Ushauri jamani, nimeshaharibu sinunui tena vitu used

Ushauri jamani, nimeshaharibu sinunui tena vitu used

Weka hewani simu Tumia tu ukiitwa na Polisi toa ushirikiano tu ukweli utajulikana tu Ondoa Shaka Mkuu kikubwa Jirizishe unakutana nao kituo Cha Polisi pia Usiende peke yako pia Wajulishe ndugu zako na uwaambie jamani Mimi Mzima siumwi chochote na Kama unaumwa waambie ili ukifanyiwa Kama yule dogo ndugu wajue.
 
Option mbili.
1. Isalimishe polisi
2. Itelekeze na uanze upya

Na suggest option two. Ila unaweza kuitunza tu home ili siku za mbeleni ukikamatwa ujitetee
Option two haitamuondolea uwezekano wa yeye kukamatwa kama simu ilitumika kufanya tukio llolote la kuvunja sheria. Option one is the best. Ingawa anweza akawa amewapa hint polisi waanze na yeye.
 
Wasikutishe mkuu
Izo simu zinazoibiwa zinatumika sana na akuna kinachotokea sema haziwekwi line
 
Maskini....nahisi namna sikuzako za usingiz kitandani zitakavyokuwa ngumu.pole mkuu
 
Option mbili.
1. Isalimishe polisi
2. Itelekeze na uanze upya

Na suggest option two. Ila unaweza kuitunza tu home ili siku za mbeleni ukikamatwa ujitetee
Kama alishaweka line ambayo kaisajili kwa jina lake basi keshaenda na maji huyo
 
Wakuu kwema? Mimi kijana wenu mtiifu nimekuja kwenu nikiwa na majanga naomba mnisaidie.

Nilinunua simu mtandaoni kupitia kupatana.com, niliona bei ni nzuri nikamcheki jamaa nikachat nae kwenye hiyo website na akanipa namba.

Nikampigia kwa simu ya kawaida maana namba haikuwa WhatsApp, tukaongea akasema yupo mbezi nije tukutane niione.

Nikakutana nae pale mbezi stendi nikaicheki cheki nikaona ipo fresh niikampa hela nikaondoka na simu.

Baada ya kuitumia kama siku mbili nikagundua ina tatizo la charge ambalo sikuligundua muda ule. Nilipojaribu kumpigia nikashangaa namba zote nilizokuwa nawasiliana naye hazipatikani.

Niliumia lakini nikakubali tu kuishi nayo hivyo hivyo, nikakubali kupigwa. Sasa kimbembe kimekuja leo asubuhi wakati naitumia hii simu nikashangaa tu mara ghafla inawasha camera na kuanza kupiga 112, halafu inapiga milio kama ya ambulance, nikawahi nikaizima.

Nimekaa nimefikiria nimeshagundua itakuwa simu ilikuwa ya wizi na mwenye nayo anaitafuta, au huenda ilikuwa ni njama ya mapolisi kunifanyia hako kamchezo.

Sasa hapa nilichofanya nimeizima, ila bado nawaza nini nifanye sasa? Maana aliyeniuzia hapatikani na hata zile message za kupatana ameshazifuta hata mimi saivi sizioni.

Nilishaona watu wanakamatwa na polisi kwa hizi njama na kulipishwa pesa mingi au kubambikiziwa kesi.

Sasa nifanyeje wakuu?
...Itupe. Umekaribishwa mjini....!
 
Vitu vya mteremko na bei chee zina madhara makubwa sana.

Kuna dogo nae juzi kakutana na jamaa ana SAMSUNG GALAXY A83.

Dogo baada ya kuchek specs za simu na bei anayouziwa akapagawa! kakopa pesa chap 200,000/= then akampa jamaa 170k jamaa eti akadai kwa vile ana shida kubwa sana ya haraka ndio maana kakubali kuipokea hiyo hela.

Mimi nimekuta washakubaliana ndo wanalipana. Kuja kuchek ile simu vizuri nikakuta ndani ni 3G tu.

Nikamuuliza jamaa simu ni yake? akajibu yes! nikamwambia airestore! hapo ndo palikuja kuwa ishu akakataa akidai kuwa eti simu za samsung zinakuja na pasword zake ambazo hazifunguki! nikamuliza wee ulifunguaje? basi hapo tukaachana nae akapita nyumbu mwingine akapigwa 200k... huyo aliyenunua akajifanya mjuaji akairestore.. simu kuja kuwaka inadai email.

Kumbe ile simu ilikuwa ya wizi na mwenyewe akaweka mitego kwa mafundi wote.

Jamaa kupeleka simu kwa fundi akadakwa. Bahati nzuri yule aliyemuuzia kuna mtu alimfahamu.
Ndo hawa utawasikia, JAMAA KAPIGWA, AMENUNUA SIMU KWA 2M WAKATI MIMI SIMU ILE ILE NIMEIPATA KWA LAKI NA NUSU
 
Ukiwasiliana na mtu Kwa nini usirekodi?

Ukinunua vitu Mtandaoni Kwa nini usiwe una-screenshot? Na kuhifadhi kwenye kumbukumbu zako hata walau mwaka mzima?

Sio kosa kununua kitu used, lakini hapo ishu itaanzia kuthibitisha kwamba umenunua, hunarisiti, huna kumbukumbu yoyote kuonyesha ni kweli unaushahidi WA kununua hiyo simu.

Mimi nikinunua kitu used huwa nafanya hivi;

1. Narekodi Mawasiliano yangu na huyo muuzaji, tena Kwa kumuuliza maswali mfano,
Simu ni Aina gani, rangi gani, inatumia laini moja au mbili, n.k.

2. Screenshot TANGAZO la bidhaa uliyoiona Mtandaoni ukainunua.

3. Mkikutana mpige picha kisiri. Hii unaenda na mtu mwingine WA ziada ambaye atakuwa anarekodi matukio bila ya muuzaji kujua.

4. Ni vyema kujua majina yake,

Kwa dunia ya sasa huwezi kuepuka kununua vitu Used
Dah yupo jamaa hapo maeneo ya Kibamba aisee, anafahamika kabsaa lakini anatumia ndumba balaah. Ukimtafuta kumpata shida .
 
Ukishatia line kwenye simi tayari tcra wanaijua namba inayotumia simu, Polisi wakienda tcra wanapewa namba inayotumia simu.

Kiufupi washakujua iwapo simu iliibiwa na alieibiwa alienda kuifatilia polisi. hata ukiitupa simu chooni haisaidii, tena itunze simu vizuri lasivyo utadaiwa na pesa ya simu hiyo mpya.

Mpe mtu unaemwamini kama laki 1 hivi, awe mtu mzima kidogo mwenye maneno ya busara akiri kwamba ulinunua simu mtaani bila kujua ni ya wizi na akuombwe msamaha kwa hio laki 1, lasivyo unaenda jela kiutani utani.

Kuwa makini sana unaponunua vitu kama modem na simu ambazo huwa zina imei inayorahisisha kazi kujua namba inayotumia kifaa.
😀 😀 😀 😀 😀LAKI TENA.. yani jamaa akitaka asikumbwe na msalaa asamehee hela atupe hiyo simu akiuza hata spare litamkuta jambooo.... zinaweza mtoka hela zaidi ya alizotoa
 
Uyo aliekuuzia simu alijua kabsa simu ya mbio na Hapo inawezkana unafatiliwa, cha msingi kajisalimishe tu au kma unandugu kwenye jeshi mjulishe aone anakusaidia vp
 
Wakuu kwema? Mimi kijana wenu mtiifu nimekuja kwenu nikiwa na majanga naomba mnisaidie.

Nilinunua simu mtandaoni kupitia kupatana.com, niliona bei ni nzuri nikamcheki jamaa nikachat nae kwenye hiyo website na akanipa namba.

Nikampigia kwa simu ya kawaida maana namba haikuwa WhatsApp, tukaongea akasema yupo mbezi nije tukutane niione.

Nikakutana nae pale mbezi stendi nikaicheki cheki nikaona ipo fresh niikampa hela nikaondoka na simu.

Baada ya kuitumia kama siku mbili nikagundua ina tatizo la charge ambalo sikuligundua muda ule. Nilipojaribu kumpigia nikashangaa namba zote nilizokuwa nawasiliana naye hazipatikani.

Niliumia lakini nikakubali tu kuishi nayo hivyo hivyo, nikakubali kupigwa. Sasa kimbembe kimekuja leo asubuhi wakati naitumia hii simu nikashangaa tu mara ghafla inawasha camera na kuanza kupiga 112, halafu inapiga milio kama ya ambulance, nikawahi nikaizima.

Nimekaa nimefikiria nimeshagundua itakuwa simu ilikuwa ya wizi na mwenye nayo anaitafuta, au huenda ilikuwa ni njama ya mapolisi kunifanyia hako kamchezo.

Sasa hapa nilichofanya nimeizima, ila bado nawaza nini nifanye sasa? Maana aliyeniuzia hapatikani na hata zile message za kupatana ameshazifuta hata mimi saivi sizioni.

Nilishaona watu wanakamatwa na polisi kwa hizi njama na kulipishwa pesa mingi au kubambikiziwa kesi.

Sasa nifanyeje wakuu?
Pole, ushapigwa ila muhimu kukumbuka kuwa siku hizi mtu akitaka simu hanunui kwa mtu, ni moja kwa moja K'koo kwenye maduka ya simu au Postaa zinapopatikana brand za aina zote.
 
Hivi unaanzaje kununua kitu kama simu mkononi kwa mtu wakati maduka yamejaa Kariakoo mpaka vichochoroni?

Assume hiyo simu mtu alidungwa kisu akaporwa,au alibakwa akaporwa kisha simu ukamatwe nayo wewe!!!

Yaani mpaka Mahakama ije ikuone hauna Hatia ya Kuua au Kubaka utakuwa umeshakaa Segerea umejaa ukurutu mpaka makalioni!!acha kabisa kununua vitu vya electronics mkononi,utakuja kubeba msalaba usio wako!!!
Hakuna anaependa kununua ktu used lakn ukosefu wa pesa ndo unamlazimisha mtu kununua used
 
Muda si mrefu utapigwa virungu vya unyayo kama yule dogo...

Point ni kwamba, simu imeshaonesha location ulipo...

Kama imepiga 112, maana yake namba yako ishajulikana, kama namba imejulikama ina maana hata jina lako limejulikana, in short ushakuwa exposed...
na camera ilijiwasha so kapigwa picha kibao tu
 
Wakuu kwema? Mimi kijana wenu mtiifu nimekuja kwenu nikiwa na majanga naomba mnisaidie.

Nilinunua simu mtandaoni kupitia kupatana.com, niliona bei ni nzuri nikamcheki jamaa nikachat nae kwenye hiyo website na akanipa namba.

Nikampigia kwa simu ya kawaida maana namba haikuwa WhatsApp, tukaongea akasema yupo mbezi nije tukutane niione.

Nikakutana nae pale mbezi stendi nikaicheki cheki nikaona ipo fresh niikampa hela nikaondoka na simu.

Baada ya kuitumia kama siku mbili nikagundua ina tatizo la charge ambalo sikuligundua muda ule. Nilipojaribu kumpigia nikashangaa namba zote nilizokuwa nawasiliana naye hazipatikani.

Niliumia lakini nikakubali tu kuishi nayo hivyo hivyo, nikakubali kupigwa. Sasa kimbembe kimekuja leo asubuhi wakati naitumia hii simu nikashangaa tu mara ghafla inawasha camera na kuanza kupiga 112, halafu inapiga milio kama ya ambulance, nikawahi nikaizima.

Nimekaa nimefikiria nimeshagundua itakuwa simu ilikuwa ya wizi na mwenye nayo anaitafuta, au huenda ilikuwa ni njama ya mapolisi kunifanyia hako kamchezo.

Sasa hapa nilichofanya nimeizima, ila bado nawaza nini nifanye sasa? Maana aliyeniuzia hapatikani na hata zile message za kupatana ameshazifuta hata mimi saivi sizioni.

Nilishaona watu wanakamatwa na polisi kwa hizi njama na kulipishwa pesa mingi au kubambikiziwa kesi.

Sasa nifanyeje wakuu?
Ipeleke polisi tu mwenyewe wape story yako watakusaidia.. Police ukijisalimisha huwa hawana shida sana, but ukisubiri wakutafute utajua kazi yao😀
 
Back
Top Bottom