mmh
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 2,910
- 5,084
Muda ni leo Jumamosi mpaka jumapili tu (16-17 february 2019).
wakili.
Hilo jina lako sijui avator imeufanya huu Uzi uwe kama movie za kishetani
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Muda ni leo Jumamosi mpaka jumapili tu (16-17 february 2019).
wakili.
Wakili,hii huduma ingekua kila mwisho wa wiki ingependeza sana, pale juu mwanzo kabisa nilikuuliza nikimuwekea dhamana mtuhumiwa polisi au mahakamani je naweza kufungwa? Au nichukue hatua zipi kukwepa mkono wa sheria?thanks
Na ukifikishwa kituoni kipi kinatakiwa nifanye na nisifanyiwe nini? maana kuna kupigwa siunajua wengine hatujui kunyenyekea na polisi wanapenda tuwaone superior.thanks
Haina ukomo mkuundio, hua kuna ukomo katika mirathi, kwa mfano marehem akifa alaf ndugu wa marehemu wakashindwa kufungua mirathi mahakamani ndani ya muda wa miaka mitatu toka kifo cha marehemu, basi mali za marehemu zitachukuliwa na kua chini ya uangalizi wa administrator general, so ukomo ni miaka mitatu toka kifo cha marehemu... njia za kuongeza muda na kurudishwa mali chini ya uangalizi wa wanandugu baada muda wa sheria kupita, ni maombi mapya yanayoweza kufanywa na wanasheria.
Asante sana. Je ukiwa hauna mali za kufidishia kilichobaki?hauwezi kufungwa, kesi za madai ni ngumu mtu kufungwa,endapo umelipa asilimia 60 ya deni basi mahakama itaamuru baadhi ya mali zako kupigwa mnada kufidishia kiasi kilicho baki.
ka kwambia nani kua hakuna ukomo? okei iko hivi, haki ya kusimamia mali za marehemu almaarufu kama mirathi ni lazima ithibitishwe na mahakama aidha marehemu awe ameacha wosia au hajaacha,vyote ni mahakama ndio itathibitisha au ita teua kutokana na mapendekezo ya ndugu wa marehemu, hatua hii huitwa application for letter of probate or application for granted probate, sasa kwa mujibu wa sheria za mirathi maombi haya yanapaswa kufanyika ndani ya miaka mitatu toka kifo cha marehemu, na muda huu ukipita basi admistrator general atapaswa kuziweka chini ya uangalizi wake mali hizo mpaka pale ndugu wa marehemu watakapo jitokeza na kuomba wapewa ruhusa na muda kuongezwa wa mahakama.
ntaangalia kwa kadri ntakavyokua napata nafasi... nimekujibu swali hili angalia hapo juu.Wakili,hii huduma ingekua kila mwisho wa wiki ingependeza sana, pale juu mwanzo kabisa nilikuuliza nikimuwekea dhamana mtuhumiwa polisi au mahakamani je naweza kufungwa? Au nichukue hatua zipi kukwepa mkono wa sheria?
Sent using Jamii Forums mobile app
haki ni nyingi mkuu, siwezi kuziandika hapa zote, lakini muhimu ni kuakikisha unatoa maelezo kwa muda usiozidi masaa manne, kuwekwa ndani muda usiozidi masaa 24, lakini kutoa maelezo kituoni hapo ktk hali huru, chini ya mwanasheria au ndugu yako, kuelezwa kosa ulilokamatiwa nalo, kuakikisha unasaini document zozote zile ambazo unaufahamu nazo na zimetokana na maelezo, endapo watakupiga na kukufosi usaini maelezo waliyo yatoa wao na wakakulazimisha uyasaini basi unaweza kukubali tu kwa kuepuka kuumizwa sanaa na utakuja kuyakana mahakamani kua hayakupatikana kwa ridhaa yako.... muhimu ni kumbuka endapo utaratibu huu utavurugwa na hao polisi basi itakua ni moja ya ticket ya kukuacha huru ata kama kosa ulilifanya kweli, kuna watu kweli waliua ila mahakama iliwaachia huru kutokana na polisi kushindwa kufuata maelekezo ya sheria.Mimi nataka kujua haki za raia kipindi unatamatwa na polisi,
Na ukifikishwa kituoni kipi kinatakiwa nifanye na nisifanyiwe nini? maana kuna kupigwa siunajua wengine hatujui kunyenyekea na polisi wanapenda tuwaone superior.
hii hua ni mtihani sana, na hapa ndipo wakopeshaji wanapoliaga, kikawaida inashauriwa kumkopa mtu ambae kama atashindwa kulipa deni husika basi awe atleast ata na mali ambayo inaendana na pesa aliyokopa, ndio maana utaona ma bank mengi yanafanya assessment za nyumba kwanza zinazowekwa bond, isije mtu akakopa milion 50 kumbe nyumba ina thamani ya milion 10 tu.
mkuu watumishi wengi wanakua chini ya sheria ndogo ndogo za almashauri husika, sheria ya umma imeruhusu taasisi za kiserikali kutengeneza sheria ndogo ndogo ambazo zitacontrol mahusiano makazini na nidhamu za wafanyakazi, uenda huyo mwajili wako ametumia sheria moja wapo kati ya hizo, na ingekua vizuri pia kupitia sheria za taasisi husika uliyopo, uenda kuna kifungu kimempa mamlaka hayo uyo afisa utumishi.Mkuu kama kwa mtumishi wa umma ni kitu gani ama ni kosa gan ama shitaka gan litakalo mpa mamlaka mwajiri wako kukutaka maelezo ndani ya masaa 24?
Naona unawalisha matango pori wadauni mfungwa wa madai ambae anakua yuko gerezani chini ya gharama za anaemdai mpaka pale atakapo kubali kulipa anachodaiwa ndio ataachiwa na kulipa na gharama zingine za usumbufu.
Asante sana mwana sheria mkuu wa JF, napenda kujifunza vitu vingi nilikua naomba huu uzi uwe endelevu siku zisizo zawiki utujibie maswali ya kisheri.haki ni nyingi mkuu, siwezi kuziandika hapa zote, lakini muhimu ni kuakikisha unatoa maelezo kwa muda usiozidi masaa manne, kuwekwa ndani muda usiozidi masaa 24, lakini kutoa maelezo kituoni hapo ktk hali huru, chini ya mwanasheria au ndugu yako, kuelezwa kosa ulilokamatiwa nalo, kuakikisha unasaini document zozote zile ambazo unaufahamu nazo na zimetokana na maelezo, endapo watakupiga na kukufosi usaini maelezo waliyo yatoa wao na wakakulazimisha uyasaini basi unaweza kukubali tu kwa kuepuka kuumizwa sanaa na utakuja kuyakana mahakamani kua hayakupatikana kwa ridhaa yako.... muhimu ni kumbuka endapo utaratibu huu utavurugwa na hao polisi basi itakua ni moja ya ticket ya kukuacha huru ata kama kosa ulilifanya kweli, kuna watu kweli waliua ila mahakama iliwaachia huru kutokana na polisi kushindwa kufuata maelekezo ya sheria.
I can feel your struggle brookei, sema ya kwako, na ikiwa tofauti nakupa laki moja hapa hapa, alafu uelewe hivi vitu sio tunaviandikaa tu hapa wenzako tunavifanya kila siku.