtakua mnasovu kesi kila siku! Kwa kifupi kama huyo jamaa hampendi binti (kuna uwezekano mkubwa ikawa hivi maana tayari kesha mbebesha mimba) mjiandae kwa vimbwanga!
Hoja ya kumuozesha ndio inapewa nguvu zaidi na wanafamilia. Kijana amemkubali binti na mwanae mtarajiwa.
 
Sheria inasema ukimpa mimba mwanafunzi ni miaka 30 ndani.

Swali ni...

Je mkienda mahakaman alafu binti akawageuka? Yaani akasema huyo sio baba!

Je mkimfunga huyo jamaa huoni kama mtoto atalelewa bila baba?

Hali kama hii wanavyo fanya watu ni kichukua mahari na kuwafungisha ndoa.. ila ujue ukifanya hivyo shule ndio imeishia hapo na kama huyo baba mtarajiwa hajielewi mtakua mnasovu kesi kila siku! Kwa kifupi kama huyo jamaa hampendi binti (kuna uwezekano mkubwa ikawa hivi maana tayari kesha mbebesha mimba) mjiandae kwa vimbwanga!
Mimi sio mwanasheria wala sijui chochote kuhusu sheria labda wanasheria watufafanulie hili swala:

Hivi serikali inapomfunga baba wa mtoto miaka 30, yenyewe (serikali) inachukua jukumu gani au inachangiaje kwenye malezi ya huyo mtoto na mama wa mtoto? Kuna fungu flani labda limetengwa la kulea watoto wa dizaini hiyo au jukumu hilo linarudishwa tena kwa wazazi wa binti aliopewa ujauzito?
 
Kuna kitoto cha jirani hapa juzi tu kimewaruka wazazi police kisa mme wa mtu na kalivyo maliza shule kakamuiba huyo mme wa mtu na kwenda kupanga sehem nyingine SASA mtoto kama huyo mkianza kuhangaika nae sana anaona kuna vitamu hamtaki avipate ndio KWANZA vinacharuka zaidi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hatareee tupu yaan.
 
Salamu Wana JF.
Naomba ushauri wa hatua za kuchukua katika mazingira haya.

Asanteni.
20220221_130149.jpg
 
kama hajabakwa, itakua ni kiherehere chake.
Kwani hata binti mwenyewe anajua kufanya matusi ni makosa. Na vibinti vya siku izi vinavyojua baikoko kuliko hata makungwi.
Iyo ya kumpa mimba tu tayari ni kosa la kufungwa miaka 30
 
Back
Top Bottom