Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

Hili jambo liko wazi kua uraia pacha una faida nyingi kuliko hasara.yaliyobaki ni ujinga wetu tu.Tuna tatizo kubwa sana lakucomplicate mambo badala ya kuyarahisisha.Wakati wenzetu wanatumia hiyo fursa ya kwenda kuchuma uko ugenini na kuleta kwao sisi bado tunawaza kuishi kwakujifungia wakati hatuna manufaa yoyote kwa nchi.Tukifunze kua opportunistic.
 
Mleta mada, hoja iwe moja:- Uraia pacha tu, faida na hasara zake. Usichanganye na mengine itakutoa kwenye mstari.

Mawazo ya kizamani. Wanasema Tanzania inahitaji ajira, wawekezaji, wakati kuna watanzania kwa mamilioni wanaishi nje.

Mitaji yao, know how, elimu, exposure ingeweza kusaidia Taifa kwenye nyanja nyingi.
Kuwekeza nchi flani sio mpaka uwe na uraia wa nchi hiyo,wanaosema eti wao wanamitaji ya kuwekeza lakini wanakwamishwa na Tanzania kukataa uraia pacha ni waongo na wazandiki mbona dangote kawekeza tanzania kwani anauraia wa Tanzania?
 
..Umenielewa vibaya. Mimi nilikuwa namjibu Econometrician.

..Umefanya vizuri ku-reserve comments zako.

..Ungeweza kupata DHAMBI za bure kwa kunituhumu kitu ambacho sicho.

..I am just being realistic here.

..Kama itakupendeza tafuta mrejesho aliofanya muwakilishi wa diaspora ktk bunge maalum la katiba.

..baada ya kumsikiliza nime-conclude kwamba ni afadhali mpiganie kuwa na ukaazi wa kudumu kuliko kuwa na uraia pacha.
Kwa mtu aliyezaliwa Tanzania , ukaazi wa kudumu siyo sahihi. Napendekeza uraia pacha...Labda huyo muwakilishinwa Diaspora, alipendekeza kwa wakati ule ambapo wengi walipinga tofauti na sasa. Ukaazi wa kudumu iwe kwa ambao hawajazaliwa Tanzania na wanataka kupata uraia nk.
 
Kuwekeza nchi flani sio mpaka uwe na uraia wa nchi hiyo,wanaosema eti wao wanamitaji ya kuwekeza lakini wanakwamishwa na Tanzania kukataa uraia pacha ni waongo na wazandiki mbona dangote kawekeza tanzania kwani anauraia wa Tanzania?
Mfano wako wa Dangote, ni irrelevant.

Tunazungimzia watanzania wazawa ambao wanataka kurudi na wasiwekewe masharti kama ya wawekezaji wageni pale wanapotaka kurudi na kuwekeza nyumbani.
 
Mfano wako wa Dangote, ni irrelevant.

Tunazungimzia watanzania wazawa ambao wanataka kurudi na wasiwekewe masharti kama ya wawekezaji wageni.
Shida ni kwamba kwa Sera zetu za kodi na sheria zinavyobadilika badilika MTU akishakua na uraia pacha in simple kuhamisha biashara zake pindi pale kunapotokea sintofahamu na serikali na kukimbilia nchi yenye unafuu ambayo kidogo imeendelea.

Pia katika maswala ya usalama ni rahisi kutumiwa na watu flani flani ambao hawalitakii mema taifa
 
Tunazungukwa na nchi zenye matatizo lukuki hapa ukanda wa maziwa makuu

Ndoto zao Ni Tz kuwa na uraia pacha ili wayakimbie matatizo Yao huko kwao

Wengine nchi zao hakuna ardhi ya kutosha .

Watakuja wakwapue ardhi yetu hapa wafanye Yao

Labda huu uraia pacha utuhusu sisi tuliozaliwa TZ sio wa kutoka nje
 
Kuwekeza nchi flani sio mpaka uwe na uraia wa nchi hiyo,wanaosema eti wao wanamitaji ya kuwekeza lakini wanakwamishwa na Tanzania kukataa uraia pacha ni waongo na wazandiki mbona dangote kawekeza tanzania kwani anauraia wa Tanzania?


Kwahiyo unaona ni sawa wewe ungeenda kutafuta maisha au kusoma baada ya kusoma ukapata kazi, halafu Uraia ( kwa maslahi matibabu bure kwako na watoto wako, elimu bure, unasafiri nchi nyingi bila visa, bughudha etc.)

Ukitaka kurudi nyumbani uombe visa? Kuwekeza uwe treated kama mgeni sehemu uliyokulia Baba,Mama, Babu Bibi, Mjomba Shangazi wote wako hapo.

Dangote ni Mnigeria.
 
Shida ni kwamba kwa Sera zetu za kodi na sheria zinavyobadilika badilika MTU akishakua na uraia pacha in simple kuhamisha biashara zake pindi pale kunapotokea sintofahamu na serikali na kukimbilia nchi yenye unafuu ambayo kidogo imeendelea.

Pia katika maswala ya usalama ni rahisi kutumiwa na watu flani flani ambao hawalitakii mema taifa
Siyo kweli. Kuhamisha biashara siyo lazima uwe na uraia pacha. Wawekezaji wakubwa kutoka nje mfano tu Dangote, nani angeweza kumzuia kuhamisha biashara kama alivyokuwa akitaka kufanya?

Kutumiwa kivipi katika masuala ya kiusalama na hao unaosema “watu flani flani” wasiolitakia mema Taifa? Ebu toa mfano mmoja kwa Taifa lenye kukubali uraia pacha na usalama wao ukaharibika kwasababu hiyo. Weka mfano wa Taifa moja tu.
 
Siyo kweli. Kuhamisha biashara siyo lazima uwe na uraia pacha. Wawekezaji wakubwa kutoka nje mfano tu Dangote, nani angeweza kumzuia kuhamisha biashara kama alivyokuwa akitaka kufanya?

Kutumiwa kivipi katika masuala ya kiusalama na hao unaosema “watu flani flani” wasiolitakia mema Taifa? Ebu toa mfano mmoja kwa Taifa lenye kukubali uraia pacha na usalama wao ukaharibika kwasababu hiyo. Weka mfano wa Taifa moja tu.
Somalia
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametooa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi nane Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha! Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balazo Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​

sisi wanyonge hatutaki uraia pacha, tutakuwa watumw kwenye nchi yetu.
Huko marekani Jaji[Watanzania wanao shika nyadhifa za Uwakili na attorneys] kama mimi analipwa Mshahara milioni 45 kwa mwezi wakati hapa tunalipwa milioni 9 tu kwa mwezi.
Sasa jaji wa Marekani si atakuja kununua mashamba yote huku, hapana hatutaki.
 
Kwahiyo unaona ni sawa wewe ungeenda kutafuta maisha au kusoma baada ya kusoma ukapata kazi, halafu Uraia ( kwa maslahi matibabu bure kwako na watoto wako, elimu bure, unasafiri nchi nyingi bila visa, bughudha etc.)

Ukitaka kurudi nyumbani uombe visa? Kuwekeza uwe treated kama mgeni sehemu uliyokulia Baba,Mama, Babu Bibi, Mjomba Shangazi wote wako hapo.

Dangote ni Mnigeria.
Sasa kama waliweza kuukana uraia wa Taifa lao ati kwa kigezo cha kupata maslahi walyo yapata huko ugenini wana uzalendo gani tena kwa taifa na kuna haja gani ya kurudi kama RAIA wa Tanzania?wao waje tu kama wawekezaji wengine milango iko wazi,watashindwa kuuza nchi kwa masilahi mazuri watakayopewa na mabeberu kama tu uraia waliukana
Kwahiyo unaona ni sawa wewe ungeenda kutafuta maisha au kusoma baada ya kusoma ukapata kazi, halafu Uraia ( kwa maslahi matibabu bure kwako na watoto wako, elimu bure, unasafiri nchi nyingi bila visa, bughudha etc.)

Ukitaka kurudi nyumbani uombe visa? Kuwekeza uwe treated kama mgeni sehemu uliyokulia Baba,Mama, Babu Bibi, Mjomba Shangazi wote wako hapo.

Dangote ni Mnigeria.
 
Mleta mada, hoja iwe moja:- Uraia pacha tu, faida na hasara zake. Usichanganye na mengine itakutoa kwenye mstari.

Mawazo ya kizamani. Wanasema Tanzania inahitaji ajira, wawekezaji, wakati kuna watanzania kwa mamilioni wanaishi nje.

Mitaji yao, know how, elimu, exposure ingeweza kusaidia Taifa kwenye nyanja nyingi.
Haahaaahaa!! Eti kuna Wa Tanzania Mamilioni wanaishi nje. Haaahaaaahaaahaaaaa
 
Unaona basi usivyo na point? Aina ile ile ya wabishiwa wivu na chuki tu.

Kwanza hao walioukana uraia, wakipewa tena uraia wa Tanzania wewe unaathirikaje, na hasa ukizingatia itawawezesha kuhamisha mitaji kuja Tanzania kirahisi?

Pili, kama hao walioukana uraia wanatamani tena kuwa Watanzania, sio lazima wawe raia pacha. Bado wanaweza kuwa raia wa Tanzania tena, kwa hiyo issue sio hiyo. Uko off kabisa.

Uraia pacha unaingia pale ambapo inakuwa rahisi kwa mtu kuhamisha capital kati ya nchi mbili (repatriation of earnings, profits or capital). Ukitaka kuona ni jinsi gani, hebu nenda Bank waambie ninataka kutuka Dola Elfu mbili kwa rafuiki yangu pale Kenya uone utakavyotolewa nje. Lakini sasa, ukiwa na uraia pacha wa Tanzania na Kenya, utaruhusiwa kirahisi kwa kuwa wewe ni raia wa Kenya pia, kwa hiyo inakubalika kwamba unafanya repatriation of profits. Ndio maana hata makampuni ya kigeni yanaruhusiwa kutoa fedha walizochuma hapa nchini kwenda nje. Ni kwa msingi huo mie nikiwa Kenya na nina uraia pacha na Tanzania, inakuwa rahisi kutuima fedha toka Kenya kuja Tanzania.

Yaani watu mnabisha wakati hivi vitu hamvielewi. Eti uzalendo, usalama, wivu tu na chuki vimewazidi. Uzalendo wako unaisaidia nini Tanzania kama hujawahi kuiingizia nchi hata dola moja toka uzaliwe?
Wewe hangaika na maisha yako. Kama uliamini ukiwa m-Nigeria ni sifa, usitusumbue kurudi nyumbani. Au unaamini tulioko TZ hatujawahi ishi nje ya nchi? Ulaya, Asia, na Amerika tunapajua boss. Kuleni kibano cha maisha, mukija likizo tambeni na waya masikioni, lakini wajuvi wa mambo tunajua hali ngumu inavyowasumbua.

Mtu anajidai eti watachangia maendeleo, wakati wanashindwa hata kuwasaidia wadogo zao wanaosota nchini. Kuna mijitu imesomba hata wadogo zao na kuwafanya vibarua nchi za watu wakiamini itawatoa, waaapi!
 
sisi wanyonge hatutaki uraia pacha, tutakuwa watumw kwenye nchi yetu.
Huko marekani Jaji kama mimi analipwa Mshahara milioni 45 kwa mwezi wakati hapa tunalipwa milioni 9 tu kwa mwezi.
Sasa jaji wa Marekani si atakuja kununua mashamba yote huku, hapana hatutaki.


Sasa hapo sio ndio tunatengeneza ajira zenyewe, exports mazao yatauzwa ndani na nje, kodi zitalipwa kwa wingi( barabara, madawa, elimu, miundombinu), kupunguza bei na uhaba wa chakula, labda kusaidia matunda yasiozee shambani (more 50% Tanga matunda yanaoza shambani). Huu ndio ufanisi wenyewe,( increase in productivity)

Kuna Watanzania wana ekari hadi elfu kumi lakini hawaziendelezi. Sana sana wanaombea mkopo.

Nimeona Njombe Kuna Wazungu kutoka South Africa wamelima Ekari 10, 000 za Maparachichi wameajiri Watanzania kibao. Kwa hiyo bora uwape wazungu uwanyime ndugu zako.

Shamba usipoliendeleza kwa miaka miwili linachukuliwa. Ardhi ya TZ ni mkopo haiuzwi, kwa hiyo haiwezi kupotea.

Pia unaweza kuweka mikataba sheria flani kuwapa kipaumbele wazawa (ndivyo ilivyo sasa).

Watasaidia pia kwenye nyanja na secka zingine. Masoko, technology, innovation etc.
 
Tunazungukwa na nchi zenye matatizo lukuki hapa ukanda wa maziwa makuu

Ndoto zao Ni Tz kuwa na uraia pacha ili wayakimbie matatizo Yao huko kwao

Wengine nchi zao hakuna ardhi ya kutosha .

Watakuja wakwapue ardhi yetu hapa wafanye Yao

Labda huu uraia pacha utuhusu sisi tuliozaliwa TZ sio wa kutoka nje
Wewe ni mmoja wapo unabisha uraia pacha juu ya kuelewa mtu anapataje uraia pacha. Hao watu unaowasema watapata uraia pacha wa Tanzania kwa vigezo gani? Wewe unafikiri uraia pacha ni kama kuomba visa?
 
Wewe hangaika na maisha yako. Kama uliamini ukiwa m-Nigeria ni sifa, usitusumbue kurudi nyumbani. Au unaamini tulioko TZ hatujawahi ishi nje ya nchi? Ulaya, Asia, na Amerika tunapajua boss. Kuleni kibano cha maisha, mukija likizo tambeni na waya masikioni, lakini wajuvi wa mambo tunajua hali ngumu inavyowasumbua.

Mtu anajidai eti watachangia maendeleo, wakati wanashindwa hata kuwasaidia wadogo zao wanaosota nchini. Kuna mijitu imesomba hata wadogo zao na kuwafanya vibarua nchi za watu wakiamini itawatoa, waaapi!
Lazima kutakuwa na ndugu yako nje amekataa kukutumia hata dola moja kukusaidia, na sasa una hasira na uraia pacha ili umkomoe!
 
Balozi Malamula hivi karibuni ametooa kauli kwamba serikali inaandaa sera ili Tanzania inufaike na Diaspora. Mimi nadhani huku ni kupotezeana muda tu. Nilishalisema sana jambo la Diaspora humu ndani.

Nilishaziponda sana point za Watanzania ambao wanadai kuwa tusiruhusu uraia pacha kwa kuwa watu watakaochukua uraia pacha sio wazalendo. Niliuliza uzalendo katika mambo gani hasa? Ni kitu gani ambacho watu wanaona mtu mwenye uraia pacha atafanya kwa nchi hii ambacho kitakuwa ni ukosefu wa uzalendo?

Hata nilisema kuna nafasi kubwa ya mtu asiye na uraia pacha kukosa uzalendo kuliko hao watakaokuwa na uraia pacha. Mnaweza kuniambia hawa mafisadi wanaoipiga sana hii nchi, wanaoiba mafuta kigamboni, watu kama kina Ole Sabaya, watu wanaokula fedha za miradi ya serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wana uraia pacha?

Hiyo nafasi ya raia pacha kuifanyia Tanzania matendo ya kukosa uzalendo itakuwa katika mambo gani? Hebu tuangalie baadhi ya nchi hapa Afrika zenye uraia pacha, na tuwaulize wameathirika vipi na ukosefu wa uzalendo kwa raia pacha wao; South Afrika, Kenya, Ghana, Botswana, Rwanda, Burundi, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda nk? Hivi kuna mtu makini mambo ya uzalendo kama Kagame? Kwamba hakutafakari hadi kuruhusu uraia pacha kwa Rwanda? Isitoshe, kwani nani alisema tutaruhusu uraia pacha bila kuweka vigezo kama ukiwa raia pacha huruhusiwi kuwa labda raisi au waziri wa Tanzania? Huo unabaki kuwa uamuzi wetu.

Kwa sasa ni nchi nyingi za Afika zinazoruhusu uraia pacha ni nyingi kuliko zisizoruhusu uraia pacha (angalia ramani hapo chini). Kuna nchi kama Somalia, Liberia, ambao wamekuwa na maraisi waliokuwa na uraia pacha, waliharibu kitu gani? Mnafikiri ni kwa nini?

Balozi Malamula, kumbuka kwa sasa Tanzania ni mojawapo ya nchi nane Afrika ambazo bado haziruhusu uraia pacha, na huenda sasa zimebaki sita, kama Ethiopia na Cameroon wamesharuhusu.

Tatizo ni kwamba watu wanaopinga uraia pacha Tanzania wanafanya hivyo kwa sababu za wivu na ubinafsi tu, wala sio uzalendo. Wengi wao hawajawahi hata kutoka nje ya Tanzania. Na wengi wao hata chembe ya huo uzalendo hawana. Isitoshe, wengi wa wanaopinga uraia pacha wala hawaelewi kanuni na utaratibu wa mtu kupata uraia pacha. Watu wanadhani mtu anaenda tu kujiandikisha mahali apewe uraia pacha, kwa hiyo labda tukiruhusu uraia pacha labda nusu ya Watanzania wataomba uraia pacha! Kuwa raia pacha sio jambo rahisi, linahitaji uwe umeishi nchi ya pili kama mkazi kwa muda mrefu mara nyingi zaidi ya miaka mitano. Tunaposema Tanzania iruhusu uraia pacha, kimsingi sio Tanzania inayoruhusu, bali ni nchi ya uraia wa pili kama itamrughusu huyo Mtanzania kuwa raia wake. Na sio suala la kusema mie nataka kuwa raia pacha na USA wakati hata USA hujawahi kufika, achilia mbali kuishi!

Kwa hiyo Balazo Malamula, suala la uraia pacha lisisubiri Katiba mpya. Mswaada wa uraia pacha upelekwe tena Bungeni, au ufufuliwe ule uliokuwa umepelekwa. Kuna wakati lilipelekwa Bungeni likapitishwa, na Kikwete ndio alishauri kwamba kwa kuwa tuna mchakato wa Katiba mpya, badala ya kulipitisha kama Sheria mpya basi liingizwe kwenye katiba mpya - na hapo ndipo tulipokosea. Tuliwapa nafasi watu wenye ubishi wa kitoto kuleta hoja zao zisizo na mshiko nyuma ya ajenda zao za wivu usio na maana.

View attachment 1808843

Thread zangu nyingine juu ya uraia pacha:

Na wengine:​

In short issue hii inacheleweshwa na baathi ya watu wachache ndani ya chama na serikali kwa sababu zao binafsi, lakini naamini Raisi SSH anauwezo wa kupindua meza iwapo itaridhira na nina imani mama ana vision kubwa hata waangusha Watanzania wenzentu kwa hofu za kutengeneza.
 
Lazima kutakuwa na ndugu yako nje amekataa kukutumia hata dola moja kukusaidia, na sasa una hasira na uraia pacha ili umkomoe!
Aliyefanikiwa nje asingeweza kuhangaikia uraia pacha. waliokwama ndo tatizo. wanaasumbuliwa na kihoro. Utaweza kubeba maboksi hadi uzeeni?

Dunia naijua boss! Niko Bongo mchana huu najiandaa jioni niingie mitaani kucheka na majirani na wine yangu. wewe endelea kudumaa akiamini mitaji iko nje na eti tunakuhitaji sana!
 
Back
Top Bottom