Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Tena wacha Vichwa vya Diaspora virudi ili Wafanye kazi na Raisi Samia Suluhu wanachoogopa hao makapuku ni kuwa nafasi zao zitatwaliwa na Watanzania wenye Elimu ya kweli na Exposure kutoka Diaspora.

View attachment 1810215
Wanaogopa tu mkuu. Watu wa Diaspora wanaotetea uraia pacha sababu hasa sio kuja kufanya kazi hizi za mishahara ya milioni mbili hadi nne na kuwanyang'anya nafasi zao au za watoto wao. Diaspora wanachotaka ni uhakika wa usalama wa mali zao kama raia wa Tanzania ikiwa watahamisha capital kuja Tanzania. Tena sasa iko wazi, kwamba nyakati fulani nchi inaweza kupata kiongozi kichaa akasumbua sana wawekezaji wasio raia.

Dangote amesumbuliwa sana katika kipindi kilichopita. Alipata vikwazo vingi kwa kuwa pia sio raia wa Tanzania. Sisemi kwamba Dangote ni mmoja wapo wa kupewa uraia pacha tukiuruhusu - maana sharti moja wapo la uraia pacha ni kuishi nchini kwa zaidi ya miaka mitano, lakini Dangote ni mfano mzuri wa tofauti ya treatment kwa mwekezaji aliye raia na asiye raia. Mwekezaji asiye raia unaweza kumpa masaa 24 kuondoka nchini kwa sababu za majungu tu. Akiwa raia huwezi kufanya hivyo.
 
Na sisi tunaotaka sio wenye nchi? Kuna watu mnajiona mna haki miliki ya Tanzania kuliko sisi wengine. Labda tatizo ndio linaanzia hapo.
nyie ndio wale mliokuwa mnasema katiba ibadilishwe nanii aongezewe miaka , mnastahili alipo.
 
Aliyefanikiwa nje asingeweza kuhangaikia uraia pacha. waliokwama ndo tatizo. wanaasumbuliwa na kihoro. Utaweza kubeba maboksi hadi uzeeni?

Dunia naijua boss! Niko Bongo mchana huu najiandaa jioni niingie mitaani kucheka na majirani na wine yangu. wewe endelea kudumaa akiamini mitaji iko nje na eti tunakuhitaji sana!
Elimu yako na upeo wako wa nadharia ya dunia hii unatia shaka. Anyway kutoa comments ni haki yako kikatiba.
 
Hili swala la uraia wa nchi mbili sidhani kama serikali imefanya utafiti wa kujua faida na hasara zake. Na huu ni uvivu tu kwani wangeweza kwenda kwenye balozi ambazo nchi zao zina ruhusu uraia pacha na kuuliza faida na hasara zake.

Mie na unga hoja ya uraia wa nchi mbili kwa wa Tanzania lakini tusiruhusu mataifa mengine kupata uraia wa Tanzania kwa njia ya makazi.

Taifa letu limeshindwa kutoa ajira za kutosha kwa raia, tukianza kuruhusu wageni wapate uraia kirahisi vijana wengi watakosa ajira.

Sheria ipite kwamba, mtanzania atakae chukua uraia wa nchi nyingine , bado ataendelea kuwa raia wa Tanzania bila kupoteza haki zozote. Thats it. Hapo mchina na mkenya watafaidika vipi?

Kuruhusu uraia pacha kwa mtanzania haimaanishi mchina, mmarekani, mkenya nae anaruhusiwa kuja Tanzania na kupewa uraia. Hio ni sheria nyingine kabisa.

Tusijitese kwa kuogopa mataifa mengine. Diaspora hao hao ndio wanawasaidia ndugu zao kila siku sasa kuna kosa gani wakiwa na uraia wa nchi mbili? Wanachuma kule wanakuja kula nyumbani kitu ambacho ni kizuri kwa uchumi wetu.
 
Wewe kuna mawili. Either ni masikini, na kama una maisha mazuri, either umekwiba, umepokea rushwa, au mzazi/mlezi wako ndio aliyetoboa. Na kama ametoboa, inawezekana na yeye alitoboa kwa wizi. In short, una mentality ya kimasikini.
Povu kubwa limekutoka !!?
hamtafanikiwa
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametooa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha! Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balozi Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana. Na karibu wote wanaobisha au kupinga uraia pacha hawajui maana ya uraia pacha na taratibu za mtu kuwa raia pacha. Si watu wa kusikilizwa katika msingi huu, waelimishwe kwanza, kutia ndani na wabunge.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​

Uraia pacha hapana. Hakuna mgao kwenye uzalendo. Sisi hatuhitaji kuja kua na wabunge na rais wenye uraia pacha. Mtu alikua mwanajeshi jeshi la marekani juzi mtu alikua jasusi wa marekani juzi leo aje anagombea ubunge au anakua balozi au rais wa tanzania. Acheni mawazo yasiyokua maana.
 
Uraia pacha hapana. Hakuna mgao kwenye uzalendo. Sisi hatuhitaji kuja kua na wabunge na rais wenye uraia pacha. Mtu alikua mwanajeshi jeshi la marekani juzi mtu alikua jasusi wa marekani juzi leo aje anagombea ubunge au anakua balozi au rais wa tanzania. Acheni mawazo yasiyokua maana.
Wewe unajuaje hawa wabunge, mabalozi, na viongozi wengine tulionao sasa hivi, hakuna anayefanya ujasusi kwa manufaa ya nchi kama marekani? Tena ni hawa wanasiasa ambao hata Nyerere aliwaita malaya na kusema heshima yao ina bei. Wananunulika kirahisi sana.
 
Uraia pacha hapana. Hakuna mgao kwenye uzalendo. Sisi hatuhitaji kuja kua na wabunge na rais wenye uraia pacha. Mtu alikua mwanajeshi jeshi la marekani juzi mtu alikua jasusi wa marekani juzi leo aje anagombea ubunge au anakua balozi au rais wa tanzania. Acheni mawazo yasiyokua maana.
Ndio maana nasema watu mnaojibu vitu hivi hamna ufahamu wa kutosha. Kwani nani amesema tukiwa na uraia pacha basi ni lazima tuwaruhusu walio na uraia pacha kuwa wabunge au raisi wetu? Kwani wabunge na maraisi wetu tunaokoteza tu, hatuna vigezo?

Na mtu aliye mwanajeshi au jajsusi Marekani leo, hajawahi kuishi Tanzania, itakuwaje aje awe raia pacha na Tanzania?

Watu msioelewa mambo ndio mnabisha zaidi.
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametooa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi kumi katika Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu. Kati ya nchi 54 za Afrika, 44 zimeruhusu uraia pacha.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha! Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balozi Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana. Na karibu wote wanaobisha au kupinga uraia pacha hawajui maana ya uraia pacha na taratibu za mtu kuwa raia pacha. Si watu wa kusikilizwa katika msingi huu, waelimishwe kwanza, kutia ndani na wabunge.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​

Mkiambiwa mlete hoja nzito za kwa nininiraia pacha hamna hoja nzito.
Kama muda wa kikwete nae alikataa basi sahauni...
 
Hili swala la uraia wa nchi mbili sidhani kama serikali imefanya utafiti wa kujua faida na hasara zake. Na huu ni uvivu tu kwani wangeweza kwenda kwenye balozi ambazo nchi zao zina ruhusu uraia pacha na kuuliza faida na hasara zake.

Mie na unga hoja ya uraia wa nchi mbili kwa wa Tanzania lakini tusiruhusu mataifa mengine kupata uraia wa Tanzania kwa njia ya makazi.

Taifa letu limeshindwa kutoa ajira za kutosha kwa raia, tukianza kuruhusu wageni wapate uraia kirahisi vijana wengi watakosa ajira.

Sheria ipite kwamba, mtanzania atakae chukua uraia wa nchi nyingine , bado ataendelea kuwa raia wa Tanzania bila kupoteza haki zozote. Thats it. Hapo mchina na mkenya watafaidika vipi?

Kuruhusu uraia pacha kwa mtanzania haimaanishi mchina, mmarekani, mkenya nae anaruhusiwa kuja Tanzania na kupewa uraia. Hio ni sheria nyingine kabisa.

Tusijitese kwa kuogopa mataifa mengine. Diaspora hao hao ndio wanawasaidia ndugu zao kila siku sasa kuna kosa gani wakiwa na uraia wa nchi mbili? Wanachuma kule wanakuja kula nyumbani kitu ambacho ni kizuri kwa uchumi wetu.
Mkuu, imesemwa hapo juu Membe akiwa Waziri wa Mambo ya Nje alilifanyia utafiti sana, na kukutana na viongozi wa Afrika na nchi za Magharibi kuelewa undani wake, na uzoefu wao baada ya kuruhusu uraia pacha. Ndio maana akatoa tamko kwamba akiwa raisi hilo ni jambo ataruhusu mara moja. Na kumbuka Membe alikuwa Mkurugenzi wa TISS, kwa hiyo hili suala la usalama wa nchi yeye aliliona kwa mapana kuliko hawa mabulikoko humu ndani wanaodai kwamba uraia pacha utaathiri usalama wa nchi
 
Uraia pacha hapana. Hakuna mgao kwenye uzalendo. Sisi hatuhitaji kuja kua na wabunge na rais wenye uraia pacha. Mtu alikua mwanajeshi jeshi la marekani juzi mtu alikua jasusi wa marekani juzi leo aje anagombea ubunge au anakua balozi au rais wa tanzania. Acheni mawazo yasiyokua maana.
Hebu toa definition ya uzalendo kwa uelewa wako.
 
Sidhani kama watakuja na point nzito zaidi ya kusema watawekeza.
Actually faida kubwa ni kuwekeza na kitu kinaitwa profit repatriation to your country of chieftainship. Ukiwa nje, kunakuwa na masharti ya kutoia fedha za kigeni, kama ilivyo hapa Tanzania. Lakini ikiwa unataka kupeleka fedha ya kigeni katika nchi ya uraia wako basi unakuwa na uhuru zaidi.

Pia unapowekeza katika nchi ambayo huna uraia nayo, kunakuwa na tax implications fulani katika nchi uliyo na uraia nayo, kwa kuwa nchi unayoishi inachukulia umetoa capital yao kwenda nchi ambayo siyo yako na hivyo kuifaidisha nchi ya wengine kuliko nchi yako. Sasa pia, ikiwa nchi uliyowekeza pia ni nchi uliyo na uraia nayo inakuwa na tax implication tofauti. Na mwisho ni kwamba, watu hawako comfortable kuwegeza katika nchi ambayo yeye anaonwa kama mgeni. Anaweza kuja raisi kichaa akabadilisha sheria za uwekezaji kwa watu wasio raia. Ethiopia kama wewe sio raia ni vigumu sana kumilikishwa chochote. Ni lazima uwe raia ndio unakuwa na uhuru wa kumiliki assets fulani fulani.

Ndio maana basi watu wanasema wazi, unaporuhusu uraia pacha, inafungulia sana capital inflow kutoka watu o wataruhusiwa kuwa na uraia pacha na Tanzania. Lakini watu wasielewe kwamba kupewa uraia pacha na Tanzania ni suala la sadaka. Kuna vigezo na mashart ya kufuata, na ni ombi ambalo Tanzania inaweza kukubali au kukataa kwa kila mtu anayeoomba, kutokana na vigezo vilivyowekwa.

Sasa unakuta mpumbavu mmoja anasema tukiruhusu uraia pacha siku moja tunaweza kujikuta tuna mbunge au raisi aliyekuwa jasusi wa Marekani, au wahindi wote watachukua uraia wa Tanzania na kuchukua ardhi yetu. Hivi watu hawa wana akili lakini? Halafu unakuta mtu anaetoa point kama hizo ni mbunge!
 
Hebu toa definition ya uzalendo kwa uelewa wako.
Sintashangaa akikuambia mzalendo maana yake Mtanzania wa kuzaliwa nchini kama Ole Sabaya! Yaani watu vihiyo ndio wako mstari wa mbele kusema uraia pacha una risk za uzalendo na usalama.
 
Tunawaonea wivu nyinyi diaspora ?

Sasa kwa nini tuhangaike kubadilisha sheria kuwasapoti watu ambao wanatukashfu tuliopo hapa nchini wakisema wao wako njema mpaka tunawaonea wivu ?

Hoja nyepesi za wana diaspora ndio hizi maskini ya Mungu.
Tunawaonea wivu kufagia vyoo ughaibuni
 
Sidhani kama watakuja na point nzito zaidi ya kusema

Sidhani kama watakuja na point nzito zaidi ya kusema watawekeza.
Mkuu dunia sikuhizi imekuwa kijiji. Jambo hili la uraia pacha sio ajenda ngeni tena pamoja na kwamba hapa nyumbani bado inaonekana kama ni cancer isiokuwa na tiba. Tambua;
  • si jukumu pekee la Diaspora kuja na point nzito za ushawishi bali ni issue ya mtanzania yoyote mwenye uelewa mpana kuliongelea.
  • Serikali haiitaji kushawishiwa kuhususiana na jambo hili bali wanatakiwa kujipanga katika kuweka mipambo na taratibu za kuratibu na kutekeleza.
  • Tukiachana na hoja ya uwekezaji wa Diaspora. Hivi unamtreat vipi mtanzania aliechukua uraia wa nchi nyingine ili kupata unafuu wa gharama za masomo na leo kafudhu katika sekta adimu kama udaktari, engineer ktk sector za gas na mafuta nk. Je, utamwajiri kama expert na umpe marupurupu kama tunavyowapa experts wengine ( particularly wazungu) au vipi?
 
Tunawaonea wivu kufagia vyoo ughaibuni
Akifagia vyoo anapoteza utanzania? Au kama ni mjomba wako, kaka, dada yako unamkana kwakua anasugua vyoo ulaya. Je, wanaosugua vyoo hapa nyumbani si watanzania kamali au nini hoja yako?
 
Mleta mada, hoja iwe moja:- Uraia pacha tu, faida na hasara zake. Usichanganye na mengine itakutoa kwenye mstari.
kweli kabisa. Thread imeandikwa kwa hasira kiasi kwamba haionyeshi ushawishi. Jikite kwenye faida na hasara zake then hata hao wanaopinga waweze kubadilika, na labda wanaounga mkono nao wabadilike pia!
 
Back
Top Bottom