Ushauri jinsi ya kuboresha anwani za makazi ili kuleta tija zaidi

Ushauri jinsi ya kuboresha anwani za makazi ili kuleta tija zaidi

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Kuwa na utaratibu wa anwani ya makazi ni jambo jema lakini maboresho makubwa yanahitajika. Faida kubwa ya kuwa na anwani ya makazi ni kujulikana kwa sehemu au eneo, mtaa mtu anapoishi ili kufika kwa urahisi bila kuelekezwa na mtu.

Hapa Mwanza katika Wilaya ya Nyamagagana tayari utaratibu huu umekwishafanyika na anwani nyingi zimewekwa karibu kila nyumba bila hata kuwashirikisha wakazi wa mitaa husika.

Mitaa mingi imepewa majina bila kuwashirikisha wanaokaa kwenye mitaa hiyo. Kama inavyofahamika Mwanza ni Jiji lenye milima. Anwani hizi wameziweka sehemu nyingi ambapo hamna barabara na milimani ambapo kama mtu anataka kwenda kwa ndugu yake yenye anwani ya makazi hawezi kufika.

Nashauri kablya kuanza na anwani ya makazi kwanza wakazi wa mitaa washirikishwe kuhusu jina la mtaa kitu ambacho hakikufanyika kwa Wilaya ya Nyamagana na pili wafungue barabara ili mtu afike kwa urahisi kwenye makazi.
 
haya mabilioni wanayotaka kuteketeza kwa kuweka mabango yanayoitwa anwani za makazi ni kufanya kazi isiyo na tija.

asilimia kubwa ya makazi yameachwa bila mpangilio na njia zake huwezi kumuelekeza mtu asiye mwenyeji.

badala ya kutumia mabilioni na kubandika mabango kwenye njia zisizo eleweka na bango kuwa useless ni bora tutumie mabilioni hayo kuchonga njia za uhakika mitaani kwetu.

Ukisha kuwa na physical adress inayoeleweka ndipo tuingie kwenye kuweka mabango.
 
Fedha zilizotengwa zitumike kwenye miradi ya kimkakati kuliko kuwa na anwani ya makazi ambapo sehemu nyingi hazifikiki na maeneo mengi nchi hii hasa mijini hakuna mpangilio wa nyumba na mitaa.
 
haya mabilioni wanayotaka kuteketeza kwa kuweka mabango yanayoitwa anwani za makazi ni kufanya kazi isiyo na tija.

asilimia kubwa ya makazi yameachwa bila mpangilio na njia zake huwezi kumuelekeza mtu asiye mwenyeji.

badala ya kutumia mabilioni na kubandika mabango kwenye njia zisizo eleweka na bango kuwa useless ni bora tutumie mabilioni hayo kuchonga njia za uhakika mitaani kwetu.

Ukisha kuwa na physical adress inayoeleweka ndipo tuingie kwenye kuweka mabango.
Kweli kabisa unaanzaje kuweka anwani za makazi katika maeneo yasiyo na mpangilio? Bora wangeanza na uboreshaji Kama vile walivyofanya Manzese enzi zile na ndipo hizo anwani zije
 
Fedha zilizotengwa zitumike kwenye miradi ya kimkakati kuliko kuwa na anwani ya makazi ambapo sehemu nyingi hazifikiki na maeneo mengi nchi hii hasa mijini hakuna mpangilio wa nyumba na mitaa.
Miradi ya kimkakati kama ipi
 
Back
Top Bottom