Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Membe akiwa Foreign Affairs alisafiri nchi nyingi za Africa na Caribbean kukusanya maoni ya faida na hasara kutoka nchi hizo ambazo zote zinaruhusu uraia pacha na hitimisho lake lilikuwa kwamba faida ni nyingi mno kuliko hasara na hakukuwa na hasara zozote. Yule mnafiki Kikwete baada ya kuona maccm wanapinga uraia pacha kwa sababu zisizo na kichwa wala miguu akamruka Membe. Hizo FACTS ziletwe mara ngapi? Unadhani nchi nyingi za Africa ambazo zimeamua kuruhusu uraia pacha ZIMEKURUPUKA bila kufanya TATHMINI ya kina?
Hoja ili ionekana ni yenye Manufaa lazima ilindwe na Hoja, lazima ilijibu changamoto Kaza wa kaza, lazima iangaliwe kwa mitazamo yote miwili i mean Hasi na Chanya na ulinganifu uwepo ili kufanya maamuzi , Sasa hili swala Uraia pacha Diaspora members wanataka tu huo urai uwepo bila hata kuleta Fact zikafanyiwa screening ! Mushaona wapi hii.

Tatizo mtu akishaenda tu inje anawaona alowaacha huko nyumbani ni Ngumbaru kuliko Maelezo ! None sense
 
Naanza kuelewa - kwamba uraia pacha uwe wa kiubaguzi fulani hivi yaani Mtanzania aliyepoteza utanzania wake kwa kuukana alipotaka kufanikiwa akiwa nje ya Tanzania, aruhusiwe ku-reclaim uraia wake wa awali bila kupoteza uraia wake wa nchi ya pili; na iwe kwa kesi hizo tu na si vinginevyo.
Pili tusichanganye diaspora na uraia pacha maana diaspora kusaidia ndugu zake hakulazimishi mpaka awe na uraia pacha, au?
Mkuu sio iwe ya kibaguzi. Kwa wale waliopoteza uraia baada kuchukua uraia wa nchi nyingine, serikali itaamua kama warudishiwe haki zao za uraia. Tunazungumzia wale ambao bado hawajuchukua uraia wa nchi nyingine kwa kuogopa kupoteza uraia wa Tanzania na baadae.

Kuhusu diaspora kusaidia ndugu nimetoa mfano tu; inakuwaje tunaogopa hawa watu kuwa na uraia wa nchi mbili wakati Tanzania tayari inafaidika kutoka kwenye kundi hili? Mfano: wanatuma hela nyingi tu kwa ndugu zao na hii inasaidia kwenye uchumi wa nchi yetu.

Naona umejaribu kuibadilisha huu mfano usomeke kama vile wasipopata uraia pacha hawatasaidia ndugu zao.

Kwa ufupi hamna sababu ya msingi taifa letu kuwakataa raia wake wa nje.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mkuu, imesemwa hapo juu Membe akiwa Waziri wa Mambo ya Nje alilifanyia utafiti sana, na kukutana na viongozi wa Afrika na nchi za Magharibi kuelewa undani wake, na uzoefu wao baada ya kuruhusu uraia pacha. Ndio maana akatoa tamko kwamba akiwa raisi hilo ni jambo ataruhusu mara moja. Na kumbuka Membe alikuwa Mkurugenzi wa TISS, kwa hiyo hili suala la usalama wa nchi yeye aliliona kwa mapana kuliko hawa mabulikoko humu ndani wanaodai kwamba uraia pacha utaathiri usalama wa nchi
Najua hilo, ndio maana nasema hakuna sababu ya muhimu zaidi ya kuendesha nchi kwa fikra za kichawi badala ya kisomi.
 
Mkuu Smart911, vipi tena kamanda wangu! Tushukuru Mungu hili swala likipitishwa, lina faida kubwa sana.. Nchi nyingi za afrika zimeruhusu uraia pacha, na zimeendelea.
Wanataka tusichakate pisi za kimalikia mpaka tunakufa ,it's not fair [emoji1787][emoji1787]
 
Kabisa Mkuu kama mimi sitafaidika basi ambaye ana nafasi ya kufaidika naye asifaidike bila kuangalia the BIG PICTURE of the whole issue about dual citizenship.
Wivu na roho mbaya itakumaliza ndugu...kwani wakiruhusu utahasirika nini!
 
Hapo umenichanganya. Dual cizitenship na uraia pacha si kitu kilekile? So how come India does not allow holding Indian citizenship and citizenship of a foreign country, but allows dual citizenship at the same time? So what is dual citizenship to India?

Overseas Citizenship of India (OCI) is a form of permanent residency available to people of Indian origin and their spouses which allows them to live and work in India indefinitely. Despite the name, OCI status is not citizenship and does not grant the right to vote in Indian elections or hold public office.[1][2] The Indian government can revoke OCI status in a wide variety of circumstances. As of 2020, there are 6 million holders of OCI cards among the Indian Overseas diaspora.[3]
Overseas Citizen of India
OCI JK.jpg
Front Cover of an OCI card
First issued2 December 2005
PurposeVisa, Identification
Eligibilitysee eligibility
Cost₹15000 (In India)
US $275 (abroad)
Renewal ₹1400 (In India)
Renewal US $25 (abroad)
The OCI scheme was introduced by The Citizenship (Amendment) Act, 2005 in response to demands for dual citizenship by the Indian diaspora. It provides Overseas citizens many of the rights available to resident citizens. However, in a notification issued in March 2021, the government of India has dramatically curtailed those rights.[4]
OCI status is not available to anyone who has ever been a Pakistani or Bangladeshi citizen, or who is a child, grandchild, or great-grandchild of such a person.
 
Membe akiwa Foreign Affairs alisafiri nchi nyingi za Africa na Caribbean kukusanya maoni ya faida na hasara kutoka nchi hizo ambazo zote zinaruhusu uraia pacha na hitimisho lake lilikuwa kwamba faida ni nyingi mno kuliko hasara na hakukuwa na hasara zozote. Yule mnafiki Kikwete baada ya kuona maccm wanapinga uraia pacha kwa sababu zisizo na kichwa wala miguu akamruka Membe. Hizo FACTS ziletwe mara ngapi? Unadhani nchi nyingi za Africa ambazo zimeamua kuruhusu uraia pacha ZIMEKURUPUKA bila kufanya TATHMINI ya kina?

Mkuu BAK, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Sisi tunasubiri nini! Aise hii nchi basi tu!! Mungu asaidie kwakweli.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Wivu na roho mbaya itakumaliza ndugu...kwani wakiruhusu utahasirika nini!
Tatizo hiyo ajenda ya roho mbaya ndio mmeishikilia na ndio inayowakwamisha! Badala kushawishi kwa hoja mnawasema wenye mamlaka wana roho mbaya unadhani watawasaidia kweli... Sasa mimi nikuonee roho mbaya ya nini wakati sina na sitamani uraia wa aina hiyo maana hustle zangu zote ni hapa hapa na natoboa hapa hapa!
 
NTIMA NYONGO Mkuu! Watu wanakuja na sababu zisizo na kichwa wala miguu oh! Watatuletea majasusi! Oh! Watakuja kufanya wizi wa kutisha kisha wakimbilie kwao wakati majizi ya nchi hii yanaishi hapa hapa nchini na wala hayana uDC na yanakwiba trillions za walipa kodi. Sitashangaa Mkuu Tanzania kama itakuwa nchi ya mwisho katika Afrika kuruhusu uraia pacha.
Mkuu BAK, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Sisi tunasubiri nini! Aise hii nchi basi tu!! Mungu asaidie kwakweli.
 
Tatizo hiyo ajenda ya roho mbaya ndio mmeishikilia na ndio inayowakwamisha! Badala kushawishi kwa hoja mnawasema wenye mamlaka wana roho mbaya unadhani watawasaidia kweli... Sasa mimi nikuonee roho mbaya ya nini wakati sina na sitamani uraia wa aina hiyo maana hustle zangu zote ni hapa hapa na natoboa hapa hapa!

Umeninukuu vibaya Mkuu Mzee Wa Kale Kabisa..Sijawasema wenye mamlaka wana roho mbaya..
 
NTIMA NYONGO Mkuu! Watu wanakuja na sababu zisizo na kichwa wala miguu oh! Watatuletea majasusi! Oh! Watakuja kufanya wizi wa kutisha kisha wakimbilie kwao wakati majizi ya nchi hii yanaishi hapa hapa nchini na wala hayana uDC na yanakwiba trillions za walipa kodi. Sitashangaa Mkuu Tanzania kama itakuwa nchi ya mwisho katika Afrika kuruhusu uraia pacha.

Very sad! Na watakuwa wamechelewa sana kuruhusu, wakati nchi zilizoruhusu zina maendeleo makubwa, sisi huku tunayachelewesha.


Mungu asaidie kwakweli, hope litafanyiwa kazi Mkuu BAK!
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
The OCI scheme was introduced by The Citizenship (Amendment) Act, 2005 in response to demands for dual citizenship by the Indian diaspora. It provides Overseas citizens many of the rights available to resident citizens. However, in a notification issued in March 2021, the government of India has dramatically curtailed those rights.[4]
OCI status is not available to anyone who has ever been a Pakistani or Bangladeshi citizen, or who is a child, grandchild, or great-grandchild of such a person.
Okay nimekuelewa Mkuu! Hiyo haina maana, kwa kuwa ni permanent residency ambayo wao wameamua kuiita citizenship. Ona wanavyoichezea;

March 2021, the government of India has dramatically curtailed those rights. OCI status is not available to anyone who has ever been a Pakistani or Bangladeshi citizen, or who is a child, grandchild, or great-grandchild of such a person.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Okay nimekuelewa Mkuu! Hiyo haina maana, kwa kuwa ni permanent residency ambayo wao wameamua kuiita citizenship. Ona wanavyoichezea;

March 2021, the government of India has dramatically curtailed those rights. OCI status is not available to anyone who has ever been a Pakistani or Bangladeshi citizen, or who is a child, grandchild, or great-grandchild of such a person.
Hapa wame curtail kwa sababu za mambo yao ya uhasama wa tamaduni zao India vs Pakistan na Bangladesh. Sisi so far hatuna hizo tofauti au sijategemea kuwa zitawekwa
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametooa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha!

Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balozi Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana. Na karibu wote wanaobisha au kupinga uraia pacha hawajui maana ya uraia pacha na taratibu za mtu kuwa raia pacha. Si watu wa kusikilizwa katika msingi huu, waelimishwe kwanza, kutia ndani na wabunge.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​

Bila shaka Mheshimiwa Balozi anajua hili, alikuwa Marekani:

§337.1 Oath of allegiance.

Except as otherwise provided in the Act and after receiving notice from the district director that such applicant is eligible for naturalization pursuant to §335.3 of this chapter, an applicant for naturalization shall, before being admitted to citizenship, take in a public ceremony held within the United States the following oath of allegiance, to a copy of which the applicant shall affix his or her signature:

I hereby declare, on oath, that I absolutely and entirely renounce and abjure all allegiance and fidelity to any foreign prince, potentate, state, or sovereignty, of whom or which I have heretofore been a subject or citizen; that I will support and defend the Constitution and laws of the United States of America against all enemies, foreign and domestic; that I will bear true faith and allegiance to the same; that I will bear arms on behalf of the United States when required by the law; that I will perform noncombatant service in the Armed Forces of the United States when required by the law; that I will perform work of national importance under civilian direction when required by the law; and that I take this obligation freely, without any mental reservation or purpose of evasion; so help me God.

BILA KUMUNG'UNYAMUNG'UNYA, PLEASE READ THE LAST SENTENCE.
 
Back
Top Bottom