Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Nchi pekee zilizobaki Afrika kuruhusu uraia pacha ni
  • Tanzania
  • Equatorial Guinea
  • DRC
  • Lesotho
  • Malawi
  • Zambia
  • Cameroon (nadhani hawa wameruhusu sasa)
  • Ethiopia (nadhani wameruhusu sasa)
  • Liberia (Sielwi ilikuwaje walikuwa na raisi mwenye uraia wa wa nchi nyingine, Ellen Johnson Sirleaf)
  • Eritrea
Sasa kama huu sio udungaembe ni nini?
Udungaembe maana yake ni Nini??.
 
Ukiangalia faida zingine kama direct investment, kuongeza biashara kati ya nchi hizo mbili, transfer of knowledge, ubunifu, investment in elimu, kilimo, afya, utalii, technology.

Pia work ethics and their self confidence will rub off others. (Wanafanya kazi kwa bidii na kujiamini itasaidia wengine. Sababu USA na EU Lazima ufanye kazi kwa bidii, ujiamini,uthubutu, uwe vizuri zaidi ya wazungu wengi, mvumilivu na uwezo kusoma vitu, mazingira haraka. Otherwise hutoboi.
bila uraia pacha hayo hayawezi kufanyika? Mimi naona linaweza kuwa jambo zuri ila mnaotoa mada bado mko too brief.
 
Israeli ina uraia pacha na raia wake bado wanaipenda nchi yao
 
Awatumie ndugu zake kuwekeza, au awekeze kama mgeni alipe mamilioni ambayo zingeenda kusaidia jamii. Unajua visa na vibali ni pesa ndefu.

Unawajua ndugu wa kibongo?
Hao ndugu si ndio atakuja kufanya nao biashara? Kama wawekezaji wanalipa mamilioni na hilo unaona ndilo tatizo, mbona wanazidi kuja? Je mamilioni hayo si yanalipwa serikalini na serikali ndiyo inayaingiza kwenye shughuli za kijamii? Kama tuna wasiwasi na serikali, then issue siyo uraia pacha bali utawala bora
 
Mfano wako wa Dangote, ni irrelevant.

Tunazungimzia watanzania wazawa ambao wanataka kurudi na wasiwekewe masharti kama ya wawekezaji wageni pale wanapotaka kurudi na kuwekeza nyumbani.
Kwa hiyo uraia pacha utakuwa wa kiubaguzi? Yaani Mhindi akitaka na uraia wa Tanzania akataliwe, ila Mtanzania akitaka na uraia wa India akubaliwe!
Hoja ya Dangote ilizaliwa na hoja kuwa watanzania walio nje (walioukana uraia) wanashindwa kuja kuwekeza Tanzania kwa kuwa si watanzania tena.
 
Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?
Labda nikuulize swali,ndani ya Tanzania kuna uwezekano wa mtu mmoja kuwa na makabila mawili tofauti?
Tumezoea hata kama mtoto ana wazazi wa makabila mawili tofauti,mtoto anatajwa kwa jina au kabila la baba yake.
Kwa mantiki hiyo habari ya kuwa na uraia wa nchi mbili au zaidi tusiuchekee,unaweza ukawanufaisha wachache lakini walio wengi wataumia.

Ushauri wangu kwa serikali kuhusu kuongeza diaspora ni kurekebisha mfumo mzima wa utoaji wa passport,
Mfumo wa sasa hivi wa kuulizwa swali la "unaenda wapi?'' ubadilishwe.
Chini ya swali hili waliotakiwa kupata passport wamekosa na wasiotakiwa wamepata, na wengi wamepata nyaraka hizo muhimu kwa uongo
na wale ambao hawakuwa tayari kuongopa wamekosa bila sababu za msingi.

Hakuna siri kwamba ajira hapa kwetu ni shida kama ilivyo kwa nchi nyingine nyingi duniani,lakini nchi nyingi zimeruhusu raia
wake kupata nyaraka za kusafiria ili kuwa ruhusu watu kutafuta maisha nje ya nchi zao kwa njia halali.
Wizara ibadilishe vigezo,kwa kuangalia labda tuseme elimu ya mtu,umri na shughuli anayoenda kuifanya badala ya maswali yasiyo na tija.

Kuna taasisi unakuta zinatoa nafasi za wafanyakazi kwenda nje kwa ajili ya mafunzo ya muda mfupi, na unakuta course hiyo
inajitokeza ghafla kufauatana na uhitaji let say kutengeneza mitambo na anatakiwa mtu mwenye passport iliyotayari
wewe ambaye huna unakosa fursa hiyo.Ukienda uhamiaji kuomba passport ili nawe uwe nayo ready to go uanaulizwa ''unaenda wapi?''
usipodanganya hupati maana kwa wakati huo unakuwa huna pa kwenda ila ni maandalizi.

Naomba wizara iangalie mambo kama haya,huwezi kwenda nje na kuishi huko mara moja
bila kwanza kwenda kutembelea kupitia fursa mbalimbali zinazojitokeza kupitia makampuni yetu.
kama kweli tunahitaji kuwa na diaspora wengi,turekebishe mfumo wetu wa utoaji wa passport.
kila mwenye umri wa miaka 18 aruhusiwe kupata passport bila mizengwe .
 
Unaona basi, na wewe huelewi kabisa maana ya uraia pacha na hujui sifa za mtu kupewa uraia pacha. ...............

Ndio maana nikasema wazi, mnaobisha juu ya uraia pacha wala hamuelewi maaana ya uraia pacha na hamjui vigezo vya mtu kupewa uraia pacha. Mnabisha tu kwa chuki na wivu, sio hoja za maana
Waeleweshe basi maana yake, vigezo nk. Usikimbilie kusema wana chuki, wivu nk. maana unaposema hawaelewi halafu unawahukumu kuwa wana wivu, chuki nk hujawatendea sawa.
 
Watu wanalazimika kuukana uraia wa Tanzania sio kwamba hawaipendi nchi yao, ni wazalendo kuliko hata hao wanaopinga bungeni na wanamanufaa kwa nchi kuliko hao wanaoikamua serikali kwa mishahara minono isiyotozwa kodi.

Diaspora wanatuma pesa kwa ndugu na kuongeza mzunguko wa pesa...hao wanaojiona ni wazalendo wao asilimia kubwa wanachukua pato kubwa kuliko wajibu wao.

Ni ngumu kuacha fursa ambayo huwezi ipata hapa bongo, na ambayo unaweza itumia kuajiri watu wengine nyumbani kupitia miradi ama support. Je, warudi kubanana kugombania kazi bongo? Nimejifunza kwa waghana, Nigerians, Somalis na waabeshi jinsi wanavyoinua uchumi wao, remittance ktk hizi nchi ni muhimu sana kwa pato la nchi.


Sasa sisi tubaki uraia pacha ati ni najisi kwa taifa....najisi hiyo kwiyo!!
 
Wanaogopa tu mkuu. Watu wa Diaspora wanaotetea uraia pacha sababu hasa sio kuja kufanya kazi hizi za mishahara ya milioni mbili hadi nne na kuwanyang'anya nafasi zao au za watoto wao. Diaspora wanachotaka ni uhakika wa usalama wa mali zao kama raia wa Tanzania ikiwa watahamisha capital kuja Tanzania. Tena sasa iko wazi, kwamba nyakati fulani nchi inaweza kupata kiongozi kichaa akasumbua sana wawekezaji wasio raia.

Dangote amesumbuliwa sana katika kipindi kilichopita. Alipata vikwazo vingi kwa kuwa pia sio raia wa Tanzania. Sisemi kwamba Dangote ni mmoja wapo wa kupewa uraia pacha tukiuruhusu - maana sharti moja wapo la uraia pacha ni kuishi nchini kwa zaidi ya miaka mitano, lakini Dangote ni mfano mzuri wa tofauti ya treatment kwa mwekezaji aliye raia na asiye raia. Mwekezaji asiye raia unaweza kumpa masaa 24 kuondoka nchini kwa sababu za majungu tu. Akiwa raia huwezi kufanya hivyo.
Mbona walisumbuliwa wengi tu hata ambao ni raia wa Tanzania? Kiongozi akisha kuwa kichaa (kama ulivyoandika) ukichaa wake unakuwa kwa wote. Mbowe, Manji, NGOs nk ni mifano michache ya waliosumbuliwa (au walidanganya?)
 
Uko sahihi Boss...nyumbani ni nyumbani tu. Ughaibuni kuzuri sana, ila asikudanganye mtu nyumba ni mwisho wa reli...utapakumbuka tu na siku zote utatamani nyumbani pawe bora zaidi.
 
Kuwa na Uraia pacha ni Uoga , Wapigaji akipiga Bongo akimbilie Marekani , utamfanya nini wakati yeye ni Mu USA !

Mleta maada pengine hoja zako juu ya Mjadara huu wa Uraia pacha ina mashiko sana, but Why ? Hoja yako inakosa supportive facts

Umeeleza vyema ya kwamba huo uraia Pacha hautolewi na nchi Mama(Inchi ulozaliwa) bali hutolewa na hiyo inchi ya pili , kwani wewe apo kama tayari unakigezo cha kuwa Raia wa china, Germany, Uk etc kwa nini uhangaike na inchi ambayo uraia wake tayari unao ?

Kwani Mnataka Kusema kwamba Mpaka leo hii hamna Watanzania ambao either wapo Tz au inje ya Tz ambao wana uraia zaidi ya huo utz? Naamini jibu ni kwamba Wapo na wanafanya shughuri zao vyema bika bughuza.

Na kama wapotayari wenye huo urai na mambo yao yanaendaaa, why kelele nyingi mpaka kudemandi hili liwepo kisheria ? What is behind of those Legal demands
 
Sijui watanzania tunakosa exposure au sera ya Ujamaa imetukaa sana
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametooa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha!

Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balozi Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana. Na karibu wote wanaobisha au kupinga uraia pacha hawajui maana ya uraia pacha na taratibu za mtu kuwa raia pacha. Si watu wa kusikilizwa katika msingi huu, waelimishwe kwanza, kutia ndani na wabunge.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​


Mkuu, umeona mbali sana.. Naunga mkono hoja kwa asilimia zote. Hili swala la uraia pacha ni muhimu, tunaomba Mulamula alipokee na alifanyie kazi. Mungu asaidie, na Amuongoze Mulamula katika majukumu yake, pamoja na Raisi wetu mama samia suluhu hassan.


Ahsante kiongozi wangu Synthesizer Mungu awe nawe!
 
Ndio maana hii nchi haiendelei, Roho mbaya na wivu ni laana Kubwa sana, ukiwaangalia usoni, ukiwasikiliza ni umasikini mtupu umejaa
Tuonyesheni vya maana mlivyofanya huko mlipo wehu nyie, mabox yakubeba yameisha mnataka kurudi
 
Hili swala la uraia wa nchi mbili sidhani kama serikali imefanya utafiti wa kujua faida na hasara zake. Na huu ni uvivu tu kwani wangeweza kwenda kwenye balozi ambazo nchi zao zina ruhusu uraia pacha na kuuliza faida na hasara zake.

Mie na unga hoja ya uraia wa nchi mbili kwa wa Tanzania lakini tusiruhusu mataifa mengine kupata uraia wa Tanzania kwa njia ya makazi.

Taifa letu limeshindwa kutoa ajira za kutosha kwa raia, tukianza kuruhusu wageni wapate uraia kirahisi vijana wengi watakosa ajira.

Sheria ipite kwamba, mtanzania atakae chukua uraia wa nchi nyingine , bado ataendelea kuwa raia wa Tanzania bila kupoteza haki zozote. Thats it. Hapo mchina na mkenya watafaidika vipi?

Kuruhusu uraia pacha kwa mtanzania haimaanishi mchina, mmarekani, mkenya nae anaruhusiwa kuja Tanzania na kupewa uraia. Hio ni sheria nyingine kabisa.

Tusijitese kwa kuogopa mataifa mengine. Diaspora hao hao ndio wanawasaidia ndugu zao kila siku sasa kuna kosa gani wakiwa na uraia wa nchi mbili? Wanachuma kule wanakuja kula nyumbani kitu ambacho ni kizuri kwa uchumi wetu.
Naanza kuelewa - kwamba uraia pacha uwe wa kiubaguzi fulani hivi yaani Mtanzania aliyepoteza utanzania wake kwa kuukana alipotaka kufanikiwa akiwa nje ya Tanzania, aruhusiwe ku-reclaim uraia wake wa awali bila kupoteza uraia wake wa nchi ya pili; na iwe kwa kesi hizo tu na si vinginevyo.
Pili tusichanganye diaspora na uraia pacha maana diaspora kusaidia ndugu zake hakulazimishi mpaka awe na uraia pacha, au?
 
Back
Top Bottom