Ushauri jamani, nimeshaharibu sinunui tena vitu used

Ushauri jamani, nimeshaharibu sinunui tena vitu used

February Makamba

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2020
Posts
2,151
Reaction score
2,983
Wakuu kwema? Mimi kijana wenu mtiifu nimekuja kwenu nikiwa na majanga naomba mnisaidie.

Nilinunua simu mtandaoni kupitia kupatana.com, niliona bei ni nzuri nikamcheki jamaa nikachat nae kwenye hiyo website na akanipa namba.

Nikampigia kwa simu ya kawaida maana namba haikuwa WhatsApp, tukaongea akasema yupo mbezi nije tukutane niione.

Nikakutana nae pale mbezi stendi nikaicheki cheki nikaona ipo fresh niikampa hela nikaondoka na simu.

Baada ya kuitumia kama siku mbili nikagundua ina tatizo la charge ambalo sikuligundua muda ule. Nilipojaribu kumpigia nikashangaa namba zote nilizokuwa nawasiliana naye hazipatikani.

Niliumia lakini nikakubali tu kuishi nayo hivyo hivyo, nikakubali kupigwa. Sasa kimbembe kimekuja leo asubuhi wakati naitumia hii simu nikashangaa tu mara ghafla inawasha camera na kuanza kupiga 112, halafu inapiga milio kama ya ambulance, nikawahi nikaizima.

Nimekaa nimefikiria nimeshagundua itakuwa simu ilikuwa ya wizi na mwenye nayo anaitafuta, au huenda ilikuwa ni njama ya mapolisi kunifanyia hako kamchezo.

Sasa hapa nilichofanya nimeizima, ila bado nawaza nini nifanye sasa? Maana aliyeniuzia hapatikani na hata zile message za kupatana ameshazifuta hata mimi saivi sizioni.

Nilishaona watu wanakamatwa na polisi kwa hizi njama na kulipishwa pesa mingi au kubambikiziwa kesi.

Sasa nifanyeje wakuu?
 
Muda si mrefu utapigwa virungu vya unyayo kama yule dogo...

Point ni kwamba, simu imeshaonesha location ulipo...

Kama imepiga 112, maana yake namba yako ishajulikana, kama namba imejulikama ina maana hata jina lako limejulikana, namba ya NIDA, in short ushakuwa exposed...
 
Hivi unaanzaje kununua kitu kama simu mkononi kwa mtu wakati maduka yamejaa Kariakoo mpaka vichochoroni?

Assume hiyo simu mtu alidungwa kisu akaporwa,au alibakwa akaporwa kisha simu ukamatwe nayo wewe!!!

Yaani mpaka Mahakama ije ikuone hauna Hatia ya Kuua au Kubaka utakuwa umeshakaa Segerea umejaa ukurutu mpaka makalioni!!acha kabisa kununua vitu vya electronics mkononi,utakuja kubeba msalaba usio wako!!!
 
Ukiwasiliana na mtu Kwa nini usirekodi?

Ukinunua vitu Mtandaoni Kwa nini usiwe una-screenshot? Na kuhifadhi kwenye kumbukumbu zako hata walau mwaka mzima?

Sio kosa kununua kitu used, lakini hapo ishu itaanzia kuthibitisha kwamba umenunua, hunarisiti, huna kumbukumbu yoyote kuonyesha ni kweli unaushahidi WA kununua hiyo simu.

Mimi nikinunua kitu used huwa nafanya hivi;

1. Narekodi Mawasiliano yangu na huyo muuzaji, tena Kwa kumuuliza maswali mfano,
Simu ni Aina gani, rangi gani, inatumia laini moja au mbili, n.k.

2. Screenshot TANGAZO la bidhaa uliyoiona Mtandaoni ukainunua.

3. Mkikutana mpige picha kisiri. Hii unaenda na mtu mwingine WA ziada ambaye atakuwa anarekodi matukio bila ya muuzaji kujua.

4. Ni vyema kujua majina yake,

Kwa dunia ya sasa huwezi kuepuka kununua vitu Used
 
Ukifanya hivi lazima uwe salama kwa lolote likitokea

Dunia ya sasa bila vielelezo lolote laweza kukupata.

Trust no one.
Kuna watu wanaoña wajinga Walioweka Rekodi kwenye simu.

Au unapoongea na Huduma Kwa Wateja wanapokuambia mazungumzo yatarekodiwaa wanafikiri wanaofanya hivyo ni wajinga.

Hata ukipewa Risiti bado kuna risiti Fake, lakini kurekodi ni muhimu sana
 
Vitu vya mteremko na bei chee zina madhara makubwa sana.

Kuna dogo nae juzi kakutana na jamaa ana SAMSUNG GALAXY A83.

Dogo baada ya kuchek specs za simu na bei anayouziwa akapagawa! kakopa pesa chap 200,000/= then akampa jamaa 170k jamaa eti akadai kwa vile ana shida kubwa sana ya haraka ndio maana kakubali kuipokea hiyo hela.

Mimi nimekuta washakubaliana ndo wanalipana. Kuja kuchek ile simu vizuri nikakuta ndani ni 3G tu.

Nikamuuliza jamaa simu ni yake? akajibu yes! nikamwambia airestore! hapo ndo palikuja kuwa ishu akakataa akidai kuwa eti simu za samsung zinakuja na pasword zake ambazo hazifunguki! nikamuliza wee ulifunguaje? basi hapo tukaachana nae akapita nyumbu mwingine akapigwa 200k... huyo aliyenunua akajifanya mjuaji akairestore.. simu kuja kuwaka inadai email.

Kumbe ile simu ilikuwa ya wizi na mwenyewe akaweka mitego kwa mafundi wote.

Jamaa kupeleka simu kwa fundi akadakwa. Bahati nzuri yule aliyemuuzia kuna mtu alimfahamu.
 
Back
Top Bottom