Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Asante nishafahamu sasa turudi kwenye mada iliyo mezani.
Nitamuomba mode jukwaa la dini liwe public ili hawa wafia dini wamalize hasira zao huko.
Pasco

Umefahamu kitu gani mbona unataka kuwaomba mods wapeleke mambo ya siasa kwenye ukumbi wa dini?? Hivi kuna aya yeyote ya biblia au quran hapo ??
 
Usijidanganye nafsi yako wewe ni mtu unayeganga njaa na ndio ukajifanya eti uko neutral . Njaa kitu hatari . Umekua kama paka lenye mikia 9 .Opportunist kinoma. Mara umgeukie magufuli dikteta mzuri. Mara uwageukie chadema msiandamane mara unawaambia chadema nitakuja kuandamana kupinga udikteta . Unafiki mtupu
Tatizo ni levels tuu za uwezo wa kusoma in between the lines, ukinisoma umetulia level yako ya uelewa itapanda na utanielewa, bandiko hili na lile la nitaandamana is the same! , ila ni kwa watu wa levels tofauti za uelewa, moja ni direct, jingine indirect but it is the same thing! .

Vivyo hivyo kwa Magufuli ni dikiteta ila ni benevolent dictator ambaye ni dikiteta mzalendo mwenye anayekerwa na rushwa na ufisadi toka ndani ya nafsi yake hivyo anaufanya huu udikiteta wake kwa nia njema na dhamira safi ya kulikomboa taifa hili toka kwenye lindi la umasikini uliotopea uliogubikwa na rushwa na ufisadi.

Pasco
 
Umefahamu kitu gani mbona unataka kuwaomba mods wapeleke mambo ya siasa kwenye ukumbi wa dini?? Hivi kuna aya yeyote ya biblia au quran hapo ??
umesehau kule ulikonielekeza kwa yule mfia dini? .

Pasco
 
umesehau kule ulikonielekeza kwa yule mfia dini? .

Pasco


KWA MFIA DINI GANI ?? WEWE HUNA DINI ??

Hakuna hata sehemu moja nimekuletea kunakozungumziwa biblia au qurani

mote mna siasa za Nyerere na kanisa dhidi ya waislamu.

Naona umechanganyikiwa
 
Tatizo ni levels tuu za uwezo wa kusoma in between the lines, ukinisoma umetulia level yako ya uelewa itapanda na utanielewa, bandiko hili na lile la nitaandamana is the same! , ila ni kwa watu wa levels tofauti za uelewa, moja ni direct, jingine indirect but it is the same thing! .

Vivyo hivyo kwa Magufuli ni dikiteta ila ni benevolent dictator ambaye ni dikiteta mzalendo mwenye anayekerwa na rushwa na ufisadi toka ndani ya nafsi yake hivyo anaufanya huu udikiteta wake kwa nia njema na dhamira safi ya kulikomboa taifa hili toka kwenye lindi la umasikini uliotopea uliogubikwa na rushwa na ufisadi.

Pasco



ETI Anakerwa na rushwa na ufisadi tehtehtehhhh , na huku unajitia unamuunga mkono na hapohapo unajifanya unaenda kumpinga . Njaa kitu hatari , Kazi ipo opportunist

Hapa nakuwekea mstari


Mathayo 6:24

"Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine.

Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
 
ETI Anakerwa na rushwa na ufisadi tehtehtehhhh , na huku unajitia unamuunga mkono na hapohapo unajifanya unaenda kumpinga . Njaa kitu hatari , Kazi ipo opportunist
Hapa nakuwekea mstari
Mathayo 6:24
"Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine.

Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
Du! ,kumbe we jamaa ni muhubiri? !.

Nimepandisha nyuzi kibao humu kuhusu udikiteta wa Magufuli ambao nchi hii iliuhitaji ila pia naunga mkono UKUTA ili kuuzuia udikiteta huu usivuke mpaka, yaani udikiteta uishie kwenye kupambana na rushwa, uzembe, ufisadi na kuchochea Maendeleo lakini wakati huo huo akiiacha demokrasia ishamiri.

Pasco
 
Katika kitabu chake Bw. Bergen, kiitwacho Development and Religion in Tanzania, katika Ukurasa wake wa 98 mwanadishi huyo anasema:- “Catholic Missionaries came to East Africa to find not new churches, but new provinces of the Roman Church” Kwa mujibu wa tafsiri yangu “Wamishionari wa Kikatoliki hawakuja hapa Afrika ya Mashariki kwa minaajili ya kuasisi Makanisa mapya, bali walikuja kuunda majimbo mapya ya Kanisa la Roma”. Ni kwamba, Tanzania (Tanganyika) ipo Afrika Mashariki, na kwa mujibu wa mwandishi Bergen, Tanzania nayo ni moja ya majimbo ya Kanisa la Roma, au kwa lugha nyepesi tuseme Tanzania ni Koloni la Vatican! Je, ni kweli Tanzania (Tanganyika) ni Koloni la Vatican? Padri. Dk. Sivalon, naye katika kitabu chake Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania Bara (1953-1985) anaeleza bayana kuwa Mwalimu Julius Nyerere Rais wa Kwanza wa nchi yetu, alikuwa kiungo pekee kati ya Chama (CCM), Serikali na Kanisa Katoliki.

Na kwa msingi huo viongozi wa Kanisa wamekuja kuwa na nafasi ya pekee kuelekeza hisia, mitazamo na siasa ya Tanzania, na wamefanya hivyo wakipania pia kuwa kuhujumu Uislamu. (Msomoe Sivalon Uk. 5-6,
katika kitabu chake hicho). Naye m mwandishi Bergen katika kitabu chake amemnukuu Mwalimu Nyerere akisema kamwe hawezi kwenda kinyume na kanisa lake. (Bergen Uk. 335). Agosti 3, 1970 Mwalimu Nyerere, alimwita Ikulu Padri Rweyemamu katika mazungumzo maalum ambapo Nyerere alimuahidi Rweyemamu kuwa, hivi sasa Kanisa ndilo lililoshika hatamu za kuongoza dola naye atahakikisha hali inaendelea kuwa hivyo. “Tanzania is not Catholic country, but Catholics is strong, I want to give the church a better chance here”. Akiwa na maana kwamba:- japo “Tanzania si nchi ya Kikatoliki, lakini Ukatoliki una nguvu, hivyo nataka kulipa Kanisa nafasi ya pekee hapa nchini” (Msome, Bergen Uk. 335). Na hali hii ya Kanisa kuwa na nafasi kubwa Serikalini iko wazi.

Waandishi wote hawa wanatuthibitishia kuwa, kuna ukweli fulani kwamba yapo mafungamano ya dhati kati ya Kanisa Katoliki na Serikali ya Tanzania. Ni mafungamano hayo hayo ndiyo yameendelea kuwapa uweza viongozi wa Kanisa Katoliki kutoa maelekezo, maagizo na vilio vyao Serikalini na wakasikilizwa pamoja na kutekelezwa yale wanayoyahitaji hata kama yamelenga kuleta maafa kwa Waislamu. Mfano, mwaka 1998, Padri Lwambano, ambaye ni Paroko wa Kanisa Katoliki Mburahati Jijini Dar es Salaam, alisema kuiambia Serikali:- “Lazima Serikali ichukue hatua kali sana kwa Waislamu wanaoendesha Mihadhara, sababu ni watu wabaya kabisa, nimepita Sinza na Mwembechai, nimekuta Waislamu hao wanamtukana Yesu wanasema Yesu si Mungu”, alisema Paroko huyo na kuongeza; “Kama Serikali imeshindwa kuchukua hatua kali kukomesha Mihadhara ya Waislamu na kuendelea kutupaka matope kwa mgongo wa chupa, Serikali hii ijue sisi tutalishughulikia jambo hilo kwa nguvu zetu zote”.

Kauli hii ya Padri Lwambano, ilirushwa hewani na Kituo cha Radio Tumaini kinachomilikiwa na Kanisa hilo hapa nchini, Februari 13, 1998. Padri Lwambano bila kujali kuwa imani yake inaamini ‘Yesu ni Mungu’ na Waislamu imani yao inaamini ‘Yesu si Mungu’, aliinyooshea kidole Serikali nayo ilifuata bila kujali yenyewe (Serikali) haina dini na raia wake wana dini, kwa imani tofauti.

Katika utekelezaji wa agizo hilo bila shaka kila mtu anakumbuka kilichotokea. Ama kwa wale ambao walikuwa ni wadogo kipindi hicho ni kwamba Jeshi la Polisi lilifika Msikiti wa Mwembechai na kuuwa Waislamu kwa risasi na kikumbukumbu ni maarufu kwa ‘Mauaji ya Mwembechai’. Kufuatia madai hayo ya Padri Lwambano, viongozi kadhaa wa nchi walifikia hatua ya kuliomba radhi Kanisa Katoliki na Wakristo kwa ujumla. Majina na vyeo vya viongozi hao wakuu wa Serikali yanafahamika.

Baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Jeshi la Polisi, kazi ya kukatili maisha ya Waislamu na kubaka haki zao, kiongozi wa Kanisa Katoliki hapa nchini Polycarp Kadinali Pengo, aliipongeza Serikali kwa upande mmoja na Polisi kwa upande wa pili kufuatia mauaji hayo hayo ya Waislamu, Mwembechai. Pongezi hizo alizitoa April 12, 1998 wakati akihojiwa na kituo cha Televisheni cha Dar es Salaam (DTV). Kanisa likionekana kuuchukukia vilivyo Uislamu, liliongeza harakati za siri na za wazi na kwa kutumia nguvu za dola ili kupunguza kwa upande mwingine nguvu ya Uislamu, maana kuuzima kabisa ni jambo lisilowezekana.

Askofu Mkuu Pengo alitoa taarifa ya kuenea Uislamu hapa Tanzania huku akihitaji msaada wa hali na mali katika kuhidhibiti hali hiyo. Na kwa kweli, Serikali ilitekeleza kudhibiti Mihadhara na Wahadhiri, ambapo wahadhiri maarufu nchini wakiongozwa na Habib Mazinge, walitiwa mbaroni na kutupwa Magerezani. Aidha sehemu ya taarifa yake ilisema hivi; “Uislamu umekuwa tishio kubwa sana kwa imani ya Kikristo nchini Tanzania, iwapo mihadhara ya Waislamu itaachwa iendelee, Kanisa litegemee kukimbiwa na waumini wake na kusilimu, kwa hiyo juhudi lazima zifanywe kuzuia Mihadhara hiyo.

“Tunashindwa kujibu hoja zao Waislamu sababu zina ukweli ndani yake”, maelezo haya yanapatikana katika kitabu cha Askofu Pengo kiitwacho Jimbo Kuu la Dar es Salaam kwenye vijilia Sinodi ya Maaskofu wa Afrika kwa ajili ya Afrika.
Kama reference yako ni huyu mdini Mkuu humu jf, endelea, jamaa kasomeshwa na misheni lakini Shukrani hana! . Kwa kukusaidia tuu, misheni ndio kila kitu na akiwa Mkristu ni lazima awe Mkatoliki, alianza Juliasi, akaja Benyamini na sasa nI Yohana, ni chaguo la Kurasini japo muungwana alimtaka Benado pia wakamleta Petiro ili kumtumia kama kichinjio cha kumchinjia Eduadi.

Tena Nyerere ni wa kumshukuru sana maana asingeifutilia mbali ile jumuiya ya mujahidina, saa hizi na sisi tungekuwa kama Somalia! .

Pasco
Gavan/Pasco,
Katika hayo aliyoweka Gavana rejea si mimi.
Soma tena uone waliofanyiwa rejea ni kina nani.

Waliofanyiwa rejea ni Bergen na Sivalon na hawa wala si Waislam.

Gavana hakuishia hapo kaweka na maelezo kuweka wazi yote yale
yaliyotokea.

Hakika mimi nimesoma shule za misheni lakini elimu yangu haikuanzia
hapo.

Nimeisoma na dini yangu na hii ndiyo ilikuwa ya kwanza kutangulia kabla
ya kitu chochote kuingia katika ubongo wangu na naendelea kusoma
hadi sasa uzeeni.

Na ukipenda kufahamu hii elimu ya majadiliano haitokani na elimu ya
sekula hii nimesoma kwa Sheikh Haruna na siku zote huwaambieni.

Unaandika umeghadhibika.
Unaghadhibika kwa kuwa huna kitu.

Mimi nina mengi ya kusomessha hapa kwa hiyo hasira haina upenyo
katika fikra yangu.

Hii ndiyo tofauti kuu baina yangu na Pasco.
 
Gavan/Pasco,
Katika hayo aliyoweka Gavana rejea si mimi.
Soma tena uone waliofanyiwa rejea ni kina nani.

Waliofanyiwa rejea ni Bergen na Sivalon na hawa wala si Waislam.

Gavana hakuishia hapo kaweka na maelezo kuweka wazi yote yale
yaliyotokea.

Hakika mimi nimesoma shule za misheni lakini elimu yangu haikuanzia
hapo.

Nimeisoma na dini yangu na hii ndiyo ilikuwa ya kwanza kutangulia kabla
ya kitu chochote kuingia katika ubongo wangu na naendelea kusoma
hadi sasa uzeeni.

Na ukipenda kufahamu hii elimu ya majadiliano haitokani na elimu ya
sekula hii nimesoma kwa Sheikh Haruna na siku zote huwaambieni.

Unaandika umeghadhibika.
Unaghadhibika kwa kuwa huna kitu.

Mimi nina mengi ya kusomessha hapa kwa hiyo hasira haina upenyo
katika fikra yangu.

Hii ndiyo tofauti kuu baina yangu na Pasco.
Swadakta.
Pasco
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.
Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"

Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.
He should be careful of what he wish for!
we unaongea kama nani kibaraka mbwabwaji tu,inawezekana hata kwenye hayo maandamano hutakuwepo.nani asiyejua km nyie ni watetea tumbo tu,hamna lolote
 
Umefahamu kitu gani mbona unataka kuwaomba mods wapeleke mambo ya siasa kwenye ukumbi wa dini?? Hivi kuna aya yeyote ya biblia au quran hapo ??

Duh Gavana Wewe si mchezo maana umemfanya Pasco akimbilie Kwa marefa.
Unanikumbusha Mwandishi wa Kimerekani
James Baldwin alipofanya hoja Na William Buckley (Mwenye siasa kali za kibaguzi USA)
Huko Cambridge union society 1965.
Hongera tu Mkuu
 
Gavan/Pasco,
Katika hayo aliyoweka Gavana rejea si mimi.
Soma tena uone waliofanyiwa rejea ni kina nani.

Waliofanyiwa rejea ni Bergen na Sivalon na hawa wala si Waislam.

Gavana hakuishia hapo kaweka na maelezo kuweka wazi yote yale
yaliyotokea.

Hakika mimi nimesoma shule za misheni lakini elimu yangu haikuanzia
hapo.

Nimeisoma na dini yangu na hii ndiyo ilikuwa ya kwanza kutangulia kabla
ya kitu chochote kuingia katika ubongo wangu na naendelea kusoma
hadi sasa uzeeni.

Na ukipenda kufahamu hii elimu ya majadiliano haitokani na elimu ya
sekula hii nimesoma kwa Sheikh Haruna na siku zote huwaambieni.

Unaandika umeghadhibika.
Unaghadhibika kwa kuwa huna kitu.

Mimi nina mengi ya kusomessha hapa kwa hiyo hasira haina upenyo
katika fikra yangu.

Hii ndiyo tofauti kuu baina yangu na Pasco.

Maalim Mohamed Said huwa nafarijika sana kusoma hoja zako Na kujifunza sana juu ya elmu Na hekma zako.Mwenye Ez Mungu akuzidishie sana Nuru ili tupate mwangaza toka kwenye Nuru yako.
 
Kijana kama unampango wakuandamana hakikisha umepata sababu kumi kwanini unataka kuandamana kama hazifiki kumi kitulize kwenu au kwako usitie watu kwenye gharama za kukupeleka hospital wakati hujui unatetea nini. Usifananishe Tanzania na huko kwa wenzetu nje hii ni Africa utapigwa halafu kiongozi alikujaza upepo uandamane aseme makamanda walipigana vyema wakati huo yuko uingereza umeshampa KIKI
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.
Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"

Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.
He should be careful of what he wish for!
Elites hawana tabia ya kubadilikabadilika kama kinyonga! Pasco kuna kitu kinakuondoa taratibu kwenye kundi la elites.

CHADEMA Wakiamua kutokuandamana maana take Ni kwamba tumeamua kuwa kama Bunge,Au kuwa kama vyombo Vya habari Tanzania.Tutaandamana! Tena tutaandamana bila kikomo. Jumatatu hadi jumamosi,Septemba yote mpaka kieleweke.
 
Asanteni Chadema kuuchukua ushauri huu na kuufanyia kazi! .

Pasco
 
Back
Top Bottom